JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,458
Siku chache baada ya kusambaa kwa taarifa juu ya uwepo wa unyanyasaji wa wafanyakazi katika Kampuni ya SBC Tanzania (Kiwanda cha Pepsi), hatimaye Serikali imetoa tamko juu ya kinachoendelea kiwandani hapo.
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira & Wenye Ulemavu) ametoa tamkoa hilo leo Machi 27, 2022 na kuelezea kuwa ana ripoti ya kinachoendelea na kuongeza kuwa atafika kiwandani hapo yeye mwenyewe katika kiwanda hicho Tawi la Dar es Salaam, kesho Jumatatu Machi 28, 2022.
HILI HAPA TAMKO RASMI LA NAIBU WAZIRI…
Nimeona jambo katika Mitandao yetu, naomba kwa ufupi kuweka kumbukumbu sahihi ili kuepusha Upotoshaji wa makusudi kuwa Serikali haijalitilia nguvu.
Suala la SBC LTD nalitambua na hatua za kisheria zinaendelea, awali nilishamuagiza Kamishina Brigedia General Francis Mbindi (Kipindi kilichopita) alienda na kulishughulikia vizuri mara ya kwanza alichukua hatua na kutoa Maagizo na Maelekezo ya Utekelezaji Sheria za Kazi pamoja na hayo alifuta Vibali vya Wafanyakazi wa kigeni waliokiuka Sheria.
Yapo yaliyotekelezwa na tulipobaini ambayo hayakutekelezwa alirudi mara ya pili na kuchukua hatua kwa mujibu wa Sheria za Kazi na kwakuwa maswala ya kazi sio jinai sio sahihi kwa waliotaka kuona watu wakiburuzwa bali kuna taratibu za kufuata kwa mujibu wa Sheria tofauti na Jinai.
Juzi nikiwa katika Kikao cha High Level Policy Conference Youth as Researchers on Covid -19 kwa niaba ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Nililazimika kukutana na Kamishina wa Kazi Bi.Suzan na timu ya Wataalamu ambao wameendelea kulifanyia Kazi vizuri na nikaagiza yafuatayo.
Mosi: nimewaagiza kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa Sheria za Kazi. Ikiwa ni Kufanya uchunguzi wa kina juu ya yanayolalamikiwa na pili kufanya ukaguzi tena kwa mapya yatakayojitokeza na kuchukua hatua.
Naomba kutoa Rai pia kwa Wafanyakazi wasisubiri shida zikithiri kwenye maeneo yao ya Kazi, watupe taarifa mapema pamoja na kwamba pia tuna taarifa ya madai mengine siyo ya kweli wapo Wafanyakazi waliofanya makosa ya kinidhamu na kuvunja Sheria za Kazi ambao wanataka kujificha katika haya na kuzusha yasiyo kweli kutafta huruma kwa jamii.
Serikali ya Mhe. Rais Mama yetu Samia Suluhu Hassani haitapendelea Mtu wala kumuonea Mtu wala kampuni, HAKI itachakatwa kwa mujibu wa Sheria na ataipata anaestahili.
Jumatatu nitapokea taarifa, hatua na Mapendekezo ya Uchunguzi na nitafika hapo mwenyewe kwa niaba ya Mhe. Waziri na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa UAMUZI, MAELEKEZO kisheria kulingana na taarifa tafiti zitakazopatikana na tutaujulisha Umma.
Nawasihi Sana Ndugu zangu tuwe na Utulivu pande zote, tutalimaza salama na kwa mujibu wa Sheria HAKI ITATENDEKA.
Patrobas Katambi,
NW OWM Kazi, Vijana na Ajira,
27.03.2022.
=====================
Pia soma...
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira & Wenye Ulemavu) ametoa tamkoa hilo leo Machi 27, 2022 na kuelezea kuwa ana ripoti ya kinachoendelea na kuongeza kuwa atafika kiwandani hapo yeye mwenyewe katika kiwanda hicho Tawi la Dar es Salaam, kesho Jumatatu Machi 28, 2022.
HILI HAPA TAMKO RASMI LA NAIBU WAZIRI…
Nimeona jambo katika Mitandao yetu, naomba kwa ufupi kuweka kumbukumbu sahihi ili kuepusha Upotoshaji wa makusudi kuwa Serikali haijalitilia nguvu.
Suala la SBC LTD nalitambua na hatua za kisheria zinaendelea, awali nilishamuagiza Kamishina Brigedia General Francis Mbindi (Kipindi kilichopita) alienda na kulishughulikia vizuri mara ya kwanza alichukua hatua na kutoa Maagizo na Maelekezo ya Utekelezaji Sheria za Kazi pamoja na hayo alifuta Vibali vya Wafanyakazi wa kigeni waliokiuka Sheria.
Yapo yaliyotekelezwa na tulipobaini ambayo hayakutekelezwa alirudi mara ya pili na kuchukua hatua kwa mujibu wa Sheria za Kazi na kwakuwa maswala ya kazi sio jinai sio sahihi kwa waliotaka kuona watu wakiburuzwa bali kuna taratibu za kufuata kwa mujibu wa Sheria tofauti na Jinai.
Juzi nikiwa katika Kikao cha High Level Policy Conference Youth as Researchers on Covid -19 kwa niaba ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Nililazimika kukutana na Kamishina wa Kazi Bi.Suzan na timu ya Wataalamu ambao wameendelea kulifanyia Kazi vizuri na nikaagiza yafuatayo.
Mosi: nimewaagiza kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa Sheria za Kazi. Ikiwa ni Kufanya uchunguzi wa kina juu ya yanayolalamikiwa na pili kufanya ukaguzi tena kwa mapya yatakayojitokeza na kuchukua hatua.
Naomba kutoa Rai pia kwa Wafanyakazi wasisubiri shida zikithiri kwenye maeneo yao ya Kazi, watupe taarifa mapema pamoja na kwamba pia tuna taarifa ya madai mengine siyo ya kweli wapo Wafanyakazi waliofanya makosa ya kinidhamu na kuvunja Sheria za Kazi ambao wanataka kujificha katika haya na kuzusha yasiyo kweli kutafta huruma kwa jamii.
Serikali ya Mhe. Rais Mama yetu Samia Suluhu Hassani haitapendelea Mtu wala kumuonea Mtu wala kampuni, HAKI itachakatwa kwa mujibu wa Sheria na ataipata anaestahili.
Jumatatu nitapokea taarifa, hatua na Mapendekezo ya Uchunguzi na nitafika hapo mwenyewe kwa niaba ya Mhe. Waziri na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa UAMUZI, MAELEKEZO kisheria kulingana na taarifa tafiti zitakazopatikana na tutaujulisha Umma.
Nawasihi Sana Ndugu zangu tuwe na Utulivu pande zote, tutalimaza salama na kwa mujibu wa Sheria HAKI ITATENDEKA.
Patrobas Katambi,
NW OWM Kazi, Vijana na Ajira,
27.03.2022.
=====================
Pia soma...