Serikali ya CCM ya Mwenyekiti Magufuli Inaumbuka. Hongereni wapinzani

KISHADA

JF-Expert Member
Oct 18, 2012
2,224
3,290
Serikali ya awamu ya tano ya mwenyekiti Dr magufuli inaumbuliwa kwa kasi. kinachoendelea nchini katika utawala huu na siasa zetu si hakikisho la amani na utulivu kama ambavyo watu wa imani na wanadini wanavyopiga kelele lakini naweza kusema inabebwa tu na busara na USTAARABU wa upinzani wa nchi hii.

Tulipo ni pabaya sana. Leo viongozi wa serikali wanapojipambanua kuvunja taratibu za wazi za chaguzi na kukaribisha mazingira ya uvunjifu wa amani bila kukemewa na viongoziu wa juu basi ujuwe ngoma inogile.

Uchafuzi huu wa chaguzi za marudio na kasi ya kile kinachoitwa wapinzani kujiuzulu na kummunga mkono rais na kuwepo taarifa za hujuma na mianya ya kifisadi wa kisiasa kufanywa mchana kweupe, kuvunjwa taratibu, Polisi kutumika kunyanyasa wapinzani kweupe si kuumbukuka kidogo kwa CCM na serikali yake.

CCM NA SIKIO LA KUFA.
Nchi inateketea kidogo kidogo kwa kupandikizwa chuki, CCM na tabaka tawala linafurahia kwa sababu ya maslahi yao. Vyombo vya dola kutumika kuharibu taratibu za chaguzi si jambo dogo. Viongozi wa serikali wakiwemo NEC na wakurugenzi wa halmashauri kutumika kuharibu taratibu wazi wazi si jambo jema kwa nchi. Tunataka tuwaulize wale CCM walio huru kiakili na maarifa hivi kweli leo CCM inapendwa kweli kweli kama tunavyoaminishwa ?

Mbona CCM inaimarishwa kwa misingi ya kuharibu taratibu za nchi na kwa kutumia mbeleko ya dola jee huku ndio kukubalika ?

Nani amseme mwenzake kuhusu huu ukimya wa viongozi wa juu na kinachoendelea kila kukicha?. CCM na uongozi wa dr Magufuli haukutosheka na kuzuia maandamano na mikutano ya kisiasa ya vyama ya wazi tu, lakini sasa inatumia vyombo vya dola na taasisi za serikali kuwahujumu wapinzani wazi wazi.

Mazingira yaliyopo hayaipi nafasi CCM kukubalika ndani ya nafsi za watu na kulazimishwa huku kwa nguvu za dola ni hatari sana kwa CCM. Juhudi za maarifa za kupandikiza itikadi sahihi za chama zilizofanywa na waliopita zinaharibiwa na viongozi waliopo leo madarakani. Hiki ndicho kifo cha CCM pale itakapofika siku mazingira yakibadilika. Pengine CCM hawaamini kuwa ipo siku mazingira yatabadilika.
Utafanye chaguzi kwa kukiuka taratibu na kuifanya CCM ishinde bila kupingwa ukiamini hicho ndicho kipimo sahihi cha kukubalika CCM?

Utatumiaje polisi kudhibiti wale wanaotaka taratibu zifuatwe ukiamini hizo ndio mbinu za kukifanya chama kukubalika kwenye jamii? SIKU CCM WAELEWA WAKISHTUKA TUTASHUHUDIA ZAIDI YA HAYA AKINA NAPE. Poleni CCM, nchi inaelekezwa kubaya kwa mikono ya wakubwa wenu na mnanyamaza kimya.

BUSARA HEKIMA AU ULEGEVU WA WAPINZANI ?
Watu wanahoji na kuwalaumu wapinzani kuwa labda wamelemaa sana. Mbinu za wapinzani za kutumia njia iliyopo leo inawafanya CCM wajianike wakiamini wameshawadhibiti wapinzani na wamefanikiwa kwa kuiacha CCM na serikali yake ijichore na kujidhihirisha MBELE YA DUNIA kuwa kweli inavunja haki za binadamu na kutoheshimu demokrasia. CCM imejiachia na dunia inashuhudia hilo sasa.

Wasioona mbali wanadhani kuwa mambo ni shwari. Mimi naona kama wapinzani wamefanya 'timing" tu. Hiki kinachoendelea hapa nchini bila ya kufanyiwa kazi basi mbele kuna giza nene. Naitafakari miaka hii mitatu ya Rais Magufuli kama Pilot kwa wapinzani. Naiona kama wametowa mwanya kwa watawala wajitafakari kwa haya wanayoyatenda. Picha imepatikana na naamini WATAALAMU NA WASOMI WA UPINZANI WATAKUJA NA JIBU HAPO BAADAE.

Tunachokiona kwa sasa walau hawa wapinzani wamekuwa waungwana sana kwa kutanguliza maslahi ya taifa ya kulinda amani na utulivu kwa vitendo kwa kutumia maarifa makubwa kutokubali kuingizwa kwenye mapambano ya kiuchokozi ya wazi. Nadhani wanajuwa walitendalo.

JEE HALI HII ILIPO ITAENDELEA HIVI MILELE ?
si dhani kuwa ni hivyo, kwanza hali hii inaipa picha Dunia nini kifanyike kuelekea uchaguzi wa 2020.Wapinzani wamefanikiwa kuionesha Dunia namna CCM na serikali ya dr Magufuli ilivyo. Lengine sidhani kuwa wapinzani hawana njia mbadala sidhani. La msingi watangulize maslahi ya taifa kwa kutumia mbinu zote zinazostahiki lakini....................

KUUMBUKA KWA SERIKALI NA CCM
wenyewe kujidhihirisha kuwa hawajali malalamiko yaliopo na kushindwa kuyafanyia kazi malalamiko ya chaguzi ndogo na kujirudia kila wakati.

Viongozi kutowa lugha tata na kuachia wasaidizi wao kuvunja taratibu bila kukemea na bila kuchukuliwa hatua

Vyombo vya serikali kugongana wenyewe unapoifika wakati wa kusimamia utatuzi wa jambo kila mmoja kutoa maelezo yake yanayopingana.

Wana CCM kusemana hadharani (baadhi) hii ni kuashiria kuwa kuna mambo hayako sawa.

Viongozi kushindwa kukemea uchafuzi wa wazi wa taratibu(chaguzi) na taratibu nyengine za uendeshaji kwenye mamlaka mbali mbali( kupindisha taratibu kwa maslaHI FULANI)

Wapinzani kuwa kimya na kuacha dhamira za watawala kutimia huku wakijidhirisha watawala peke yao kwa kufanya vitendo vinavyoashiria uvunjivu wa amani


MASWALI MUHIMU.

Jee kukubalika kwa CCM kunaendena na uhalisia au kuna kulazimishwa ?

Kuongezeaka kwa wapinzani kujiunga CCM kwa sasa Jee CCM inakuwa au inakufa ?

Tutarajie hatma gani kwa nchi kutokana na hali halisi ya mazingira ya kisiasa na kiutawala iliyopo?



MWISHO
Tunaamini CCM IMARA itajengwa kwa ustaarabu wa kutumia njia sahihi za kidemokrasia za kutumia ushawishi wa hoja na itikadi na si kwa nguvu na kutumia vyombo vya dola

waswahili wana msemo maarufu "MAPENZI HAYALAZIMISHWI"

Tunahitaji CCM imara, tunahitaji UPINZANI imara ili nchi isonge mbele.



Kishada.
 
Wanavyofikiri ni kuwa nchi itajengwa kwa CCM kurasimishwa kuwa dola na kuacha misingi ya haki na kikatiba pembeni. Bila ya kufuatwa taratibu tulizojiwekea ni vurugu tu. Ona leo CCM inavyojichora na kiuharibu misingi iliyotengenezwa na baba wa taifa na wenzake.

Unakubali vyama vingi halafu unawasumbuwa watanzania wenzakoi halafu unatamani uitwe Malaika. Huyo mungu itakuwa ana kazi gani. Tutarajie anguko tu
 
Fisiemu inatumia ubabe ili ipendwe!
Haina tofauti na mwanaume aliyekatawaliwa anaamua abake ili apate alichoshindwa kupata kwa kutongoza!

Fisiemu haina haya wala aibu, haihofii wananchi na wala haina mpango nao!, Wao wanachojua ni madaraka tu hata kwa kupora kama majambazi. Shame on them!!

Limekuwa kama genge fulani hivi la wahuni wasio na aibu!
 
Tukifika mahali tukaharibu taratibu kwa kuamini kupita njia fupi (short cut) kwa makosa yaliyofanywa na CCM hii hii huko nyuma, tukiamini njia hizo zifuatwe hata kwa kuvunja taratibu, ili Tanzania tunayoiota itimie itakuwa tumekosa maarifa sana ya kisiasa. badala ya kujenga tutabomowa. Neno "PRINCIPLE" likumbukwe sana na hawa WATAWALA WA CCM waliopo madarakani leo. Utaachaje kufanya critical analysis ya siasa za kidunia za leo ili kuierndesha nchi na badala yake unakuja na THEORY OF UNKNOWN eti unaamini kwa kuja watu WASIOJULIKANA na kupoteza watu utakuwa salama na kuipeleka nchi mbele. Thinking .
 
Unaamini kuwa viongozi wa CCM waliopita walifanya makosa sana kuruhusu demokrasia na kupelekea watu kuhoji na kwa hivyo kuisumbuwa CCM kutawala wewe unakuja na njia ya mkato ya kuuwa na kuvuruga vyama ukiamini ndio muarubaini basi utakuwa unahitaji uombewe.

Dunia ya leo unatakiwa kutumia akili sana. Kwenye utawala wa nchi LAZIMA uwe na uelewa wa mwelekeo wa dunia na matakwa yake. Nchi inavyokwenda kwa sasa haihitaji short cut


KATIBA MPYA ndio suluhisho la matatizo yaliyofanywa na CCM huko nyuma. Vyenginevyo tutarudi nyuma sana .
 
nilipokuwa kijana niliwahi kusikia kuwa ukitaka kufanya siasa na kuwa mwanasiasa mahili watu walienda urusi na uchina kusoma sayansi ya siasa na propaganda...upinzani mkubwa ilikuwa ni kuambiwa fulani ni fisadi au ana tabia zisizo kubalika na jamii kama ulevi a umalaya lakini siku hizi ukitaka siasa lazima ujiongeze kidogo hata kurusha mateke kama siyo judo na karate au uwe unaweza kidogo kutumia buduki au uwe na ujuzi wa kuvumilia vipao na vipigo wa raia wenzetu wa jeshi la polisi
 
Kadiri ukandamizwaji unapozidi, ndio kwanza kunaibuka wapinzani wengi. Hapa Tanzania kuna wapinzani wengi kwenye makundi mawili makubwa

Wapinzani wa wazi (Vyama na wanaharakati n.k)

Wapinzani wa moyoni (Marafiki zako na makundi mengine)

hili kundi la pili naona kama linazidio kuongezeaka sana. Ogopa hili kundi la pili. Unapambana kuvuruga kundi la kwanza unaongeza kundi la pili.
 
Wanavyofikiri ni kuwa nchi itajengwa kwa CCM kurasimishwa kuwa dola na kuacha misingi ya haki na kikatiba pembeni. Bila ya kufuatwa taratibu tulizojiwekea ni vurugu tu. Ona leo CCM inavyojichora na kiuharibu misingi iliyotengenezwa na baba wa taifa na wenzake.

Unakubali vyama vingi halafu unawasumbuwa watanzania wenzakoi halafu unatamani uitwe Malaika. Huyo mungu itakuwa ana kazi gani. Tutarajie anguko tu
Mimi huwa inaniwia ngumu kutofautisha vyombo vya ulinzi na usalama na chama cha mapinduzi, mfano , mwanausalama yeyote Nina muona kwamba ni muajiriwa wa chama cha mapinduzi ccm , hili la kulinda usalama wa RAIA , Mali , na nchi ni jukumu Dogo sana na la mwisho ...but no longer at ease

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tunatengeneza awamu mpya ya matatizo badala ya kutatuwa matatizo yaliyofanywa na CCM. CCM inahitaji viongozi imara kuijenga upya sio hii safu ya kuasisi matatizo mapya ili kuijenga CCM. Shida si kuwa mfanya biashara mkubwa, shida ni kuwa mfanyabiashara mkubwa ambaye mali yake ameichuma kwa njia haramu. Tunatamani Tanzania iendelee hata kesho lakini kwa misingi ya HAKI NA USAWA
 
Fursa bado ipo. Lakini kwanza tuwe tayari kukosolewa na kuoneshwa njia. upepo wa siasa za kiafrika unaovuma hasa hapa afrika Mashariki sio role Model ya Tanzania.

Tusimsumbuwe baba wa Taifa bure kwa kukosa uelewa wa mambo. Nchi si muda mrefu itavuliwa nguo.
 
Serikali ya awamu ya tano ya mwenyekiti Dr magufuli inaumbuliwa kwa kasi. kinachoendelea nchini katika utawala huu na siasa zetu si hakikisho la amani na utulivu kama ambavyo watu wa imani na wanadini wanavyopiga kelele lakini naweza kusema inabebwa tu na busara na USTAARABU wa upinzani wa nchi hii.

Tulipo ni pabaya sana. Leo viongozi wa serikali wanapojipambanua kuvunja taratibu za wazi za chaguzi na kukaribisha mazingira ya uvunjifu wa amani bila kukemewa na viongoziu wa juu basi ujuwe ngoma inogile.

Uchafuzi huu wa chaguzi za marudio na kasi ya kile kinachoitwa wapinzani kujiuzulu na kummunga mkono rais na kuwepo taarifa za hujuma na mianya ya kifisadi wa kisiasa kufanywa mchana kweupe, kuvunjwa taratibu, Polisi kutumika kunyanyasa wapinzani kweupe si kuumbukuka kidogo kwa CCM na serikali yake.

CCM NA SIKIO LA KUFA.
Nchi inateketea kidogo kidogo kwa kupandikizwa chuki, CCM na tabaka tawala linafurahia kwa sababu ya maslahi yao. Vyombo vya dola kutumika kuharibu taratibu za chaguzi si jambo dogo. Viongozi wa serikali wakiwemo NEC na wakurugenzi wa halmashauri kutumika kuharibu taratibu wazi wazi si jambo jema kwa nchi. Tunataka tuwaulize wale CCM walio huru kiakili na maarifa hivi kweli leo CCM inapendwa kweli kweli kama tunavyoaminishwa ?

Mbona CCM inaimarishwa kwa misingi ya kuharibu taratibu za nchi na kwa kutumia mbeleko ya dola jee huku ndio kukubalika ?

Nani amseme mwenzake kuhusu huu ukimya wa viongozi wa juu na kinachoendelea kila kukicha?. CCM na uongozi wa dr Magufuli haukutosheka na kuzuia maandamano na mikutano ya kisiasa ya vyama ya wazi tu, lakini sasa inatumia vyombo vya dola na taasisi za serikali kuwahujumu wapinzani wazi wazi.

Mazingira yaliyopo hayaipi nafasi CCM kukubalika ndani ya nafsi za watu na kulazimishwa huku kwa nguvu za dola ni hatari sana kwa CCM. Juhudi za maarifa za kupandikiza itikadi sahihi za chama zilizofanywa na waliopita zinaharibiwa na viongozi waliopo leo madarakani. Hiki ndicho kifo cha CCM pale itakapofika siku mazingira yakibadilika. Pengine CCM hawaamini kuwa ipo siku mazingira yatabadilika.
Utafanye chaguzi kwa kukiuka taratibu na kuifanya CCM ishinde bila kupingwa ukiamini hicho ndicho kipimo sahihi cha kukubalika CCM?

Utatumiaje polisi kudhibiti wale wanaotaka taratibu zifuatwe ukiamini hizo ndio mbinu za kukifanya chama kukubalika kwenye jamii? SIKU CCM WAELEWA WAKISHTUKA TUTASHUHUDIA ZAIDI YA HAYA AKINA NAPE. Poleni CCM, nchi inaelekezwa kubaya kwa mikono ya wakubwa wenu na mnanyamaza kimya.

BUSARA HEKIMA AU ULEGEVU WA WAPINZANI ?
Watu wanahoji na kuwalaumu wapinzani kuwa labda wamelemaa sana. Mbinu za wapinzani za kutumia njia iliyopo leo inawafanya CCM wajianike wakiamini wameshawadhibiti wapinzani na wamefanikiwa kwa kuiacha CCM na serikali yake ijichore na kujidhihirisha MBELE YA DUNIA kuwa kweli inavunja haki za binadamu na kutoheshimu demokrasia. CCM imejiachia na dunia inashuhudia hilo sasa.

Wasioona mbali wanadhani kuwa mambo ni shwari. Mimi naona kama wapinzani wamefanya 'timing" tu. Hiki kinachoendelea hapa nchini bila ya kufanyiwa kazi basi mbele kuna giza nene. Naitafakari miaka hii mitatu ya Rais Magufuli kama Pilot kwa wapinzani. Naiona kama wametowa mwanya kwa watawala wajitafakari kwa haya wanayoyatenda. Picha imepatikana na naamini WATAALAMU NA WASOMI WA UPINZANI WATAKUJA NA JIBU HAPO BAADAE.

Tunachokiona kwa sasa walau hawa wapinzani wamekuwa waungwana sana kwa kutanguliza maslahi ya taifa ya kulinda amani na utulivu kwa vitendo kwa kutumia maarifa makubwa kutokubali kuingizwa kwenye mapambano ya kiuchokozi ya wazi. Nadhani wanajuwa walitendalo.

JEE HALI HII ILIPO ITAENDELEA HIVI MILELE ?
si dhani kuwa ni hivyo, kwanza hali hii inaipa picha Dunia nini kifanyike kuelekea uchaguzi wa 2020.Wapinzani wamefanikiwa kuionesha Dunia namna CCM na serikali ya dr Magufuli ilivyo. Lengine sidhani kuwa wapinzani hawana njia mbadala sidhani. La msingi watangulize maslahi ya taifa kwa kutumia mbinu zote zinazostahiki lakini....................

KUUMBUKA KWA SERIKALI NA CCM
wenyewe kujidhihirisha kuwa hawajali malalamiko yaliopo na kushindwa kuyafanyia kazi malalamiko ya chaguzi ndogo na kujirudia kila wakati.

Viongozi kutowa lugha tata na kuachia wasaidizi wao kuvunja taratibu bila kukemea na bila kuchukuliwa hatua

Vyombo vya serikali kugongana wenyewe unapoifika wakati wa kusimamia utatuzi wa jambo kila mmoja kutoa maelezo yake yanayopingana.

Wana CCM kusemana hadharani (baadhi) hii ni kuashiria kuwa kuna mambo hayako sawa.

Viongozi kushindwa kukemea uchafuzi wa wazi wa taratibu(chaguzi) na taratibu nyengine za uendeshaji kwenye mamlaka mbali mbali( kupindisha taratibu kwa maslaHI FULANI)

Wapinzani kuwa kimya na kuacha dhamira za watawala kutimia huku wakijidhirisha watawala peke yao kwa kufanya vitendo vinavyoashiria uvunjivu wa amani


MASWALI MUHIMU.

Jee kukubalika kwa CCM kunaendena na uhalisia au kuna kulazimishwa ?

Kuongezeaka kwa wapinzani kujiunga CCM kwa sasa Jee CCM inakuwa au inakufa ?

Tutarajie hatma gani kwa nchi kutokana na hali halisi ya mazingira ya kisiasa na kiutawala iliyopo?



MWISHO
Tunaamini CCM IMARA itajengwa kwa ustaarabu wa kutumia njia sahihi za kidemokrasia za kutumia ushawishi wa hoja na itikadi na si kwa nguvu na kutumia vyombo vya dola

waswahili wana msemo maarufu "MAPENZI HAYALAZIMISHWI"

Tunahitaji CCM imara, tunahitaji UPINZANI imara ili nchi isonge mbele.



Kishada.









Pole sana kwa uchungu ulionao muda wa leba huu.
 
Nilikuwa nawaza tu, ingekuwaje wapinzani wangekubali kuingizwa siasa za chuki hao watawala wangetulia kufanya kazi zao au ingekuwaje? Hata kama dola ingewadhibiti ipasavyo sawa. Jee hilo ndio likngekuwa suluhisho. Nahisi pangekosekana utulivu hata wa akili. Ndio nikasema hongereni wapinzani. Dhamira za wenye Dola kwa sasa zimejichora wazi. Hongereni kwa kuusoma mchezo na kuliacha jiwe lijipasuwe wenyewe.
 
CCM ilishakufa Siku nyingi sana

Sent using Jamii Forums mobile app

Kilichotokea kule Zanzibar haijawa fundisho kwa miaka yote ya siasa tokea 1995.Sasa wanahamishiwa mikakati yao Bara. Imefika wakati huajiriwi SMZ mpaka uwe CCm na uwe na kadi yao. sasa hivi nasikia kule kadi za CCM ni dili na wenyewe wamedhibiti utoaji wa kadi kwa wanachama wapya. Katika hali hiyo unajenga Taifa la aina gani. Bado kiburi cha Utawala kimewazonga CCm kuwa watabaki milele.

Naona siasa za Zanzibar zinaletwa kwa kasi sana bara.
 
Licha ya kutambuwa ukweli kuwa CCM Zanzibar imeshakataliwa kitambo na bila aibu watakwambia inaongoza na kupendwa kwa sababu inatekelkeza ilani lakini ukifika uchaguzi wanatumia vikosi vyote wakishindwa wanamtumia Jecha kufuta uchaguzi wote na hapo huwa ndio mwisho wa mchezo. Cha kushangaza halafu unawasikia wakijiapiza eti serikali itawashughulikia wavunja amani.

Wameachwa wenyewe wafanye watakavyo kimya. Nafsi zinawasuta kule wameuwa GNU na umoja Zanzibar uliopo Kikatiba, wanaajiri watu wao tu, sasa na huku bara wanavunja umoja na mshikamano kwa nguvu zote Kwa kulazimisha CCM ipendwe.

Ghafla tulishuihudia watu wasiojulikana, Sasa kuna watu wanavunja Taratibu na SHERIA WAZI WAZI , WANAJULIKANA LAKINI HAWACHUKULIWI HATUWA.

Tutafika.
 
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom