Serikali ya Magufuli ni amani, utulivu, ulinzi na Maendeleo (Peace, Stability, Security and Development)

AUGUSTINO CHIWINGA

JF-Expert Member
Apr 23, 2017
220
689
Hapana shaka kwamba ili Taifa letu liendelee na kufikia uchumi wa kati, linahitaji sana Amani utulivu na Usalama ili watu waweze kuchapa kazi na kulipa kodi na kuleta maendeleo.

Lakini tunao Watanzania wenzetu wanaopenda tukose mambo hayo manne kwa ajili ya manufaa ya mabebebru wanaowatuma pamoja na wao binafsi. Ndio maana siku zote Rais wetu anajitahidi katika kiuhuburi Umoja, Upendo na Amani kwa sababu anajua hatua ardhi nyingine tunayoweza kuiita nchi iwapo tutaivuruga amani hii iliyopo.

Pasipo na Amani hapana maji, hapana umeme, hapana chakula hapana maenedeleo.Wachochezi hao wanatumia miatandao ya kijamii kuvumisha taarifa za uongo zenye ghiliba chuki wakiwa na malengo ya kuhamasisha wananchi kuichukia Serikali.

Wachochezi wa uvunjivu wa amani wakae wakitambua kwamba Watanzania tunasimama imara na Rais wetu katika kupigania amani utulivu, usalama, na maendeleo ilitufikie uchumi wakati.

AUGUSTINO CHIWINGA
065943889.
MUNGU MBARIKI RAIS MAGUFULI MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Back
Top Bottom