Kichankuli
JF-Expert Member
- Dec 18, 2008
- 887
- 189
Baada ya kuziweka hadharani memo zilizokuwa zikielekeza mateso kwa watuhumiwa wa ugaidi waliokuwa wakishikiliwa na Serikali ya Marekani iliyokuwa ikiongozwa na Rais Bush, Serikali ya Rais Obama imeeleza nia ya kuziweka hadharani (kati ya sasa na mwezi Mei 2009) picha nyingine zaidi za mateso ya watuhumiwa na wafungwa wa ugaidi katika Jela ya Abugraib ambazo hazikuonyeshwa awali. Habari hizi ni kwa mujibu wa CNN leo asubuhi