Serikali ya Rais Magufuli ilikosea kwenye sukari, kwanini inarudia tena kosa kwenye mafuta ya kula?

AbaMukulu

JF-Expert Member
Jan 1, 2018
2,048
3,568
Bei ya sukari 2015 ilikuwa 1800-2200 kwa kilo. Baada ya tangazo la marufuku ya kuingiza sukari toka nje bei ilipaa na hadi sasa hivi iko kuanzia 2600-3000 kwa kilo.

Marufuku ile ililenga kulinda uzalishaji wa ndani wa sukari kitu ambacho ni nia njema kabisa.

Matokeo ya uamuzi hayajawa mazuri hadi leo. Hapa kuna swala kubwa la kujifunza kwa utawala wa Magufuli.

Rais inabidi abadilike namna anavyofanya maamuzi yake.

Bei ya sukari isingepanda kama kulikuwa na mipango madhubuti ya kutuvusha kipindi cha mpito ambacho tungekuwa tunajenga kiwanda kipya au tunaongeza uzalishaji wa vilivyopo huku tukiendelea kuagiza nje.

Baada ya kupita kipindi cha mpito na kuna uhakika wa uzalishaji ndipo serikali ingepiga marufuku uagizwaji wa sukari toka nje sababu tungekuwa tunajitosheleza uzalishaji wa ndani.

Tukirudi kwenye suala la mafuta ya kula naona maamuzi mabovu yaliyofanyika yanajirudia tena kwenye serikali ambayo ina zaidi ya miaka miwili na nusu madarakani.

Na Waswahili wanasema "Kosea njia wakati wa kwenda sio wakati wa kurudi"

Kabla ya kupiga marufuku mafuta ya nje ingebidi serikali ijiridhishe yafuatayo

1. Uhakika wa Viwanda vya uzalishaji
2. Malighafi za uzalishaji kwa viwanda hivyo
3. Upatikanaji wa Nishati ya uhakika

Mambo yote hayo hayako kwenye mazingira mazuri ili kukidhi uzalishaji wa ndani. Serikali iyafanyie kazi kwanza kwa matokeo chanya.

Naunga mkono uzalishaji wa viwanda vya ndani lakini maamuzi ya kufikia lengo hilo yanafanyika hovyo na kuleta matokeo hasi.


Uamuzi mbovu kwenye suala mafuta ya kula ndio unasababisha bei kupanda na kumuumiza mwananchi.

Kwa wale wachezaji wa draft wanajua kwamba kila kete utakayosogeza basi ina athari kwenye ushindi/kushindwa kwako.

ANGALIZO
EAC imepiga marufuku uagizwaji wa mitumba ifikapo 2019.

Mitumba kupigwa marufuku Afrika Mashariki

JUHUDI ZIANZE MAPEMA, TUKICHELEWA TUTAVALISHWA NGUO NA WANYARWANDA WAKATI TUNA PAMBA NA UWEZO WA KUTOSHA WA UZALISHAJI.
 
Leo nimeona kwenye gazeti la mwananchi wameandika habari kuwa mafuta yataanxa kuadimika kama sukari,

Kwenye mafuta hapa atagusa wengi hadi vijijini,

Maana issue ya sukari vijijini wengi wao hawanywagi chai,

Ngoja tuhifadhi kumbu kumbu

Tujiandae kisaikolojia na msako wa 'waficha mafuta'
 
Mkuu jifunze kutumia mbadala wa mafuta ya kula, mf karanga ili uepukane na kadhia ya uadimikaji, yaani ni kama unatumia umeme wa tanesco uwe na angalau solar!

Mimi natumia alizeti ambayo nayo yamepanda bei.

Na watu wengi wa kipato cha chini na mama ntilie wanatumua yale palm oil kwa sababu ya bei rafiki.
Na hayo ndio yamekumbwa sana na athari ya maamuzi haya kurupushi
 
Mimi natumia alizeti ambayo nayo yamepanda bei.

Na watu wengi wa kipato cha chini na mama ntilie wanatumua yale palm oil kwa sababu ya bei rafiki.
Na hayo ndio yamekumbwa sana na athari ya maamuzi haya kurupushi
na hata hivyo yameshaanza kupanda,dumu la lita 20 ni 70elfu kutoka 64,000 ndoo ya lita 10 ni 35,000 kutoka 32,000 hiyo ni bei ya hapa kibaha,
 
Bei ya sukari 2015 ilikuwa 1800-2200 kwa kilo. Baada ya tangazo la marufuku ya kuingiza sukari toka nje bei ilipaa na hadi sasa hivi iko kuanzia 2600-3000 kwa kilo.

Marufuku ile ililenga kulinda uzalishaji wa ndani wa sukari kitu ambacho ni nia njema kabisa.

Matokeo ya uamuzi hayajawa mazuri hadi leo. Hapa kuna swala kubwa la kujifunza kwa utawala wa Magufuli.

Rais inabidi abadilike namna anavyofanya maamuzi yake.

Bei ya sukari isingepanda kama kulikuwa na mipango madhubuti ya kutuvusha kipindi cha mpito ambacho tungekuwa tunajenga kiwanda kipya au tunaongeza uzalishaji wa vilivyopo huku tukiendelea kuagiza nje.

Baada ya kupita kipindi cha mpito na kuna uhakika wa uzalishaji ndipo serikali ingepiga marufuku uagizwaji wa sukari toka nje sababu tungekuwa tunajitosheleza uzalishaji wa ndani.

Tukirudi kwenye suala la mafuta ya kula naona maamuzi mabovu yaliyofanyika yanajirudia tena kwenye serikali ambayo ina zaidi ya miaka miwili na nusu madarakani.

Na Waswahili wanasema "Kosea njia wakati wa kwenda sio wakati wa kurudi"

Kabla ya kupiga marufuku mafuta ya nje ingebidi serikali ijiridhishe yafuatayo

1. Uhakika wa Viwanda vya uzalishaji
2. Malighafi za uzalishaji kwa viwanda hivyo
3. Upatikanaji wa Nishati ya uhakika

Mambo yote hayo hayako kwenye mazingira mazuri ili kukidhi uzalishaji wa ndani. Serikali iyafanyie kazi kwanza kwa matokeo chanya.

Naunga mkono uzalishaji wa viwanda vya ndani lakini maamuzi ya kufikia lengo hilo yanafanyika hovyo na kuleta matokeo hasi.


Uamuzi mbovu kwenye suala mafuta ya kula ndio unasababisha bei kupanda na kumuumiza mwananchi.

Kwa wale wachezaji wa draft wanajua kwamba kila kete utakayosogeza basi ina athari kwenye ushindi/kushindwa kwako.

ANGALIZO
EAC imepiga marufuku uagizwaji wa mitumba ifikapo 2019.

Mitumba kupigwa marufuku Afrika Mashariki

JUHUDI ZIANZE MAPEMA, TUKICHELEWA TUTAVALISHWA NGUO NA WANYARWANDA WAKATI TUNA PAMBA NA UWEZO WA KUTOSHA WA UZALISHAJI.
Umeongea point mkuu yaani matamko yake yanazidisha ukali wa maisha kila kukicha badala ya kuleta afueni.
 
Bei ya sukari 2015 ilikuwa 1800-2200 kwa kilo. Baada ya tangazo la marufuku ya kuingiza sukari toka nje bei ilipaa na hadi sasa hivi iko kuanzia 2600-3000 kwa kilo.

Marufuku ile ililenga kulinda uzalishaji wa ndani wa sukari kitu ambacho ni nia njema kabisa.

Matokeo ya uamuzi hayajawa mazuri hadi leo. Hapa kuna swala kubwa la kujifunza kwa utawala wa Magufuli.

Rais inabidi abadilike namna anavyofanya maamuzi yake.

Bei ya sukari isingepanda kama kulikuwa na mipango madhubuti ya kutuvusha kipindi cha mpito ambacho tungekuwa tunajenga kiwanda kipya au tunaongeza uzalishaji wa vilivyopo huku tukiendelea kuagiza nje.

Baada ya kupita kipindi cha mpito na kuna uhakika wa uzalishaji ndipo serikali ingepiga marufuku uagizwaji wa sukari toka nje sababu tungekuwa tunajitosheleza uzalishaji wa ndani.

Tukirudi kwenye suala la mafuta ya kula naona maamuzi mabovu yaliyofanyika yanajirudia tena kwenye serikali ambayo ina zaidi ya miaka miwili na nusu madarakani.

Na Waswahili wanasema "Kosea njia wakati wa kwenda sio wakati wa kurudi"

Kabla ya kupiga marufuku mafuta ya nje ingebidi serikali ijiridhishe yafuatayo

1. Uhakika wa Viwanda vya uzalishaji
2. Malighafi za uzalishaji kwa viwanda hivyo
3. Upatikanaji wa Nishati ya uhakika

Mambo yote hayo hayako kwenye mazingira mazuri ili kukidhi uzalishaji wa ndani. Serikali iyafanyie kazi kwanza kwa matokeo chanya.

Naunga mkono uzalishaji wa viwanda vya ndani lakini maamuzi ya kufikia lengo hilo yanafanyika hovyo na kuleta matokeo hasi.


Uamuzi mbovu kwenye suala mafuta ya kula ndio unasababisha bei kupanda na kumuumiza mwananchi.

Kwa wale wachezaji wa draft wanajua kwamba kila kete utakayosogeza basi ina athari kwenye ushindi/kushindwa kwako.

ANGALIZO
EAC imepiga marufuku uagizwaji wa mitumba ifikapo 2019.

Mitumba kupigwa marufuku Afrika Mashariki

JUHUDI ZIANZE MAPEMA, TUKICHELEWA TUTAVALISHWA NGUO NA WANYARWANDA WAKATI TUNA PAMBA NA UWEZO WA KUTOSHA WA UZALISHAJI.

Serikali haijapiga marufuku mafuta kutoka nje tafuta ukweli kabla ya kutetea. Watanzania mnataka kuendelea kula sumu mpaka lini? Mnajua mafuta waingizaji mafuta nchini wanachanganya na nini ili kukwepa kodi? na mnajua madhara ya hizo kemikali wanazotumia kuchakachua mafuta kwa tamaa na faida? Hivi watu hawajiulizi kwanini kuna ongezeko saratani?
 
Mimi natumia alizeti ambayo nayo yamepanda bei.

Na watu wengi wa kipato cha chini na mama ntilie wanatumua yale palm oil kwa sababu ya bei rafiki.
Na hayo ndio yamekumbwa sana na athari ya maamuzi haya kurupushi

Hasa hayo Palm.
 
Hii awamu kila mtu anakuwa mbabe, kila kiongozi anataka aonekane mchapa kazi. Lastly tunaumia sisi wanyonge. Hili la mafuta linahitaji busara la sivyo andazi la TZS 100 litauzwa TZS 200
 
Back
Top Bottom