Serikali ya CCM kusaliti maendeleo maendeleo ya Watanzania?

Dingswayo

JF-Expert Member
May 26, 2009
4,019
2,923
Katika taarifa ya habari ya ITV nimemsikia waziri Nagu, katika kampeni za Arumeru, akisema kuwa shughuli za maendeleo yaliyopangwa na serikali katika sehemu hizo, yatacheleweshwa (kwa makusudi) iwapo wanachi watamchagua mgombea wa chama cha upinzani. Binafsi mimi nimeona kuwa hii ni 'blackmail' inayofanywa makusudi na viongozi wa serikali ili kuwatisha wananchi na kuwalazimisha wachague mgombea ambao hao viongozi wa serikali wanamtaka. Maendeleo ni ya raia wote bila kujali muelekeo wao wa kichama.
 
kwanza kauli za wanasiasa wetu zinatolewakutokana na sisi wananchi kutoijua siasa, kwani tumengangania uchama sana, kama chadema bc yy chadema,ccm,yy ccm,kama cuf,yy cuf, hatuangalii vipi mtu anaweza kusaidia jamii hta kma yupo chama kingine,hivyo mkiwekewa waropokaji kama hao mtawachagua tu.
:sleepy:
 
hivi maendeleo huletwa na serikali au jitihada za wananchi wenyewe? huyu mama ana mimba ya uzeeni...
 
Huyo mama "guNa" ni kama ana mtindio wa ubongo sijui kwa nini bado ni waziri sijui ana output gani ya maana kwa watz hadi jk mng'ang'anie kiasi hicho
 
waziri katoa kauli ya serikali kuwa majimbo yote yaliyo na wabunge wa upinzani wanacheleweshewa maendeleo yanayogharamiwa na serikali? tunaomba mwongozo wa kiongozi mkuu! majimbo yenye wapinzani poleni.
 
waziri katoa kauli ya serikali kuwa majimbo yote yaliyo na wabunge wa upinzani wanacheleweshewa maendeleo yanayogharamiwa na serikali? tunaomba mwongozo wa kiongozi mkuu! majimbo yenye wapinzani poleni.
NAGU
ACHA KICHAAAAAAAAAAAAAAAAA....UHUNIIIIIIIIIIIIIIIIII na ULEVIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIII ...unamwaibisha RAIS.
 
Back
Top Bottom