Serikali ya muungano/shirikishi – wizara 3 tosha sana..

Mwamba Usemao Kweli

JF-Expert Member
Oct 5, 2012
744
186

Kwa maoni yangu naomba serikali 3 zitakazoundwa ile ya Tanganyika, Zanzibar na ile ya shirikisho ziwe na mamlaka na mgawanyo wa wizara na kitaasisi kama ifuatavyo: -

Serikali ya shirikisho/muungano iwe na wizara 3 tu nazo ni: -

  1. Wizara ya Ulinzi na jeshi la kujenga Taifa.
  2. Wizara ya Uraia na uhamiaji (Idara ya vizazi na vifo, Idara ya vitambulisho vya taifa na uhamiaji).
  3. Wizara ya Mambo ya Nje na ushirikiano wa kimataifa.

Mengineyo katika serikali ya shirikisho ni pamoja na: -

1.Kila wizara ya shirikisho hapo juu iwe na watumishi wachache na iwe ni nusu kwa nusu ya watumishi toka kila upande unao unda shirikisho.

2. Kuwepo na mamlaka inayoratibu masuala ya fedha katika nchi wanachama yenye mamlaka sawa na Central Bank of Tanzania. Majukumu yake iwe ni pamoja na kusimamia masuala ya kuprint fedha ya Tanzania na kuziwa kilisha bank kuu za kila mwanachama nje ya shirikisho. Chombo hiki kifanye uratibu wa michango toka serikali wanachama ili kufanikisha uendeshaji wa serikali ya shirikisho.

3. Kuwepo na bunge dogo la watu 30 litakalotoa wabunge kila upande wa nchi mwanachama. Tanganyika itoe wabunge 25 na Zanzibar wabunge 5. Wabunge hawa watoke kila mkoa mbunge mmoja mmoja.


4. Mahakama ya juu ya shirikisho yenye mamlaka ya kusimamia kesi za uchaguzi wa viongozi wa shirikisho na masuala yenye migogoro inayosimamiwa na shirikisho.

5. Kila mwanachama achangie uendeshaji wa taasisi zote zilizopo kwenye shirikisho (serikali, bunge na mahakama ya juu) kutokana na ushiriki wake. Hii maana yake ni kuwa kila mwanachama achangie kutegemeana na idadi ya uwakilishi wake. Kwa mfano Tanganyika ina wabunge wengi ichangie garama za wabunge wake na Zanzibar hivyohivyo kwa wabunge wake. Ifanyike hivyo kwenye wizara za shirikisho pia.

Serikali ya Zanzibar na Tanganyika kila moja iwe na wizara zote zenye mamlaka kamili kusimamia rasilimali zilizopo kwenye nchi husika isipokuwa wizara 3 tajwa hapo juu. Kuwepo pia na wizara/mamlaka zifuatazo kwa kila nchi: -

  1. Wizara ya Fedha na taasisi zake kama Revenue Authorities (TRA & ZRA).
  2. Wizara ya Mambo ya ndani na usalama wa raia (Polisi na Magereza/chuo cha mafunzo).
  3. Mahakama za ngazi zote hadi rufaa kila nchi iwe na za kwake isipokuwa mahakama ya juu itakayokuwa kwenye shirikisho.
  4. Kila nchi mwanachama aruhusiwe kushiriki biashara na mahusiano na jumuia za kimataifa bila kuingiliwa na mwanachama mwenzake. Hii ikiwa ni pamoja na tafiti, biashara, na kukopa nje ya nchi bila kuingiliwa na mwenzake. Serikali ya shirikisho itakuwa na jukumu la kuratibu tu kupitia taasisi ya fedha ya shirikisho na wizara ya mambo ya nchi za nje.
 

Kwa maoni yangu naomba serikali 3 zitakazoundwa ile ya Tanganyika, Zanzibar na ile ya shirikisho ziwe na mamlaka na mgawanyo wa wizara na kitaasisi kama ifuatavyo: -

Serikali ya shirikisho/muungano iwe na wizara 3 tu nazo ni: -

  1. Wizara ya Ulinzi na jeshi la kujenga Taifa.
  2. Wizara ya Uraia na uhamiaji (Idara ya vizazi na vifo, Idara ya vitambulisho vya taifa na uhamiaji).
  3. Wizara ya Mambo ya Nje na ushirikiano wa kimataifa.

Mengineyo katika serikali ya shirikisho ni pamoja na: -

1.Kila wizara ya shirikisho hapo juu iwe na watumishi wachache na iwe ni nusu kwa nusu ya watumishi toka kila upande unao unda shirikisho.

2. Kuwepo na mamlaka inayoratibu masuala ya fedha katika nchi wanachama yenye mamlaka sawa na Central Bank of Tanzania. Majukumu yake iwe ni pamoja na kusimamia masuala ya kuprint fedha ya Tanzania na kuziwa kilisha bank kuu za kila mwanachama nje ya shirikisho. Chombo hiki kifanye uratibu wa michango toka serikali wanachama ili kufanikisha uendeshaji wa serikali ya shirikisho.

3. Kuwepo na bunge dogo la watu 30 litakalotoa wabunge kila upande wa nchi mwanachama. Tanganyika itoe wabunge 25 na Zanzibar wabunge 5. Wabunge hawa watoke kila mkoa mbunge mmoja mmoja.


4. Mahakama ya juu ya shirikisho yenye mamlaka ya kusimamia kesi za uchaguzi wa viongozi wa shirikisho na masuala yenye migogoro inayosimamiwa na shirikisho.

5. Kila mwanachama achangie uendeshaji wa taasisi zote zilizopo kwenye shirikisho (serikali, bunge na mahakama ya juu) kutokana na ushiriki wake. Hii maana yake ni kuwa kila mwanachama achangie kutegemeana na idadi ya uwakilishi wake. Kwa mfano Tanganyika ina wabunge wengi ichangie garama za wabunge wake na Zanzibar hivyohivyo kwa wabunge wake. Ifanyike hivyo kwenye wizara za shirikisho pia.

Serikali ya Zanzibar na Tanganyika kila moja iwe na wizara zote zenye mamlaka kamili kusimamia rasilimali zilizopo kwenye nchi husika isipokuwa wizara 3 tajwa hapo juu. Kuwepo pia na wizara/mamlaka zifuatazo kwa kila nchi: -

  1. Wizara ya Fedha na taasisi zake kama Revenue Authorities (TRA & ZRA).
  2. Wizara ya Mambo ya ndani na usalama wa raia (Polisi na Magereza/chuo cha mafunzo).
  3. Mahakama za ngazi zote hadi rufaa kila nchi iwe na za kwake isipokuwa mahakama ya juu itakayokuwa kwenye shirikisho.
  4. Kila nchi mwanachama aruhusiwe kushiriki biashara na mahusiano na jumuia za kimataifa bila kuingiliwa na mwanachama mwenzake. Hii ikiwa ni pamoja na tafiti, biashara, na kukopa nje ya nchi bila kuingiliwa na mwenzake. Serikali ya shirikisho itakuwa na jukumu la kuratibu tu kupitia taasisi ya fedha ya shirikisho na wizara ya mambo ya nchi za nje.

Mawazo mazuri sana haya ndugu,hasa hapo kwenye wizara hizo 3 zenye mawaziri 6(Mawazir na Manaibu) zatosha kabisa! Lakin wabunge inabid wapungue wafikie 10 Tanganyika 6 Zanzibar 4 hawa ndo wataenda kujadili yale mambo 7 ya Muungano. Na kwa mfumo huu hakutakuwa na garama za kuendesha serikali,ni mawazo tu lakini!
 
Back
Top Bottom