VODA wameshalalamika biashara yao ya huduma za kifedha kushuka hasa maeneo ya vijijini, kuna hatari makampuni yakaanza kuhamisha mitaji na kuathiri maendeleo kwenye sekta nzima ya mawasiliano.....tutarudi enzi za kupanda juu ya miti ili uweze kupata network.
Kulalamika kwa kampuni fulani kwamba huduma zao zimeanza kuzorota sio excuse ya maana. Wao wenyewe VODA gharama zao za huduma zinalalamikiwa kuwa ni aghali kuliko mitandao mingine mbona wamekomaa na gharama zao zile zile? Jibu ni simpo, wamefanya analysis wakaona hiyo ndiyo business model yao itakayowaletea faida. Wasioweza kutumia voda wahamie mitandao mingine.

Kwa nini serikali ndiyo icompromise mambo yake? Labda kama hawana shabaha ya wanataka nini na watafikaje hapo, vinginevyo ni kazi ya serikali kujenga hoja na kuijenga kwa vitendo, kwamba kabla ya tozo hizi tulikuwa hatuwezi kufanya haya lakini baada ya hizi tozo tumefanya hivi.
 
Tozo haiwezekani kuondolewa kwa sababu hadi sasa hakuna impacts yoyote ya maana na Serikali ilikuwa inavuta mda tuu iangalie kwa mwezi mmja watumiaji wamepungua kama wapiga propaganda au watu bado wanatumia?

Bila shaka wamejiridhisha kwamba hakuna impacts yoyote ya kuathiri kampuni za simu au mawakala au watu kujazana benki.

Na kwa kuwa nchi yetu watu sio waaminifu kwenye kitimiza wajibu wao kwenye kulipa kodi serikali haiwezi kutoa hiyo tozo na mimi naunga mkono.

Nina ushahidi kuna watu wanatengenezea wafanyabiashara risiti za efd Ili zioneshe wamelipa VAT kumbe usanii mtupu,sasa kwa Ukwepaji huu wa kodi itakuwa ajabu serikali ikiondoa tozo.

Mwisho tayari sheria ya bajeti ilishasainiwa na Rais na ilipitishwa na Bunge tena wabunge waliunga mkono kwa vile pesa zinaenda kwenye barabara,afya,elimu na maji ambazo ni kero kwa wananchi wao.

Kuondoa au kufuta tozo kwa sasa ni kusababisha bajeti isitekelezeke maana zaidi ya 1.2 Tilioni zitapotea, serikali itatoa wapi hii nakisi?

Kana kwamba haitoshi huwezi kopa nje ya mpango wa bajeti kwa hiyo kiufupi haitekelezeki.
 
Katika muendelezo uleule wa kudanganyadanganya wananchi serikali ya Samia imeanza kupiga chenga juu ya kupunguza tozo kubwa sana za miamala ya fedha.

Baada ya kelele kubwa na kukasirishwa kwa wananchi juu ya tozo kubwa za miamala ya fedha, serikali ya Samia ilijifanya kupoza kelele hizo kwa kuahidi kulifanyia kazi suala hilo. Lakini inaonekana hiyo ilikuwa ni tekniki ya kupoza hali huku wakiendelea kuwakamua wananchi pesa zao.

Hata Msemaji wa Serikali Gerson Msigwa anasema tozo hizo haziwezi kuondolewa kwa sababu eti ziko kisheria.

Hoja hiyo ni hoja Muflisi kwa sababu hata Kikokotowo kilikuwepo kisheria lakini kiliahirishwa kutumika.

Tunaitaka serikali iitishe kikao cha dharura cha bunge ili bunge lipunguze hizo tozo mara moja.

Watanzania hatuwezi kuishi kwa kudanganywadanganywa

View attachment 1876301
Jibu la wapumbavu ni vitendo tu dawa ni kuachana na huduma zenye tozo hela tuna tumiana cash ,hapo makampuni ya simu yatashindwa kuipatia serikali hiyo pesa waliyo kuwa wanawakusanyia mafisadi wa chama na serikali
 
Nadhani sasa akili zimeanza kurudi kwa baadhi ya watu.

Tulisema kwamba hatutegemei tofauti kubwa sana kati ya huyu na watangulizi wake.

Sasa wamegoma, mtawafanya nini?

Intelligence guided with experience…..you can’t beat that!
Acha kufananisha magufuli na mabo ya kipumbaavuu
 
Hana ujanja, miradi aliyoachiwa na Magufuli ni mingi na inahitaji pesa nyingi amejua akicheza haitakamilika.

Kuanzia SGR, Nyerere Dam, Kigongo Busisi, daraja la kule Mikocheni baharani, bado miradi mingine ya barabara, maji safi na salama, umeme vijijini, inahitajika kama kawaida.

Kama Magufuli alikuwa anawapora watu pesa zao isivyo halali, basi Samia anachukua pesa kwa watu kihalali kwa msaada wa sheria kandamizi zilizopitishwa na bunge feki.
Mbona wakati wa magu ilikuwa inaendelea bila ya tozo ? Sema mama kawa fleva mafisadi sasa anajua uchumi utaporomoka maana kaacha makinikia na tanzanite kuibiwa kaacha matumizi mabovu kwa viongozi hivyo anataka kuziba gepu kwa kuwakamua masikini
 
Sasa hiyo tozo tunalipa wananchi wanyonge pekee?

Mbona hao wabunge pamoja na mamilioni wanayolipwa, lakini hawalipi PAYE kutoka kwenye mishahara yao??
lipa tozo kwa faida ya maendeleo yako, mwanao na mjukuu wako.
acha ubahili, hakuna vya bure. tujifunze kujitegemea.
 
Na kwa kuwa nchi yetu watu sio waaminifu kwenye kitimiza wajibu wao kwenye kulipa kodi serikali haiwezi kutoa hiyo tozo na mimi naunga mkono.

Nina ushahidi kuna watu wanatengenezea wafanyabiashara risiti za efd Ili zioneshe wamelipa VAT kumbe usanii mtupu,sasa kwa Ukwepaji huu wa kodi itakuwa ajabu serikali ikiondoa tozo.
Hadi unatia aibu. Yan umeisha jua watu wanakwepa kodi badala ya kutafta njia ya kuwafanya wasikwepe kodi ww unakuja na njia ya kuongeza tatizo.
Ebu niambia ni jinsi gani mtumiaji wa miamala alikuwa anakwepa kulipia kodi(VAT) kwenye miamala aliyokuwa anaifanya?
 
Watanzania bhana!!yaan kitu kimesomwa kwenye budget watu wanaowawakilisha wamekaa wanapiga makofi nyie muda huo mko busy kutumbuliwa kwa Chalamila budget ikapitishwa
Et leo mnashangaa mnataka tozo zifutwe!!wkt wa buget mlikuwa wap
 
Katika muendelezo uleule wa kudanganyadanganya wananchi serikali ya Samia imeanza kupiga chenga juu ya kupunguza tozo kubwa sana za miamala ya fedha.

Baada ya kelele kubwa na kukasirishwa kwa wananchi juu ya tozo kubwa za miamala ya fedha, serikali ya Samia ilijifanya kupoza kelele hizo kwa kuahidi kulifanyia kazi suala hilo. Lakini inaonekana hiyo ilikuwa ni tekniki ya kupoza hali huku wakiendelea kuwakamua wananchi pesa zao.

Hata Msemaji wa Serikali Gerson Msigwa anasema tozo hizo haziwezi kuondolewa kwa sababu eti ziko kisheria.

Hoja hiyo ni hoja Muflisi kwa sababu hata Kikokotowo kilikuwepo kisheria lakini kiliahirishwa kutumika.

Tunaitaka serikali iitishe kikao cha dharura cha bunge ili bunge lipunguze hizo tozo mara moja.

Watanzania hatuwezi kuishi kwa kudanganywadanganywa

View attachment 1876301
Hao wadau kwann wasirekodi namba zao kisha wawakate hizo tozo wao pekee yao. Nani anaweza pendekeza upuuzi kama huo...?!
 
Mimi naamini wataitoa wenyewe tu. Bahati mbaya watafanya hivyo wakati imeshaleta madhara makubwa kwa mapato ya serikali. Kama kabla ya tozo walikuwa wanaweza kukusanya say Sh100bn kutoka kwa miamala, kwa kuweka hizo tozo likely wakakusanya less than Sh100bn. Watu wameacha/wamepunguza kutumia miamala ya simu. Binafsi nimepunguza karibu 90% ya matumizi yangu ya miamala ya simu. Natumia benki na cash zaidi kiliko awali. Nimeanza kuzoea!

Watu wakishazoea hizo alternatives wanazotumia sasa kukwepa unyang'anyi kipitia tozo, itachukua muda kuwarudisha watu kutumia miamala ya simu hata kwa kuondoa tozo! Imechukua muda mrefu watu kuamini utumaji na upokeaji wa pesa kupitia simu za mkononi.

Kuna kazi kubwa makampuni ya simu yalifanya kujenga base ya mawakala nchi nzima......tozo hizi zitapunguza vipato vya mawakala na wengi wataacha hiyo biashara. naamini tozo hizi zina madhara ni makubwa kuliko serikali ilivyofikiria kabla . Muda utazungumza.
 
10 Reactions
Reply
Back
Top Bottom