Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 39,795
- 71,214
CCM kila siku inajisifu "sisi ni chama Tawala" bila kuwaonyesha chini ya utawala wao kipi cha kujivunia hasa katika dunia ya leo tuwezacho kuionyesha dunia?
Ona hii, leo 2021 Waziri wa Viwanda anasimama kwa mbwembwe kuzindua Trela la kwanza kuundwa nchini na kujisifu kwa uvumbuzi huo wakati wenzetu majirani miaka kadhaa nyuma 2018 walizindua Setellite yao kwa kushirikiana na Japan.
Kweli sie kutengeneza Trela la mizigo ni suala la kitaifa wakati hayo mambo yalikuwa yanaweza kuwa yanazalishwa na vyuo vya VETA huko vijijini?
Hii ni dhahiri kuwa CCM kwa nyakati hizi sio nyakati zake na sio tu kuwa CHAMA TAWALA hata kuwa CHAMA KIKUU CHA UPINZANI haistahili, zaidi ya kuwa chama marehemu au kikundi cha vikoba au chama cha kufa na kuzikana.
Ona hii, leo 2021 Waziri wa Viwanda anasimama kwa mbwembwe kuzindua Trela la kwanza kuundwa nchini na kujisifu kwa uvumbuzi huo wakati wenzetu majirani miaka kadhaa nyuma 2018 walizindua Setellite yao kwa kushirikiana na Japan.
Kweli sie kutengeneza Trela la mizigo ni suala la kitaifa wakati hayo mambo yalikuwa yanaweza kuwa yanazalishwa na vyuo vya VETA huko vijijini?
Hii ni dhahiri kuwa CCM kwa nyakati hizi sio nyakati zake na sio tu kuwa CHAMA TAWALA hata kuwa CHAMA KIKUU CHA UPINZANI haistahili, zaidi ya kuwa chama marehemu au kikundi cha vikoba au chama cha kufa na kuzikana.