Serikali yaingiwa na hofu jinsi mbunge anavyopata taarifa nyeti

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,005
Wananchi hawana imani na serikali ndiyo maana wanatoa nyeti ili labda wasaidie kuleta mabadiliko kwa manufaa ya Watanzania wote. Nyeti za serikali zitaendelea kutoka tu mpaka pale Watanzania wawe na imani na serikali iliyipo madarakani ipo pale kwa manufaa ya Watanzania wote na siyo kundi la mafisadi wachache

Date::6/29/2008
Serikali yaingiwa na hofu jinsi mbunge anavyopata taarifa nyeti
Na Kizitto Noya, Dodoma
Mwananchi

SERIKALI inaumiza kichwa kujua mtandao unaotumiwa na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk Willibrod Slaa, kupata taarifa zake za siri na kuzianika hadharani.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera), Philip Marmo amekiri bungeni juzi jioni kuwa, Dk Slaa ana mtandao mkubwa usiofahamika anaoutumia kupata nyaraka za siri za serikali kinyume na taratibu.

Kauli ya Marmo ilifuatia swali la Dk Slaa kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda wakati Kamati ya Bunge ilipokuwa inapitia vifungu kwa ajili ya kupitisha Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, kuwa ni aina gani ya nyaraka za serikali zinapaswa kuwa siri.

Dk Slaa alitaka kujua endapo nyaraka za serikali ambazo zimejaa kumbukumbu za kifisadi na ambazo wabunge wakiziomba kwa utaratibu wa kawaida wananyimwa, zinapaswa kuwa siri.

Akiwa na nyaraka kadhaa mkononi alizosema kuwa ni sehemu ya zile za serikali zinazopaswa kuwa siri, lakini watu aliowaita wasamaria wema wamempa, Dk Slaa alisema haelewi mantiki ya nyaraka hizo kuwa siri wakati hazina faida kwa taifa.

Mheshimiwa Waziri Mkuu, mimi naomba kuuliza ni nyaraka gani hasa za serikali zinapaswa kuwa siri. Hata zile ambazo zimejaa uongo? Mimi ninazo hapa na kama

Mheshimiwa Marmo anataka kuwatuma polisi waje wanikamate niko tayari, lakini nyaraka hizi zina maana gani kwa taifa? alihoji Dk Slaa akionyesha nyaraka hizo.

Kwa mujibu wa Dk Slaa wapinzani wanajua umuhimu wa usiri wa nyaraka za serikali, lakini inapofikia mahala mfumo wa serikali unaanza kuporomoka, hawana sababu ya kuogopa kutafuta nyaraka hizo kwa njia ya mkato na kuzitumia kuweka mambo hadharani.

Lakini kama mfumo wa serikali unaanza kuanguka na serikali ikaonyesha nia ya dhati kudhibiti tatizo hilo, sisi ni wazalendo pia hatutazitafuta wala kutoa tena siri za serikali hadharani, alisisitiza.

Akijibu suali hilo kwa upole, Marmo alisema, inaonekana Dk Slaa ana mtandao mkubwa katika kupata taarifa hizo za siri na amekuwa mjanja katika kuzizungumzia kuwa anafahamu kuwa kufanya hivyo ni kosa la jinai.

Dk Slaa ni mjanja sana anajua anachofanya kuwa ni kosa la jinai. Pana jinai hapa na ndio maana hata katika hii nyaraka ya EPA amesema, nimeondoa jina la source (chanzo cha Habari) kwa usalama wake, alisema Marmo akinukuu nyaraka ya siri ya serikali aliyodai kuwa imepatikana kutoka kwa Dk Slaa.

Marmo alisema nyaraka za serikali lazima ziwe za siri na kuwa nazo mtu asiyehusika ni kosa la jinai ingawa kama kuna umuhimu wa mtu kuzipata anaweza kufanya hivyo katika utaratibu unaokubalika.

Aliwataka wabunge wanaotaka kujua mambo ya serikali kupitia nyaraka zake za siri kufuata utaratibu badala ya kutumia njia ya mkato kisha kuanika siri za serikali

hadharani. Mimi naomba tufuate utaratibu, kinyume chake huko ni kuidhalilisha serikali, alisema Marmo.

Kwa muda mrefu sasa Dk Willibrod Slaa na chama chake cha CHADEMA amekuwa akiibua tuhuma mbalimbali za ufisadi ndani ya serikali kwa kutumia nyaraka za siri za serikali.

Baadhi ya tuhuma hizo ni upotevu wa mabilioni ya shilingi katika Akaunti ya Madeni ya Nje ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (EPA), rushwa katika upatikanaji wa zabuni ya

kuzalisha umeme wa dharura na Kampuni ya Richmond na mikataba mibovu katika migodi ya madini.

Juzi, Dk Slaa alipingana na Waziri Mkuu Mizengo Pinda katika majibu yake kwamba hawezi kuzungumzia suala la Meremeta kwa sababu za ulinzi na usalama.

Dk Slaa na Mwenyekiti wa Chama cha UDP, John Cheyo walimweleza Pinda kuwa Meremeta wanayomtaka azungumzie ni ile ya pili baada ya jeshi kumaliza kazi na kampuni waliyodai kuwa ni 'Meremeta ya kwanza'.

Cheyo alisema alitaka suala la Meremeta kufanyiwa uchunguzi wa kina na kwamba kulihusisha na suala hilo na jeshi sio sawa na kwamba Waziri Mkuu anapaswa kuwatendea haki Watanzania kwa kuzungumzia suala hilo.

Kama kweli kuna Sh12 bilioni Tangold, tunazihitaji kwa ajili ya miradi ya maji, alisema Cheyo.

Hata hivyo, Pinda alishikilia msimamo wake na kugoma kuzungumzia kampuni hiyo yenye makampuni tanzu ya Tangold, Deep Green na Green Finance kwa maelezo kuwa yanahusiana na Jeshi na kwamba yuko tayari kusulubiwa kwa hilo.
 
Dr. Slaa ni dume la mbegu. Hata mimi ningelikuwa na hizo siri ningempelekea.

Jamaa kawakamata pabaya hasa. Hata wakimpata Dr. Slaa, wengine watatokea tena.

Mambo mengine yanaudhi mno na ni muhimu kufichuliwa.
 
Hongera sana Dr Slaa,

hili suala nilishawahi kulisema hapa JF............kwa nini watu wafanye ufisadi na documents associated ziwe classified as Secret?...........huu ni upumbavu.

Secrets should be kwa manufaa ya umma na si vinginevyo...........statements za Mizengo Pinda zinakatisha tamaa beyond belief...............it appears mafisadi fought for this PM position............now they have it!!!........guys lets forget abt mafisadi......atleast for now.........honestly ni vita ngumu sana.............kwa sababu mafisadi now have got all means necessary for their cover.....
 
Hongera sana Dr Slaa,

hili suala nilishawahi kulisema hapa JF............kwa nini watu wafanye ufisadi na documents associated ziwe classified as Secret?...........huu ni upumbavu.

Secrets should be kwa manufaa ya umma na si vinginevyo...........statements za Mizengo Pinda zinakatisha tamaa beyond belief...............it appears mafisadi fought for this PM position............now they have it!!!........guys lets forget abt mafisadi......atleast for now.........honestly ni vita ngumu sana.............kwa sababu mafisadi now have got all means necessary for their cover.....

Ni kweli vita dhidi ya mafisadi ni ngumu mno, lakini tusilegeze kamba. Chama Cha Mafisadi kitafunga watu na hata kuwaua ili kulinda maslahi yao na ya mafisadi wachache lakini kamwe tusikate tamaa kwa sababu tukishindwa kwenye vita hii ambayo inaendeshwa kwa amani basi matokeo yake yatakuwa mabaya zaidi.
 
Hakuna cha siri wala nini hapa kwani kama siri ni juu ya kuficha waizi na majambazi ambao wametuibia basi hizo sio siri hata kidogo kwani hakuna siri kwenye wizi .

Kuna kila sababu ya kuhakikisha kuwa tunaendeleza mapambano haya hata kama kuna watakao umia sawa ila siku ya mwisho tuweze kutoka salama .
 
Wananchi hawana imani na serikali ndiyo maana wanatoa nyeti ili labda wasaidie kuleta mabadiliko kwa manufaa ya Watanzania wote. Nyeti za serikali zitaendelea kutoka tu mpaka pale Watanzania wawe na imani na serikali iliyipo madarakani ipo pale kwa manufaa ya Watanzania wote na siyo kundi la mafisadi wachache

Date::6/29/2008
Serikali yaingiwa na hofu jinsi mbunge anavyopata taarifa nyeti
Na Kizitto Noya, Dodoma
Mwananchi

SERIKALI inaumiza kichwa kujua mtandao unaotumiwa na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk Willibrod Slaa, kupata taarifa zake za siri na kuzianika hadharani.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera), Philip Marmo amekiri bungeni juzi jioni kuwa, Dk Slaa ana mtandao mkubwa usiofahamika anaoutumia kupata nyaraka za siri za serikali kinyume na taratibu.

Kauli ya Marmo ilifuatia swali la Dk Slaa kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda wakati Kamati ya Bunge ilipokuwa inapitia vifungu kwa ajili ya kupitisha Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, kuwa ni aina gani ya nyaraka za serikali zinapaswa kuwa siri.

Dk Slaa alitaka kujua endapo nyaraka za serikali ambazo zimejaa kumbukumbu za kifisadi na ambazo wabunge wakiziomba kwa utaratibu wa kawaida wananyimwa, zinapaswa kuwa siri.

Akiwa na nyaraka kadhaa mkononi alizosema kuwa ni sehemu ya zile za serikali zinazopaswa kuwa siri, lakini watu aliowaita wasamaria wema wamempa, Dk Slaa alisema haelewi mantiki ya nyaraka hizo kuwa siri wakati hazina faida kwa taifa.

Mheshimiwa Waziri Mkuu, mimi naomba kuuliza ni nyaraka gani hasa za serikali zinapaswa kuwa siri. Hata zile ambazo zimejaa uongo? Mimi ninazo hapa na kama

Mheshimiwa Marmo anataka kuwatuma polisi waje wanikamate niko tayari, lakini nyaraka hizi zina maana gani kwa taifa? alihoji Dk Slaa akionyesha nyaraka hizo.

Kwa mujibu wa Dk Slaa wapinzani wanajua umuhimu wa usiri wa nyaraka za serikali, lakini inapofikia mahala mfumo wa serikali unaanza kuporomoka, hawana sababu ya kuogopa kutafuta nyaraka hizo kwa njia ya mkato na kuzitumia kuweka mambo hadharani.

Lakini kama mfumo wa serikali unaanza kuanguka na serikali ikaonyesha nia ya dhati kudhibiti tatizo hilo, sisi ni wazalendo pia hatutazitafuta wala kutoa tena siri za serikali hadharani, alisisitiza.

Akijibu suali hilo kwa upole, Marmo alisema, inaonekana Dk Slaa ana mtandao mkubwa katika kupata taarifa hizo za siri na amekuwa mjanja katika kuzizungumzia kuwa anafahamu kuwa kufanya hivyo ni kosa la jinai.

Dk Slaa ni mjanja sana anajua anachofanya kuwa ni kosa la jinai. Pana jinai hapa na ndio maana hata katika hii nyaraka ya EPA amesema, nimeondoa jina la source (chanzo cha Habari) kwa usalama wake, alisema Marmo akinukuu nyaraka ya siri ya serikali aliyodai kuwa imepatikana kutoka kwa Dk Slaa.

Marmo alisema nyaraka za serikali lazima ziwe za siri na kuwa nazo mtu asiyehusika ni kosa la jinai ingawa kama kuna umuhimu wa mtu kuzipata anaweza kufanya hivyo katika utaratibu unaokubalika.

Aliwataka wabunge wanaotaka kujua mambo ya serikali kupitia nyaraka zake za siri kufuata utaratibu badala ya kutumia njia ya mkato kisha kuanika siri za serikali

hadharani. Mimi naomba tufuate utaratibu, kinyume chake huko ni kuidhalilisha serikali, alisema Marmo.

Kwa muda mrefu sasa Dk Willibrod Slaa na chama chake cha CHADEMA amekuwa akiibua tuhuma mbalimbali za ufisadi ndani ya serikali kwa kutumia nyaraka za siri za serikali.

Baadhi ya tuhuma hizo ni upotevu wa mabilioni ya shilingi katika Akaunti ya Madeni ya Nje ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (EPA), rushwa katika upatikanaji wa zabuni ya

kuzalisha umeme wa dharura na Kampuni ya Richmond na mikataba mibovu katika migodi ya madini.

Juzi, Dk Slaa alipingana na Waziri Mkuu Mizengo Pinda katika majibu yake kwamba hawezi kuzungumzia suala la Meremeta kwa sababu za ulinzi na usalama.

Dk Slaa na Mwenyekiti wa Chama cha UDP, John Cheyo walimweleza Pinda kuwa Meremeta wanayomtaka azungumzie ni ile ya pili baada ya jeshi kumaliza kazi na kampuni waliyodai kuwa ni 'Meremeta ya kwanza'.

Cheyo alisema alitaka suala la Meremeta kufanyiwa uchunguzi wa kina na kwamba kulihusisha na suala hilo na jeshi sio sawa na kwamba Waziri Mkuu anapaswa kuwatendea haki Watanzania kwa kuzungumzia suala hilo.

Kama kweli kuna Sh12 bilioni Tangold, tunazihitaji kwa ajili ya miradi ya maji, alisema Cheyo.

Hata hivyo, Pinda alishikilia msimamo wake na kugoma kuzungumzia kampuni hiyo yenye makampuni tanzu ya Tangold, Deep Green na Green Finance kwa maelezo kuwa yanahusiana na Jeshi na kwamba yuko tayari kusulubiwa kwa hilo.
Hivi huyu Marmo kwa sababu aliwahi kuwa waziri wa utawala uliojaa uchafu anataka kujibu kila kitu kinachohusiana na mambo ya utawala mchafu? Yeye ni nani hadi ajifanye nchi hii ni mali yake?
Hizo nyaraka tutaendelea kuwa nazo na kwa taarifa yake nyaraka zote zilizo jaa ufisadi lakini zikafanywa ni siri, tutazipeleka kwa wananchi wenyewe tena wa jimbo lake ili wakate mashauri wao, na tuone hiyo siri yake. Au to be straight 'wizi wake'.
 
Ni wazi viongozi wetu tuliowaweka wenyewe madarakani wamejisahau kabisa na sasa wanadhani serekali ni mali yao na si wananchi. Kila wakibanwa watoe maelezo kwa kila soo linalobumburuka sasa hivi style yao ya kuzima issue ni kutisha watu kwa kusema ni 'siri' na kinyume cha sheria. Siri ya nani? Its shocking how anyone can say serekali inadhalilishwa! Sisi wananchi tusemeje ikiwa kila jambo tunalotaka maelekezo toka kwa watumishi wetu linageuka kuwa siri?
 
Ni wazi viongozi wetu tuliowaweka wenyewe madarakani wamejisahau kabisa na sasa wanadhani serekali ni mali yao na si wananchi. Kila wakibanwa watoe maelezo kwa kila soo linalobumburuka sasa hivi style yao ya kuzima issue ni kutisha watu kwa kusema ni 'siri' na kinyume cha sheria. Siri ya nani? Its shocking how anyone can say serekali inadhalilishwa! Sisi wananchi tusemeje ikiwa kila jambo tunalotaka maelekezo toka kwa watumishi wetu linageuka kuwa siri?

KKN, si ndiyo maana ikaitwa SIRI KALI.....:(
 
Inaonyesha Waziri Mkuu amepewa kimemo kuwa kimya na kujiepusha na suala hilo kama anaitaka roho yake ,ndio akaona bora asulubiwe au kwa lugha ya kileo awajibishwe ili kuinusuru roho yake ,naweza kusema wananchi ndio wenye uamuzi wa mwisho juu ya mafisadi hawa.
 
Mimi nilifikiria serikali ingempongeza Dr. Slaa kwa kufatilia mambo ya aina hii hili angalau watendaji wake waweze kufanya kazi kwa ufanisi na umakini zaidi.

Badala yake sasa tunaweza kuona jinsi serikali yetu inavyopenda sana watendaji wabovu wenye kuweka mambo mabovu yasiyo na maana na kuyaita siri za serikali.

Hili limetuonyesha jinsi tunavyohitaji mbinu za makusudi kuwaondoa hawa watawala wabovu wanaokaa na uchafu na kuuita ndio siri zao.

Nafikiri Dr. Slaa sasa inatakiwa aongeze nguvu katika kufichua maovu kwa manufaa ya jamii nzima ya tanzania. Ongera Dr. Slaa.
 
Hawa watafichua mpaka watazeeka na mengine hawajayamaliza na bado mengine kuyagusa ,natumai wangemata moja mpaka wajue mwisho wake kuliko kila siku kuvumbua jengiene ,mwisho wananchi nao wataona ni kamchezo tu huko bungeni.
 
Wait a minute,

hizi siri kwa nini zinaibuka sasa hivi na si wakati ule ambao zilikuwa effected?..............je hii ina namna fulani ya kum-discredit mtu au?

naomba niamini kuwa wanaoziibua (ni very intelligent guys) hizo siri wanajua kuwa hazifai kuwa siri (kwa ajilia ya usalama kama inavyodaiwa) ndio maana wanaziibua na kuwapa watu kama akina Dr Slaa.

.......i mean something ain't right here.......
 
Kwa maneno mengine Waziri Marmo kawadhibitishia wananchi kuwa asemayo Dr.Slaa yote ni hakika na kweli ila tu inatakiwa kuwa siri duh mambo mengine mtu mzima bora kupiga kimya.

Sasa na hili matumizi mabaya ya fedha kuishia kuwa siri kwa faida ya nani waliotumbua pesa au taifa.
 
Wananchi hawana imani na serikali ndiyo maana wanatoa nyeti ili labda wasaidie kuleta mabadiliko kwa manufaa ya Watanzania wote. Nyeti za serikali zitaendelea kutoka tu mpaka pale Watanzania wawe na imani na serikali iliyipo madarakani ipo pale kwa manufaa ya Watanzania wote na siyo kundi la mafisadi wachache

Date::6/29/2008
Serikali yaingiwa na hofu jinsi mbunge anavyopata taarifa nyeti
Na Kizitto Noya, Dodoma
Mwananchi

SERIKALI inaumiza kichwa kujua mtandao unaotumiwa na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk Willibrod Slaa, kupata taarifa zake za siri na kuzianika hadharani.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera), Philip Marmo amekiri bungeni juzi jioni kuwa, Dk Slaa ana mtandao mkubwa usiofahamika anaoutumia kupata nyaraka za siri za serikali kinyume na taratibu.

Kauli ya Marmo ilifuatia swali la Dk Slaa kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda wakati Kamati ya Bunge ilipokuwa inapitia vifungu kwa ajili ya kupitisha Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, kuwa ni aina gani ya nyaraka za serikali zinapaswa kuwa siri.

Dk Slaa alitaka kujua endapo nyaraka za serikali ambazo zimejaa kumbukumbu za kifisadi na ambazo wabunge wakiziomba kwa utaratibu wa kawaida wananyimwa, zinapaswa kuwa siri.

Akiwa na nyaraka kadhaa mkononi alizosema kuwa ni sehemu ya zile za serikali zinazopaswa kuwa siri, lakini watu aliowaita wasamaria wema wamempa, Dk Slaa alisema haelewi mantiki ya nyaraka hizo kuwa siri wakati hazina faida kwa taifa.

Mheshimiwa Waziri Mkuu, mimi naomba kuuliza ni nyaraka gani hasa za serikali zinapaswa kuwa siri. Hata zile ambazo zimejaa uongo? Mimi ninazo hapa na kama

Mheshimiwa Marmo anataka kuwatuma polisi waje wanikamate niko tayari, lakini nyaraka hizi zina maana gani kwa taifa? alihoji Dk Slaa akionyesha nyaraka hizo.

Kwa mujibu wa Dk Slaa wapinzani wanajua umuhimu wa usiri wa nyaraka za serikali, lakini inapofikia mahala mfumo wa serikali unaanza kuporomoka, hawana sababu ya kuogopa kutafuta nyaraka hizo kwa njia ya mkato na kuzitumia kuweka mambo hadharani.

Lakini kama mfumo wa serikali unaanza kuanguka na serikali ikaonyesha nia ya dhati kudhibiti tatizo hilo, sisi ni wazalendo pia hatutazitafuta wala kutoa tena siri za serikali hadharani, alisisitiza.

Akijibu suali hilo kwa upole, Marmo alisema, inaonekana Dk Slaa ana mtandao mkubwa katika kupata taarifa hizo za siri na amekuwa mjanja katika kuzizungumzia kuwa anafahamu kuwa kufanya hivyo ni kosa la jinai.

Dk Slaa ni mjanja sana anajua anachofanya kuwa ni kosa la jinai. Pana jinai hapa na ndio maana hata katika hii nyaraka ya EPA amesema, nimeondoa jina la source (chanzo cha Habari) kwa usalama wake, alisema Marmo akinukuu nyaraka ya siri ya serikali aliyodai kuwa imepatikana kutoka kwa Dk Slaa.

Marmo alisema nyaraka za serikali lazima ziwe za siri na kuwa nazo mtu asiyehusika ni kosa la jinai ingawa kama kuna umuhimu wa mtu kuzipata anaweza kufanya hivyo katika utaratibu unaokubalika.

Aliwataka wabunge wanaotaka kujua mambo ya serikali kupitia nyaraka zake za siri kufuata utaratibu badala ya kutumia njia ya mkato kisha kuanika siri za serikali

hadharani. Mimi naomba tufuate utaratibu, kinyume chake huko ni kuidhalilisha serikali, alisema Marmo.

Kwa muda mrefu sasa Dk Willibrod Slaa na chama chake cha CHADEMA amekuwa akiibua tuhuma mbalimbali za ufisadi ndani ya serikali kwa kutumia nyaraka za siri za serikali.

Baadhi ya tuhuma hizo ni upotevu wa mabilioni ya shilingi katika Akaunti ya Madeni ya Nje ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (EPA), rushwa katika upatikanaji wa zabuni ya

kuzalisha umeme wa dharura na Kampuni ya Richmond na mikataba mibovu katika migodi ya madini.

Juzi, Dk Slaa alipingana na Waziri Mkuu Mizengo Pinda katika majibu yake kwamba hawezi kuzungumzia suala la Meremeta kwa sababu za ulinzi na usalama.

Dk Slaa na Mwenyekiti wa Chama cha UDP, John Cheyo walimweleza Pinda kuwa Meremeta wanayomtaka azungumzie ni ile ya pili baada ya jeshi kumaliza kazi na kampuni waliyodai kuwa ni 'Meremeta ya kwanza'.

Cheyo alisema alitaka suala la Meremeta kufanyiwa uchunguzi wa kina na kwamba kulihusisha na suala hilo na jeshi sio sawa na kwamba Waziri Mkuu anapaswa kuwatendea haki Watanzania kwa kuzungumzia suala hilo.

Kama kweli kuna Sh12 bilioni Tangold, tunazihitaji kwa ajili ya miradi ya maji, alisema Cheyo.

Hata hivyo, Pinda alishikilia msimamo wake na kugoma kuzungumzia kampuni hiyo yenye makampuni tanzu ya Tangold, Deep Green na Green Finance kwa maelezo kuwa yanahusiana na Jeshi na kwamba yuko tayari kusulubiwa kwa hilo.

Meremeta ama kweli sasa ina WAMEREMETEA WABONGO NA KUWAUMIZA MAFISADI.

OR...At least tunaweza ku assume kuwa...Kama wabunge hao wakiamua kupambana...Then ni wazi MEREMETE INA UWEZEKANO WA KULIMEREMETESHA TAIFA LETU NA SI WATU FLAN FLAN.

Nimeshangazwa kidogo na hayo majina...Lakini nikatafakari kwani ndugu zangu tumepigana vita na sasa HATA HABARI ZA VITA VYA ZIMBABWE NA MUGABE INAZUNGUMZIWA BILA PROPAGANDA ZA KIFISADI!

NA YES I SAY!

MUGABE AKIGOMBEA TANZANIA NITAMPA KURA YANGU KABLA YA TSIVANGIRAI,KIKWETE,KICHAKA,BLAIR,GORDON BROWN ETC ETC!

NA OBAMA MWENYEWE AWEZA KUWA RAIS WA DUNIA!

MARK MA WORDS!

KIKWETE HAJUI HISTORY!

UTASAPOTI VIPI KICHAKA?

So..Na hayo majina Deep GREEN,GREEN THIS...TANI ZA GOLD(TAN GOLD)

Ama kweli zilipewa majina hayo kwa mpango wa MUNGU.

Ni wazi sasa kumbe...Licha ya maisha ya tabu kwa AFRIKA...WENGINE NI TANI ZA GOLDI NA KILA KITU GREEN!

Huku wengine...PANGU PAKAVU TUUU!

WE WANT THE WHOLE COUTRY AND AFRIKA "GREEN"

BECAUSE OFCOURSE WE HAVE TONS OF GOLD AND DIAMONDS TO BE ABLE TO DO SO.

KAMPENI YA OBAMA WAMEKUBALI USHAURI WANGU NA SASA BUSH ANALIMWA HAPA KWA KUMANIPULATE NEWS ZA IRAQI,ZIMBABWE NK!

WAINGEREZA WAMECHOSHWA NA BLAIR NA GORDON.

WAMAREKANI WAMECHOSHWA NA KICHAKA NA HATA MAC BUSH!

Tanzania je?

TUMECHOSHWA NA HAO WOTE EXCEPT FOR OBAMA,THABO MBEKI,MANDELA NA WENGINEO!

LAKINI KAMWE SI MWALIMU WALA MKAPA NA KIKWETE!

DK SLAA PAMBANA! WANANCHI TUKO NYUMA YAKO!

Kwani tumeshajua ukweli kuwa SI KWELI kuwa MEREMETA ILIKUWA IKILIMEREREMTEA JESHI!

AT LEAST SI HIYO WANAYOIITA YA PILI VS YA KWANZA!

VILE VILE MEREMETA YENYEWE HAIJAWAFANYIA WANANCHI LOLOTE.

ZAIDI ZAIDI INAMILIKIWA NA MAFISADI!
 
Na hilo jina la eti DEEP GREEN!

WATANZANIA...HILO JINA LENYEWE LIMEKAA KIMAREKANI MAREKANI...
GREEN NI PESA!

SASA NI DEEP PESA DEEP!

At the same time...GREEN Ni NEEMA!

TUNATAKA NEEMA KWA WOTE!

HAYA MAMBO YA MUNGU MAFISADI HAMUWEZI ZUIA TENA!

KULE KWENYE THREAD YA OBAMA NILIONYA HATA KABLA HAJATEULIWA KUWA MGOMBEA WA DEMOCRACTS!

KUWA...ccm WAKAE MKAO WA KIUHURU UHURU!

Tena Nikawaambia kuwa nitawaonyesha kuwa ni kwanini maneno ya OBAMA si ya kupuuziwa!

Sasa wanayaona!

Tena hata Kikwete mwenyewe nilimpa hint!

Yeye ni BUSH,YOUNG,CLINTON NA MAUPUUZI YAO YA KULIRUDISHA BARA LETU UTUMWANI KWA KUWATUMIA WEUSI HAO MAMLUKI WACHAFU HUKU WAKITUMIA MAJINA KAMA SULLIVAN!

ANDREW YOUNG NI PANDIKIZI LA KIFISADI AMBALO LISHATEGWA NALO!
HUYU JAMAA ALIKUWA KARIBU SANA MARTIN LUTHER KING NA HATA ALIPOUWAWA!
LAKINI KAULI YAKE HIVI MAJUZI KUWA CLINTON NI MWEUSI KULIKO OBAMA ILINISHTUA SANA MTU KAMA MIMI AMBAYE NAIFAHAMU VYEMA WORLD HISTORY!
INATOFAUTIANA SANA NA VITENDO VYA MLK!
NA HUU ULINZI WA OBAMA SI BURE!
KWANI HATA MLK MWENYEWE NANI ANAJUWA KAMA ANDREW YOUNG NA YEYE KAMA SAFI?
ATAMPINGA VIPI OBAMA KAMA KWELI ANA AKILI HUYU?
ETI ALISEMA CLINTON KATEMBEA NA WANANWAKE WENGI WEUSI ZAIDI YA OBAMA NA HIVYO WEUSI WAMSIKILIZE!
HIYO NDIYO SABABU KIKWETE AKAMWALIKA KWENYE MBINU ZAO ZA KUUZA AFRIKA HUKU WAKICHEKA CHEKA!
WATANZANIA AMKENI!
SERIKALI...MNAJUA LA KUFANYA....HAKI HAKI AND MORE HAKIZ!

KIKWET SOMA HISTORIA NA UCHAGUWE MOJA!
 
WanaJF, hamuoni kama hawa watu baada ya kumfuata Dr.Slaa wataanza kuwafatilia watu wanaoendesha huu mtandao kwasababu nyaraka zingine zinapatikana hapa ambayo "ni siri za serikali"?
 
Wait a minute,

hizi siri kwa nini zinaibuka sasa hivi na si wakati ule ambao zilikuwa effected?..............je hii ina namna fulani ya kum-discredit mtu au?

naomba niamini kuwa wanaoziibua (ni very intelligent guys) hizo siri wanajua kuwa hazifai kuwa siri (kwa ajilia ya usalama kama inavyodaiwa) ndio maana wanaziibua na kuwapa watu kama akina Dr Slaa.

.......i mean something ain't right here.......

Nakubaliana na wewe kwenye hili.....just a minute ago nilikuwa nasoma classified documents za CIA kuhusu Iran(watu wanapika vita)...I hope uvujaji wa hizi siri ni kwa ajili ya manufaa ya Taifa and not otherwise.
 
Back
Top Bottom