Serikali yaendelea kuwasomesha namba wanafunzi wa vyuo vikuu.

Molembe

JF-Expert Member
Dec 25, 2012
9,817
11,485
Hali ya sintofahamu imeendelea kuwakumba vijana wa vyuo vikuu ambao bado hawajapata pesa zao ambazo walitegemea kupata katikati ya mwezi wa 5, ikumbukwe kwamba wiki iliyopita bodi ya mikopo vyuo vikuu (Heslb) ilitoa tamko kwamba wiki hii vijana hao wangepata pesa yao lakini mpaka sasa hawajapata pesa hizo na kila wakifuatilia wanaambiwa bodi hawajatuma pesa.

Hali hii imesababisha wanafunzi wengi kuishi kwa hofu kutokana na madeni huku wengine wakifukuzwa kwenye vyumba walivyokuwa wamepanga, vilevile kuna baadhi ya vyuo vimewazuia wanafunzi wake kufanya mitihani inayoanza wiki ijayo kwa kigezo cha kushindwa kulipa ada, ieleweke kwamba wanafunzi hao walikuwa wanajilipia ada kutokana na pesa wanazopata toka bodi ya mikopo.
 
Sasa hao mafinalists wanaoondoka si wanaacha madeni kwa mama ntilie.....
 
Hali ni mbaya kuna chuo kimoja wanafunzi wamefukuzwa kwenye vyumba walivyopanga
Pesq za kukopeshwa kama unapewa bure bwana.....udsm walianzishaanzisha kamgomo na raisi alikua abakuja wikii hiyo ndio wakazitoa....wanawanyanyasa sana!
 
Acha waisome namba, si hao ndio walikuwa wanamshabikia huyu anayependa sifa?
Halafu huu mtindo wa kutupiana lawama kwa kila anayeguswa na matatizo yanawasababishwa na serikali kwamba waendelee kuteseka kwa sababu walishabikia chama tawala wala hauwezi ufikisha upinzani popote pale. Maana kila anayekumbwa na tatizo awamu hii mnasema "wacha waisome namba" ina maana upinzani hakuna aliyeshabikia ambaye matatizo hayamkumbi. Acheni hizo bhana.
 
Zile ni ngonjera mkuu.

Yaani, mkuu. Ipo siku mistari ya ngojera itakwisha. Watashindwa kughani mistari...

Wafanyabiashara wananyimwa fursa za kufanya biashara kwa uhuru, kupitia kodi rafiki. Unategemeaje makusanyo

yaongezeke? Ndoto.
 
Hakika wanatusomesha namba. Yaani sasa wanatutesa kupita kiasi. Ukiwauliza wanasema hela hawana kwamba hawajapewa na hazina lakini wakiulizwa wanakana kwamba taarifa za kwamba bodi haina fedha ni za Uongo. Sasa tunashindwa kuelewa jibu moja ni lipi!

Enyi vibaraka wa Mkuu wa Kaya mfikishieni taarifa Mkuu muambueni wanafunzi tunateseka na hakika kilio chetu hakitamuacha hivihivi.
 
Hakika wanatusomesha namba. Yaani sasa wanatutesa kupita kiasi. Ukiwauliza wanasema hela hawana kwamba hawajapewa na hazina lakini wakiulizwa wanakana kwamba taarifa za kwamba bodi haina fedha ni za Uongo. Sasa tunashindwa kuelewa jibu moja ni lipi!

Enyi vibaraka wa Mkuu wa Kaya mfikishieni taarifa Mkuu muambueni wanafunzi tunateseka na hakika kilio chetu hakitamuacha hivihivi.
wamfikishie taarifa watumbuliwe hadharani? mwe!
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom