Mmawia
JF-Expert Member
- Aug 20, 2013
- 121,947
- 95,237
Miwashukuru wale wote waliofanya kisomo cha albadiri
Mwanzo walikuwa wanasema uchumi unapaa na Tanzania inaongoza kwa uchumi wake kupanda barani Afrika, juzi Dr Mpango amekiri wazi kuwa uchumi wa nchi unaporomoka.
Walikuwa wanakataa serikali haijashitakiwa kwenye mahakama ya usuluhishi ya kimataifa, leo Dr. Kabudi kasema ni kweli makampuni ya Pangea Mineral Limited na Bulyanhulu Gold Mining yameishitaki serikali.
Kwa trend hii kuna siku serikali itakuja kukiri wazi kuwa inawajua wasiojulikana, inajua waliko Ben na Azory, inawajua waliomteka MO nk.
Wakati ni mwalimu mzuri sana tega sikio.