Chenge
JF-Expert Member
- Oct 5, 2011
- 1,073
- 377
[h=3]Bhoke Ametuponza: Serikali Yapiga Marufuku Watanzania Kushiriki Big Brother !!!![/h]
SERIKALI imepinga Tanzania kushiriki shindano la Big Brother Afrika kwa kuwa shindano hilo linapotosha maadili ya kiafrika na kuharibu kizazi cha watoto wa Tanzania.
Akizungumza bungeni jana, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Emmanuel Nchimbi alisema shindano hilo ni kero kubwa kwa serikali na taifa kwa ujumla na hawajui linafundisha nini kwa jamii.
"Hatujui linafundisha nini watoto wetu, linapotosha jamii, ni kero kubwa hatushabikii shindano hili na wanaoenda kushiriki wajue hawana baraka za serikali ndio maana hatujawahi kwenda kuwapokea na bahati yao mawasiliano yao ya kushiriki wanafanya kwa njia ya mtandao,"alisema Nchimbi.
Alisema shindano hilo limekuwa likichochea uvunjifu wa maadili kwa washiriki na hata kwa wale wanaobaki nchini.
Kauli ya Nchimbi imekuja baada ya wabunge kuhoji umuhimu wa shindano hilo ambalo limekuwa likichochea vitendo vya ngono kutokana na kuonyeshwa live kila kitu kinachoendelea ndani ya jumba hilo kinyume na maadili ya kiafrika.
Hivi karibuni mshiriki wa Tanzania, Bhoke Egina alikumbwa na kashfa kubwa ya kujiingiza kwenye uhusiano wa mapenzi na mshiriki toka Uganda Enerst.
Washiriki wengine watanzania walioshiriki shindano hilo na hawakukwepa kashfa ya kujiingiza kwenye uhusiano wa kimapenzi ni Mwisho Mwampamba, Richard Benezueout na Latoya.
Shindano hilo huandaliwa na M - Net Afrika na kurushwa moja kwa moja na kituo hicho, limekuwa likifanyika nchini Afrika Kusini kwa kushirikisha nchi zaidi ya 20 barani Afrika.
Wakati huo huo; Wabunge wameendelea kuishutumu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa kushindwa kukidhi mahitaji ya wasanii, wanamichezo, wanahabari pamoja na kutunza mila destruri na utamaduni wa nchi.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana wakati wa kujadili bajeti ya Wizara hiyo wabunge hao walionyesha dhahiri kusikitshwa na baadhi ya vyombo husika vilivyo chini ya Wizara hiyo, vinavyoshughulikia masula ya Michezo na Utamaduni kushindwa kufanya kazi kwa ufasaha kwa kuzingatia maslahi ya wahitaji ambao wengi wao ni vijana.
Akichangia hoja Mbunge wa Kinondoni, Iddi Mohamed Azzan alisema Wizara hiyo ina sera na sheria mbovu za zamani zisizokidhi mahitaji ya sasa kwa watu walioamua kujiajiri katika sekta ya sanaa na michezo kutokana na maendeleo sayansi na teknolojia ya sasa, watendaji ni wabovu na vyombo vilivyopewa mamlaka kama BASATA na COSOTA havifanyi kazi ipasavyo.
"Kutokana na kuwepo kwa watendaji wabovu waliolala usingizi mzito na kutawaliwa na rushwa kamwe hatuwezi kuendelea, la sivyo sera na sheria za zamani zisizokidhi mahitaji ya walioamua kujikita katika masula ya sanaa na michezo zifanyiwe mabadiliko ya hali ya juu,alisema Azzan.
Kwa upande wake Mbunge wa Peramiho (CCM), Jenista Mhagama alisema kiasi kilichotengwa kwa ajili ya utekelezaji wa mipango ya Idara ya Maendeleo ya Vijana hakitoshi, kwa sababu asilimia kubwa ya wananchi wa Tanzania ni vijana ambao wengi wao wamejiari katika taaluma ya habari, michezo, muziki na utamaduni.
Hivyo aliomba bajeti katika Idara hizo iongezwe fedha ili kukidhi mahitaji ya vijana wengi waliopo vijiweni bila ajira na kushauri vijiwe hivyo vitumike kama vikundi vya maendeleo kwa kuvipatia mitaji.
(Vicky Kimaro na Furaha Maugo)
Friday, 12 August 2011 21:11
SERIKALI imepinga Tanzania kushiriki shindano la Big Brother Afrika kwa kuwa shindano hilo linapotosha maadili ya kiafrika na kuharibu kizazi cha watoto wa Tanzania.
Akizungumza bungeni jana, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Emmanuel Nchimbi alisema shindano hilo ni kero kubwa kwa serikali na taifa kwa ujumla na hawajui linafundisha nini kwa jamii.
"Hatujui linafundisha nini watoto wetu, linapotosha jamii, ni kero kubwa hatushabikii shindano hili na wanaoenda kushiriki wajue hawana baraka za serikali ndio maana hatujawahi kwenda kuwapokea na bahati yao mawasiliano yao ya kushiriki wanafanya kwa njia ya mtandao,"alisema Nchimbi.
Alisema shindano hilo limekuwa likichochea uvunjifu wa maadili kwa washiriki na hata kwa wale wanaobaki nchini.
Kauli ya Nchimbi imekuja baada ya wabunge kuhoji umuhimu wa shindano hilo ambalo limekuwa likichochea vitendo vya ngono kutokana na kuonyeshwa live kila kitu kinachoendelea ndani ya jumba hilo kinyume na maadili ya kiafrika.
Hivi karibuni mshiriki wa Tanzania, Bhoke Egina alikumbwa na kashfa kubwa ya kujiingiza kwenye uhusiano wa mapenzi na mshiriki toka Uganda Enerst.
Washiriki wengine watanzania walioshiriki shindano hilo na hawakukwepa kashfa ya kujiingiza kwenye uhusiano wa kimapenzi ni Mwisho Mwampamba, Richard Benezueout na Latoya.
Shindano hilo huandaliwa na M - Net Afrika na kurushwa moja kwa moja na kituo hicho, limekuwa likifanyika nchini Afrika Kusini kwa kushirikisha nchi zaidi ya 20 barani Afrika.
Wakati huo huo; Wabunge wameendelea kuishutumu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa kushindwa kukidhi mahitaji ya wasanii, wanamichezo, wanahabari pamoja na kutunza mila destruri na utamaduni wa nchi.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana wakati wa kujadili bajeti ya Wizara hiyo wabunge hao walionyesha dhahiri kusikitshwa na baadhi ya vyombo husika vilivyo chini ya Wizara hiyo, vinavyoshughulikia masula ya Michezo na Utamaduni kushindwa kufanya kazi kwa ufasaha kwa kuzingatia maslahi ya wahitaji ambao wengi wao ni vijana.
Akichangia hoja Mbunge wa Kinondoni, Iddi Mohamed Azzan alisema Wizara hiyo ina sera na sheria mbovu za zamani zisizokidhi mahitaji ya sasa kwa watu walioamua kujiajiri katika sekta ya sanaa na michezo kutokana na maendeleo sayansi na teknolojia ya sasa, watendaji ni wabovu na vyombo vilivyopewa mamlaka kama BASATA na COSOTA havifanyi kazi ipasavyo.
"Kutokana na kuwepo kwa watendaji wabovu waliolala usingizi mzito na kutawaliwa na rushwa kamwe hatuwezi kuendelea, la sivyo sera na sheria za zamani zisizokidhi mahitaji ya walioamua kujikita katika masula ya sanaa na michezo zifanyiwe mabadiliko ya hali ya juu,alisema Azzan.
Kwa upande wake Mbunge wa Peramiho (CCM), Jenista Mhagama alisema kiasi kilichotengwa kwa ajili ya utekelezaji wa mipango ya Idara ya Maendeleo ya Vijana hakitoshi, kwa sababu asilimia kubwa ya wananchi wa Tanzania ni vijana ambao wengi wao wamejiari katika taaluma ya habari, michezo, muziki na utamaduni.
Hivyo aliomba bajeti katika Idara hizo iongezwe fedha ili kukidhi mahitaji ya vijana wengi waliopo vijiweni bila ajira na kushauri vijiwe hivyo vitumike kama vikundi vya maendeleo kwa kuvipatia mitaji.
Source: Mwananchi