Serikali yaajiri Madaktari wapya 610 ili kuongeza nguvu katika kuboresha huduma za afya

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,495
9,275
7d034f94945a3a79ee1bd68341f5bd96

Serikali kupitia Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), imetangaza kuajiri madaktari wapya 610, watakaokwenda kutoa huduma kwa wananchi katika maeneo mbalimbali nchini, pamoja na kusaidia kukabiliana na janga la Virusi vya Corona.

Akitoa taarifa mbele ya Waandishi wa habari jijini Dodoma, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI) Bw. Selemani Jaffo, amewataka wakurugenzi wa halmashauri kuhakikisha posho za kujikimu kwa madaktari hao wapya wanapewa kwa wakati, huku hakuna mabadiliko ya vituo vya kazi yatakayofanywa.

Aidha, Waziri Jaffo akawa na ujumbe mahususi kwa madaktari hao wapya wanaotakiwa kuripoti kati ya tarehe 11 hadi 25 ya mwezi huu, na kwenda kuhudumu katika Hospitali za wilaya 98, vituo vya afya 433 na zahanati 368.

Kuajiriwa kwa madaktari hao 610, kunafanya sasa toka serikali ya awamu ya tano iingie madarakani, madaktari 9,839 waweze kupata ajira serikalini.
 
Jambo moja linatudiwarudiwa mara dufu ilimradi tu Magufuli asifiwe.
Kikwete aliyekuwa akiajiri madaktari na walimu mpaka sekta binafsi zinakosa madaktari alikuwa hapigi mbiu hivi.
Sekta binafsi walimu na wataalamu wa afya walikuwa wakilipwa vizuri ili wabembelezwe wasikimbilie serikalini but now daktari akienda hospital ya binafsi anapangiwa mshahara na kuambiwa akitaka apige kazi akitaka aache
 
Jambo moja linatudiwarudiwa mara dufu ilimradi tu Magufuli asifiwe.
Kikwete aliyekuwa akiajiri madaktari na walimu mpaka sekta binafsi zinakosa madaktari alikuwa hapigi mbiu hivi.
Sekta binafsi walimu na wataalamu wa afya walikuwa wakilipwa vizuri ili wabembelezwe wasikimbilie serikalini but now daktari akienda hospital ya binafsi anapangiwa mshahara na kuambiwa akitaka apige kazi akitaka aache

Asee


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Jambo moja linatudiwarudiwa mara dufu ilimradi tu Magufuli asifiwe.
Kikwete aliyekuwa akiajiri madaktari na walimu mpaka sekta binafsi zinakosa madaktari alikuwa hapigi mbiu hivi.
Sekta binafsi walimu na wataalamu wa afya walikuwa wakilipwa vizuri ili wabembelezwe wasikimbilie serikalini but now daktari akienda hospital ya binafsi anapangiwa mshahara na kuambiwa akitaka apige kazi akitaka aache
True
 
Jambo moja linatudiwarudiwa mara dufu ilimradi tu Magufuli asifiwe.
Kikwete aliyekuwa akiajiri madaktari na walimu mpaka sekta binafsi zinakosa madaktari alikuwa hapigi mbiu hivi.
Sekta binafsi walimu na wataalamu wa afya walikuwa wakilipwa vizuri ili wabembelezwe wasikimbilie serikalini but now daktari akienda hospital ya binafsi anapangiwa mshahara na kuambiwa akitaka apige kazi akitaka aache
Kikwete anawachora tu huko alipo maana vitu kama hivi kwake haikuwa habari kabisa, ila saivi wakiajiri hata watu 10 tu utasikia kila mwanasiasa wa ccm anatangaza hayo magazeti yao ndio usiseme yaani.

Juzi bungeni wamepitisha bajeti ya ajira mpya hayo magazeti ya ccm yalivyo andika utazani hizo ajira tayari zimesha fanyiwa utekelezaji wakati ni yaleyale tu tangu enzi hizo za Angela akiwa Waziri wa hiyo wizara ya utumishi.
 
Kikwete anawachora tu huko alipo maana vitu kama hivi kwake haikuwa habari kabisa, ila saivi wakiajiri hata watu 10 tu utasikia kila mwanasiasa wa ccm anatangaza hayo magazeti yao ndio usiseme yaani.

Juzi bungeni wamepitisha bajeti ya ajira mpya hayo magazeti ya ccm yalivyo andika utazani hizo ajira tayari zimesha fanyiwa utekelezaji wakati ni yaleyale tu tangu enzi hizo za Angela akiwa Waziri wa hiyo wizara ya utumishi.
Kukosoa ni rahisi sana,
 
Kukosoa ni rahisi sana,
Hakuna mtu anae kosoa ila tunaongea ukweli ulivyo kwani ni mara ngapi bungeni bajeti za ajira mpya zimepitishwa kwa mbwembwe ila hakuna utekelezaji wowote? Hata hizo zilizo pitishwa juzi bungeni na Wizara ya mambo ya ndani ngoja uone utekelezaji wake hawaajiri hata mtu mmoja pale maana ni kawaida yao
 
hongera zao, wana wamekula msoto mtu wa 2016 anakuja kuajiliwa na wa 2018.
 
Kikwete anawachora tu huko alipo maana vitu kama hivi kwake haikuwa habari kabisa, ila saivi wakiajiri hata watu 10 tu utasikia kila mwanasiasa wa ccm anatangaza hayo magazeti yao ndio usiseme yaani.

Juzi bungeni wamepitisha bajeti ya ajira mpya hayo magazeti ya ccm yalivyo andika utazani hizo ajira tayari zimesha fanyiwa utekelezaji wakati ni yaleyale tu tangu enzi hizo za Angela akiwa Waziri wa hiyo wizara ya utumishi.
Vijana wanatusumbua huku mtaani wakiulizia hizo ajira. Zinavyonadiwa utadhani tayari zishamwagwa tayari.
Kuna mmoja hataki kuomba ajira za Mahakama anasubiri za uhamiaji zilizotangazwa magazetini.
Kweli watanzania hawataki kujifinza na hawana kumbukukumbu jinsi walivyofanyiwa miaka hii 5
 
Vijana wanatusumbua huku mtaani wakiulizia hizo ajira. Zinavyonadiwa utadhani tayari zishamwagwa tayari.
Kuna mmoja hataki kuomba ajira za Mahakama anasubiri za uhamiaji zilizotangazwa magazetini.
Kweli watanzania hawataki kujifinza na hawana kumbukukumbu jinsi walivyofanyiwa miaka hii 5
Huyo anae subiri ajira za uhamiaji nampa pole sana maana kati ya ajira ambazo hazita tekelezwa hata kwa asilimia moja ni hizo za wizara ya mambo ya ndani.
 
Back
Top Bottom