Serikali yaagiza Mtoto Charles Mathias arushwe Darasa kutoka Chekechea hadi Primary, Babu Tale aahidi kumlipia ada

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,915
141,869
Serikali mkoani Morogoro imeagiza mtoto Charles Mathias mwenye umri wa miaka 6 arushwe darasa kutoka Chekechea hadi darasa la kwanza baada ya kuonyesha kipaji kikubwa kwenye somo la Hisabati.

Afisa tawala wa mkoa bwana Kobehelo amesema agizo hilo lianze kutekelezwa mara moja.

Naye mbunge wa jimbo la Morogoro Kusini Mashariki, Hamis Taletale ameahidi kugharamia elimu ya mtoto huyo hapo kijijini.

Chanzo: ITV habari

Maendeleo hayana vyama!
 
Back
Top Bottom