Serikali ya Libya yajitokeza Kusaidia Athari Za Mafuriko Kilosa kuwajengea Nyumba 200

Ng'wanza Madaso

JF-Expert Member
Oct 21, 2008
2,268
333
Ndugu zanguni wana JF nilikuwa ninaperuzi kwa Michuzi nimekutana na habari hii Serikali ya Libya yajitokeza kusaidia Athari za mafiriko kilosa kuwa itawajengea nyumba 200 waathirika zenye thamani ya shilingi 1.5 bilioni.

Nikajiuliza serikali hii iliyosaidiwa imegharimika kumjengea mtu mmoja (Gavana) nyumba yenye thamani ya nyumba 200 ambazo wangejengewa watu wa kilosa lakini Serikali hii hii imeshindwa kuwajengea hawa waathirika na kuomba msaada. Je kama waliweza kumjengea Gavana nyumba yenye thamani hiyo imekuwaje wameshindwa kuwajengea hawa waathirika?

=====
Jamhuri ya watu wa Libya imetoa msaada wa vifaa mbalimbali kwa wahanga wa mafuriko ya Kilosa mkoani Morogoro. ikiwa ni pamoja na kuwajengea nyumba 200 zenye thamani ya shilingi bilioni 1.5.

Akiongea na wanahabari katika uwanja wa ndege Dar es Salaam Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Uratibu na Bunge) Mheshimiwa Philip Marmo alisema msaada huo umekuja wakati muafaka kwani hali ya wahanga hao si ya kuridhisha

Aidha Waziri Marmo alizitaka nchi rafiki,Jumuiya za Kimataifa pamoja na Watanzania kwa ujumla kutoa misaada kwa hiari yao kwa kadri wanavyoguswa kwa wahanga wa mafuriko ya Kilosa.

“Uwezo wa Serikali ni mdogo na hauwezi kutosheleza kila kitu hivyo tunaomba Jumuiya mabalimbali za Kimataifa na Watanzania Kushirikiana katika kutoa misaada”.Alisema.

Pia alizitaka Kamati za maafa husika kutekeleza wajibu wao kwa kufikisha misaada hiyo kwa wahusika na alimhakikishia balozi wa Libya nchini Ahmed Abdusalaam Al Ashaab ambaye alikabidhi msaada huo kwa niaba ya nchi yake kuwa itawafikia walengwa na magari yataanza kupeleka misaada hiyo kesho.

Akikabidhi msaada huo balozi wa Libya nchini bwana Ahmed Abdulsalaam Al Ashaab alisema msaada huo umetolewa na jumuiya mbalimbali nchini humo kutokana na ushirikiano uliopo kati ya Tanzania na Libya.

Vifaa vilivyotolewa ni magaro 1100, Blanketi 400, Mahema 1300, Mito 1200, Maboksi 500 ya madawa ikiwa ni pamoja na vifaa vya huduma ya kwanza.


Source: Michuzi Blog

Soma


 
Ndugu zanguni wana JF nilikuwa ninaperuzi kwa Michuzi nimekutana na habari hii Serikali ya Libya yajitokeza kusaidia Athari za mafiriko kilosa kuwa itawajengea nyumba 200 waathirika zenye thamani ya shilingi 1.5 bilioni.

Nikajiuliza serikali hii iliyosaidiwa imegharimika kumjengea mtu mmoja (Gavana) nyumba yenye thamani ya nyumba 200 ambazo wangejengewa watu wa kilosa lakini Serikali hii hii imeshindwa kuwajengea hawa waathirika na kuomba msaada. Je kama waliweza kumjengea Gavana nyumba yenye thamani hiyo imekuwaje wameshindwa kuwajengea hawa waathirika?

Soma hapa http://issamichuzi.blogspot.com/2010/01/serikali-ya-libya-yajitokeza-kusaidia.html#comments

Hawa si binadamu, wana mikono ya damu
Ni walafi sina hamu, wastahili kali hukumu
Tumuachie kaumu, yeye ataamua yao dumu!
 
I know this is irrelevant, lakini ni vyema kulisema hili ili tusije tukawaacha baadhi ya watu wasiotaka kujua gravity ya vitu wanavyoviona kwa nje bila kujua undani wake. Agenda ya Muamar al Qud'dhafi ni kueneza Uislamu ili baadae kuanzisha dola ya Kisilamu ulimwenguni, na nashawishika hii ni mojawapo ya strategy, na tumeshaona sarakasi za namna hii nyingi ktk siku za karibuni. Uzuri tu hatujafikia hatua ya kulazimishana kwa upanga, ila maandalizi twayaona. Tuombee Mungu yote iwe kheri bila shari.
 
Kwanza tujiulize Libya imeanza lini urafiki na Tanzania!!!!, au baada ya Nyerere kufariki ndipo Libya inajitokeza tokeza je, ni kwa mazuri au kwa lengo gani!!!? TUJIULIZE!!!!
 
Ndugu Mpendanchi, kwani ule msikiti ulioko Musoma kijijini kwa Nyerere si umefadhiliwa na Gaddafi? Tena wakati huo Nyerere bado alikuwa hai.

Sasa kusaidia hizo nyumba imekuwa kuna ajenda ya siri?

Najaribu tu kutafakari jinsi tulivo ndumilakuwili
 
Kusaidiwa sio tatizo ila ni kwa mazingir yapi,maana tusijikute tunabanwa na utumwa mamboleo.
 
I know this is irrelevant, lakini ni vyema kulisema hili ili tusije tukawaacha baadhi ya watu wasiotaka kujua gravity ya vitu wanavyoviona kwa nje bila kujua undani wake. Agenda ya Muamar al Qud'dhafi ni kueneza Uislamu ili baadae kuanzisha dola ya Kisilamu ulimwenguni, na nashawishika hii ni mojawapo ya strategy, na tumeshaona sarakasi za namna hii nyingi ktk siku za karibuni. Uzuri tu hatujafikia hatua ya kulazimishana kwa upanga, ila maandalizi twayaona. Tuombee Mungu yote iwe kheri bila shari.

Jamani kuna mambo ya ajabu,lakini pia yapo ya kushangaza. Hii post yako inanishangaza? Hivi yale mafuriko yalibagua huyu Muislam na huyu Muanglikana au huyu hafuati dini yoyote? mm!chuki hufunika busara.

Unaonaje endapo taasisi rasmi za kidini kama Vatican na nyinginezo zingetoa misaada hiyo,suala la kueneza Uislamu lingekuwepo?

Binadamu yeyote anayepatwa na matatizo ni muhimu wenzake wakamsaidia. Je,umechangia kiasi gani ili kuwanusuru na Uislamu ambao kwako inaonekana ni nongwa kubwa?
 
Nakubaliana na wasemao hatukuwa na haja ya kuanza kutembeza bakuli la kujenga nyumba 200 kule kilosa wakati tuna uwezo wa kujenga nyumba 1 kwa mtu 1 yenye gharama sawia...Ila napatwa na ukakasi na kichefu chefu kwa wenzangu wanaoangalia msaada wa Libya km mtego wa kueneza dini....huo ni mtazamo finyu...Matonya anapotembeza bakuli lake hachagui ni muislamu au mkristo au hta huyo mchangiaji ana malengo gani ya kiimani kwa msaada anaopewa...la muhimu kwake msaada umepatikana na hako ni ka ugonjwa na nina wasiwasi Nchi yetu inayotimiza nusu karne tokea kupata uhuru imeanza kuugua...Kama hadithi ya Matonya, usishangae kuona na kesho yake tena yupo barabarani bila aibu yeyote hata km jana alipata pesa nyingi na akazitumia kuhonga wanawake au kulewa pombe....
 
Jamani kuna mambo ya ajabu,lakini pia yapo ya kushangaza. Hii post yako inanishangaza? Hivi yale mafuriko yalibagua huyu Muislam na huyu Muanglikana au huyu hafuati dini yoyote? mm!chuki hufunika busara.
Unaonaje endapo taasisi rasmi za kidini kama Vatican na nyinginezo zingetoa misaada hiyo,suala la kueneza Uislamu lingekuwepo?
Binadamu yeyote anayepatwa na matatizo ni muhimu wenzake wakamsaidia. Je,umechangia kiasi gani ili kuwanusuru na Uislamu ambao kwako inaonekana ni nongwa kubwa?

Labda nikuulize..ati na wewe ni Great Thinker?? Hivi uliielewa post yangu au basi tu ili mradi uongeze post JF??
 
I know this is irrelevant, lakini ni vyema kulisema hili ili tusije tukawaacha baadhi ya watu wasiotaka kujua gravity ya vitu wanavyoviona kwa nje bila kujua undani wake. Agenda ya Muamar al Qud'dhafi ni kueneza Uislamu ili baadae kuanzisha dola ya Kisilamu ulimwenguni, na nashawishika hii ni mojawapo ya strategy, na tumeshaona sarakasi za namna hii nyingi ktk siku za karibuni. Uzuri tu hatujafikia hatua ya kulazimishana kwa upanga, ila maandalizi twayaona. Tuombee Mungu yote iwe kheri bila shari.
Kweli umeshasema wewe mwenyewe ni Irrelevant. Last year Gaddaf alikuwa Italy kwenye ziara yake ndefu nchini humo na nchi kadhaa. Huko alienda kueneza hiyo dini? Abdulhalim mbona unaota dini kila siku? Mie nadhani kila nchi inatafuta trading partner maana km unazalisha unahitaji kuwa na soko. Na kadiri siku zinavyoenda Afrika ndio linaonekana kuwa soko linalokuwa kwa nguvu.
 
Nashauri waangalie aina za nyumba zinazoweza kumudu mafuriko. Nyumba za asili katika sehemu kama hizi zilijengwa kwenye milingoti. Hizo za matofali ya kuchoma zinaweza zikawa adha badala ya heri. Kumbuka New Orleans yaliyowapata pamoja na nyumba zao kuwa za kisasa! Wakiwapelekea prefabs. watakuwa hawajafanya kitu.

Amandla........
 
Tatizo ni serikali ya Chama Cha Majambazi kusahau wajibu wake wa kujenga makazi bora kwa raia wake.
 
jamani, ifike hatua tuwe reasonable, mimi naamini msaada ni msaada tu hata kama umetoka wapi, kwani kuna tatizo gani tukisaidiwa na Gaddafi?mbona Obama amesaidia ktk janga la Haiti na mpo kimya?kunani Great Thinkers?Au kuna watu duniani ndio wana haki ya kusaidia wenzao panapokua na maafa kama hayo ya Kilosa?
 
Serikali kazi yake si kujenga bali ni kuwawezesha wananchi waweze kujenga nyumba bora. Wakati fulani nadhani watu wanavyotoa commens zao wanakuwa usingizini.
 
Kweli umeshasema wewe mwenyewe ni Irrelevant. Last year Gaddaf alikuwa Italy kwenye ziara yake ndefu nchini humo na nchi kadhaa. Huko alienda kueneza hiyo dini. Abdulhalim mbona unaota dini kila siku? Mie nadhani kila nchi inatafuta trading partner maana km unazalisha unahitaji kuwa na soko. Na kadiri siku zinavyoenda Afrika ndio linaonekana kuwa soko linalokuwa kwa nguvu.

Nafuu wewe umeliona hili la kueneza dini. Maana wengine hawalioni hili na watakataa katakata hata kwa mjeledi hawatalikubali. Kwenye post yangu sijakataa watu kusaidiwa wanapokuwa na shida au wanapoletewa uchaguzi wa dini 'mpya' au vinginevyo, ndio maana nikamalizia na post yangu kuwa tuombe hizi sarakasi zote ziishie kwa kheri. Ila historia haiendani na hii dua yangu, na ukweli kwamba maazimio ya baadhi ya dini ya kutawala dunia is simply beyond dictatorship & fascism combined.
 
Nafuu wewe umeliona hili la kueneza dini. Maana wengine hawalioni hili na watakataa katakata hata kwa mjeledi hawatalikubali. Kwenye post yangu sijakataa watu kusaidiwa wanapokuwa na shida au wanapoletewa uchaguzi wa dini 'mpya' au vinginevyo, ndio maana nikamalizia na post yangu kuwa tuombe hizi sarakasi zote ziishie kwa kheri. Ila historia haiendani na hii dua yangu, na ukweli kwamba maazimio ya baadhi ya dini ya kutawala dunia is simply beyond dictorship.
Duh narekebisha post yangu. Kumbe unaweza kukosea kitu kidogo ukawa quoted wrong. Hakueneza dini bali aliizungumzia dini yake km unakumbukumbu vizuri. Weka alama ya kuuliza pls
 
Back
Top Bottom