Serikali yakusanya mapato zaidi ya matumizi

Prof ndulu jua kua watz tunashida sana na maisha yetu yapo hatarini san,kwa ivyo punguza utani acha kuzidi kuaminisha watu kua mnawaibia mpendavyo
 
I expected more from this professor, the info which he was providing has to be done by their information officer!! Amwange vitu zaidi ya hivyo!
 
kujichanganya kwingine bwana! wakati deni la ndani limeongezeka yeye anasema wamepata kuliko matumizi.sasa walikopa ili iweje wakati fedha walikuwa nazo?ukweli ni kwamba unakopa kwenye vyombo vya fedha vya ndani unapo kuwa na shida ya fedha ya kuendeshea serikali ikiwa ni pamoja na kulipa mishahara ya wafanyakazi na kugharimia huduma muhimu kama elimu,afya n.k AMEANZA HEKAYA ZA ABUNUASI MCHANA KWEUPE SIJUI KWA FAIDA YA NANI??? NDULU BWANA!!
 
Prof ndulu jua kua watz tunashida sana na maisha yetu yapo hatarini san,kwa ivyo punguza utani acha kuzidi kuaminisha watu kua mnawaibia mpendavyo

Shida ya maisha yakomkama hujaitatuwa mwenyewe hawezi ndulu wala Mtei kukutatulia. Shida zako ujitatulie mwenyewe. Wewe kaa umchangie Mbowe na Slaaa kwenye kopo kwenye mikutano ya M4C huku mwenzako anazi"kopa' hizohizo kumjengea nyumba Josephine, halafu unalia unashida, yeye awache kujitatulia shida zake na walio karibu yake akujuwe wewe?

Punguzeni kuwa tegemezi na kudanganywa kuwa kuna Serikali itakayokuja ikupe fedha za sadaka. Sahau.
 
hii inaweza kuwa kweli?mbona halmashauri na hata wizara mambo ni magumu na miradi mingi imekwama kwa kukosa pesa!kwa nini mjiwekee malengo mepesi hivyo!yaani unavuka malengo lakini hautosheki kukamilisha miradi yote uliyopanga ila "matumizi ya kawaida"
 
NA Tausi Mbowe | Mwananchi - Sept 01, 2012

TANZANIA imeweza kukusanya mapato yaliyozidi matumizi kwa zaidi ya asilimia tatu kwa mara ya kwanza tangu mtikisiko wa uchumi uikumbe dunia.

Akizungumza katika ufunguzi wa Mfumo wa Dhamana ya Serikali kwa njia ya mtandao, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndulu alisema kuwa hadi kufikia Juni 30 mwaka huu, Serikali kupitia vyanzo mbalimbali imeweza kukusanya mapato ya zaidi ya Sh7.2 tirioni.

Gavana Ndullu alisema pamoja na makusanyo hayo makubwa Serikali imeweza kutumia Sh6.9 tirioni pekee kama matumizi yake ya kawaida tofauti na miaka iliyopita ambapo matumizi yalikuwa makubwa ukilinganisha na mapato yaliyopatikana.

"Hii ni mara ya kwanza kwa miaka mitatu mfululizo tangu msukosuko wa uchumi utokee, Serikali ilikuwa hafikii lengo la makusanyo na matumizi, mara zote mapato yalikuwa madogo ukilinganisha na matumizi. Serikali ilikuwa ikitumia zaidi ya mapato inayoyapata lakini sasa imeweza kutumia kidogo ukilinganisha na mapato yaliyopatikana," alisema Profesa Ndullu.

Alisema kwa sasa Serikali imeweza kugharamia matumizi yake ya kawaida lakini pia imeweza kuchangia bajeti yake yenyewe.

Akizungumia mfumuko wa bei, Profesa Ndulu alisema, kasi ya ongezeko la bei imeanza kuteremka na kufikia asilimia 15.7 kutoka 19.8 za awali.

Alisema ni matarajio ya Serikali kuwa kasi hiyo itazidi kuteremka kutokana na viashiria vingi kuonyesha wazi bei za bidhaa mbalimbali zinashuka ikiwemo bei ya mafuta.

Kwa upande wa thamani ya shilingi, Professa Ndulu alisema, kuanzia Januari mpaka sasa thamani ya shilingi imekaa katika sehemu nzuri ambapo kwa sasa Dola ya Marekani inanunuliwa kati ya Sh1,575 mpaka 1,590.

"Kwa kipindi kirefu pesa yetu ilishuka na kufikia Sh1,825 lakini tangu kuanza kwa mwaka huu imeweza kupanda na kubaki hapo hapo," alisisitiza Ndullu.

Kuhusu mfumo huo mpya, Ndullu alisema, utasaidia kufanya mnada na hati fungani za Serikali kwa kutumia mtandao wa kompyuta ambapo kila mshiriki ataweza kutumia mtandao huo pale alipo na kuileza BoT na taarifa hizo zitafika.

Alisema Tanzania ni nchi ya kwanza katika nchi za Afrika Mashariki kuwa na mfumo huo ambapo tayari wadau mbalimbali wataruhusiwa kushiriki ikiwemo Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) ambapo kwa sasa si lazima wapitie katika mabenki au wakala.

Alisema mfumo huo umekamilishwa na Watanzania wenyewe wakiwemo wataalam kutoka BoT hivyo kuokoa fedha za walipa kodi ambazo zingetumika kununua kutoka nje ya nchi.
Blaah Blaah tu
 
Kila wakati wanakusanya zaidi ya malengo. Malengo yenyewe tunaweka kiduchu ili zingine tuchukuwe na pengo lizibwe na mikopo na matokeo ya omba omba wetu.

Hapa sasa hivi watuambie tu kwamba safari hii hazijachotwa sana kujengea majumba na viwanda vya spirit. maana lazima ukoo wetu uwe na nyumba kila mkoa.

Au sasa vituo vya mafuta vimeanza kuleta faida na hatuhishaji tena kuchota? Tumbee magari yetu ya usafirishaji yasipate ajari!
 
Back
Top Bottom