Idimi
JF-Expert Member
- Mar 18, 2007
- 14,604
- 9,789
Mishahara sekta binafsi mwakani
na Irene Mark, Dodoma
SERIKALI imeahirisha kuanza kutumika kwa viwango vipya vya mishahara katika sekta binafsi.
Tangazo la kuahirishwa kuanza kutolewa kwa mishahara hiyo mipya, lilitolewa mjini hapa jana na Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Kapteni John Chiligati, wakati akizungumza na waandishi wa habari.
Kapteni Chiligati alisema kuwa, imeamriwa sasa kuwa, viwango vipya vya mishahara ya watumishi wa sekta binafsi vitaanza kutumika rasmi Januari mwakani.
Mapema mwezi uliopita, serikali iliwataka waajiri wa sekta binafsi kuongeza viwango vya mishahara ya watumishi wao, kulingana na hali halisi ya maisha, nyongeza iliyotakiwa kuanza leo.
Kwa mujibu wa Chiligati, uamuzi huo wa serikali umekuja baada ya kupokea maombi kutoka kwa waajiri binafsi wa sekta mbalimbali, wakiomba muda zaidi ili kuweka sawa bajeti zao.
Alisema baada ya serikali kutamka viwango vipya vya mishahara ya watumishi binafsi, waajiri wao walipeleka malalamiko wizarani, wakiomba kuongezewa muda ili wapange upya bajeti zao.
"Serikali iliwataka waajiri wa sekta binafsi waongeze mishahara ya watumishi wao ili kwenda sambamba na hali ngumu ya maisha kwa watumishi wa sekta hiyo... kwa zaidi ya miaka minne watumishi wa sekta binafsi hawajawahi kuongezewa mishahara," alisema Chiligati.
Alitaja baadhi ya sababu zinazotajwa na waajiri ni fungu dogo la mishahara lililopo kwenye bajeti yao na kwamba taarifa ya serikali imekuja katika kipindi kifupi hali iliyowapa mshtuko, hasa walipotembelewa na Bodi ya Mishahara.
Kapteni Chiligati alitaja sababu nyingine kuwa ni wazalishaji wa bidhaa za nje watalazimika kuongeza bei ya bidhaa zao na kusababisha kupanda kwa gharama ya uuzaji hali itakayoporomosha soko la kazi zao nje ya nchi.
Aidha, Waziri Chiligati aliwaonya waajiri wanaowafukuza kazi watumishi wao kwa kisingizio cha kupanda kwa gharama za malipo, kuwa watapelekwa mahakamani.
Pamoja na hilo, waziri huyo aliwataka wote waliowafukuza kazi watumishi wao kuwarejesha kazini na kuendelea kuwalipa kwa viwango vya zamani hadi Januari watakapoanza kuwalipa mishahara ya nyongeza.
Chanzo: Tanzania Daima, 1/11/2007
Ina maana mpaka waziri na kamati yake waanapanga mikakati hii ya mishahara mipya walikuwa hawajajadiliana na waajiri binafsi?
Ona sasa wafanyakazi wengi wameachishwa kazi kutokana na kukurupuka huku!
Aibu!!
na Irene Mark, Dodoma
SERIKALI imeahirisha kuanza kutumika kwa viwango vipya vya mishahara katika sekta binafsi.
Tangazo la kuahirishwa kuanza kutolewa kwa mishahara hiyo mipya, lilitolewa mjini hapa jana na Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Kapteni John Chiligati, wakati akizungumza na waandishi wa habari.
Kapteni Chiligati alisema kuwa, imeamriwa sasa kuwa, viwango vipya vya mishahara ya watumishi wa sekta binafsi vitaanza kutumika rasmi Januari mwakani.
Mapema mwezi uliopita, serikali iliwataka waajiri wa sekta binafsi kuongeza viwango vya mishahara ya watumishi wao, kulingana na hali halisi ya maisha, nyongeza iliyotakiwa kuanza leo.
Kwa mujibu wa Chiligati, uamuzi huo wa serikali umekuja baada ya kupokea maombi kutoka kwa waajiri binafsi wa sekta mbalimbali, wakiomba muda zaidi ili kuweka sawa bajeti zao.
Alisema baada ya serikali kutamka viwango vipya vya mishahara ya watumishi binafsi, waajiri wao walipeleka malalamiko wizarani, wakiomba kuongezewa muda ili wapange upya bajeti zao.
"Serikali iliwataka waajiri wa sekta binafsi waongeze mishahara ya watumishi wao ili kwenda sambamba na hali ngumu ya maisha kwa watumishi wa sekta hiyo... kwa zaidi ya miaka minne watumishi wa sekta binafsi hawajawahi kuongezewa mishahara," alisema Chiligati.
Alitaja baadhi ya sababu zinazotajwa na waajiri ni fungu dogo la mishahara lililopo kwenye bajeti yao na kwamba taarifa ya serikali imekuja katika kipindi kifupi hali iliyowapa mshtuko, hasa walipotembelewa na Bodi ya Mishahara.
Kapteni Chiligati alitaja sababu nyingine kuwa ni wazalishaji wa bidhaa za nje watalazimika kuongeza bei ya bidhaa zao na kusababisha kupanda kwa gharama ya uuzaji hali itakayoporomosha soko la kazi zao nje ya nchi.
Aidha, Waziri Chiligati aliwaonya waajiri wanaowafukuza kazi watumishi wao kwa kisingizio cha kupanda kwa gharama za malipo, kuwa watapelekwa mahakamani.
Pamoja na hilo, waziri huyo aliwataka wote waliowafukuza kazi watumishi wao kuwarejesha kazini na kuendelea kuwalipa kwa viwango vya zamani hadi Januari watakapoanza kuwalipa mishahara ya nyongeza.
Chanzo: Tanzania Daima, 1/11/2007
Ina maana mpaka waziri na kamati yake waanapanga mikakati hii ya mishahara mipya walikuwa hawajajadiliana na waajiri binafsi?
Ona sasa wafanyakazi wengi wameachishwa kazi kutokana na kukurupuka huku!
Aibu!!