Serikali ya Iran yaibwaga Serikali ya Marekani kwenye Mahakama ya Kimataifa

MALCOM LUMUMBA

JF-Expert Member
Jul 26, 2012
20,897
63,783
Mahakama ya dunia al maarufu kama The International Court of Justice (ICJ) imetoa hukumu yake leo tarehe 3/10/2018 kwenye kesi ambayo Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ilifungua mnamo tarehe 17/7/2018 dhidi ya Shirikisho la mataifa yaliyoungana ya Marekani (United States of America). Iran ilifungua kesi hii kupinga vikwazo ambavyo Serikali ya Raisi Donald Trump iliiwekea punde baada ya Marekani kujitoa kwenye Mkataba wa Nyuklia (The Joint Comprehensive Plan of Action).

Jamhuri ya Iran ilidai kwamba maamuzi hayo yanakwenda kinyume kabisa na Mkataba wa Urafiki uliosainiwa baina ya Serikali ya Iran na Marekani mnamo mwaka 1955 (The Treaty of Amity, 1955). Mkataba huo unazitaka serikali za Marekani na Iran kuheshimu raia, kampuni na mali za nchi zao wakati wote wa uhai wa mkataba huu.

Mahakama hiyo ya kimataifa, katika hukumu yake imeamuru kwamba Marekani iitolee Iran vikwazo kwenye bidhaa zote ambazo ni muhimu kwa uhai na usalama wa raia (Humanitarian Goods) na usafiri wa anga wa nchi hiyo: Hivyo vitu kama madawa, vyakula , bidhaa za kilimo na vyombo vya usafiri wa anga havitakiwi kabisa kuwekewa vikwazo na Marekani.

Hivyo jopo la majaji 15 wakiongozwa na Raisi wa Mahakama hiyo, Jaji Abdulqawi Ahmed Yusuf limeamuru Marekani isitishe hivyo vikwazo kwa muda.

 
Tatizo ni kwamba Marekani ana ubavu wa kupuuza uamuzi wa hiyo mahakama na hakuna wakumfanya chochote (iwe nchi au mahakama yenyewe) kama Urusi alichukua Crimea bila kuhofia hiyo mahakama japo aliwekewa vikwazo basi hiyo hukumu si chochote kwa Marekani muhimu mahakama imetimiza majukumu yake na hukumu imeionesha Iran ni nchi inayoheshimu Sheria za kimataifa ila wasitegemee jipya.
 
Sidhani kama mkataba wa kirafiki wa Iran na Marekani wa mwaka 1955 ulizingatiwa baada ya Mapinduzi ya Iran ya mwaka 1979 maana huo urafiki ulishakufa kitambo baada ya Mapinduzi.
Mahusiano yamekufa, hili unalisema wewe au Wamarekani ???
Kama yangekuwa yameshakufa kama wewe unavyotaka watu waamini hapa basi Marekani asingekubali kupeleka wawakilishi kwenye mahakama ya kimataifa kuhusiana na huo mkataba. Pili usichokijua ni kwamba Marekani alipeleka kesi kwenye hii mahakama ya kimataifa mwaka 1979 ili kusaidia mabalozi wake waachiwe, wewe utasemaje yamekufa ? Kama Mkataba huu ungekuwa umeshavunjika sidhani kama ICJ ingepoteza muda wake kusikiliza hii kesi tokea mwaka 2016.
 
Tatizo ni kwamba Marekani ana ubavu wa kupuuza uamuzi wa hiyo mahakama na hakuna wakumfanya chochote (iwe nchi au mahakama yenyewe) kama Urusi alichukua Crimea bila kuhofia hiyo mahakama japo aliwekewa vikwazo basi hiyo hukumu si chochote kwa Marekani muhimu mahakama imetimiza majukumu yake na hukumu imeionesha Iran ni nchi inayoheshimu Sheria za kimataifa ila wasitegemee jipya.
Kupuuza siyo tatizo, tatizo ni kwamba Mahakama imesema kwamba hivi vikwazo viko kinyume kabisa na Sheria za kimataifa. Hivyo nchi nyingine zinaruhusiwa kuendelea kufanya biashara na Iran kwenye bidhaa muhimu kwa ajili ya binadamu, bila kusahau usafiri wa anga.
 
Mahusiano yamekufa, hili unalisema wewe au Wamarekani ???
Kama yangekuwa yameshakufa kama wewe unavyotaka watu waamini hapa basi Marekani asingekubali kupeleka wawakilishi kwenye mahakama ya kimataifa kuhusiana na huo mkataba. Pili usichokijua ni kwamba Marekani alipeleka kesi kwenye hii mahakama ya kimataifa mwaka 1979 ili kusaidia mabalozi wake waachiwe. Kama Mkataba huu ungekuwa umeshavunjika sidhani kama ICJ ingepoteza muda wake kusikiliza hii kesi tokea mwaka 2016.
Labda Trump ataheshimu mkataba tusubiri.
 
Labda Trump ataheshimu mkataba tusubiri.
Usikimbie kuvuli chako: Umesema kwamba huo mkataba ulikufa kitambo baada ya 1979.
Wamarekani wenyewe wanasema huu mkataba bado upo. Kutokuheshimu mkataba kwa upande wa Trump hakufanyi huu Mkataba kuvunjika. Mara ngapi Serikali haziheshimu mikataba na bado inaendelea kuwepo ?
 
Usikimbie kuvuli chako: Umesema kwamba huo mkataba ulikufa kitambo baada ya 1979.
Wamarekani wenyewe wanasema huu mkataba bado upo. Kutokuheshimu mkataba kwa upande wa Trump hakufanyi huu Mkataba kuvunjika. Mara ngapi Serikali haziheshimu mikataba na bado inaendelea kuwepo ?
Kama ukiwepo na hauheshimiki ni sawa na umekufa tuu
 
Kwahiyo Mexico na Canada walivyokuwa hawaheshimu NAFTA,
Au ambavyo Marekani na Uchina hawaheshimu The Marrakesh Agreement (World Trade Organization)
Inamaanisha kwamba NAFTA na WTO zilikuwa zimekufa, si ndiyo ???
Huwezi kulinganisha hiyo mikataba na huu wa Iran (uliosainiwa kabla ya Mapinduzi) mambo yameshabilika umebaki kwenye karatasi tu ila utekelezaji sifuri.
 
Huwezi kulinganisha hiyo mikataba na huu wa Iran (uliosainiwa kabla ya Mapinduzi) mambo yameshabilika umebaki kwenye karatasi tu ila utekelezaji sifuri.
Na kama utekelezaji wa Mkataba ungekuwa ni sifuri kwanini mwaka 2016 Raisi Obama alikubali kuilipa serikali ya Iran deni la USD 1.2 Billion ambalo alikuwa anadaiwa na Serikali ya Shah kabla ya mapinduzi ya 1979 ? Kwanini Raisi Obama alihangaika kulipa deni la linalotokana na mkataba uliobaki kwenye Makaratasi tu ?
 
Na kama utekelezaji wa Mkataba ungekuwa ni sifuri kwanini mwaka 2016 Raisi Obama alikubali kuilipa serikali ya Iran deni la USD 1.2 Billion ambalo alikuwa anadaiwa na Serikali ya Shah kabla ya mapinduzi ya 1979 ? Kwanini Raisi Obama alihangaika kulipa deni la mkataba uliobaki kwenye Makaratasi tu ?
Obama alikua ana heshimu mikataba ndo maana hata wa mabadiliko wa Hali ya hewa alikubali kusaini na huenda aliilipa Iran kama njia ya kuilainisha ili kupunguza shughuli zao za kinyuklia ila utawala wa Marekani umebadilika kama mkataba wa nyuklia Trump kaukataa na wa mabadiliko wa Hali ya hewa kaukataa hata huo wa Iran wa mwaka 1955 sidhani kama ni kosa kusema umeshakufa.
 
Huwezi kulinganisha hiyo mikataba na huu wa Iran (uliosainiwa kabla ya Mapinduzi) mambo yameshabilika umebaki kwenye karatasi tu ila utekelezaji sifuri.
Marekani anaimiliki Guantanamo bay kwa mkataba upi na wa mwaka gani....mbona alivunja uhusiano wa kibalozi mwaka 1959 na Cuba baada ya mapinduzi ya kikomunist lakn hakusema mkataba wa kuimiliki Guantanamo hautambui kwa kuwa hakuingia na mkomunist Fidel Castol....Soma kwanza maana ya mikataba ya kimataifa halafu urudi jamvini....
 
Na kama utekelezaji wa Mkataba ungekuwa ni sifuri kwanini mwaka 2016 Raisi Obama alikubali kuilipa serikali ya Iran deni la USD 1.2 Billion ambalo alikuwa anadaiwa na Serikali ya Shah kabla ya mapinduzi ya 1979 ? Kwanini Raisi Obama alihangaika kulipa deni la linalotokana na mkataba uliobaki kwenye Makaratasi tu ?
Mwache kumpa nondo utamuua mkuu..
 
Obama alikua ana heshimu mikataba ndo maana hata wa mabadiliko wa Hali ya hewa alikubali kusaini na huenda aliilipa Iran kama njia ya kuilainisha ili kupunguza shughuli zao za kinyuklia ila utawala wa Marekani umebadilika kama mkataba wa nyuklia Trump kaukataa na wa mabadiliko wa Hali ya hewa kaukataa hata huo wa Iran wa mwaka 1955 sidhani kama ni kosa kusema umeshakufa.
Inaonyesha hata hujui unachokizungumza hapa: Huo Mkataba wa Mabadiliko ya hali ya hewa au The Paris Agreement unaanza kufanya kazi mwaka 2020. Hivyo kujitoa kwa Donald Trump hakuna madhara sana.

Hii hoja yako hapa ni mufilisi, tafuta mfano hai kisha twendelee!
 
Marekani anaimiliki Guantanamo bay kwa mkataba upi na wa mwaka gani....mbona alivunja uhusiano wa kibalozi mwaka 1959 na Cuba baada ya mapinduzi ya kikomunist lakn hakusema mkataba wa kuimiliki Guantanamo hautambui kwa kuwa hakuingia na mkomunist Fidel Castol....Soma kwanza maana ya mikataba ya kimataifa halafu urudi jamvini....
Mhhhh, umefikiri kwa nguvu sana hadi umeniogopesha. Naomba nikupe hongera nyingi sana katika hili ndugu yangu. Naisoma hoja yako huku nikiwa na tabasamu kubwa sana usoni mwangu.
 
Marekani anaimiliki Guantanamo bay kwa mkataba upi na wa mwaka gani....mbona alivunja uhusiano wa kibalozi mwaka 1959 na Cuba baada ya mapinduzi ya kikomunist lakn hakusema mkataba wa kuimiliki Guantanamo hautambui kwa kuwa hakuingia na mkomunist Fidel Castol....Soma kwanza maana ya mikataba ya kimataifa halafu urudi jamvini....
Kwan mkataba wa nyuklia wa Iran uliokataliwa na Trump na ule wa mabadiliko wa Hali ya hewa haikua ya kimataifa? mbona Marekani kajitoa tu sembuse huo wa mwaka 1955 usiotekelezeka.
 
Kwan mkataba wa nyuklia wa Iran uliokataliwa na Trump na ule wa mabadiliko wa Hali ya hewa haikua ya kimataifa? mbona Marekani kajitoa tu sembuse huo wa mwaka 1955 usiotekelezeka.
Bado hujajibu swali la mdau: Marekani aliendeleaje kumiliki Guantanamo baada ya Mapinduzi ?
Halafu narudia tena, The Paris Agreement utaanza kuwa Mkataba wa Kimataifa kuanzia mwaka 2020.
Sasa hivi bado wako kwenye kipindi cha mpito, tafuta mfano mwingine hai halafu tuendelee.
 
Bado hujajibu swali la mdau: Marekani aliendeleaje kumiliki Guantanamo baada ya Mapinduzi ?
Halafu narudia tena, The Paris Agreement utaanza kuwa Mkataba wa Kimataifa kuanzia mwaka 2020.
Hilo ni taifa kubwa kuendelea kumiliki Guantanamo si ajabu mbona huko Syria amepeleka askari wake bila idhini ya Assad ndo tabia yake hakuna jipya hapo na nimesema kama kajitoa huo wa Hali ya hewa hata huo na Iran wa 1955 usipotekelezwa si ajabu.
 
Back
Top Bottom