Serikali ya Rais John Magufuli yathibitisha umahiri wake katika kupambana na corona na kuwalinda wananchi wake

Wiki moja iliyopita Rais Trump alikuwa na mtazamo kama wa JPM na hakutaka kabisa lockdown iliyokuwa imewekwa katika baadhi ya majimbo iendelee. Hovyo akatangaza nia yake ya kusitisha hiyo lockdown. Hapo ndipo wataalam wake wakampa ukweli kuwa hali ni mbaya na wamarekani si chini ya 100,000 watakufa kutokana na corona. Ndipo Trump akasema "Nothing can be worse than declaring victory before victory is won", yaani hakuna kitu kibaya kama kutangaza ushindi kabla ya ushindi haujapatikana.

Kumbukeni pia ya kwamba kisa cha kwanza huko USA kilitangazwa January 20, na baada ya hapi vifo viliongezeka kwa kasi ndogo sana hadi March 16 ndipo hali ikabadilika. Sisi Tanzania kisa cha kwanza kilitangazwa March 16 na mpaka sasa hali haijawa ya kutisha. Hali hii isitufanye tuamini kwamba tayari tumeshinda vita. Muda ndo utaamua. Kwa sasa tujiepusha na kusifia!
Hivi kama muungwana,unashindwaje kusema maamuzi ya Raisi Magufuli ni ya akili kubwa?.Huku ni Ku appreciate alichotufanyia watanzania.Haishii kwenye maamuzi na mandalizi ni makubwa pia
 
Maamuzi ya Mh.Dk John Joseph Pombe Magufuli ni maamuzi magumu na ya kihistoria ambayo yatakumbukwa na vizazi vijavyo katika mchakato huu wa kupambana na virus vya COVID19. Tumeona mataifa menig yakifunga mipaka na kuzuia watu kutoka nje kwa kuwalinda raia wao wasipate maambukizi ya Corana. Nchi zilizotumia mbinu hizo nyingi ni zilizo endelea kiuchumi mfano USA na China. Kabla sjaendelea kuandika uzi wangu embu tujiulize , ‘mfano wewe upo vitani anakuja adui kuwashambulia wewe pamoja na rafiki yako. Wewe upo na risasi 2 mwenzako ana magazin nne zote zimejaa risas, rafiki yako akatumia risas nyingi kumuua yule adui na hatimaye adui akafa. Swali linakuja je, wewe mwenye risasi 2 ungetumia risasi hizohizo tu au ungekubali kufa na risas zako. Jibu ni wewe lazma ungejitete na risasi zako 2. Na hivi ndivyo ilivyo kwa Tanzania yetu, ni lazma tujitetee na vitu na mikakati iliyo ndani ya uwezo wetu. USA wanampango wa kugawa $1200 kwa kila mwananchi ili aweze kujikimu na ndio maana wakafunga mipaka. Leo kwa sisi hapa pangu pakavu tia mchuzi Mh Rais akiamua kufunga mipaka na tusitoke nje ni nan ataumia? Nilijaribu kupitia kurasa mbalimbali za kijamii za mitandaoni nikakutana na Tweet ya Mh Zitto Kabwe akishinikiza kufungwa kwa mipaka na watu kukaa ndani. Nikajiuliza ‘huyu kweli ni mwana uchumi’? Tusipende kupinga vitu ilimradi tumepinga tu, tuangalie ni kwa namna gani tunaweza kupambana na huyu Corona kikwetukwetu.

Abdulkarim Mzee
 
Maamuzi ya Mh.Dk John Joseph Pombe Magufuli ni maamuzi magumu na ya kihistoria ambayo yatakumbukwa na vizazi vijavyo katika mchakato huu wa kupambana na virus vya COVID19. Tumeona mataifa menig yakifunga mipaka na kuzuia watu kutoka nje kwa kuwalinda raia wao wasipate maambukizi ya Corana. Nchi zilizotumia mbinu hizo nyingi ni zilizo endelea kiuchumi mfano USA na China. Kabla sjaendelea kuandika uzi wangu embu tujiulize , ‘mfano wewe upo vitani anakuja adui kuwashambulia wewe pamoja na rafiki yako. Wewe upo na risasi 2 mwenzako ana magazin nne zote zimejaa risas, rafiki yako akatumia risas nyingi kumuua yule adui na hatimaye adui akafa. Swali linakuja je, wewe mwenye risasi 2 ungetumia risasi hizohizo tu au ungekubali kufa na risas zako. Jibu ni wewe lazma ungejitete na risasi zako 2. Na hivi ndivyo ilivyo kwa Tanzania yetu, ni lazma tujitetee na vitu na mikakati iliyo ndani ya uwezo wetu. USA wanampango wa kugawa $1200 kwa kila mwananchi ili aweze kujikimu na ndio maana wakafunga mipaka. Leo kwa sisi hapa pangu pakavu tia mchuzi Mh Rais akiamua kufunga mipaka na tusitoke nje ni nan ataumia? Nilijaribu kupitia kurasa mbalimbali za kijamii za mitandaoni nikakutana na Tweet ya Mh Zitto Kabwe akishinikiza kufungwa kwa mipaka na watu kukaa ndani. Nikajiuliza ‘huyu kweli ni mwana uchumi’? Tusipende kupinga vitu ilimradi tumepinga tu, tuangalie ni kwa namna gani tunaweza kupambana na huyu Corona kikwetukwetu.

Abdulkarim Mzee
Well said Abdulkarim Mzee,
Wasomi wetu wameharibiwa na elimu hizi za kikoloni,kuiga mambo ambayo sio sahihi kwa mazingira yetu.Zitto Kabwe na wenzake ni watu wa kugoogle tu hakuna uchumi kichwani...nchi zilizofungia watu wake sasa zinaidadi kubwa ya vifo na maqmbukizi pamoja na mqtatizo mengine
 
Ugonjwa wa Corona umeanza December 2019 katika mji wa Wuhan nchini China.Mpaka hivi sasa ugonjwa huu umeshasambaa kwa watu takribani 819,025 na kusababisha vifo vya watu wapatao 39,794 duniani kote akiwemo raia mmoja wa Tanzania.

Kusambaa kwa ugonjwa huu duniani kumeleta taharuki kubwa kwa viongozi wa nchi mbalimbali duniani.Nchi nyingi zimechukua maamuzi ambayo wataalamu wamebaini madhara makubwa ya hatua zilizochukuliwa zaidi ya madhara halisi ya janga la corona katika nchi hizo.

Mfano zipo nchi zilizochukua maamuzi ya kuwazuia watu wake kutoka nyumbani na kufunga kabisa shughuli za uzalishaji,na zipo nchi zilizochukua maamuzi ya kufunga mipaka yake kutokuruhusu kuingia na kutoka kwa wananchi wake.Lakini cha kustaajabu nchi hizi zimeendelea kukabiliwa na maambukizi na kuongeza ukubwa wa tatizo kwa wananchi wake.Ukubwa wa tatizo hili katika baadhi ya nchi unaongezwa na msongo wa mawazo na kukata tamaa kwa wananchi,uchumi wa familia unaoambatana na ukosefu wa chakula kutokana na kutokuwepo maandalizi stahiki na mlipuko wa magonjwa mengine ya kijamii.

Anasema Professor Lina Lindhard wa International University of Professional Studies, namnukuu

”If what is happening in Europe is anything to go on, we really do not know how many confirmed cases there are for people who have it at home are not being tested. Also in France and I believe Germany, unless the person dies in a hospital from the corona virus, it is is not counted amongst the deaths. So people dying at home and old age homes are not included. As this moves to less developed countries the statistics will also become more confused.”

Ni wazi kuwa kuna maambukizi yanayoweza kuendelea kwa kufungia watu ndani,kujifungia ndani kwa watu ambao wamepima na kutokuwa na maambukizi yanaweza kusaidia,lakini kufungia watu ndani na ikatokea miongoni mwa mwanafamilia aliejifungia anamaambukizi anaweza kuwaambukiza wengine na kuendeleza maambukizi kwa haraka bila taarifa kuifikia serikali au mamlaka husika.

Wataalamu mbalimbali wa ugonjwa huu wanatoa maoni juu ya namna nzuri ya kukabiliana na janga la ugonjwa huu hatari wa corona.Mbinu ya kwanza ni kutoa elimu sahihi juu ya mbinu za kukabiliana na ugonjwa huu kwa ngazi ya mtu mmoja mmmoja,familia,kikundi na nchi kwa jumla.Mbinu ya pili ni kuhakikisha wananchi wanafuata kanunu za afya na tahadhari zingine ili kuepuka maambukizi mapya.Mbinu ya tatu ni kuthibiti maambukizi yaliyopo na kutokomeza kabisa ugonjwa.

Njia hizi hata kabla ya kutolewa na wataalamu ndizo zilizotumika Tanznaia na zinazoendela kutumika chini ya uongozi imara wa Raisi Dr. John Pombe Magufuli .Tofauti na nchi zingine njia hizi zimeweza kuleta matuamaini makubwa kwa Watanzania kwani idadi ya maambukizi mapya imekua kwa kiwango kidogo kulinganisha na nchi zingine.Maamuzi haya ya Raisi John Magufuli yamepunguza na kudhibiti madhara ambayo sio ya moja kwa moja yatokanayo na janga la ugonjwa wa corona,madhara hayo ni kama vile kufa na njaa kwa wananchi wanaotegemea kipato cha siku,msongo wa mawazo,kupoteza ajira,kuvunja uchumi wa mtu mmoja mmoja,familia na nchi kwa ujumla.

Kutokana na maamuzi haya ya serikali ya Raisi wetu Dr John Magufuli unadhirisha wazi kwa Watanzania na dunia kwa ujumla kuwa uzalendo,hofu ya Mungu na umakini katika maamuzi yenye mustakabali mwema na nchi unahitajika na sio kuiga wanachofanya viongozi wa nchi zingine ambao wana mazingira tofauti na ya kwetu.

Nisije nikawa mwizi wa fadhila,kwa kutokushare na ninyi sifa za kiongozi wetu Raisi Dr,John Magufuli katika mapambano haya:

1.Kiongozi bora ni yule anayetoa matumaini na kuweza kuthibitisha yale matumaini wakati wale anaowaongoza wakiwa wamekata tamaa.

Madhara yanayoweza kupatikana kwa hofu kubwa ya jambo yanaweza kuwa makubwa kuliko madhara yanayoweza patikana kutokana na lile janga.Mfano janga la kinu cha kuzalisha umeme cha Fukushima Daichi Japan.Professor Fred Peace anasema namnukuu.

“In Fukushima accident for many, the psychological damage is far more profound than the health effects”

Kwa maana kuwa madhara yaliypatikana kwa uoga,na hofu baada ya ajali yalikuwa makubwa kuliko madhara madogo yaliyotokea kutokana na ajali ya kinu cha nuklia.Hili linajidhihirisha kwenye janga la corona baada ya ugonjwa huu kuaza kusambaa na kuonekana madhara yake,na baadhi ya watanzania kupata maambukizi ilitokea taharuki ambayo kama sio busara na hekima za Raisi madhara ya taharuki hii yangekua makubwa kuliko athari za ugonjwa wenyewe.

Tunajua mazigira halisi ya wanachi wetu wengi,wanategemea kazi za kila siku kujipatia kipato,kuwafungia ndani kungewakosesha chakula,huduma za afya na huduma nyingine muhimu.Ndio maana Raisi akiwa Dodoma alisema maneno haya,nanukuu
“Watu tusitishane,tunatishana mno.Niwaombe ndugu Wakristo na Watanzania kwa ujumla wa madhehebu yote,huu ndio wakati mzuri sana wa kumtegemea Mungu kuliko wakati wote,tuendelee kuchapa kazi,tuendelee kujenga uchumi wetu,hatuwezi kusalimu amri kwa ugonjwa huu wa Corona na kushindwa kumtegemea Mungu na na tukashindwa kuendeleza uchumi wetu.”

2.Kiongozi bora ni yule anayeweza kuyasoma mazingira yake na kukabiliana na changamoto zinazomkabili kulingana na mazingira yaliyopo na ya baadae.
Siku zote uelewa sahihi juu ya madhara yanayopatikana kutokana na janga fulani unaweza kuondoa hofu inayoweza kusababisha madhara zaidi yanayoweza kupatikana ziada ya madhara ya lile janga.Mfano,watu wanauoga wa kupima afya zao kwa khofu ya kujua hali ya afya yake lakini wanasahau kuwa madhara ya kuchelewesha kutibu tatizo la kiafya ni makubwa kuliko kulifahamu mapema.

Jukumu kubwa la serikali chini ya uongozi wa Rais John Magufuli ulikua ni kuwaelimisha watu juu ya madhara ya ugonjwa huu na tahadhari stahiki.Jambo hili lilifanyika kwa umakini na kwa kutumia mbinu za kisayansi kufikisha ujumbe.

3.Kiongozi imara huweka njia sahihi na thabiti za mawasiliano na kupashana habari katika kipindi cha taharuki.

Tunafahamu kuwa,katika jamii yeyote hawakosekani wahalifu wenye nia mbaya ambao hutumia majanga au taharuki kufanikisha malengo yao.Wapo viongozi wa kisiasa walianza kutumia mlipuko huu wa ugonjwa kuleta madhara makubwa katika jamii,wapo ambao walipinga maamuzi ya Raisi na baada ya kupingwa na wananchi kuunga maamuzi sahihi ya Raisi.

Kitaalamu,wakati wa taharuki,ujumbe unaotoka katika malaka sahihi na inayoaminika kwa umma unasaidia kuongeza usalama wa nchi,kuweka tahadhari stahiki ya ugonjwa,kuongeza imani na matumaini ya wananchi na kuunganisha jamii kupambana na janga.

Raisi amelidhirisha hili ndani ya serikali yake na kiwango cha taharuki na tahadhari imechukuliwa kwa hali ya juu.

Ombi langu kwa Watanzania, tunaye kiongozi Mcha Mungu, Mzalendo na mwenye huruma kwa wanachi wake.Tuendelee kumuombea na kumsikiliza kwa kila analotuambia.
Mungu inusuru Tanzania na Watu wake, Mungu wanusuru walimwengu na ugonjwa huu wa corona.
Ndugu yangu umeandika vyema kulingana na upeo wa wengi. Lakini nikuombe uweke huu waraka wako pembeni kwa siku 14 tuzijazo, unaweza kupata picha halisi na kuifahamu Corona. Wataalamu wa magonjwa ya kuambukiza (experts in Infectious disease) na wale wa epidemiologia wanakwenda mbali zaidi ya kutoa tu pongezi pasipo na vigezo.
Mfano nikikuuliza Serikali imechukua hatua gani zaidi ya kuwaambia watu wanawe mikono na kuandaa sehemu za kuwatibia waathirika (zisizofahamika au kuwa wazi) kwa wengi? Kuomba na kumtegemea Mungu yafaa sana, lakini pasipo kuwa na wajibu kutoka kwetu pamoja na serikali ni kazi bure.

Ukweli ni kuwa maendelea ni hatua, na historia inatuonyesha maarifa na uzoefu kuwa miongoni mwa sababu za mafanikio. Sijui sisi tunakiwango gani kikubwa kuliko hao wanaoangamia kwa janga hili sasa.

Nikupe tu takwimu za karibu, Italia tar 21 Feb walikuwa na wagonjwa 21 na kifo 1 tu (Hii ni kama hapa tulipo sasa). Wiki mbili baadae walikuwa na wagonjwa zaidi ya 5800 na jumla ya vifo takribani 233. Wiki mbili baadae, unaweza kujisemea mwenyewe (vifo zaidi ya 800 kwa siku), nchi kadhaa zimeunga behewa zikiwemo USA, UK, Ufaransa, Spain, Belgium nk. Inawezekana tukawa na sababu mbalimbali zinazoweza kupelekea hali kwetu isiwe mbaya sana, lkn vilevile inawezekana ikawa hata mbaya zaidi. Hivyo ni wajibu wetu kuchukua tahadhari na kufanya yale ya msingi zaidi ya yale yanayoagizwa na serikali kupambana na janga hili. Mfano matumizi ya maski, kuepuka misongamano hususan kwenye mabasi/daladala, kuepuka kwenda baa na sehemu zinazofanana na hizo, kuzingatia usafi kwa maji yanayotirirka n.k

Hiki sio kipindi cha kufikiria kwenye ushindani wa kisiasa, na nashangaa wengi mnaofikiria vyeo vya kisiasa wakati uhakiki wa kuishi ukiwa umetishiwa kwa kiaisi hiki. Uchumi unakwenda kuanguka kuliko unavyoweza kufikiri nk. Ni wakati wa kuja pamoja kama taifa tupigane dhidi ya adui mmoja tu ambaye ni CORONA.
 
Wiki chumvi kali.
Abdalah Abdulrahman, Maandishi yako ni marefu sana, ila ukumbuke China sio Tanzania , wenzetu wanatambua maambukizi kwakuwa wanavipimo vya kutosha nchi nzima, sisi hadi sample ichukuliwe ipelekwe maabara kuu, majibu baada ya week,

hebu jiulize aliyopo huko niombe usagatikwa anaeumwa atapimwa na kipimo kipi, mwisho atakufa nahajakujua ni corona imemuua, kiukweli Bado tupo nymama kitaalamu na kiuwezo kupambana na ugonjwa huu, sisi twendelee kumuomba Mungu kila kuitwao leo .

Goodmorning

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app by My phone
 
Corona kuathiri wachache ni swala ambalo sidhani kama rais anahusika nalo na kama mtu anamsifu kwa hilo basi labda anafanya hivyo kwa maslahi yake binafsi.

Vivyo hivyo pia huwezi ukawalaumu viongozi ktk zile nchi ambazo maambukizi yamekuwa makubwa kwani hawawajibiki kwa njia yoyote na kusambaa kwa janga hili ktk nchi zao.

Watu wenye ufinyu wa fikra kama kawaida watatumia tukio lolote lile kama fursa ya kueneza propaganda feki za kisiasa which is not only shallow thinking but a reflection of parochial mind.
 
Katika mambo ya Msingi kama haya ambayo yanahitaji Umakini mkubwa kutokana na Janga lenyewe lilivyo duniani kwa sasa na linavyozidi Kupukutisha Watu kila Uchao ' Logically ' sidhani kama COVID-19 imekuja Kutupulizia Filimbi ya Kusifia ( Kupamba ) na Kuanza Kampeni kabla ya wakati hivi.

Nakubali kwamba chini ya Serikali yake wanapambana na Elimu inatolewa mara kwa mara kwa Watanzania ila bado Serikali yake ina Safari ndefu katika Kupambana na Kuutafutia Suluhisho ama la muda au la kudumu la huu Ugonjwa ambao sasa nao unaanza Kuzoeleka ndani ya Watanzania kwa idadi ya Walioupata na huyu Mmoja aliyetutangulia kutuwekea Makazi yetu mema huko Mavumbini na baadae Ahera kabisa.
Ila wewe Antibayotike unaijua akili yako mwenyewe eti baadae Ahera kabisa ahahhahahaaaa
 
Huko Kenya Polisi wameshaua watu 3 kuwalazimisha kukaa ndani,na bado wanaendelea,corona imeua less than that...
Akili kubwa ni kubwa tu,...tuendelee kuangalia.
 
Wabongo bana mataifa yenye uwezo watu wanapukutika alafu unaleta hadithi za kusifia sifia.weka akiba ya maneno.
 
Au sio lakini Muda bado na corona bado lipo linawapoteza watu tayari mbongo mmoja kashaondoka kama likija kuripuka baadae naomba usije kukana kauli zako na kumkana mzee nijambo la muda omba sana lisiripuke mkuu
Ulipuke vipi wakati measures zinachukuliwa.? Ndoo za maji kila sehemu na watu wananawa. Sanitizers hadi zimeisha na watu wanatengeneza za kwao kwa kutia dettol.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Well said Abdulkarim Mzee,
Wasomi wetu wameharibiwa na elimu hizi za kikoloni,kuiga mambo ambayo sio sahihi kwa mazingira yetu.Zitto Kabwe na wenzake ni watu wa kugoogle tu hakuna uchumi kichwani...nchi zilizofungia watu wake sasa zinaidadi kubwa ya vifo na maqmbukizi pamoja na mqtatizo mengine
Yes brother, Hali ya sas inabid Tushikamane
 
Kuna watu wanataka total lockdown Kwa malengo yao .

Watu wenye kipato cha juu ambao wanaweza kumudu maisha hayo kwa kipindi kirefu,huku wale wenye maisha ya chini wakifa njaa ndani au kuvamia nyumba za watu na kupora kama yanayiendelea katika nchi za Kenya,Uganda na South Africa.
 
12 Reactions
Reply
Back
Top Bottom