Serikali yabainisha walimu 58 wenye PhD shule za msingi!

Ustaadh

JF-Expert Member
Oct 25, 2009
413
19
WIZARA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imebainisha kuwa hadi kufikia Juni mwaka huu, shule za msingi zilikuwa na walimu wapatao 58 wenye Shahada ya Udakatari wa Falsafa (PhD) wakati walio na Shahada ya Uzamili ni 75, Shahada ya Kwanza 1,099 na Stashahada ya Ualimu ni walimu 6,512.

Hata hivyo, pamoja na makundi hayo matatu, pia imeonesha kuwa idadi ya walimu wa Daraja la Tatu A ni 148,986 na wa Daraja B na C idadi yao ni 9, 123 sawa na asilimia 5.8 kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na Taasisi ya BEST 2006-2010.

Mkurugenzi wa Mafunzo ya Ualimu katika Wizara hiyo, Rose Massenga, alibainisha hayo Novemba 8 wakati akimkaribisha mgeni rasmi, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia Elimu, Jumanne Sagini, kufungua mkutano wa wakuu wa vyuo vya ualimu vya Serikali na visivyo vya Serikali mjini hapa.

Kwa mujibu wa Masenga, upande wa walimu wa shule za sekondari wanaofundisha kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita, wenye Shahada ni 9,910, Stashahada 22,171, wenye leseni ni 3,997 sawa na asilimia 12.46 na wengine 4, 439 sawa na asilimia 13.84.

Hata hivyo, alisema mahitaji ya walimu wa elimu ya awali na msingi kwa mujibu wa PEDP katika mwaka 2010 hadi 2011, wanahitajika walimu 18, 783 kati ya hao 15, 783 ni wa msingi na 3,000 wa elimu ya awali, ambapo elimu ya sekondari kwa kipindi hicho wanahitajika walimu 30,075.

Alisema mafanikio ya utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya elimu ya msingi na ule wa elimu ya sekondari, imesababisha ujenzi wa shule nyingi za msingi na sekondari uliambatana na uandikishaji wa wanafunzi wengi kwenye ngazi hizo na matokeo yake kusababisha mahitaji makubwa ya walimu.

Hivyo alisema ni vyema ieleweka kuwa msimamizi wa utoaji wa mafunzo ya ualimu unazingatia mambo mengi vikiwemo sheria, kanuni na miongozo mbalimbali inayoelezeka katika viwango vya kitaifa na kimataifa.

Naye mgeni rasmi, Sagini alisema shule za msingi zina uhaba wa walimu wasiopungua 45,000, wakati upungufu ni mkubwa zaidi kwa sekondari katika masomo ya sayansi.

Hata hivyo, alisema ngazi ya elimu ya msingi idadi ya wanafunzi imeongezeka maradufu kutoka milioni nne mwaka 2001 hadi milioni 8.4 mwaka 2010, ambapo shule za sekondari idadi ya wanafunzi imeongezeka kutoka chini ya 300,000 mwaka 2001 hadi milioni 1.6 mwaka 2010.

Sagini alisema wakati idadi ya wanafunzi ikiongezeka kwa kiwango hicho kikubwa, idadi ya walimu imekuwa ikiongezeka kwa kiasi kidogo ambacho hakitoshelezi mahitaji ya ngazi ya msingi na sekondari.

Pamoja na hayo, amekipongeza Chama cha Walimu Tanzania (CWT) kwa kupendekeza na kukubaliana kutafakari hoja ya kuimarisha mafunzo ya ualimu na kupata utaratibu wa mafunzo ya ualimu ulio bora zaidi utakaowezesha kufanikisha malengo ya elimu kuanzia elimu ya awali hadi vyuo vya ualimu na vyuo vikuu.
 
PhD..............!!!!!!!!!!! .............Primary................!!!!!!!!!!!!!! there must be a typing error somewhere............
 
USTAADH hebu tufafanulie hizo PhD zinazofundisha Shule za msingi wakati baadhi ya Universities wanatafuta
 
Give me a break!!!! PhD wanafundisha promary schools au sijakuelewa?

Wala usishangae, hawa ni watanzania wajariamali wenye PhD ambao wamewekeza katika sekta ya elimu na kufungua shule za msingi (English Medium, St Mama Mdogo etc) ambao katika kuwasilisha orodha za waalimu, wameweka na majina yao!! Unashangaa nini, mbona kuna Dispensary zina waganga ambao ni Professors? Yaani watanzania Professors wajariamali ambao wamewekeza katika sekta ya afya na kufungua dispensaries ambao katika kuwasilisha orodha za waganga wakaweka majina yao! Ukitaka kushangaa ya Musa nenda huko shuleni/dispensary kama utawakuta wakifanya kazi, wanaofundisha huko ni walimu wa kawaida (UPE with long experience, Grade A, Diploma etc) / wanaotibu huko ni waganga wa kawaida (Medical Assistants. Assitant Medical Officers etc) . Wao ni owners, please, give me a break!
 
quote_icon.png
Originally Posted by StaffordKibona
USTAADH hebu tufafanulie hizo PhD zinazofundisha Shule za msingi wakati baadhi ya Universities wanatafuta



hapo napo



Bongo zipo hizi jamani, mnasahau Open university wanatoa PhD! Hizi ndo PhD za hawa walimu wa primary. I am sure if they are confident enough that they hold PhD, they would not continue to be where they are.
 
Wala usishangae, hawa ni watanzania wajariamali wenye PhD ambao wamewekeza katika sekta ya elimu na kufungua shule za msingi (English Medium, St Mama Mdogo etc) ambao katika kuwasilisha orodha za waalimu, wameweka na majina yao!! Unashangaa nini, mbona kuna Dispensary zina waganga ambao ni Professors? Yaani watanzania Professors wajariamali ambao wamewekeza katika sekta ya afya na kufungua dispensaries ambao katika kuwasilisha orodha za waganga wakaweka majina yao! Ukitaka kushangaa ya Musa nenda huko shuleni/dispensary kama utawakuta wakifanya kazi, wanaofundisha huko ni walimu wa kawaida (UPE with long experience, Grade A, Diploma etc) / wanaotibu huko ni waganga wa kawaida (Medical Assistants. Assitant Medical Officers etc) . Wao ni owners, please, give me a break!
Mama Mdogo,
Hao wajasiriamali wenye St. Mama wewe, hawafundishi wao, wao wanakusanya mafungu tu.Wenyewe wanashughuli zao zenye fungu nene, tena wengine ni waheshimiwa. Hata hizo dispensari waganga ni wale wale wa Mount Meru, muhimbili, Meta na rufaa, Morogoro,Dodoma na Mawenzi. asubuhi hospitali ya serikali jioni kwa wajasiriamali. So hakuna phd,masters,degree wala diploma huko shule za msingi hata za magumashi kama za watu fulani.
 
Wala usishangae, hawa ni watanzania wajariamali wenye PhD ambao wamewekeza katika sekta ya elimu na kufungua shule za msingi (English Medium, St Mama Mdogo etc) ambao katika kuwasilisha orodha za waalimu, wameweka na majina yao!! Unashangaa nini, mbona kuna Dispensary zina waganga ambao ni Professors? Yaani watanzania Professors wajariamali ambao wamewekeza katika sekta ya afya na kufungua dispensaries ambao katika kuwasilisha orodha za waganga wakaweka majina yao! Ukitaka kushangaa ya Musa nenda huko shuleni/dispensary kama utawakuta wakifanya kazi, wanaofundisha huko ni walimu wa kawaida (UPE with long experience, Grade A, Diploma etc) / wanaotibu huko ni waganga wa kawaida (Medical Assistants. Assitant Medical Officers etc) . Wao ni owners, please, give me a break!

Good explanation! unanikumbusha enzi hizo kampuni yetu ikiomba consultancy, kwenye CV za team members tunaazima mpaka majina ya PHD holders halafu mkienda field wanashangaa huyo DR. anakuja siku ya kwanza siku zinazofuata kazi inapigwa na nyoka (diploma/bachelor holders).....uchakachuaji uko kila kona, sijui kama tutaendelea siye wabongo!
 
Kuna mpaka mama wa nyumbani wenye Phds mbona. Wanawake na phds zao ambao wamefungua makampuni yao kwenye mikoba na muda mwingi wako kwenye mizunguko ya kazini, lakini kwa vile hawana address maalum, utasikia mama wa nyumbani.

takwimu zilizokuwa hazijafanyiwa analysis ya kutosha ndio kaa hizi.
 
wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi imebainisha kuwa hadi kufikia juni mwaka huu, shule za msingi zilikuwa na walimu wapatao 58 wenye shahada ya udakatari wa falsafa (phd) wakati walio na shahada ya uzamili ni 75, shahada ya kwanza 1,099 na stashahada ya ualimu ni walimu 6,512.

Hata hivyo, pamoja na makundi hayo matatu, pia imeonesha kuwa idadi ya walimu wa daraja la tatu a ni 148,986 na wa daraja b na c idadi yao ni 9, 123 sawa na asilimia 5.8 kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na taasisi ya best 2006-2010.

Mkurugenzi wa mafunzo ya ualimu katika wizara hiyo, rose massenga, alibainisha hayo novemba 8 wakati akimkaribisha mgeni rasmi, naibu katibu mkuu wa wizara ya tawala za mikoa na serikali za mitaa anayeshughulikia elimu, jumanne sagini, kufungua mkutano wa wakuu wa vyuo vya ualimu vya serikali na visivyo vya serikali mjini hapa.

Kwa mujibu wa masenga, upande wa walimu wa shule za sekondari wanaofundisha kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita, wenye shahada ni 9,910, stashahada 22,171, wenye leseni ni 3,997 sawa na asilimia 12.46 na wengine 4, 439 sawa na asilimia 13.84.

Hata hivyo, alisema mahitaji ya walimu wa elimu ya awali na msingi kwa mujibu wa pedp katika mwaka 2010 hadi 2011, wanahitajika walimu 18, 783 kati ya hao 15, 783 ni wa msingi na 3,000 wa elimu ya awali, ambapo elimu ya sekondari kwa kipindi hicho wanahitajika walimu 30,075.

Alisema mafanikio ya utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya elimu ya msingi na ule wa elimu ya sekondari, imesababisha ujenzi wa shule nyingi za msingi na sekondari uliambatana na uandikishaji wa wanafunzi wengi kwenye ngazi hizo na matokeo yake kusababisha mahitaji makubwa ya walimu.

Hivyo alisema ni vyema ieleweka kuwa msimamizi wa utoaji wa mafunzo ya ualimu unazingatia mambo mengi vikiwemo sheria, kanuni na miongozo mbalimbali inayoelezeka katika viwango vya kitaifa na kimataifa.

Naye mgeni rasmi, sagini alisema shule za msingi zina uhaba wa walimu wasiopungua 45,000, wakati upungufu ni mkubwa zaidi kwa sekondari katika masomo ya sayansi.

Hata hivyo, alisema ngazi ya elimu ya msingi idadi ya wanafunzi imeongezeka maradufu kutoka milioni nne mwaka 2001 hadi milioni 8.4 mwaka 2010, ambapo shule za sekondari idadi ya wanafunzi imeongezeka kutoka chini ya 300,000 mwaka 2001 hadi milioni 1.6 mwaka 2010.

Sagini alisema wakati idadi ya wanafunzi ikiongezeka kwa kiwango hicho kikubwa, idadi ya walimu imekuwa ikiongezeka kwa kiasi kidogo ambacho hakitoshelezi mahitaji ya ngazi ya msingi na sekondari.

Pamoja na hayo, amekipongeza chama cha walimu tanzania (cwt) kwa kupendekeza na kukubaliana kutafakari hoja ya kuimarisha mafunzo ya ualimu na kupata utaratibu wa mafunzo ya ualimu ulio bora zaidi utakaowezesha kufanikisha malengo ya elimu kuanzia elimu ya awali hadi vyuo vya ualimu na vyuo vikuu.




nafikiri ni kutokana na hivyo ndio maana examiner,s report inaonyesha darasa la saba wanamaliza wakiwa hawajui kusoma wala kuandika
 
Bongo zipo hizi jamani, mnasahau Open university wanatoa PhD! Hizi ndo PhD za hawa walimu wa primary. I am sure if they are confident enough that they hold PhD, they would not continue to be where they are. [/QUOTE]

Kwani PhD za Open University ni tofauti na zingine?
 
Hii kasumba ya ubwana mkubwa katika maisha ni mbaya kwelikweli.
sasa ni nini cha ajabu hapo mtu mwenye PHD kuwa mwalimu wa primary?. vipi kuhusu mapenzi ya mtu binafsi kufundisha?, vipi kuhusu ile hisia za kupenda kuwasaidia wengine, hususan watoto wadogo?.

Jamani elimu ni kwa ajili ya huduma, na pale mtu anapotoa huduma hivi kweli inafaa adharauliwe au apongezwe?.
kwa taarifa zenu siyo kila mwenye phd anaweza kufundisha vyuoni.
 
Wala usishangae, hawa ni watanzania wajariamali wenye PhD ambao wamewekeza katika sekta ya elimu na kufungua shule za msingi (English Medium, St Mama Mdogo etc) ambao katika kuwasilisha orodha za waalimu, wameweka na majina yao!! .. Wao ni owners, please, give me a break!

Mama Mdogo,

Hivi mmiliki wa Shule anaweza kuwa kwenye list ya waajiriwa wa shule "as a member of staff"?

Kwahiyo wakija wakaguzi naye anakaguliwa "Kitabu cha Maadalizi ya somo e.t.c"!

Kweli Tanzania hakuna lisilowezekana!
 
What is the difference between Harvard PhD and Open University PhD? especially when the OUT PhD is not honorary one like Boyz II Men ones :lalala::lalala:
 
Back
Top Bottom