Mmexico
JF-Expert Member
- Nov 1, 2016
- 369
- 328
Vitendo vya kifisadi vimechangia kwa kiasi kibubwa kuharibu taswira ya hii nchi na kuirudisha nyuma kimaendeleo. Vimeichafua hii nchi kuliko hata kina Lissu inasemekana wanaichafua. Uzalendo namba moja kwa Mwananchi wa Tanzania ni kuchukia ufisadi na mafisadi.
Dokta Slaa enzi hizo CHADEMA wakiwa CHADEMA aliwahi kusema, ''Tatizo kubwa kuliko yote nchi hii sio CCM, wala Sio Elimu, wala Sio Magonjwa. Tatizo kubwa na linayoimaliza Tanzania ni Ufisadi na ndio maana wao wamejipanga kupambana nao mpaka pumzi ya mwisho"
Limekuwa ni jambo la kawaida sana kwa Wezi wa mali za umma nchi hii, kufunguliwa kesi na kutoka kilahisi kabisa tena kwa jeuli zote. Kesi zao wakiwa nje huunguruma lakini siku ya hukumu jambo moja huwa linajulikana ni kuwa watatoka nje na kuwa huru.
Matajiri wengi waliopata mali kwa wizi hutumia:
I.MIANYA YA SHERIA ZETU MBOVU (walizotunga wenyewe) Eg Kina Chenge jeur yao ipo hapa.
II. Nguvu ya fedha zao kutoa RUSHWA kwa Majaji na maofisa wa serikali kuharibu upelelezi na hata mlolongo wa Kesi nzima. Refer kesi ya Iddi Simbaa au ile Madabida na ARV feki.
III. Silaha yao nyingine huwa ni KUPATA MAWAIKILI BINAFSI WENYE UWEZO WA JUU KUWATETEA. Refer Kesi ya Mohamed Kirua na Lukuvi juzi juzi.
IV.Kesi zao kuwa na mkono wa RAIS ambaye ana kinga ya kutoshtakiwa Eg Mramba kesi na hata Jeuri ya EL kusema kama yye fisadi kwenye Richmond basi afunguliwe kesi mahakamani akijua fika walishirikiana na rafiki yake JK.
KWA KUONA HILO MAGUFULI na serikali yake wamekuja kivingine, Wao ni mwendo wa kukufungulia kesi nyingi nyingi ikiwamo ya uhujumu uchumi wakijua fika huwezi kupata dhamana. Then jarada la kesi yako litazungushwa kwa miaka kadhaa na mwisho wa siku utafutiwa Kesi yako/zenu na kuachiliwa huru.
Siku chache mbele utafunguliwa mashtaka mapya na cycle ya usumbufu huku wewe ukiwa ndani unaendelea mpaka ipite miaka kadhaa.
Kwa mbinu hizo Mafisadi na hela zao zote wanajikuta wapo ndani, mbinu zao zote wanazotegemea kuwachomoa zinaishia huko na zinakuwa hazifanyi kazi. Option itakayobaki ni either kurudisha mali ya umma kwa namna flani au uende na maji.
Kuna mtu mmoja aliwahi kusema, Sheria zimeundwa kuwafunga maskini, lakini zama hizi tunaona mengine kabisa.
Dokta Slaa enzi hizo CHADEMA wakiwa CHADEMA aliwahi kusema, ''Tatizo kubwa kuliko yote nchi hii sio CCM, wala Sio Elimu, wala Sio Magonjwa. Tatizo kubwa na linayoimaliza Tanzania ni Ufisadi na ndio maana wao wamejipanga kupambana nao mpaka pumzi ya mwisho"
Limekuwa ni jambo la kawaida sana kwa Wezi wa mali za umma nchi hii, kufunguliwa kesi na kutoka kilahisi kabisa tena kwa jeuli zote. Kesi zao wakiwa nje huunguruma lakini siku ya hukumu jambo moja huwa linajulikana ni kuwa watatoka nje na kuwa huru.
Matajiri wengi waliopata mali kwa wizi hutumia:
I.MIANYA YA SHERIA ZETU MBOVU (walizotunga wenyewe) Eg Kina Chenge jeur yao ipo hapa.
II. Nguvu ya fedha zao kutoa RUSHWA kwa Majaji na maofisa wa serikali kuharibu upelelezi na hata mlolongo wa Kesi nzima. Refer kesi ya Iddi Simbaa au ile Madabida na ARV feki.
III. Silaha yao nyingine huwa ni KUPATA MAWAIKILI BINAFSI WENYE UWEZO WA JUU KUWATETEA. Refer Kesi ya Mohamed Kirua na Lukuvi juzi juzi.
IV.Kesi zao kuwa na mkono wa RAIS ambaye ana kinga ya kutoshtakiwa Eg Mramba kesi na hata Jeuri ya EL kusema kama yye fisadi kwenye Richmond basi afunguliwe kesi mahakamani akijua fika walishirikiana na rafiki yake JK.
KWA KUONA HILO MAGUFULI na serikali yake wamekuja kivingine, Wao ni mwendo wa kukufungulia kesi nyingi nyingi ikiwamo ya uhujumu uchumi wakijua fika huwezi kupata dhamana. Then jarada la kesi yako litazungushwa kwa miaka kadhaa na mwisho wa siku utafutiwa Kesi yako/zenu na kuachiliwa huru.
Siku chache mbele utafunguliwa mashtaka mapya na cycle ya usumbufu huku wewe ukiwa ndani unaendelea mpaka ipite miaka kadhaa.
Kwa mbinu hizo Mafisadi na hela zao zote wanajikuta wapo ndani, mbinu zao zote wanazotegemea kuwachomoa zinaishia huko na zinakuwa hazifanyi kazi. Option itakayobaki ni either kurudisha mali ya umma kwa namna flani au uende na maji.
Kuna mtu mmoja aliwahi kusema, Sheria zimeundwa kuwafunga maskini, lakini zama hizi tunaona mengine kabisa.