sulphadoxine
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 2,257
- 645
Mwenyekiti wa chama cha NCCR Mageuzi,James Mbatia,amesema katiba iliyo andaliwa na serikali inayotarajiwa kufikishwa bungeni kwa ajili ya kujadiliwa imenakiliwa kutoka katiba ya kenya.Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es salaam,kwa niaba ya wanachama wake mwenyekiti wa chama hicho alisema muswada wa katiba unaotarajiwa kuletwa na serikali ni marejeo ya katiba namba tisa(9)ya mwaka 2008Alisema kilichofanyika katika katiba mpya iliyo andaliwa ni uigaji na hata kunakili moja kwa moja sheria ya nchi nyingine hali ambayo itasababisha hatari ya kuingiza sheria isiyoandamana na mila,desturi,siasa na hata utamaduni wa wananchi.