Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,216
- 113,519
Prof. Nicas Mahinda
Prof. Athumani Livigha
Prof. Jwani Mwaikusa
Dr. Sengondo Mvungi
Dr. Steven [Stephen?] Ulimboka
Tundu Lissu
Ben Saanane
Mohammed Dewji
Abdul Nondo
Roma Mkatoliki......
Kwa nini nimewaorodhesha hao watu?
Nimewaorodhesha kwa sababu, wote hao wana ‘common denominator’ katika yaliyowatokea, hususan baada ya [ma]tukio.
Mpaka leo bado hakuna taarifa za uhakika kwa nini Prof. Nicas Mahinda aliuwawa!
Dr. Ulimboka alitekwa na baadaye akaja kukutwa/ kuokotwa huko Mabwepande akiwa hajitambui.
Ben Saanane haijulikani alipo.
Mpaka sasa hatujui ni nani alitaka kumuua Tundu Lissu pale Dodoma.
Roma Mkatoliki naye alitekwa lakini akaja kuachiwa akiwa mzima.
Majuzi tu hapa bilionea Mo Dewji alitekwa halafu eti akaja kutupwa usiku wa manane kwenye viwanja vya Gymkhana.
Matukio yote hayo ya watu kutekwa, kujaribiwa kuuwawa, na kupotea kabisa, hayana maelezo yaliyokamilika wala kunyooka.
Watu hata hatujui kwa nini Mo alitekwa, achilia mbali alitekwa na nani!
Ni zaidi ya mwaka sasa baada ya Lissu kujaribiwa uhai wake na hakuna hata mshukiwa/ washukiwa.
Sasa mimi nauliza, hivi serikali ya Tanzania ina ‘hit squad’ yake au?
Matukio yote haya ya uhalifu dhidi ya raia, wananchi hatupewi taarifa za kutosha zinazoyahusu.
Kwa nini hasa?
Ukosefu wa taarifa za kutosha na kuridhisha ni moja ya sababu zinazowafanya baadhi ya watu waamini kuwa huko serikalini kuna ‘hit squad’ na kuna watu wanaojua fika kinachoendelea.
Kama hakuna ‘hit squad’, mbona hatupewi taarifa?
Hali inatisha.....
Prof. Athumani Livigha
Prof. Jwani Mwaikusa
Dr. Sengondo Mvungi
Dr. Steven [Stephen?] Ulimboka
Tundu Lissu
Ben Saanane
Mohammed Dewji
Abdul Nondo
Roma Mkatoliki......
Kwa nini nimewaorodhesha hao watu?
Nimewaorodhesha kwa sababu, wote hao wana ‘common denominator’ katika yaliyowatokea, hususan baada ya [ma]tukio.
Mpaka leo bado hakuna taarifa za uhakika kwa nini Prof. Nicas Mahinda aliuwawa!
Dr. Ulimboka alitekwa na baadaye akaja kukutwa/ kuokotwa huko Mabwepande akiwa hajitambui.
Ben Saanane haijulikani alipo.
Mpaka sasa hatujui ni nani alitaka kumuua Tundu Lissu pale Dodoma.
Roma Mkatoliki naye alitekwa lakini akaja kuachiwa akiwa mzima.
Majuzi tu hapa bilionea Mo Dewji alitekwa halafu eti akaja kutupwa usiku wa manane kwenye viwanja vya Gymkhana.
Matukio yote hayo ya watu kutekwa, kujaribiwa kuuwawa, na kupotea kabisa, hayana maelezo yaliyokamilika wala kunyooka.
Watu hata hatujui kwa nini Mo alitekwa, achilia mbali alitekwa na nani!
Ni zaidi ya mwaka sasa baada ya Lissu kujaribiwa uhai wake na hakuna hata mshukiwa/ washukiwa.
Sasa mimi nauliza, hivi serikali ya Tanzania ina ‘hit squad’ yake au?
Matukio yote haya ya uhalifu dhidi ya raia, wananchi hatupewi taarifa za kutosha zinazoyahusu.
Kwa nini hasa?
Ukosefu wa taarifa za kutosha na kuridhisha ni moja ya sababu zinazowafanya baadhi ya watu waamini kuwa huko serikalini kuna ‘hit squad’ na kuna watu wanaojua fika kinachoendelea.
Kama hakuna ‘hit squad’, mbona hatupewi taarifa?
Hali inatisha.....