Serikali ya Magufuli kutoza VAT kwenye "on transit goods" ni aibu na fedheha!

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,874
Kuna vitu vingine mtu au watu kuvifanya ni lazima wajiulize mara mbilimbili na kutafakari kwa kina madhara yake.

Serikali tukufu ya rais John Magufuli kwa mwaka wa fedha ulioanzia July moja, ilianza kutoza VAT kwa "on transit goods" mizigo ambayo inatoka bandarini eidha ya Dar es Salaam ama nyingine za hapa nchini kupitia ardhi ya Tanzania kwenda nchi jirani hasa za Congo (DRC) na Zambia. Hii bila kumung'unya maneno ni jambo lisilo sahihi kabisa!

Mzigo unakotoka (kule kiwandani) umelipiwa tayari VAT na wenzetu wakienda kuuza nchini mwao wanalipa VAT, sasa wewe Tanzania unataka VAT kwa biashara gani uliyofanya?

Isitoshe jambo hilo limetokomezea mbali uhusiano mzuri wa kibiashara baina ya Tanzania na mataifa hayo, mambo sasa yanaenda ndivyo sivyo. Mimi kama mdau wa Maendeleo ya nchi napinga utozaji holela wa VAT usiofuata tararibu za kikodi hivyo napingana na mipango ya waziri Mpango juu ya VAT.

Tusipoiangalia hii VAT tunayotoza kiholela tutajikuta tukiwapa mzigo mkubwa watu wengi huku tukiishia kupoteza fursa muhimu.

Rai yangu ni kuwa swala la ulipaji VAT lishughulikiwe kwa umakini na serikali isione kama ni sehemu ya kupatia ahueni bila kufuata taratibu za kodi.

Niliwahi kutoa maoni humu kuwa sasa serikali ya Magufuli iwe na "sites" maalum za kukusanyia VAT. Kuwa na EFD nyingi zilizozagaa mtaani siyo suluhisho la ukusanyaji mapato bali nyingi ni zile zinazoumiza nakuzorotesha biashara pamoja na maisha ya kila siku.
 
Mfalme J. in the making.

Kuna makubaliano ya kikodi yanaitwa double taxation agreements. Ikiwa nchi mbili zikikubaliana kuwa nchi moja itoze kodi kwa kutumia "Origin Principle", basi nchi nyingine isitoze kodi. AU,

Ikiwa zikakubaliana kutumia "destination principle", basi kodi itatozwa kule bidhaa inakokwenda na haitatozwa kule inakotoka, au itatozwa kwa kutafuta tofauti ya kodi iliyotozwa kwenye origin (ilikotoka) na ile itakayotozwa kwenye destination (inakokwenda).

Kinyume na hapo, kutakuwa na double taxation.

Washauri wa Rais Mpooo??????
 
Kuna vitu vingine mtu au watu kuvifanya ni lazima wajiulize mara mbilimbili na kutafakari kwa kina madhara yake.

Serikali tukufu ya rais John Magufuli kwa mwaka wa fedha ulioanzia July moja, ilianza kutoza VAT kwa "on transit goods" mizigo ambayo inatoka bandarini eidha ya Dar es Salaam ama nyingine za hapa nchini kupitia ardhi ya Tanzania kwenda nchi jirani hasa za Congo (DRC) na Zambia. Hii bila kumung'unya maneno ni jambo lisilo sahihi kabisa!

Mzigo unakotoka (kule kiwandani) umelipiwa tayari VAT na wenzetu wakienda kuuza nchini mwao wanalipa VAT, sasa wewe Tanzania unataka VAT kwa biashara gani uliyofanya?

Isitoshe jambo hilo limetokomezea mbali uhusiano mzuri wa kibiashara baina ya Tanzania na mataifa hayo, mambo sasa yanaenda ndivyo sivyo. Mimi kama mdau wa Maendeleo ya nchi napinga utozaji holela wa VAT usiofuata tararibu za kikodi hivyo napingana na mipango ya waziri Mpango juu ya VAT.

Tusipoiangalia hii VAT tunayotoza kiholela tutajikuta tukiwapa mzigo mkubwa watu wengi huku tukiishia kupoteza fursa muhimu.

Rai yangu ni kuwa swala la ulipaji VAT lishughulikiwe kwa umakini na serikali isione kama ni sehemu ya kupatia ahueni bila kufuata taratibu za kodi.

Niliwahi kutoa maoni humu kuwa sasa serikali ya Magufuli iwe na "sites" maalum za kukusanyia VAT. Kuwa na EFD nyingi zilizozagaa mtaani siyo suluhisho la ukusanyaji mapato bali nyingi ni zile zinazoumiza nakuzorotesha biashara pamoja na maisha ya kila siku.

UPOTOSHAJI. Nosense and Rubish!

Kinachotakiwa kulipiwa VAT ni Mapato yanayotozwa hapa nchini kwa huduma zinazotolewa kwa mizigo hiyo na si mizigo yenyewe.

Watanzania tulipe kodi tuacha uzushi wa visingizio ili tusilipe kodi.
 
UPOTOSHAJI. Nosense and Rubish!

Kinachotakiwa kulipiwa VAT ni Mapato yanayotozwa hapa nchini kwa huduma zinazotolewa kwa mizigo hiyo na si mizigo yenyewe.

Watanzania tulipe kodi tuacha uzushi wa visingizio ili tusilipe kodi.

Kuna watu wanatumiwa na wafanyabiashara ili kuipotosha jamii. Lipeni kodi hizo on transit zinapita hewani? si ndo hizo zinaharibu mpaka barabara zetu
 
Kuna vitu vingine mtu au watu kuvifanya ni lazima wajiulize mara mbilimbili na kutafakari kwa kina madhara yake.

Serikali tukufu ya rais John Magufuli kwa mwaka wa fedha ulioanzia July moja, ilianza kutoza VAT kwa "on transit goods" mizigo ambayo inatoka bandarini eidha ya Dar es Salaam ama nyingine za hapa nchini kupitia ardhi ya Tanzania kwenda nchi jirani hasa za Congo (DRC) na Zambia. Hii bila kumung'unya maneno ni jambo lisilo sahihi kabisa!

Mzigo unakotoka (kule kiwandani) umelipiwa tayari VAT na wenzetu wakienda kuuza nchini mwao wanalipa VAT, sasa wewe Tanzania unataka VAT kwa biashara gani uliyofanya?

Isitoshe jambo hilo limetokomezea mbali uhusiano mzuri wa kibiashara baina ya Tanzania na mataifa hayo, mambo sasa yanaenda ndivyo sivyo. Mimi kama mdau wa Maendeleo ya nchi napinga utozaji holela wa VAT usiofuata tararibu za kikodi hivyo napingana na mipango ya waziri Mpango juu ya VAT.

Tusipoiangalia hii VAT tunayotoza kiholela tutajikuta tukiwapa mzigo mkubwa watu wengi huku tukiishia kupoteza fursa muhimu.

Rai yangu ni kuwa swala la ulipaji VAT lishughulikiwe kwa umakini na serikali isione kama ni sehemu ya kupatia ahueni bila kufuata taratibu za kodi.

Niliwahi kutoa maoni humu kuwa sasa serikali ya Magufuli iwe na "sites" maalum za kukusanyia VAT. Kuwa na EFD nyingi zilizozagaa mtaani siyo suluhisho la ukusanyaji mapato bali nyingi ni zile zinazoumiza nakuzorotesha biashara pamoja na maisha ya kila siku.
Mizigo ya Transit ilikukwa haitozwi kodi yoyote ile lakini wasafirishaji walitumia mwanya huo kudanganya. Kwa mfano gari la mafuta ya petroli ambalo linapaswa kwenda DRC lakini linaishia chalinze na makaratasi hupigwa muhuri kana kwamba lile gari lilivuka mpaka wa nchi kwenda huko. matokeo ya matumizi mabaya ya namna hii ndiyo maana mizigo hiyo inalipishwa VAT na wakisha wakilisha mizigo hiyo nje ya nchi hurejeshewa hizo pesa walizolipa kama VAT.
Kilichokuwepo hivi sasa ni kampeni za wenye magari makubwa wakitaka huruma ya jamii ili waendelee kutuhujumu.
HAYA NI MATOKEO YA KUTOFANYA BIASHARA KIUADILIFU- muwe wapole na mlipe tu hiyo hela halafu muombe refund kama sheria inavyosema.
 
Kwa kukusaidia, VAT imeanza kutozwa tokea Julai 2015.

Kwa nini wanaanza kulalamika sasa kuhusu VAT wakati sheria ilikuwepo kuanzia mwaka 2015?

Serikali ya Rais Magufuli inachofanya ni kusimamia kwa ukamilifu sheria ambayo imeanza mwaka mmoja uliopita.

Kwa kukusaidia zaidi, VAT is charged on all ancillary transit cargo handling services like wharfage, stuffing, handling charges, stevedoring, agency fee, stripping etc.

Kikubwa zaidi, VAT waliyolipa huwa wanarudishiwa wakifika mipakani. Hawa wanaopiga kelele kuhusu VAT inawezekana ni wale walikuwa wanadanganya kama mizigo wanaipeleka nje wakati sivyo.

Fanya kwanza utafiti kabla ya kuja na thread isiyo na ukweli.
 
Hivi hiyo VAT si inakuwa refunded mzigo ukifika border ?


Huu utaratibu hutumiwa Dunia nzima, hata watu wa Balozi kwa mfano ambao huwa hawalipi, VAT nchi nyingine hutoza VAT kwa madiplomat halafu huenda TRA ya kwao na kurudishiwa hiyo fedha, hili linawezekana kabisa ndiyo linalofanyika ili kuondoa wizi uliokuwa unafanyika kwamba mzigo unaingizwa kama transit haulipiwi kodi lkn unaishia mitaani, sasa inawezekana kabisa wakishalipa wakati wanavuka boda hii fedha wanarudishiwa!

Tatizo sisi Wabongo tunajifanya watalaamu wa kila kitu!
 
Hivi hakuna control nyingine ktk kuangalia haya magari ya transit yamepita au la ili kuondoa hii VAT kwao kwa sababu naona ni usumbufu tu
 
UPOTOSHAJI. Nosense and Rubish!

Kinachotakiwa kulipiwa VAT ni Mapato yanayotozwa hapa nchini kwa huduma zinazotolewa kwa mizigo hiyo na si mizigo yenyewe.

Watanzania tulipe kodi tuacha uzushi wa visingizio ili tusilipe kodi.


Kwani mkuu sasa ukitoza kodi na wao si wataongeza gharama ya huduma?
 
ni utaratibu wa kawaida tu sema wanaotoa hii miongozi huwa wanapresume kuwa tuko kwenye vichwa vyao hivyo tunajua kinachoendelea. shame on them.
 
Mizigo ya Transit ilikukwa haitozwi kodi yoyote ile lakini wasafirishaji walitumia mwanya huo kudanganya. Kwa mfano gari la mafuta ya petroli ambalo linapaswa kwenda DRC lakini linaishia chalinze na makaratasi hupigwa muhuri kana kwamba lile gari lilivuka mpaka wa nchi kwenda huko. matokeo ya matumizi mabaya ya namna hii ndiyo maana mizigo hiyo inalipishwa VAT na wakisha wakilisha mizigo hiyo nje ya nchi hurejeshewa hizo pesa walizolipa kama VAT.
Kilichokuwepo hivi sasa ni kampeni za wenye magari makubwa wakitaka huruma ya jamii ili waendelee kutuhujumu.
HAYA NI MATOKEO YA KUTOFANYA BIASHARA KIUADILIFU- muwe wapole na mlipe tu hiyo hela halafu muombe refund kama sheria inavyosema.


Mkuu hapa sijakuelewa kwa mfano nimebeba mzigo wa 100 milioni kwa maana hiyo nitatakiwa nilipe kwanza 18 milioni halafu nikishafikisha nirudishiwe?
 
Wewe ulieandika mada hii inabidi ushitakiwe kwa kupotosha jamii, kinachotozwa kodi siyo MZIGO bali ni HUDUMA zitolewazo wakati wa kupokea mzigo huo. Fanyeni research na siyo kupotosha jamii.
Kama ujaelewa narudia ni huduma zitolewazo na siyo mzigo wa transit.
 
UPOTOSHAJI. Nosense and Rubish!

Kinachotakiwa kulipiwa VAT ni Mapato yanayotozwa hapa nchini kwa huduma zinazotolewa kwa mizigo hiyo na si mizigo yenyewe.

Watanzania tulipe kodi tuacha uzushi wa visingizio ili tusilipe kodi.

I wish i could get details zaidi kabla sija comment. Lazima nikiri kuwa i am pro JPM lakini hili kidogo limeniacha hoi. Nimesikia kwenye Power Breakfast Clouds Radio na impression niliyopata si nzuri. Wanatoza VAT kwenye nini hasa?

Kwa maelezo yako mkuu, nahisi (sina uhakika) kwa mfano, mwenye mzigo akimlipa msafirishaji kiasi fulani cha pesa kupeleka mzigo labda Congo DRC, basi huyo msafirishaji ndiyo analipa hiyo VAT kutokana na kipato chake.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom