bwashee2020
Member
- Dec 8, 2020
- 43
- 59
Tunarudi tena jukwaani wana JF kutoa shukrani za dhati kwa Mheshimiwa Rais Magufuli kwa kutupatia kiongozi bora wana Temeke; Ndg. Godwin Gondwe ambaye siku ya jana(tar 24/12/2020) alifanya ziara katika hospitali ya Dar Group akiambatana na mganga mkuu wa wilaya, DAS, OCD, mwenyekiti wa Serikali ya mtaa , afsa rasilimali watu na ma-afsa usalama, na kuwapa nafasi wafanyakazi kuelezea kero zao.
Baada ya kuwasikiliza wafanyakazi , muheshimiwa mkuu wa wilaya pia aliwapa management nafasi ya kuongea na kuleta usuluhishi kati ya wafanyakazi na management ya hospitali hiyo inayohudumia zaidi ya wateja 400 kwa siku na zaidi ya wateja 11,000 kwa mwezi.
Aidha muheshimiwa mkuu wa wilaya alitoa maagizo yafuatayo:
1. Kuheshimu taaluma za wafanya kazi na kuacha kunyanyasa wafanyakazi mara moja.
2. Wafanyakazi kutimiza wajibu wao wa kuhudumia wagonjwa na kufata taratibu za kazi.
3. Mikataba kupitiwa upya na kumpa mfanyakazi taarifa ya siku 28 kabla ya mkataba wake kuisha na unapoisha apewe stahiki zake.
4. Kuacha mara moja kutuma mtu kuchuguza vyumba vya madaktari na kuingia bila taarifa kwani tiba ni siri kati ya mgonjwa na tabibu.
5.Kuacha mara moja kuwashinikiza madaktari kuongeza vipimo visivyo na tija kwa wagonjwa ili kuongeza kipato kwani kufanya hivyo ni kuwaumiza wagonjwa na kuhujumu mifuko ya bima za afya na kuhujumu uchumi wa nchi.
6. Watumishi waende likizo kwa wakati na wapewe malipo yao ya likizo.
7. Kuacha mara moja tabia ya kuwasumbua wafanyakazi mara wapatapo ujauzito kazini, ikiwemo kuwafukuza kazi sababu ya ujauzito, kwani ujauzito ni zawadi kutoka kwa Mungu.
8. Kurudishwa mara moja kazini kwa daktari daraja la pili ambaye ilithibitika alisimamishwa kwa uoenevu.
9. Pia mkuu wa wilaya amesema ataunda tume maalumu itakayoichunguza kwa kina hospital ya Dar group, tume hiyo itaanza kazi tarehe 26 December na ameomba wafanya kazi waipe ushirikiano tume hiyo bila kuogopa vitisho.
SHUKRANI
Ahsante Mheshimiwa Rais kwa kutupatia Godwin Gondwe wana Temeke, viongozi wengine vijana wajifunze kwa mkuu huyu wa wilaya ya Temeke.
Tunaishukuru wizara ya Afya chini ya Dr Gwajima kwa kuendelea kuisimamia vyema sekta ya Afya.
Tunaushukuru uongozi mzima wa wilaya ya Temeke na DMO wa Temeke kwa kulipa jambo hili uzito unaostahili na kulishughulikia ipasavyo.
Tunashukuru bodi ya Wakurugenzi na Wafanyakazi wa JamiiForums kwa kutusaidia kupaza sauti zetu. Mungu aendekee kuwalinda na awabariki.
Shukrani ziende pia kwa wahudumu wote wa Afya nchini kwa kuendelea kufanya kazi zao kwa weledi licha ya changamoto wanazozipitia.
WITO
Viongozi wakumbuke vyeo ni dhamana wajitahidi kuongoza kwa kuzingatia haki na usawa bila kuweka makundi baina ya wanaowaongoza na wajitahidi kuwa VIONGOZI kuliko kuwa WATAWALA.
MUNGU IBARIKI AFRIKA, MUNGU IBARIKI TANZANIA.
Baada ya kuwasikiliza wafanyakazi , muheshimiwa mkuu wa wilaya pia aliwapa management nafasi ya kuongea na kuleta usuluhishi kati ya wafanyakazi na management ya hospitali hiyo inayohudumia zaidi ya wateja 400 kwa siku na zaidi ya wateja 11,000 kwa mwezi.
Aidha muheshimiwa mkuu wa wilaya alitoa maagizo yafuatayo:
1. Kuheshimu taaluma za wafanya kazi na kuacha kunyanyasa wafanyakazi mara moja.
2. Wafanyakazi kutimiza wajibu wao wa kuhudumia wagonjwa na kufata taratibu za kazi.
3. Mikataba kupitiwa upya na kumpa mfanyakazi taarifa ya siku 28 kabla ya mkataba wake kuisha na unapoisha apewe stahiki zake.
4. Kuacha mara moja kutuma mtu kuchuguza vyumba vya madaktari na kuingia bila taarifa kwani tiba ni siri kati ya mgonjwa na tabibu.
5.Kuacha mara moja kuwashinikiza madaktari kuongeza vipimo visivyo na tija kwa wagonjwa ili kuongeza kipato kwani kufanya hivyo ni kuwaumiza wagonjwa na kuhujumu mifuko ya bima za afya na kuhujumu uchumi wa nchi.
6. Watumishi waende likizo kwa wakati na wapewe malipo yao ya likizo.
7. Kuacha mara moja tabia ya kuwasumbua wafanyakazi mara wapatapo ujauzito kazini, ikiwemo kuwafukuza kazi sababu ya ujauzito, kwani ujauzito ni zawadi kutoka kwa Mungu.
8. Kurudishwa mara moja kazini kwa daktari daraja la pili ambaye ilithibitika alisimamishwa kwa uoenevu.
9. Pia mkuu wa wilaya amesema ataunda tume maalumu itakayoichunguza kwa kina hospital ya Dar group, tume hiyo itaanza kazi tarehe 26 December na ameomba wafanya kazi waipe ushirikiano tume hiyo bila kuogopa vitisho.
SHUKRANI
Ahsante Mheshimiwa Rais kwa kutupatia Godwin Gondwe wana Temeke, viongozi wengine vijana wajifunze kwa mkuu huyu wa wilaya ya Temeke.
Tunaishukuru wizara ya Afya chini ya Dr Gwajima kwa kuendelea kuisimamia vyema sekta ya Afya.
Tunaushukuru uongozi mzima wa wilaya ya Temeke na DMO wa Temeke kwa kulipa jambo hili uzito unaostahili na kulishughulikia ipasavyo.
Tunashukuru bodi ya Wakurugenzi na Wafanyakazi wa JamiiForums kwa kutusaidia kupaza sauti zetu. Mungu aendekee kuwalinda na awabariki.
Shukrani ziende pia kwa wahudumu wote wa Afya nchini kwa kuendelea kufanya kazi zao kwa weledi licha ya changamoto wanazozipitia.
WITO
Viongozi wakumbuke vyeo ni dhamana wajitahidi kuongoza kwa kuzingatia haki na usawa bila kuweka makundi baina ya wanaowaongoza na wajitahidi kuwa VIONGOZI kuliko kuwa WATAWALA.
MUNGU IBARIKI AFRIKA, MUNGU IBARIKI TANZANIA.
Tunaomba Serikali iingilie kati Hospitali ya Dar Group (T.O.H.S), Mmiliki hajulikani
Kwa siku za hivi karibuni, hospital ya Dar Group (T.O.H.S) imekuwa na mgogoro na wafanyakazi wake, hali inayopelekea mzoroto wa huduma za afya katika hospitali hiyo iliyopo eneo la Tazara ikiwa imetazamana na Azam TV, Mfugale flyover na kupakana na TBC. Chanzo cha mgogoro katika hospitali hiyo...
www.jamiiforums.com