Serikali yakanusha 'kujiuzulu' kwa Magufuli

vipofu wanapoongozana, 'kujiuzulu' siyo 'kujiudhuru'

Mkuu kipilipili, waache tu hao vipofu wakatumbukizane huko kunako handaki. Nchi ikishapoteza dira na mwelekeo tabu sana..hapa tatizo si la hao vipofu wawili hapo juu, ila ni mfumo mbovu wa elimu, na kwenye lugha tatizo halijatuhurumia hata chembe..angalia unaanza 'kendagateni" unafundishwa kwa kiswahili, unaingia la kwanza mpaka la saba ni kiswahili...akili inaanza kujengeka vizuri na kujipanga....mara vuuuuuu bin vuuuuuu unaanza kushindiliwa "kingeledha" unapoanza "fomu wani"...huna msingi wa hicho kiingeledha.. so ka-msingi ni ka kujenga nyumba ndongo ya vyumba viwili, lakini hatimaye linakuja kulazimishwa ghorofa la "floo" kumi juu ya hako ka-mzingi--teh teh tehi!!!!!!!!!!! matokeo kwenye kingeledha hatumo kwenye kiswahili hatumo. tumejaribu kuunda lugha-pori yakusaidia kupunguza tatizo - "kiswa-inglidhi" lakini nacho tabu tu zaidi. solusheni ya haraka ya watawala vichwa maji ni kugawa wanafunzi..wa watawala "wa-enroool" kwenye "akademiiiz" na "seints" na wale wa wakulima "wa-enirool" kwenye zile za kata, lakini kodi wote wanachanga.....matokeo yake ndo hawa vipofu, "akchuale" si hawa vipovu ndo vipovu ila ka-nchi kalikokuwa kametukuka sasa kamekuwa kipofu, hakaoni tena na kanaelekea handakini. mafisadi yanakata tawi walilokalia, nayo yatatumbukia huko huko kunako handakini...Nyie ngojeni tu "T" will "T"(Time will Tell)

mafisadi yanatutesa na kutulostisha sana watoto wa pizants...lakini ipo siku Insha-Allah...
 
BAKITA wamo humu eee, jitahidini kurekebisha kiswahili wengine wanakibomoa makusudi kabisaaa. Mfano neo bwana wanasema bana aah badilikeni.
 
BAKITA wamo humu eee, jitahidini kurekebisha kiswahili wengine wanakibomoa makusudi kabisaaa. Mfano neo bwana wanasema bana aah badilikeni.

warekebisha kuwa fasaha au kibovu? kama warekebishe kuwa kibovu zaid sna neno nakuelewa, ila kama una maana warekebishe kuwa kizuri, tueleze wafanye hivo for what wakti nchi haikitaki kiswahili? badala ya kupoteza mda kurekebisha kiswahili kiwe kidhuli/fasaha waambie wajifunze tu kingeledha...
 
Katuni Mach 16.jpg
Sema tusikie,kwa sababu utazungumza nini sasa wakati ajenda ilikuwa ni bomoabomoa.Na baraza la mawaziri lilikutana bomoabomoa haikuwa mojawapo ya ajenda,Sasa kimya.Sema upo au umeachia UJENGE SIFA sema usisemewe na katibu wako.?
 
Hili linashangaza! Hili suala msemaji alitakiwa kuwa magufuli mwenyewe.
 
Aseme nini na anasubiri barua yake ijibiwe?

Hana lolote huyo angekuwa anataka kujiuzulu kweli na kama kweli amemtwanga mkwere barua ya kujiuzulu kwa nini asiite press conference kuujuza umma na kusema kuwa anasubiri majibu y barua yake ya kujiuzulu toka kwa Rais.
 
Je wakudhibitisha kujiudhulu kwako ni Rais au katibu wa wizara yako.?
mkuu hata mimi ilinishangaza! sana iweje katibu amsemee kwani ndiye aliyeandikiwa barua??
barua iliandikwa kwa raisi kwa hiyo wakukanusha alikuwa ni magufuli au ofisi ya raisi! mimi sijui haya mambo yanakwendaje??
 
Hana lolote huyo angekuwa anataka kujiuzulu kweli na kama kweli amemtwanga mkwere barua ya kujiuzulu kwa nini asiite press conference kuujuza umma na kusema kuwa anasubiri majibu y barua yake ya kujiuzulu toka kwa Rais.

Nafikiri kila mtu ana namna yake ya kufikisha ujumbe wake kwenye jamii,uliyoisema ni mojawapo ya njia!!cha msingi tuheshimu mawazo yake!!
 
Alikuwa anapima upepo tu,Hakuna wazir wa Ccm mwenye uzalendo wa kweli,Magufuli anataka sifa tu.HANA LOLOTE
 
Hana lolote huyo angekuwa anataka kujiuzulu kweli na kama kweli amemtwanga mkwere barua ya kujiuzulu kwa nini asiite press conference kuujuza umma na kusema kuwa anasubiri majibu y barua yake ya kujiuzulu toka kwa Rais.

Maswari mengi yasiyokuwa na majibu hapo?.Aikuzushwa tu ukweli hupo.?
 
huo ni ukweli usiopingika, magufuli kajiuzulu ila wanaficha tu na ukweli utajulikana tu.
 
Ni kweli, kwa utamaduni wa viongozi wetu hakuna mwenye ujasiri wa kuachia ngazi kwa maana ya kujiuzuru. Na nijuavyo mimi kama kweli umedhamilia kuacha kazi huwezi kuomba utakachofanya ni kutoa taarifa kwamba kuanzia tarehe hii mimi siyo waziri tena. Raisi hwezi kumlazimisha mtu kufanya kazi.

Huyu Mh kama mlivyosema anapima upepo, sasa sina uhakika ameona unavumaje, na unavuma kuelekea wapi. Jibu analo yeye na Mh Pinda.
 
Ni kweli, kwa utamaduni wa viongozi wetu hakuna mwenye ujasiri wa kuachia ngazi kwa maana ya kujiuzuru. Na nijuavyo mimi kama kweli umedhamilia kuacha kazi huwezi kuomba utakachofanya ni kutoa taarifa kwamba kuanzia tarehe hii mimi siyo waziri tena. Raisi hwezi kumlazimisha mtu kufanya kazi.

Huyu Mh kama mlivyosema anapima upepo, sasa sina uhakika ameona unavumaje, na unavuma kuelekea wapi. Jibu analo yeye na Mh Pinda.

Tangu nimsikie Mh.DR. kitu kinachomhusu kusemewa na mtu,wanasema jamaa yule yupo makini.? Je kwa hili au nalo anatafuta umaarufu wa kujiudhulu??
 
Kwanza katibu mkuu yuko chini ya waziri nilishangaa sana kuona anamjibia waziri wake na kusema magufuli hajawahi kuwa na wazo la kujiudhuru kana kwamba yeye yuko kwenye ubongo wake. Kauli za katibu mkuu zimekaa kisiasa zaidi ukweli ni kwamba bado wanambembeleza magufuli asitishe uamuzi wake ndio maana hata magufuli hajajitokeza kukanusha na akipigiwa simu na waandishi hapokei simu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom