Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Ni jambo unaloweza kulitizama kwa mashaka na wepesi. Lakini kutokana na upepo wa kisiasa ulivyo hili si jambo la kushangaza kwani linaweza kutokea. Harakati za CDM zinaweza kufikia hatua ya kuundwa kwa serikali ya mseto katika chaguzi za usoni zijazo.
Bora hili litokee mapema ili kuleta chachu ya kuchochea maendeleo ya nchi hii. Naamini wale wanachama wa CDM wanaweza kuliona jambo hili kama upuuzi.
Hata kwa upande wa wale wa CCM wanaweza kuchukulia kuwa ni jambo gumu kwao. Lakini linaweza kutokea kutokana na nguvu na misigino ya kisiasa. Bora serikali ya mseto itokee kwanza kuliko CCM kuendelea kubaki madarakani milele.
CCM yenye watendaji wachache waadilifu inaweza kuwa na changamoto motomoto iwapo itaongezewa nguvu na watendaji kutoka CDM katika mseto. Hii inaweza kuwa tiba, au nusu tiba kwa Tanzania inayougua.
Bora hili litokee mapema ili kuleta chachu ya kuchochea maendeleo ya nchi hii. Naamini wale wanachama wa CDM wanaweza kuliona jambo hili kama upuuzi.
Hata kwa upande wa wale wa CCM wanaweza kuchukulia kuwa ni jambo gumu kwao. Lakini linaweza kutokea kutokana na nguvu na misigino ya kisiasa. Bora serikali ya mseto itokee kwanza kuliko CCM kuendelea kubaki madarakani milele.
CCM yenye watendaji wachache waadilifu inaweza kuwa na changamoto motomoto iwapo itaongezewa nguvu na watendaji kutoka CDM katika mseto. Hii inaweza kuwa tiba, au nusu tiba kwa Tanzania inayougua.