Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,463
- 39,929
(Makala hii imetoka Tanzania Daima Feb 17, 2010)
NILIWAHI kuandika huko nyuma juu ya uhuru wa mahakama zetu. Somo hili bado halijawaingia wanasiasa wetu hususan wale waliokaa kwenye kiti cha madaraka.
Baada ya uongozi wa CCM kufanikiwa kuliingilia Bunge na kuligeuza kuwa "baraza la washauri wa serikali" naanza kuona kile ambacho nilikihofia miaka karibu mitatu iliyopita; kwamba CCM itajiinua kwa kiburi dhidi ya mahakama na mahakama zetu zitanyang'anywa uhuru wake.
Tukikubali kwamba serikali isitii uamuzi halali wa mahakama kwa kisingizio cha "kukosa muda" na kusema kuwa ni "suala nyeti" basi tutaruhusu jambo la hatari sana kwa demokrasia yetu.
Ndugu zangu, utawala wa demokrasia mojawapo ya misingi yake mikubwa zaidi ni uhuru wa mahakama. Kitendo cha Mbunge wa Mbulu ambaye pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge), Phillip Marmo, kumjibu Jaji Mkuu na kupingana naye wazi ni kitendo cha hatari na kinachotakiwa kulaaniwa na kila Mtanzania kwani tukikubali hata kwenye usingizi tutakuwa tumewapa watawala wetu nguvu wasizokuwa nazo.
Nazungumzia nini? Mahakama ya Rufani ya Tanzania imeanza kusikiliza rufaa ya serikali kupinga uamuzi wa Mahakama Kuu ambao uliruhusu wagombea binafsi katika kesi iliyoletwa na Mchungaji Christoper Mtikila. Rufaa hiyo imekuja baada ya Mchungaji Mtikila kushinda mara mbili sasa kwenye mahakama zetu ambapo mara hizo zote mahakama zimekubali kuwa kulazimisha Mtanzania kugombea nafasi ya uongozi kwa kupitia chama cha siasa ni kinyume na Katiba.
Ni kutokana na hilo katika hukumu yao ya mwisho kwenye suala hili Mahakama Kuu iliamua kuwa hukumu ya awali ya Lugakingira (mwaka 1995) inaruhusu wagombea huru na wao (mwaka 2006) waliona zaidi ya kusema kuwa wagombea huru wanaruhusiwa tu (kama alivyofanya Jaji Lugakingira) bali pia ilitoa amri kwa serikali kuhakikisha kuwa inaandaa mpango na utaratibu wa jinsi gani wagombea huru watashiriki uchaguzi mkuu ujao (yaani wa 2010).
Sasa, serikali ikakusudia kukata rufaa kupinga uamuzi huo wa Mahakama Kuu. Aliyekuwa Mwanasheria Mkuu, Johnson Mwanyika, ndiye aliyetekeleza maagizo ya viongozi wa kisiasa kukata rufaa.
Sababu kubwa ya watawala kukataa wagombea binafsi ni kuwa "Tanzania haiko tayari kuwa na wagombea binafsi" na pia hawawaamini Watanzania kuwa wanaweza kumchagua mtu anayewafaa bila kuangalia chama chake.
Hata hivyo ukweli ni kuwa endapo wagombea binafsi wataruhusiwa Chama cha Mapinduzi ndicho kitakachopoteza sana kwani hadi hivi sasa kinaendeleza itikadi ya uongo kuwa wabunge huchaguliwa kuwakilisha "chama" na siyo wananchi!
Ukweli ni kuwa tayari wananchi (wenye vyama na wasiyo na vyama) wamekuwa wakipiga kura kuchagua viongozi wao kwa miaka nenda rudi na ni wananchi hao hao ambao leo hii wanajikuta wanalazimishwa kuchagua viongozi ambao lazima wawe wamepitishwa na vyama vyao kugombea na hivyo Watanzania wengine ambao wanapenda kuwatumia wananchi wenzao lakini hawataki kuwa vibaraka wa vyama hivyo wanakatwa kugombea kwa sababu CCM haitaki wagombee kama watu binafsi!
Lakini zaidi wanachohofia ni uwezekano wa wana CCM ambao wataona kuwa hawawezi kusimama kugombea kwa sababu chama chao kimewaengua kwenye kura za maoni lakini wana CCM hao hawako tayari kujiunga na chama kingine cha upinzani lakini wanakubalika katika majimbo yao; sasa kwa nini hawa wasiruhusiwe kugombea kama watu binafsi na yule anayekubalika (aliye na chama au la) ndiye achaguliwe?
Nyerere aliunga mkono wagombea binafsi
Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere aliunga mkono suala la wagombea binafsi waziwazi na pasipo kujiuma maneno. Katika hotuba yake (ambayo kila Mtanzania anapaswa kuisoma) aliyoitoa pale Uwanja wa Sokoine mwaka 1995 (kwenye siku kuu ya Mei Mosi) Nyerere alisema kuwa serikali haiwezi kufuta haki ya mwananchi kiholela hivyo.
Aliwakumbusha CCM kuwa wagombea binafsi ni haki ya msingi na inawezekana kufanyika tena Tanzania kwani tayari Tanzania imewahi kuruhusu huko nyuma. Nyerere alikumbushia jinsi TANU ilivyosimamisha mgombea asiyekubalika kule Mbulu (jimbo la Marmo!) lakini mgombea aliyekuwa akikubalika Chief Sarwatt akaenguliwa lakini akaruhusiwa kugombea kama mgombea huru. Chief Sarwatt alishinda!! Hoja ya Mwalimu ilikuwa nyepesi tu kuwa hatuwezi kuwanyima wananchi haki ya kumchagua kiongozi wanayemtaka hata kama kiongozi huyo hayumo ndani ya chama cha siasa.
Uamuzi wa Mahakama Kuu hata hivyo ulijikita zaidi katika hoja za Kikatiba. Mara zote mbili (uamuzi wa Lugakingira na uamuzi wa kina Manento) Mahakama Kuu imeshindwa kushawishika kuwa mabadiliko ya kulazimisha mgombea kuwa na chama hayakiuki haki za msingi za Kikatiba.
Jaji Lugakingira alipompa ushindi Mtikila na kurejesha timamu katika demokrasia yetu alitangaza hivi katika hukumu yake ile maarufu (ambayo natabiri itaendelea kusimama hata katika rufaa ya sasa)
"It shall be lawful for independent candidates along with candidates sponsored by political parties to contest, presidential, parliament and local council elections." Yaani, "itaruhusiwa kisheria kuwepo kwa wagombea huru pamoja na wale watakaosimamishwa na vyama vya siasa kugombea katika uchaguzi wa rais, Bunge, na serikali za mitaa".
Uamuzi wa kina Manento hata hivyo ulienda mbele zaidi; uliamua hivi:
"We shall also declare in the present case that in principle it shall be lawful for private candidates to contest for the posts of President and Member of Parliament along with candidates nominated by political parties. However unlike the learned late judge we will not just leave it at that. Exercising our powers under any other relief as prayed in the petition and cognizant of the fact that a vacuum might give birth to chaos and political pandemonium we shall proceed to order that (the government) between now and the next general elections, put in place, a legislative mechanism that will regulate the activities of private candidates. So as to let the will of the people prevail as to whether or not such candidates are suitable."
Yaani, "na sisi tunatangaza katika kesi hii kuwa kimsingi itaruhusiwa kwa wagombea binafsi kugombea nafasi za Urais na Ubunge pamoja na wagombea watakaosimamishwa na vyama. Hata hivyo, zaidi ya uamuzi wa Jaji Lugakingira sisi hatutaishia hapo tu.
Tukitumia madaraka yetu ya kutoa nafuu kama tulivyoombwa na tukizingatia kuwa tunaweza kuacha kuwe na ombwe ambalo laweza kusababisha vurugu na mgongano wa kisiasa tunatoa amri kwa (serikali) kati ya sasa na uchaguzi mkuu ujao kuweka utaratibu wa kisheria wa kusimamia wagombea binafsi. Wananchi ndio wataamua kama wagombea binafsi wanakubalika au la."
Ni kutokana na uamuzi huo hapo juu serikali ikaamua kukata rufaa. Tukumbuke kuwa uamuzi huo wa mahakama kuu ulichukuliwa Mei 2006. Hii ina maana kuwa serikali imekuwa na miaka karibu minne ya kuandaa utaratibu wa kisheria wa kuandaa sheria na namna wagombea binafsi wataweza kushiriki pasipo kuweka vikwazo ambavyo vitafanya wagombea hao kuwa na mzigo mkubwa kuliko ule wa wagombea wa vyama.
Rufaa hiyo ya serikali ndiyo imeanza kusikilizwa na kama tunavyojua ilipotajwa kwa mara ya kwanza Jaji Mkuu na majaji wengine sita wameamua kuisikiliza kutokana na uzito wake. Jaji Mkuu hata hivyo alifanya kitu ambacho ndicho hasa kinanifanya niamini kuwa CCM hawako tayari kutii Mahakama zetu na watafanya wanaloweza kuzidunisha mbele ya wananchi.
Jaji Augustino Ramadhani alisema hivi kumkumbusha Naibu Mwanasheria Mkuu: "Hata hivyo, ili kuondoa utata wowote tunapenda kumkumbusha Naibu Mwanasheria Mkuu na timu yake kuwa kukata rufaa haina maana uamuzi unaokatiwa rufaa umesitishwa mara moja. Hivyo, sheria ilivyo sasa na kuelekea kwenye uchaguzi mkuu Oktoba ni kile ambacho Mahakama Kuu imeshaamua yaani wagombea huru wanaruhusiwa".
Ni kutokana na kauli hiyo ya Mahakama ya Rufani Waziri Marmo akaona kuwa mahakama ni ya kupuuzia; na amefanya hivyo bila kusahihishwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali wala na Rais. Kwa maneno mengine, Rais Kikwete, Baraza lake la Mawaziri na Mwanasheria Mkuu wote wameamua kutotii uamuzi wa Mahakama Kuu! Yaani, kwao wako juu ya sheria!
Marmo (Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia mambo ya taratibu za Bunge vile vile) alinukuliwa kusema kuwa "suala hili bado ni gumu sana na hata mahakama ikiamua hivyo, haitawezekana kwa sasa maana mpaka wananchi waulizwe kama watakubaliana na jambo hilo na liwekwe kwenye Katiba... Mtu akiachiwa nchi bila ushauri wa kikundi ni hatari sana."
Kauli hiyo ya Marmo na ambayo hadi hivi sasa naamini ndiyo kauli ya serikali kimsingi imemjibu Jaji Mkuu (mahakama yetu) kuwa haijalishi mahakama itaamua nini na itaagiza nini, msimamo wa serikali ni kuwa wagombea binafsi hawaruhusiwi mwaka huu.
Hii si mara ya kwanza
Endapo serikali itakataa kutekeleza uamuzi wa mahakama kama ilivyokwishaamriwa haitakuwa mara ya kwanza kufanya hivyo. Kwa wale wanaokumbuka mojawapo ya kesi ambazo zimezungusha sana taifa letu ni ile ya Valambhia ambayo serikali ilijaribu hata kubadilisha sheria ili isitekeleze agizo la mahakama.
Ndugu zangu, sasa hivi demokrasia yetu iko matatani na endapo kucha za watawala wetu zitakitwa kwenye migongo ya mahakama zetu basi ule uhuru kidogo tulionao ndiyo utakuwa umefikia mwisho. Endapo kina Marmo watakubaliwa wasitii mahakama zetu na waziwazi kuipinga mahakama katika kesi iliyoko mahakamani naamini ni ukosefu mkubwa wa nidhamu na kutokujua mipaka iliyopo.
Ndiyo maana natoa wito kwamba Watanzania wapuuzie kauli ya Marmo kwani ni kauli ya kipuuzi (namaanisha hilo). Ni ya kipuuzi kwa sababu kwanza tayari uamuzi wa mahakama kuu ulitolewa miaka minne iliyopita na walipewa nafasi ya kutosha kufanya mabadiliko ya sheria kuruhusu wagombea huru na walikuwa na nafasi ya kufanyia majaribio taratibu hizo katika chaguzi ndogo mbalimbali zilizofanyika miaka minne iliyopita.
Lakini hawakufanya hivyo kwa sababu hawakutaka kutii mahakama. Pili, ni ya kipuuzi kwa sababu tuna ushahidi wa kutosha wa serikali kufanyia mabadiliko sheria mbalimbali na mambo mengine makubwa ndani ya muda mfupi tu. Leo hii wameshakubaliana kuunda serikali ya mseto na tayari wameandaa kura ya maoni Zanzibar na tayari tunajua kuwa hilo litafanyika mwaka huu huu!
Lakini zaidi ni ya kipuuzi kwa sababu Marmo kama mtu wa Mbulu anajua kuwa Chifu Sarwatt ambaye jina lake linadumu kule Mbulu aligombea kama mgombea binafsi na akashinda na akachaguliwa hata kuwa Spika wa Bunge la Jumuiya ya Afrika ya Mashariki!
Sasa kama tulikuwa na utaratibu wa kumruhusu mgombea binafsi miaka ya sitini na akashiriki na kushinda na tukaheshimu uamuzi huo leo hii ni mwaka 2010 halafu watu wanaofikiriwa wako timamu wanadai eti haiwezekani!
Mahakama isikubali idharauliwe
Ni matarajio yangu kuwa kikao cha Mahakama ya Rufani kitakapokaa tena kuendelea na kesi hii mwezi Aprili kitachukua msimamo wa wazi kuiasa serikali kuwa kama imeshadhamiria kutotekeleza uamuzi wa mahakama hiyo kama ilivyosemwa na Marmo waseme wazi ili kesi iondolewe. Mahakama ya Rufani isikubali kuendelea na kesi ambayo maamuzi yake tayari yameshakataliwa na yule anayetakiwa kutekeleza na hasa tukizingatia kuwa wao ndiyo mahakama ya mwisho nchini mwetu!
Kama Mahakama ya Rufani itatoa uamuzi ambao unakataliwa kutekelezwa na chombo chenye nguvu kuna maana gani kutoa uamuzi huo isipokuwa Mahakama ya Rufani sasa naamini inalazimishwa mambo mawili; kwanza kutoruhusu wagombea binafsi na pili kuongeza muda ili uamuzi wowote usitekelezwe kwenye uchaguzi huu wa mwaka huu.
Lakini Mahakama ya Rufani itawezaje kuwa huru endapo wanasiasa tayari wameshaamua ni nini wangependa mahakama hiyo iamue? Tunaweza vipi kukimbilia Mahakama ya Rufani endapo pale maslahi ya CCM yanapoguswa basi watawala wanaweza kuamua kutoyatekeleza bila kujali kitakachokuwa?
Mimi naamini ni lazima utokee mgongano ambao ni muhimu kwa kukomaa kwa demokrasia. Karibu mahali pote duniani ambapo viongozi wa kisiasa wameshambulia mahakama wamejikuta wakishindwa.
Mfano mzuri zaidi ni kile kilichojaribiwa kule Pakistan wakati wa Gen. Musharraf pale alipoamua kumvua madaraka Jaji Mkuu na kusababisha maandamano ambayo yalichangia kuanguka kwake; hata kule Uganda kina Museveni walipojaribu kuingilia uhuru wa Mahakama wakajikuta kwenye matatizo ya kutosha tu! Tanzania tusikubali kina Marmo na viongozi wenzake wa CCM watunyang'anye mahakama yetu kama walivyofanya kwa Bunge.
Na kubwa zaidi ni kuwa Mahakama ya Rufani ni lazima itume ujumbe wa wazi, wa makusudi na usio na utata kuwa endapo uamuzi wake unakataliwa kabla haujatolewa au unapuuzwa baada ya kutolewa basi Mahakama nzima ya Rufani itajiuzulu hadi serikali itoe kauli isiyo na utata kuwa uamuzi wowote wa Mahakama ya Rufani utazingatiwa na kutekelezwa. Kuna wakati ambapo watu huyumba; na kuna wakati watu huchukua msimamo. Huu ndio wakati kama huo.
NILIWAHI kuandika huko nyuma juu ya uhuru wa mahakama zetu. Somo hili bado halijawaingia wanasiasa wetu hususan wale waliokaa kwenye kiti cha madaraka.
Baada ya uongozi wa CCM kufanikiwa kuliingilia Bunge na kuligeuza kuwa "baraza la washauri wa serikali" naanza kuona kile ambacho nilikihofia miaka karibu mitatu iliyopita; kwamba CCM itajiinua kwa kiburi dhidi ya mahakama na mahakama zetu zitanyang'anywa uhuru wake.
Tukikubali kwamba serikali isitii uamuzi halali wa mahakama kwa kisingizio cha "kukosa muda" na kusema kuwa ni "suala nyeti" basi tutaruhusu jambo la hatari sana kwa demokrasia yetu.
Ndugu zangu, utawala wa demokrasia mojawapo ya misingi yake mikubwa zaidi ni uhuru wa mahakama. Kitendo cha Mbunge wa Mbulu ambaye pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge), Phillip Marmo, kumjibu Jaji Mkuu na kupingana naye wazi ni kitendo cha hatari na kinachotakiwa kulaaniwa na kila Mtanzania kwani tukikubali hata kwenye usingizi tutakuwa tumewapa watawala wetu nguvu wasizokuwa nazo.
Nazungumzia nini? Mahakama ya Rufani ya Tanzania imeanza kusikiliza rufaa ya serikali kupinga uamuzi wa Mahakama Kuu ambao uliruhusu wagombea binafsi katika kesi iliyoletwa na Mchungaji Christoper Mtikila. Rufaa hiyo imekuja baada ya Mchungaji Mtikila kushinda mara mbili sasa kwenye mahakama zetu ambapo mara hizo zote mahakama zimekubali kuwa kulazimisha Mtanzania kugombea nafasi ya uongozi kwa kupitia chama cha siasa ni kinyume na Katiba.
Ni kutokana na hilo katika hukumu yao ya mwisho kwenye suala hili Mahakama Kuu iliamua kuwa hukumu ya awali ya Lugakingira (mwaka 1995) inaruhusu wagombea huru na wao (mwaka 2006) waliona zaidi ya kusema kuwa wagombea huru wanaruhusiwa tu (kama alivyofanya Jaji Lugakingira) bali pia ilitoa amri kwa serikali kuhakikisha kuwa inaandaa mpango na utaratibu wa jinsi gani wagombea huru watashiriki uchaguzi mkuu ujao (yaani wa 2010).
Sasa, serikali ikakusudia kukata rufaa kupinga uamuzi huo wa Mahakama Kuu. Aliyekuwa Mwanasheria Mkuu, Johnson Mwanyika, ndiye aliyetekeleza maagizo ya viongozi wa kisiasa kukata rufaa.
Sababu kubwa ya watawala kukataa wagombea binafsi ni kuwa "Tanzania haiko tayari kuwa na wagombea binafsi" na pia hawawaamini Watanzania kuwa wanaweza kumchagua mtu anayewafaa bila kuangalia chama chake.
Hata hivyo ukweli ni kuwa endapo wagombea binafsi wataruhusiwa Chama cha Mapinduzi ndicho kitakachopoteza sana kwani hadi hivi sasa kinaendeleza itikadi ya uongo kuwa wabunge huchaguliwa kuwakilisha "chama" na siyo wananchi!
Ukweli ni kuwa tayari wananchi (wenye vyama na wasiyo na vyama) wamekuwa wakipiga kura kuchagua viongozi wao kwa miaka nenda rudi na ni wananchi hao hao ambao leo hii wanajikuta wanalazimishwa kuchagua viongozi ambao lazima wawe wamepitishwa na vyama vyao kugombea na hivyo Watanzania wengine ambao wanapenda kuwatumia wananchi wenzao lakini hawataki kuwa vibaraka wa vyama hivyo wanakatwa kugombea kwa sababu CCM haitaki wagombee kama watu binafsi!
Lakini zaidi wanachohofia ni uwezekano wa wana CCM ambao wataona kuwa hawawezi kusimama kugombea kwa sababu chama chao kimewaengua kwenye kura za maoni lakini wana CCM hao hawako tayari kujiunga na chama kingine cha upinzani lakini wanakubalika katika majimbo yao; sasa kwa nini hawa wasiruhusiwe kugombea kama watu binafsi na yule anayekubalika (aliye na chama au la) ndiye achaguliwe?
Nyerere aliunga mkono wagombea binafsi
Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere aliunga mkono suala la wagombea binafsi waziwazi na pasipo kujiuma maneno. Katika hotuba yake (ambayo kila Mtanzania anapaswa kuisoma) aliyoitoa pale Uwanja wa Sokoine mwaka 1995 (kwenye siku kuu ya Mei Mosi) Nyerere alisema kuwa serikali haiwezi kufuta haki ya mwananchi kiholela hivyo.
Aliwakumbusha CCM kuwa wagombea binafsi ni haki ya msingi na inawezekana kufanyika tena Tanzania kwani tayari Tanzania imewahi kuruhusu huko nyuma. Nyerere alikumbushia jinsi TANU ilivyosimamisha mgombea asiyekubalika kule Mbulu (jimbo la Marmo!) lakini mgombea aliyekuwa akikubalika Chief Sarwatt akaenguliwa lakini akaruhusiwa kugombea kama mgombea huru. Chief Sarwatt alishinda!! Hoja ya Mwalimu ilikuwa nyepesi tu kuwa hatuwezi kuwanyima wananchi haki ya kumchagua kiongozi wanayemtaka hata kama kiongozi huyo hayumo ndani ya chama cha siasa.
Uamuzi wa Mahakama Kuu hata hivyo ulijikita zaidi katika hoja za Kikatiba. Mara zote mbili (uamuzi wa Lugakingira na uamuzi wa kina Manento) Mahakama Kuu imeshindwa kushawishika kuwa mabadiliko ya kulazimisha mgombea kuwa na chama hayakiuki haki za msingi za Kikatiba.
Jaji Lugakingira alipompa ushindi Mtikila na kurejesha timamu katika demokrasia yetu alitangaza hivi katika hukumu yake ile maarufu (ambayo natabiri itaendelea kusimama hata katika rufaa ya sasa)
"It shall be lawful for independent candidates along with candidates sponsored by political parties to contest, presidential, parliament and local council elections." Yaani, "itaruhusiwa kisheria kuwepo kwa wagombea huru pamoja na wale watakaosimamishwa na vyama vya siasa kugombea katika uchaguzi wa rais, Bunge, na serikali za mitaa".
Uamuzi wa kina Manento hata hivyo ulienda mbele zaidi; uliamua hivi:
"We shall also declare in the present case that in principle it shall be lawful for private candidates to contest for the posts of President and Member of Parliament along with candidates nominated by political parties. However unlike the learned late judge we will not just leave it at that. Exercising our powers under any other relief as prayed in the petition and cognizant of the fact that a vacuum might give birth to chaos and political pandemonium we shall proceed to order that (the government) between now and the next general elections, put in place, a legislative mechanism that will regulate the activities of private candidates. So as to let the will of the people prevail as to whether or not such candidates are suitable."
Yaani, "na sisi tunatangaza katika kesi hii kuwa kimsingi itaruhusiwa kwa wagombea binafsi kugombea nafasi za Urais na Ubunge pamoja na wagombea watakaosimamishwa na vyama. Hata hivyo, zaidi ya uamuzi wa Jaji Lugakingira sisi hatutaishia hapo tu.
Tukitumia madaraka yetu ya kutoa nafuu kama tulivyoombwa na tukizingatia kuwa tunaweza kuacha kuwe na ombwe ambalo laweza kusababisha vurugu na mgongano wa kisiasa tunatoa amri kwa (serikali) kati ya sasa na uchaguzi mkuu ujao kuweka utaratibu wa kisheria wa kusimamia wagombea binafsi. Wananchi ndio wataamua kama wagombea binafsi wanakubalika au la."
Ni kutokana na uamuzi huo hapo juu serikali ikaamua kukata rufaa. Tukumbuke kuwa uamuzi huo wa mahakama kuu ulichukuliwa Mei 2006. Hii ina maana kuwa serikali imekuwa na miaka karibu minne ya kuandaa utaratibu wa kisheria wa kuandaa sheria na namna wagombea binafsi wataweza kushiriki pasipo kuweka vikwazo ambavyo vitafanya wagombea hao kuwa na mzigo mkubwa kuliko ule wa wagombea wa vyama.
Rufaa hiyo ya serikali ndiyo imeanza kusikilizwa na kama tunavyojua ilipotajwa kwa mara ya kwanza Jaji Mkuu na majaji wengine sita wameamua kuisikiliza kutokana na uzito wake. Jaji Mkuu hata hivyo alifanya kitu ambacho ndicho hasa kinanifanya niamini kuwa CCM hawako tayari kutii Mahakama zetu na watafanya wanaloweza kuzidunisha mbele ya wananchi.
Jaji Augustino Ramadhani alisema hivi kumkumbusha Naibu Mwanasheria Mkuu: "Hata hivyo, ili kuondoa utata wowote tunapenda kumkumbusha Naibu Mwanasheria Mkuu na timu yake kuwa kukata rufaa haina maana uamuzi unaokatiwa rufaa umesitishwa mara moja. Hivyo, sheria ilivyo sasa na kuelekea kwenye uchaguzi mkuu Oktoba ni kile ambacho Mahakama Kuu imeshaamua yaani wagombea huru wanaruhusiwa".
Ni kutokana na kauli hiyo ya Mahakama ya Rufani Waziri Marmo akaona kuwa mahakama ni ya kupuuzia; na amefanya hivyo bila kusahihishwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali wala na Rais. Kwa maneno mengine, Rais Kikwete, Baraza lake la Mawaziri na Mwanasheria Mkuu wote wameamua kutotii uamuzi wa Mahakama Kuu! Yaani, kwao wako juu ya sheria!
Marmo (Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia mambo ya taratibu za Bunge vile vile) alinukuliwa kusema kuwa "suala hili bado ni gumu sana na hata mahakama ikiamua hivyo, haitawezekana kwa sasa maana mpaka wananchi waulizwe kama watakubaliana na jambo hilo na liwekwe kwenye Katiba... Mtu akiachiwa nchi bila ushauri wa kikundi ni hatari sana."
Kauli hiyo ya Marmo na ambayo hadi hivi sasa naamini ndiyo kauli ya serikali kimsingi imemjibu Jaji Mkuu (mahakama yetu) kuwa haijalishi mahakama itaamua nini na itaagiza nini, msimamo wa serikali ni kuwa wagombea binafsi hawaruhusiwi mwaka huu.
Hii si mara ya kwanza
Endapo serikali itakataa kutekeleza uamuzi wa mahakama kama ilivyokwishaamriwa haitakuwa mara ya kwanza kufanya hivyo. Kwa wale wanaokumbuka mojawapo ya kesi ambazo zimezungusha sana taifa letu ni ile ya Valambhia ambayo serikali ilijaribu hata kubadilisha sheria ili isitekeleze agizo la mahakama.
Ndugu zangu, sasa hivi demokrasia yetu iko matatani na endapo kucha za watawala wetu zitakitwa kwenye migongo ya mahakama zetu basi ule uhuru kidogo tulionao ndiyo utakuwa umefikia mwisho. Endapo kina Marmo watakubaliwa wasitii mahakama zetu na waziwazi kuipinga mahakama katika kesi iliyoko mahakamani naamini ni ukosefu mkubwa wa nidhamu na kutokujua mipaka iliyopo.
Ndiyo maana natoa wito kwamba Watanzania wapuuzie kauli ya Marmo kwani ni kauli ya kipuuzi (namaanisha hilo). Ni ya kipuuzi kwa sababu kwanza tayari uamuzi wa mahakama kuu ulitolewa miaka minne iliyopita na walipewa nafasi ya kutosha kufanya mabadiliko ya sheria kuruhusu wagombea huru na walikuwa na nafasi ya kufanyia majaribio taratibu hizo katika chaguzi ndogo mbalimbali zilizofanyika miaka minne iliyopita.
Lakini hawakufanya hivyo kwa sababu hawakutaka kutii mahakama. Pili, ni ya kipuuzi kwa sababu tuna ushahidi wa kutosha wa serikali kufanyia mabadiliko sheria mbalimbali na mambo mengine makubwa ndani ya muda mfupi tu. Leo hii wameshakubaliana kuunda serikali ya mseto na tayari wameandaa kura ya maoni Zanzibar na tayari tunajua kuwa hilo litafanyika mwaka huu huu!
Lakini zaidi ni ya kipuuzi kwa sababu Marmo kama mtu wa Mbulu anajua kuwa Chifu Sarwatt ambaye jina lake linadumu kule Mbulu aligombea kama mgombea binafsi na akashinda na akachaguliwa hata kuwa Spika wa Bunge la Jumuiya ya Afrika ya Mashariki!
Sasa kama tulikuwa na utaratibu wa kumruhusu mgombea binafsi miaka ya sitini na akashiriki na kushinda na tukaheshimu uamuzi huo leo hii ni mwaka 2010 halafu watu wanaofikiriwa wako timamu wanadai eti haiwezekani!
Mahakama isikubali idharauliwe
Ni matarajio yangu kuwa kikao cha Mahakama ya Rufani kitakapokaa tena kuendelea na kesi hii mwezi Aprili kitachukua msimamo wa wazi kuiasa serikali kuwa kama imeshadhamiria kutotekeleza uamuzi wa mahakama hiyo kama ilivyosemwa na Marmo waseme wazi ili kesi iondolewe. Mahakama ya Rufani isikubali kuendelea na kesi ambayo maamuzi yake tayari yameshakataliwa na yule anayetakiwa kutekeleza na hasa tukizingatia kuwa wao ndiyo mahakama ya mwisho nchini mwetu!
Kama Mahakama ya Rufani itatoa uamuzi ambao unakataliwa kutekelezwa na chombo chenye nguvu kuna maana gani kutoa uamuzi huo isipokuwa Mahakama ya Rufani sasa naamini inalazimishwa mambo mawili; kwanza kutoruhusu wagombea binafsi na pili kuongeza muda ili uamuzi wowote usitekelezwe kwenye uchaguzi huu wa mwaka huu.
Lakini Mahakama ya Rufani itawezaje kuwa huru endapo wanasiasa tayari wameshaamua ni nini wangependa mahakama hiyo iamue? Tunaweza vipi kukimbilia Mahakama ya Rufani endapo pale maslahi ya CCM yanapoguswa basi watawala wanaweza kuamua kutoyatekeleza bila kujali kitakachokuwa?
Mimi naamini ni lazima utokee mgongano ambao ni muhimu kwa kukomaa kwa demokrasia. Karibu mahali pote duniani ambapo viongozi wa kisiasa wameshambulia mahakama wamejikuta wakishindwa.
Mfano mzuri zaidi ni kile kilichojaribiwa kule Pakistan wakati wa Gen. Musharraf pale alipoamua kumvua madaraka Jaji Mkuu na kusababisha maandamano ambayo yalichangia kuanguka kwake; hata kule Uganda kina Museveni walipojaribu kuingilia uhuru wa Mahakama wakajikuta kwenye matatizo ya kutosha tu! Tanzania tusikubali kina Marmo na viongozi wenzake wa CCM watunyang'anye mahakama yetu kama walivyofanya kwa Bunge.
Na kubwa zaidi ni kuwa Mahakama ya Rufani ni lazima itume ujumbe wa wazi, wa makusudi na usio na utata kuwa endapo uamuzi wake unakataliwa kabla haujatolewa au unapuuzwa baada ya kutolewa basi Mahakama nzima ya Rufani itajiuzulu hadi serikali itoe kauli isiyo na utata kuwa uamuzi wowote wa Mahakama ya Rufani utazingatiwa na kutekelezwa. Kuna wakati ambapo watu huyumba; na kuna wakati watu huchukua msimamo. Huu ndio wakati kama huo.