Serikali ya Tanzania na Siasa za Bakwata: Ushirikiano wa Dhulma

Status
Not open for further replies.
Binafsi naunga mkono tupeane mitihani ya kidini misikitini, kanisani,nk hii haitakuwa na kelele hata zikiwepo zitaishia huko huko misikitini na makanisani..maana lililopo sasa waislamu wakiangilia matokeo ya bible knowledge wakaona A,B za kumwaga wakaangalia islamic wakaona C,D,F au kinyume chake wakristo waone bible knowledge ni C,D,F wakati islamic A,B kuna anza kuwa na mawazo kwamba wenzetu wanabebwa,bila kujali kwamba waliosahihisha ni imani moja nao au la na bila kujali mtihani ulikuwaje..
Upo sahihi kwa kiwango kikubwa ila katika ufaulu wa haya masomo ya dini ikiwa wanafunzi wa dini ya walalamishi hata wote wapate A na B halafu wale wanafunzi wa dini ya wasio walalamishi wapate wote D na F sidhani kama kutakuwa na tatizo sana ukifananisha na ikitokea kinyume chake. Ufike wakati serikali ijitoe katika hizi lawama zisizo na ulazima na iache haya masomo ya dini yafundishwe huko huko kwenye nyumba za ibada za imani husika, kwa kufanya hivyo utegemezi na kulia lia serikalini kutapungua kwa kiasi kikubwa maana sasa hivi imefikia imani nyingine kila kitu wanataka serikali iwafanyie, watataka hata watoto wao nyumbani walelewe na serikali halafu wenyewe washinde kucheza bao na kunywa kahawa vijiweni. Kama kila kitu ni haki yao kudai serikali iwasaidie, wawapeleke na wake zao serikalini ili serikali iwasaidie yale mambo, tena akina Mwigulu na Malima watafurahi sana lol!!
 
Shehe Ponda leo baada ya swala ya Ijumaa alikuwa ameandaa maandamano ya kwenda NECTA kumng'oa Ndalichako! Maandamano haya yangefanyika kwa kila mmoja kwenda kivyake na hatimaye kukutana katika viwanja vya NECTA.

Hata hivyo mmoja wa viongozi wa taasisi zilizoandaa maandamano hayo Shehe Issa kupitia Radio Iman alionyesha kubadili mawazo baada ya tahadhari iliyotolewa na Kamanda Kova. Shehe Issa alitanabahisha kuwa hiyo isije ikatafsiriwa kuwa yeye ni mwoga!

Kwa mliyo karibu na viwanja vya NECTA mnaweza kutupa updates?

Hapakuwa evil intention iliyokuwepo katika kosa la kompyuta lililotokea. Sidhani kama kuandamana kutaondoa msingi wa shule za kiislamu kufeli mitihani kama hawataondoa mizizi ya tatizo. Hata wakamweka muislamu, hata amrisha waislamu wapewe marks za bure. tafakari kwa undani ndugu waislamu wapendwa.
 
Mtazamo wako kwangu mimi ni sahihi. Sie tuliosoma zamani, dini ilikuwepo lakini ilikuwa independent. Actuaaly ilikuwa Ijumaa wakati waislamu wanakwenda msikitini, wakristo walikuwa wnaingia kipindi cha dini. You might be right!

Hapo umenena mkuu,naona wahusika waichukue na kuifanyia kazi haraka sana,ikiwezeka kama inahitaji kupitishwa na Bunge basi Octaber nadhani kuna kikao waipeleke.Thankx
 
Mohamed Said. Thanks for the nice story you have posted. You are a good writer, a good storyteller.

Just out of curiousity, based on your understanding of islam, would you say it is ok to concoct and fabricate stories as long as the intention is to defend certain islamic agenda? Is it right to tell lies and hide some facts just to win sympathy of fellow muslims?

Please, give me an honest answer!
 
Sote tunajua kuwa kwa mujibu wa katiba ya nchi serikali haina dini. It is high time kwa serikali kutopoteza raslimali zake kwa kuhangaika na mitihani ya dini ambayo mwishowe inatuletea usumbufu. Pia haileti maana kwa mtz kusubiri kubebwa na mitihani ya dini kwenye matokeo ya mwisho. Vinginevyo wapagani pia watataka mitihani yao rahisi iwekwe ili iwabebe katika matokeo ya mitihani yao ya kitaifa. Nashauri kila dini iwapime waumini wake kwa kutunga na kusahisha mitihani yake na bila kuiweka kitaifa zaidi. Udini sasa umeshaanza kuingizwa kwenye kitu ambacho kina epukika kabisaaa. Ila hapa sasa zile dini za kulilia serikali iwasaidie hata katika mambo ya binafsi ya dini nitaona comments zao kali hapa. Kwani serikali kujua ufaulu wa watu ktk dini zao unaisaidia vipi katika kupanga mipango ya maendeleo?....na km kweli dini ni muhimu sana kuwepo kwenye mitihani ya taifa mbona vyuoni hakuna divinity? IT IS HIGH TIME KWA SERIKALI KUJIONDOA KABISA KTK MAMBO YA IMANI ZA WATU VINGINEVYO ITAENDELEA KUPATA LAWAMA ZISIZO NA MSINGI.
AM HERE TO BE CORRECT IF AM WRONG!
NAWASILISHA!

Nakuunga mkono !
ila kumbukumbu zangu zinatuonyesha vipindi vya dini mashuleni ni hiyari kuvihudhuria (optional) hiyo imepelekea wanafunzi wengi kutotilia mkazo na pia kutohudhuria vipindi vya dini mashuleni na kuwa busy na mambo yao binafsi.Ili kudhibiti mahudhurio na kuongeza umakini wake ikabidi mafunzo yake na mitihani yake ikaingizwa kuwa kama yalivyo masomo mengine ya kawaida.Lengo likiwa ni kuendelea kuwalea vijana katika misingi mema kutokana na dini zao.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom