Serikali ya CCM yatoa vitisho na kuwachangisha fedha Watumishi wa Umma kwa lazima

Lituye

JF-Expert Member
Dec 27, 2015
1,862
5,680
Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke iliyopo Jiji la Dare Salaam Bwana Mwakibibi, ameagiza watumishi wote wa halmashauri hiyo kuchangia pesa za Ujenzi wa Vyumba vya Madarasa na matundu ya vyoo katika harambee ambayo ameiandaa mwishoni mwa mwezi huu.

Akiongea katika kikao na walimu wake jana, mkuu wa shule mmoja jina tunalihifadhi aliwaeleza kuwa "tumeagizwa kila shule kuchangia laki mbili. Hivyo tutazigawa hizi lakimbili kwa idadi ya walimu tuliopo kisha tutajua kila mtu atachanga kiasi gani".

Aidha mkuu huyo alieleza kuwa Wakuu wa Idara wote wa halmashauri hiyo wameagizwa kutoa Milioni moja kila mtu na wasaidizi wao kutoa laki tano. Pia watumishi wengine wote kila mtu atachangia kiasi kisichopungua elfu kumi.

Harambee hiyo inatarajiwa kufanyika katika ukumbi wa Mlimani City mwisho wa mwezi huu wa tatu na mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais Mstaafu ndugu Jakaya Mrisho Kikwete.

Jambo la kushangaza zaidi kama sio vichekesho ni kuwa taarifa zinanyetisha hata bwana yule mnunua midege kwa pesa taslimu huku akiacha Wanafunzi wakijisaidia vichakani na kusomea chini ya miti na wengine kukosa mikopo elimu ya juu eti naye atakuwepo kuchangia harambee.

Huu ni ukatili mkubwa kwa watumishi wa umma hapa nchini kuwalazimisha kuchangia michango bila hiari yao. Watumishi ambao hawajapandishwa mishara takribani miaka mitano sasa wanaishi maisha magumu. Huku wengine wameongezewa deni la bodi ya mikopo elimu ya juu wanapewa mzigo wa kuisadia Serikali inayo jitapa kuwa inazo hela za kutosha.

Vyama vya wafanya kazi vipo kimya kabisaa vinaangalia tuu maagizo haya ya kinyama kwa watumishi wa umma yakitekelezwa.

Maendeleo hayana vyama.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nadhani mtoa maada unataka kupotosha,Hilo zoezi hata huku Monduli lilishafanyika ila mkurugenzi aliomba keep la mtumishi kuchangia elfu kumi,ila haikuwa LAZIMA.
Sasa hapo kwa Temeke ndo napata Shaka maana umeripoti shule kuchangia,hata walimu wasipochangia basi fungu linalopelekwa shule yawezekena laki mbili zikatolewa na kupelekwa.

Sijaona walipo lazmisha walimu
 
Nadhani mtoa maada unataka kupotosha,Hilo zoezi hata huku Monduli lilishafanyika ila mkurugenzi aliomba keep la mtumishi kuchangia elfu kumi,ila haikuwa LAZIMA.
Sasa hapo kwa Temeke ndo napata Shaka maana umeripoti shule kuchangia,hata walimu wasipochangia basi fungu linalopelekwa shule yawezekena laki mbili zikatolewa na kupelekwa.

Sijaona walipo lazmisha walimu
Una akili sana aisee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Baadhi washaanza kucheka, mishahara inaongezwa kimyakimya, walianza TRA kwa asilimia karibu 100 na sasa TARURA nao wameongezewa asilimia zaidi ya 100. Labda mpango ni kupunguza nguvu ya watumishi kupiga kelele kwa pamoja. Divide and Rule
 
Aaagh.....mbona unawakata stimu hawa walevi!?? Wape pumzi wajifariji angalau na hiki kihabari.

Mimi nipo hapa na Halima Mdee namkagua kama kuna kiungo kingine kimeumizwa.
Nadhani mtoa maada unataka kupotosha,Hilo zoezi hata huku Monduli lilishafanyika ila mkurugenzi aliomba keep la mtumishi kuchangia elfu kumi,ila haikuwa LAZIMA.
Sasa hapo kwa Temeke ndo napata Shaka maana umeripoti shule kuchangia,hata walimu wasipochangia basi fungu linalopelekwa shule yawezekena laki mbili zikatolewa na kupelekwa.

Sijaona walipo lazmisha walimu
 
Wakitoa pesa hizo basi hao watumishi ni matajiri
Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke iliyopo Jiji la Dare Salaam Bwana Mwakibibi, ameagiza watumishi wote wa halmashauri hiyo kuchangia pesa za Ujenzi wa Vyumba vya Madarasa na matundu ya vyoo katika harambee ambayo ameiandaa mwishoni mwa mwezi huu.

Akiongea katika kikao na walimu wake jana, mkuu wa shule mmoja jina tunalihifadhi aliwaeleza kuwa "tumeagizwa kila shule kuchangia laki mbili. Hivyo tutazigawa hizi lakimbili kwa idadi ya walimu tuliopo kisha tutajua kila mtu atachanga kiasi gani".

Aidha mkuu huyo alieleza kuwa Wakuu wa Idara wote wa halmashauri hiyo wameagizwa kutoa Milioni moja kila mtu na wasaidizi wao kutoa laki tano. Pia watumishi wengine wote kila mtu atachangia kiasi kisichopungua elfu kumi.

Harambee hiyo inatarajiwa kufanyika katika ukumbi wa Mlimani City mwisho wa mwezi huu wa tatu na mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais Mstaafu ndugu Jakaya Mrisho Kikwete.

Jambo la kushangaza zaidi kama sio vichekesho ni kuwa taarifa zinanyetisha hata bwana yule mnunua midege kwa pesa taslimu huku akiacha Wanafunzi wakijisaidia vichakani na kusomea chini ya miti na wengine kukosa mikopo elimu ya juu eti naye atakuwepo kuchangia harambee.

Huu ni ukatili mkubwa kwa watumishi wa umma hapa nchini kuwalazimisha kuchangia michango bila hiari yao. Watumishi ambao hawajapandishwa mishara takribani miaka mitano sasa wanaishi maisha magumu. Huku wengine wameongezewa deni la bodi ya mikopo elimu ya juu wanapewa mzigo wa kuisadia Serikali inayo jitapa kuwa inazo hela za kutosha.

Vyama vya wafanya kazi vipo kimya kabisaa vinaangalia tuu maagizo haya ya kinyama kwa watumishi wa umma yakitekelezwa.

Maendeleo hayana vyama.



Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom