Aidha kwa bahati mbaya au kwa makusudi, Waziri wa Tamisemi ndugu Aggrey Mwanri aliliambia bunge kuhusu mradi wa maji wa Sakare- Bungu umeendelea kutengewa hela na serikali (Gazeti la Mwananchi tarehe 21/6/2012).
Hizi habari sio za kweli. Toka ulipoanza mpaka sasa mradi huu umekuwa ukifadhiliwa na Shirika la World Vision kwa fedha kutoka kwa wafadhili wa Hong Kong. Hata wahandisi wa serikali wanapofanya kazi za ufuatiliaji na usimamizi wa huu mradi wamekuwa wakilipwa posho na shirika la World Vision. Hizi habari za serikali kutenga shilingi milioni 229 ni za uongo kabisa. Serikali haijawahi kutoa senti tano kwa ajili ya utekelezaji wa huu mradi. Kama hizi pesa ziliwahi kutolewa na serikali kuu ufuatiliaji ufanyike.
Ninadhani ni vizuri kujenga tabia ya kufanya kazi na kusema ukweli. Tunazidi kurudi nyuma kimaendeleo kwa ajili ya uongo. INAKERA KWA KWELI!!!
Hizi habari sio za kweli. Toka ulipoanza mpaka sasa mradi huu umekuwa ukifadhiliwa na Shirika la World Vision kwa fedha kutoka kwa wafadhili wa Hong Kong. Hata wahandisi wa serikali wanapofanya kazi za ufuatiliaji na usimamizi wa huu mradi wamekuwa wakilipwa posho na shirika la World Vision. Hizi habari za serikali kutenga shilingi milioni 229 ni za uongo kabisa. Serikali haijawahi kutoa senti tano kwa ajili ya utekelezaji wa huu mradi. Kama hizi pesa ziliwahi kutolewa na serikali kuu ufuatiliaji ufanyike.
Ninadhani ni vizuri kujenga tabia ya kufanya kazi na kusema ukweli. Tunazidi kurudi nyuma kimaendeleo kwa ajili ya uongo. INAKERA KWA KWELI!!!