YEHODAYA
JF-Expert Member
- Aug 9, 2015
- 36,911
- 51,889
Kupata Watanzania wengi matajiri sio rahisi tusiporuhusu watu kununua hisa na kuuza kwenye masoko makubwa ya hisa Duniani yaliyoko Ulaya, Marekani na Japan. Huko ndiko matajiri wa dunia huzalishwa kwenye hayo masoko
Pia Kuwezesha nchi kuwa na pesa nyingi za kigeni badala tu ya kutegemea mauzo ya mazao ya korosho sijui dengu na mazao mengine ya mashambani yanayotegemea Hali ya hewa
Kwenye hayo masoko ndiko kwenye mikampuni mikubwa Duniani inayoongoza kupata faida ambayo huuza hisa na kununua
Bila Tanzania kuwa active kwa Watanzania kushiriki biashara ya hisa ya kimataifa umaskini utaendelea
Soko la ndani la hisa Ni dogo na maskini ndio maana unakuta hata kampuni Kama Vodacom hisa zimedoda sokoni.
Soko maskini halizalishi matajiri.Ndio maana impact ya soko la hisa la Tanzania haionekani kwa Mwananchi wa kawaida kubadili maisha yake akinunua hisa!!!
Kuna masoko zamani madogo lofa yalikuwa yakiitwa soko mjinga.Ukipata meza Hapo ya kuuza ujue utaondoka kapa Kama Ni nyanya zitakuozea kwenye meza
Pia Kuwezesha nchi kuwa na pesa nyingi za kigeni badala tu ya kutegemea mauzo ya mazao ya korosho sijui dengu na mazao mengine ya mashambani yanayotegemea Hali ya hewa
Kwenye hayo masoko ndiko kwenye mikampuni mikubwa Duniani inayoongoza kupata faida ambayo huuza hisa na kununua
Bila Tanzania kuwa active kwa Watanzania kushiriki biashara ya hisa ya kimataifa umaskini utaendelea
Soko la ndani la hisa Ni dogo na maskini ndio maana unakuta hata kampuni Kama Vodacom hisa zimedoda sokoni.
Soko maskini halizalishi matajiri.Ndio maana impact ya soko la hisa la Tanzania haionekani kwa Mwananchi wa kawaida kubadili maisha yake akinunua hisa!!!
Kuna masoko zamani madogo lofa yalikuwa yakiitwa soko mjinga.Ukipata meza Hapo ya kuuza ujue utaondoka kapa Kama Ni nyanya zitakuozea kwenye meza