Serikali ya CCM ina kitu cha kujifunza kinachotokea kuhusu Rais Mstaafu Zuma nchini Afrika Afrika

SankaraBoukaka

JF-Expert Member
Jul 2, 2019
910
1,394
Nafkiri Serikali ya CCM na Watanzania kwa ujumla wetu kuna kitu cha kujifunza kupitia VURUGU zinazoendelea kuhusu kifungo cha ZUMA.

Kiuhalisia asilimia kubwa ya hao wanaondamana na kuleta fujo ni wale ambao wameona wamepata FURSA ya kuonyesha na kupunguza STRESS na HASIRA zao kwa mambo mengi mabovu yanayoendelea kwenye nchi yao haswa baada ya kuingiliwa na COVID 19.

Tanzania ni nchi ya 6 kwa UWINGI wa watu Afrika, ikiwa nyuma ya Nigeria, Ethiopia, Misri, DR Congo na Afrika ya Kusini. Ukiangalia kwa makini hizo nchi zote zimepitia au zinapitia matatizo ambayo kwa asilimia kubwa yameletwa na Uongozi Mbovu wa hizo nchi.

Katika Tanzania yetu kwa sasa ajira ni tatizo linaloonekana kuanza kukua pole pole, kama serikali haitokuwa na mipango thabiti ya kupanua njia za ajira basi tutegemee kuwa hawa watu wanaomwagika mitaani kila mwaka baada ya kumaliza Elimu zao ipo siku wataibua matatizo makubwa... Nikiwa na maana kwamba siku uvumilivu ukiwashinda na kwa jinsi hii idadi yao inavyozidi kua kubwa kila mwaka, ina maana iko siku watatafuta chochote ili waonyeshe MAUMIVU yao.

Serikali ya CCM ni muda sasa wa kupanua njia za ajira na kuacha kufikiria KUSHINDA CHAGUZI ZINAZOFUATA... na sekta pekee ambayo inaweza kupunguza makali ya ni SEKTA YA KILIMO,, kwa hakika mwaka ambao Serikali itaamua kulivalia njuga kikamilifu KILIMO ili kiwe na TIJA itafungua njia nyingi za ajira... LA SIVYO TUSUBIRIE MLIPUKO WA BOMU TUNALOJITEGEA WENYEWE..
 
Nafkiri Serikali ya CCM na Watanzania kwa ujumla wetu kuna kitu cha kujifunza kupitia VURUGU zinazoendelea kuhusu kifungo cha ZUMA.

Kiuhalisia asilimia kubwa ya hao wanaondamana na kuleta fujo ni wale ambao wameona wamepata FURSA ya kuonyesha na kupunguza STRESS na HASIRA zao kwa mambo mengi mabovu yanayoendelea kwenye nchi yao haswa baada ya kuingiliwa na COVID 19.

Tanzania ni nchi ya 6 kwa UWINGI wa watu Afrika, ikiwa nyuma ya Nigeria, Ethiopia, Misri, DR Congo na Afrika ya Kusini. Ukiangalia kwa makini hizo nchi zote zimepitia au zinapitia matatizo ambayo kwa asilimia kubwa yameletwa na Uongozi Mbovu wa hizo nchi.

Katika Tanzania yetu kwa sasa ajira ni tatizo linaloonekana kuanza kukua pole pole, kama serikali haitokuwa na mipango thabiti ya kupanua njia za ajira basi tutegemee kuwa hawa watu wanaomwagika mitaani kila mwaka baada ya kumaliza Elimu zao ipo siku wataibua matatizo makubwa... Nikiwa na maana kwamba siku uvumilivu ukiwashinda na kwa jinsi hii idadi yao inavyozidi kua kubwa kila mwaka, ina maana iko siku watatafuta chochote ili waonyeshe MAUMIVU yao.

Serikali ya CCM ni muda sasa wa kupanua njia za ajira na kuacha kufikiria KUSHINDA CHAGUZI ZINAZOFUATA... na sekta pekee ambayo inaweza kupunguza makali ya ni SEKTA YA KILIMO,, kwa hakika mwaka ambao Serikali itaamua kulivalia njuga kikamilifu KILIMO ili kiwe na TIJA itafungua njia nyingi za ajira... LA SIVYO TUSUBIRIE MLIPUKO WA BOMU TUNALOJITEGEA WENYEWE..
Sidhan kama watakuelewa hawa wanaowaza kwa matumbo
 
Back
Top Bottom