tpaul
JF-Expert Member
- Feb 3, 2008
- 21,772
- 18,183
- Thread starter
- #61
Kwa sasa ninaishi kama sina ajira vile maana ni kama sina mshahara. Kodi na makato kwenye mshakara ni kubwa. Serikale inatufirikiraje sisi wafanyakazi lakini? Kila siku tunalalamika mishahara midogo badala ya kufikiria namana ya kutusaidia wao wanabuni njia za kuendelea kutunyonya na kutunyang'anya mishahara. Walilazimisha kutukata mishahara ili kulipia bima ya afya lakini huduma hakuna, tukiugua tunalazimika tena kutoa fedha zetu kujilipia ili tupate matibabu. Mimi mfanyakazi wa Tanzania nitaishije kama serikali itaishia kunipokonya tena hako kamshahara kote kiduchu kupitia kodi na makato? Jaribu kuangalia makato anayokatwa mfanyakazi wa kitanzania leo labda utanielewa vizuri zaidi;
KODI YA MAPATO (PAYE) = 14%
PENSHION = 5%
BIMA YA AFYA = 3%
VYAMA VYA WAFANYAKAZI (kama amejiunga) = 1%
HESLB (KAMA ALISOMA KWA MKOPO TOKA HESLB) = 8%
AKINUNUA BIDHAA YOYOTE ANALIPIA VAT = 18%
JUMLA YA KODI NA MAKATO KWA MFANYAKAZI WA TANZANIA = 49%
HII NI KUSEMA MFANYAKAZI ANAPATA TU NUSU YA MSHAHARA WAKE, NUSU NYINGINE INACHUKULIWA NA SERIKALI KAMA KODI NA MAKATO. SASA MFANYAKAZI HUYU ATAISHIJE KWA NUSU MSHAHARA?
Asante kwa uchambuzi makini, mkuu, Ni bahati mbaya kuna baadhi ya maCCM wanaoamua kujitoa akili na kutetea wizi huu wa mchana kweupe! Jamani tuweni na huruama kwa wafanyakazi. Hivi nyie CCM mnajisikiaje wafanyakazi wanavyonyonywa hivi?