Serikali ya Kikwete ni dhaifu kupita zote duniani

ibange

JF-Expert Member
Dec 31, 2010
1,543
550
serikali ya jk imeonyesha udhaifu mkubwa katika mambo mengi. lakini hili la loliondo limevunja record. hakuna serikali yoyote duniani inayoweza kuruhusu watu watumie dawa bila ku prove usalama wa dawa hiyo. hapa swala la imani halipo so long as watu wanakunywa dawa. ingekuwa kuombewa ndio ingekuwa imani. je ikigundulika baadae ina madhara watakufa watu milioni ngapi? je, mbona wasimpime mtu aliyepona na wakatoa taarifa rasmi? je, nchi inaweza kuishi kwa rumours tu? serikali makini ingechukua hatua muafaka
http://www.google.com
 
serikali ya jk imeonyesha udhaifu mkubwa katika mambo mengi. lakini hili la loliondo limevunja record. hakuna serikali yoyote duniani inayoweza kuruhusu watu watumie dawa bila ku prove usalama wa dawa hiyo. hapa swala la imani halipo so long as watu wanakunywa dawa. ingekuwa kuombewa ndio ingekuwa imani. je ikigundulika baadae ina madhara watakufa watu milioni ngapi? je, mbona wasimpime mtu aliyepona na wakatoa taarifa rasmi? je, nchi inaweza kuishi kwa rumours tu? serikali makini ingechukua hatua muafaka
Google

I guess there is apoint here!!! serikali makini haiwezi kuruhusu kitu ambacho ni kinyume cha SHERIA. As long as imani inaingilia sheria ya nchi, basi sheria ya nchi ina-prevail over the other. Suppose dawa ya babu inaperpertuate cancer after 10 years, who will be to blame.
ILA SIJUI KAMA SERIKALI YA JK NDIO DHAIFU KULIKO ZOTE DUNIANI
 
Kemikali za kupimia hao waliotibiwa zitatoka wapi. Uwezo huo upo? Watu walishagundua kwamba nchi hii haina kitu. Ni kwa sababu hiyo kipimo chao ni kupona. Yanayokuja baadae kwa Mtanzania si muhimu.
Ipo siku taifa zima litaangamia kwa sababu hizi hizi. Mkemia mkuu tunaye, lakini hebu kumbuka yale maji yenye mercury kule Mara majibu ya mkemia mkuu yalitolewa hadi leo? Kama sina hakika imepita miaka mitatu. Mercury inavipimo vyake vinavyojulikana duniani lakini kutoa majibu imechukua miaka mitatu.
Kwa staili hii majibu ya madhara ya dawa ya babu wa Loliondo itachukua karne ngapi? Rafiki yangu sidhani kama unaifahamu Tanzania. Nchi hii ipo katika lindi la usingizi. Watu weke wamezama katika mashimo yaliyochini ya vilindi vya bahari je wataiona lini ile nuru?
Acha kufikiri kama vile upo magharibi, hapa siyo. Nchi yetu ni hakuna, hakuna, hakuna kabisa.
 
Kemikali za kupimia hao waliotibiwa zitatoka wapi. Uwezo huo upo? Watu walishagundua kwamba nchi hii haina kitu. Ni kwa sababu hiyo kipimo chao ni kupona. Yanayokuja baadae kwa Mtanzania si muhimu.
Ipo siku taifa zima litaangamia kwa sababu hizi hizi. Mkemia mkuu tunaye, lakini hebu kumbuka yale maji yenye mercury kule Mara majibu ya mkemia mkuu yalitolewa hadi leo? Kama sina hakika imepita miaka mitatu. Mercury inavipimo vyake vinavyojulikana duniani lakini kutoa majibu imechukua miaka mitatu.
Kwa staili hii majibu ya madhara ya dawa ya babu wa Loliondo itachukua karne ngapi? Rafiki yangu sidhani kama unaifahamu Tanzania. Nchi hii ipo katika lindi la usingizi. Watu weke wamezama katika mashimo yaliyochini ya vilindi vya bahari je wataiona lini ile nuru?
Acha kufikiri kama vile upo magharibi, hapa siyo. Nchi yetu ni hakuna, hakuna, hakuna kabisa.

Ndugu, kwa maoni yangu una hoja ila si kwa kuwa serikali imechelewa/zembea kuchunguza dawa ya Babu bali kwa kuwa serikali yetu always inazembea kwenye mambo ya msingi yakiwamo yale yanayogusa afya za wananchi moja kwa moja. Wewe unakuwa na hofu na dawa ya Babu kwamba inaweza kuleta madhara baada ya miaka kadhaa; sawa inawezekana lakini madhara hayo, kama yatakuwepo ni madogo mno kulinganisha na madhara mengine mengi ambayo wananchi WOTE (na siyo wagonjwa wachache tu kama ilivyo kwa Babu) tunayapata katika maisha yetu ya kila siku bila serikali yetu kujishughulisha. Hebu fikiria mifano michache ifuatayo:-

(i) Vyakula - nyama ya kuku wa kisasa:- Hivi unajua aina ya vyakula ambavyo kuku wa kisasa wanalishwa? Inadaiwa baadhi ya wafugaji wamefikia hata hatua ya kuwalisha ARVs, vidonge vya uzazi, na madawa mengine mengi ambayo yana madhara makubwa kwa binadamu. Je, ulishawahi kusikia serikali yetu angalau ikijishughulisha kufanya uchunguzi wa nyama ya kuku inayoingia sokoni? Ni maelfu ya watanzania wangapi wanaotumia nyama ya kuku kila siku?

(ii) Vyakuala - Maziwa ya ng'ombe:- Hivi unajua baadhi ya wafugaji hawafuati masharti pindi ng'ombe wanapokuwa kwenye dozi? Serikali imewahi kujishughulisha kufuatilia ubora wa maziwa yanayoingia sokoni kila siku?

(iii) Vyakula - Samaki:- Ni wazi kuwa baadhi ya wavuvi hutumia sumu kwenye uvuvi wao na hata usafirishaji na uhifadhi wa samaki haukidhi viwango. Je, serikali inajishughulisha kwa hilo?

(iv) Vyakula - Nguruwe:- Kama ilivyo kwa nyama ya kuku, je, ni maelfu ya watanzania wangapi wanakula nguruwe ambao hawana ubora kiafya? Serikali inajali?

(vi) Vyakula - nafaka:- Hivi unajua mbolea na madawa ya kilimo yakitumiwa bila kuzingatia viwango athari zake zinabaki hata kwenye vyakula vitokanavyo na mazao hayo - tena hapo ndio kansa imelala; fikiria DDT, n.k; Je serikali inajali kupima,kwa mfano unga unaosagwa pale Manzese na maharage yanayouzwa pale Tandale na kwingineko kama yana ubora kiafya?

(v) Mfumo wa maisha - moshi wa magari:- Serikali yetu inajali kuhakikisha kwa mfano uchafuzi wa anga hauzidi viwango vianvyotakiwa? Moshi wa magari ni kansa tupu ile!

(vi) Madawa ya binadamu:- Serikali inao udhibiti inavyotakiwa kwamba madawa yanayotumika nchini yana viwango vinavyotakiwa na yanatumika kama inavyotakiwa na kwa wakati?

(vii) Vyakula vya viwandani:- Serikali inadhibiti kikamilifu vyakula vinavyozalishwa viwandani na je wananchi wanazingatia matumizi yake inavyostahili? Expiry dates, n.k. Hapo pia kansa imelala.

(viii) Mifumo ya maisha - ulevi:- Serikali inadhibiti mifumo mbali mbali ya maisha kwa wananchi wake hasa kwenye suala la ulevi? Fikiria ni watu wangapi wamepata kansa kutokana na ulevi ikiwapo matumizi ya gongo, sigara, n.k.

(ix) ... n.k., ... n.k. orodha ingeweza kuwa ndefu kadiri uanvyotaka.

Kwa wenzetu Ulaya huwezi ukazalisha mavitu yako huko halafu ukalisha wananchi bila ukaguzi na udhibiti wa serikali makini. Labda ndio maana wenzetu hata "life expectancy" zao ni zaidi ya 80! Hapa kwetu nasikia tuko 46!

Hivyo, msururu unaoonekana kwa Babu, kwa sehemu kubwa, ni matokeo ya kupuuzia hayo yaliyoorodheshwa hapo juu. Vinginevyo, tatizo lisengekuwa kubwa kama linavyoonekana hivyo pengine Babu leo hii asingekuwa na kazi ya kufanya. Kwa ufupi athari za dawa ya Babu, kama zitakuwepo, ni ndogo mno kulinganisha na athari tunazokutana nazo kwenye maisha yetu ya kila siku. Kitaalamu tungeweza kusema ni "negligible".

Tafakari na chukua hatua!
 
unamaana waliokunywa wote wanaweza kusepa kwa sir GOD kwa wakati mmoja?
Na nina uhakika hakuna atakayejiuzulu ati.
 
Kutokana na hoja tajwa hapo juu, ipo wazi kuwa serikali yetu ni dhaifu kuliko serikali zote duniani.
 
serikali ya jk imeonyesha udhaifu mkubwa katika mambo mengi. lakini hili la loliondo limevunja record. hakuna serikali yoyote duniani inayoweza kuruhusu watu watumie dawa bila ku prove usalama wa dawa hiyo. hapa swala la imani halipo so long as watu wanakunywa dawa. ingekuwa kuombewa ndio ingekuwa imani. je ikigundulika baadae ina madhara watakufa watu milioni ngapi? je, mbona wasimpime mtu aliyepona na wakatoa taarifa rasmi? je, nchi inaweza kuishi kwa rumours tu? serikali makini ingechukua hatua muafaka
Google
Mkuu.
Ujumbe umefika ila nafikiri kichwa cha habari cha mada yako hakikukaa sawa.
Kwa kawaida serikali dhaifu huanguka, huondoshwa kirahisi sana.
sasa hii ya JK au serikali ya CCM si dhaifu.

Usahihi ni kuwa utendaji wa serikali ni mbovu una mapungufu mengi..lakini serikali yenyewe si dhaifu. wanatenda walitakalo bila kupingwa. kwa hiyo wayafanyayo si kwa bahati mbaya..ndio style yao ya kuongoza..kama tunaweza kusema huko ndio kuongoza.

Wananchi wa TZ ndio dhaifu kupita wananchi wa nchi yoyote duniani.Ungesema hivi basi tungekubaliana 100% kwa mia.
 
Mimi nafikiri wewe ndiye mdhaifu kuliko wote duniani kwa kigezo changu mimi kama ulivyotumia kigezo chako kwa kikwete. Huko ni kuongeza chumvi pasipo sababu.
 
Ndugu, kwa maoni yangu una hoja ila si kwa kuwa serikali imechelewa/zembea kuchunguza dawa ya Babu bali kwa kuwa serikali yetu always inazembea kwenye mambo ya msingi yakiwamo yale yanayogusa afya za wananchi moja kwa moja. Wewe unakuwa na hofu na dawa ya Babu kwamba inaweza kuleta madhara baada ya miaka kadhaa; sawa inawezekana lakini madhara hayo, kama yatakuwepo ni madogo mno kulinganisha na madhara mengine mengi ambayo wananchi WOTE (na siyo wagonjwa wachache tu kama ilivyo kwa Babu) tunayapata katika maisha yetu ya kila siku bila serikali yetu kujishughulisha. Hebu fikiria mifano michache ifuatayo:-

(i) Vyakula - nyama ya kuku wa kisasa:- Hivi unajua aina ya vyakula ambavyo kuku wa kisasa wanalishwa? Inadaiwa baadhi ya wafugaji wamefikia hata hatua ya kuwalisha ARVs, vidonge vya uzazi, na madawa mengine mengi ambayo yana madhara makubwa kwa binadamu. Je, ulishawahi kusikia serikali yetu angalau ikijishughulisha kufanya uchunguzi wa nyama ya kuku inayoingia sokoni? Ni maelfu ya watanzania wangapi wanaotumia nyama ya kuku kila siku?

(ii) Vyakuala - Maziwa ya ng'ombe:- Hivi unajua baadhi ya wafugaji hawafuati masharti pindi ng'ombe wanapokuwa kwenye dozi? Serikali imewahi kujishughulisha kufuatilia ubora wa maziwa yanayoingia sokoni kila siku?

(iii) Vyakula - Samaki:- Ni wazi kuwa baadhi ya wavuvi hutumia sumu kwenye uvuvi wao na hata usafirishaji na uhifadhi wa samaki haukidhi viwango. Je, serikali inajishughulisha kwa hilo?

(iv) Vyakula - Nguruwe:- Kama ilivyo kwa nyama ya kuku, je, ni maelfu ya watanzania wangapi wanakula nguruwe ambao hawana ubora kiafya? Serikali inajali?

(vi) Vyakula - nafaka:- Hivi unajua mbolea na madawa ya kilimo yakitumiwa bila kuzingatia viwango athari zake zinabaki hata kwenye vyakula vitokanavyo na mazao hayo - tena hapo ndio kansa imelala; fikiria DDT, n.k; Je serikali inajali kupima,kwa mfano unga unaosagwa pale Manzese na maharage yanayouzwa pale Tandale na kwingineko kama yana ubora kiafya?

(v) Mfumo wa maisha - moshi wa magari:- Serikali yetu inajali kuhakikisha kwa mfano uchafuzi wa anga hauzidi viwango vianvyotakiwa? Moshi wa magari ni kansa tupu ile!

(vi) Madawa ya binadamu:- Serikali inao udhibiti inavyotakiwa kwamba madawa yanayotumika nchini yana viwango vinavyotakiwa na yanatumika kama inavyotakiwa na kwa wakati?

(vii) Vyakula vya viwandani:- Serikali inadhibiti kikamilifu vyakula vinavyozalishwa viwandani na je wananchi wanazingatia matumizi yake inavyostahili? Expiry dates, n.k. Hapo pia kansa imelala.

(viii) Mifumo ya maisha - ulevi:- Serikali inadhibiti mifumo mbali mbali ya maisha kwa wananchi wake hasa kwenye suala la ulevi? Fikiria ni watu wangapi wamepata kansa kutokana na ulevi ikiwapo matumizi ya gongo, sigara, n.k.

(ix) ... n.k., ... n.k. orodha ingeweza kuwa ndefu kadiri uanvyotaka.

Kwa wenzetu Ulaya huwezi ukazalisha mavitu yako huko halafu ukalisha wananchi bila ukaguzi na udhibiti wa serikali makini. Labda ndio maana wenzetu hata "life expectancy" zao ni zaidi ya 80! Hapa kwetu nasikia tuko 46!

Hivyo, msururu unaoonekana kwa Babu, kwa sehemu kubwa, ni matokeo ya kupuuzia hayo yaliyoorodheshwa hapo juu. Vinginevyo, tatizo lisengekuwa kubwa kama linavyoonekana hivyo pengine Babu leo hii asingekuwa na kazi ya kufanya. Kwa ufupi athari za dawa ya Babu, kama zitakuwepo, ni ndogo mno kulinganisha na athari tunazokutana nazo kwenye maisha yetu ya kila siku. Kitaalamu tungeweza kusema ni "negligible".

Tafakari na chukua hatua!

That's one of the best replies I've ever read. Keep it up Ndugu yangu! JF itanufaika sana kama members wengi tutachukua muda kujibu au kujadili hoja za msingi kwa namna yako. Congrats!
 
Acheni ujuha nyie!!! Kwani serikali zote duniani hufanya utafiti wa dawa zote za mitishamba ambazo zinatumiwa na traditional healers? Sisi kule kwetu kuna mganga anaitwa Tagalu, huyu bwana huweza kuchemsha vichwa vya nyoka na kuvitumia kama dawa. Je ni serikali gani inayoweza kutathimini kujua kwamba vile vichwa vya Nyoka ni salama?

Kijijini kwenu kuna waganga wangapi wa jadi? Mizizi yote wanayotumia kutibia inapimwa? Hakuna serikali hata moja duniani ambayo huweza kufanyia utafiti dawa zote za kienyeji. Na sababu ya msingi ya kushindwa kufanya hivyo ni kutokana na kukosekana kwa ushahidi wa kisayansi unaoonyesha kwamba vitu hivyo vinavyotumiwa na waganga wa jadi, ni dawa. Vingi vinatibu kwa imani!! Kwa mfano, mkemia mkuu anawezaje kutafiti ufanyaji kazi wa hirizi? Kuna watu wanamezeshwa mdomo(beak) wa tai, je mkemia mkuu anawezaje kuthibitisha kwamba mdomo wa tai ni dawa? Ni mkemia gani anayeweza kuthibitisha kwamba mkia wa simba unatibu?

Angalieni hoja za kuilaumu serikali nanyi!!! Halafu siyo hekima kabisa kusema serikali ya Kikwete ndiyo dhaifu kupita zote duniani kwa kuwa eti imeshindwa kuingilia masuala ya imani! Kwa kusema hivyo ni kama kumtuma kikwete kujishughulisha na mambo yote yakiwemo ya ushirikina na imani juu ya Mungu. Kuna mkemia anayeweza kuthibitisha kwamba kuna Mungu?
 
Haya ndiyo matokeo ya serikali isiyotokana na watu na isiyokuwepo kwa ajili ya watu. Viongozi wake wapo kwa ajili ya maslahi yao binafsi, na hivyo hawana ile "sense of responsibility" wanaendesha dola kama kuendesha kioski binafsi tu. Kukosekana kwa uzalendo kwa viongozi kumeitumbukiza nchi mahali pa aibu kwenye maswala mengi sana, na kama hali hii ikiendelea huko tuendapo hakutabiriki.
 
jamani mbona nasikia hata UNCLE mwenyewe ameenda kunywa kikombe cha juice ya babu??
 
Back
Top Bottom