Serikali ya mseto tanzania?

Kadogoo

JF-Expert Member
Feb 26, 2007
2,073
341
Kwanza nachukua nafasi hii kumpongeza mheshimiwa jakaya mrisho kikwete na chama chake kwa kushinda uchaguzi pamoja na kuwa na kasoro za hapa na pale ambazo ningeshangaa sana kama zingekosekana maana hata marekani na uingereza chaguzi zao hazikosi kasoro!

Pili namuomba slaa na chama chake wakubali matokeo na kuwaheshimu wa tz waliomchagua kikwete na ccm na kuweka kando ushabiki wa kisiasa kwa manufaa ya taifa letu!

Tatu, nakushauri rais wetu uweke u-ccm nyuma na unda serikali inayojumuisha wapinzani ikiwa katiba yetu inaruhusu ili kujenga umoja wa kitaifa na kuchochea maendeleo!

Mwisho, ili kudhibiti matumizi ya serikali nakushauri uunde serikali yenye wizara kama hizi:

1 waziri mkuu
2 wizara ya mambo ya nje na jumuia ya ea
3 wizara ya fedha na uchumi
4 wizara ya ulinzi
5 wizara ya sheria na katiba (futa wizara ya mambo ya ndani)
6 wizara ya elimu
7 wizara ya kilimo,uvuvi na mifugo
8 wizara ya afya na mazingira
9 mali asili na utalii (hii inajumuisha na madini)
10 wanawake na watoto

ama kuhusu wizara ya michezo, utamaduni, habari nk. Naona hakuna haja za kuziundia wizara bali unaweza kuziweka zikawa chini ya wizara zingine! Halafu ikulu inayo msemaji wake sasa kuna haja gani ya kuwa na waziri wa habari? Ni mzigo kwa wananchi kuwa wizara nyingi ambazo hazina tija kwa taifa!!!!
 
Back
Top Bottom