Katika muendelezo uleule wa kudanganyadanganya wananchi serikali ya Samia imeanza kupiga chenga juu ya kupunguza tozo kubwa sana za miamala ya fedha.

Baada ya kelele kubwa na kukasirishwa kwa wananchi juu ya tozo kubwa za miamala ya fedha, serikali ya Samia ilijifanya kupoza kelele hizo kwa kuahidi kulifanyia kazi suala hilo. Lakini inaonekana hiyo ilikuwa ni tekniki ya kupoza hali huku wakiendelea kuwakamua wananchi pesa zao.

Hata Msemaji wa Serikali Gerson Msigwa anasema tozo hizo haziwezi kuondolewa kwa sababu eti ziko kisheria.

Hoja hiyo ni hoja Muflisi kwa sababu hata Kikokotowo kilikuwepo kisheria lakini kiliahirishwa kutumika.

Tunaitaka serikali iitishe kikao cha dharura cha bunge ili bunge lipunguze hizo tozo mara moja.

Watanzania hatuwezi kuishi kwa kudanganywadanganywa

View attachment 1876301
Safi
 
Huyu maza ni mnyanganyi hana tofauti na mwenda zake
Bora mwendezake alikuwa ana nyanganya vitu tuna viona, huyu ameiga mfumo wa serikal ya awam ya 4 ya matumiz yanayozidi kipato, kwenye bajet yake bajet ya maendeleo ni ndogo na bajet ya matuzi ya kiofis ni kubwa, chai na vitafunwa, ukarabati wa ikulu Kwa billion 9 zimerud tena, semina , Safar za nje zimerud tena.
 
Hadi unatia aibu. Yan umeisha jua watu wanakwepa kodi badala ya kutafta njia ya kuwafanya wasikwepe kodi ww unakuja na njia ya kuongeza tatizo.
Ebu niambia ni jinsi gani mtumiaji wa miamala alikuwa anakwepa kulipia kodi(VAT) kwenye miamala aliyokuwa anaifanya?
VAT ni ndogo Sana huwezi kwepa, Serikali kamatieni hapo hapo.Nyie mnaolia Lia kama vifaranga ukute hujawahi dai risiti yoyote toka umeanza kufanya manunuzi.
 
VAT ni ndogo Sana huwezi kwepa, Serikali kamatieni hapo hapo.Nyie mnaolia Lia kama vifaranga ukute hujawahi dai risiti yoyote toka umeanza kufanya manunuzi.
Ujajibu swali langu. Acha kuruka ruka.
Kwaiyo unataka kusema kuwa wameongeza kodi ya miamala ili kufidia magepu ya watu wanaokwepa kutoa lisiti? Hiv unaona hiyo n hoja ya kuisema mbele za watu wenye akili timamu?
 
Ujajibu swali langu. Acha kuruka ruka.
Kwaiyo unataka kusema kuwa wameongeza kodi ya miamala ili kufidia magepu ya watu wanaokwepa kutoa lisiti? Hiv unaona hiyo n hoja ya kuisema mbele za watu wenye akili timamu?
Ndio nimejibu hivyo.Hicho unachouliza ndio jibu lenyewe.Unataka haki ila hutaki wajibu wako,sasa utatimiza wajibu kwa njia hizo
 
Akiongeza taxation kwenye madini vipi?
Hana ujanja, miradi aliyoachiwa na Magufuli ni mingi na inahitaji pesa nyingi amejua akicheza haitakamilika.

Kuanzia SGR, Nyerere Dam, Kigongo Busisi, daraja la kule Mikocheni baharani, bado miradi mingine ya barabara, maji safi na salama, umeme vijijini, inahitajika kama kawaida.

Kama Magufuli alikuwa anawapora watu pesa zao isivyo halali, basi Samia anachukua pesa kwa watu kihalali kwa msaada wa sheria kandamizi zilizopitishwa na bunge feki.
 
Wataachia tu..., sio kwamba wataacha sababu wanawapenda wananchi bali sababu yale mapato watashangaa sio mengi..., LABDA tu kama wanataka kuua mfumo wa mobile money kwa kufanya watu watumie Bank

 
10 Reactions
Reply
Back
Top Bottom