Serikali ya CCM iliahidi kutengeneza njia nne mlima wa Mbalizi Mbeya hadi leo kimya, Dr. Tulia sasa wewe ndio mbunge wa Mbeya, unasubiri vifo vingapi?

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,023
18,563
Hakuna kitu kinakera kama ahadi za uwongo wa wanasiasa. Na mbaya zaidi ni pale ambapo wanaahidi uongo kwa vitu ambavyo vinagharimu maisha ya watu. Kwa nini wanasiasa wanapenda kusema uongo?

Tuchukulie huu mteremko wa Mbalizi unapotoka Mbeya mjini kwenda Songwe airport, Mbozi Tunduma na hata Zambia, Zimbabwe, Botswana, Afrika Kusini, Congo nk. Ni barabara muhimu sana hii, na sehemu hii imeua watu wengi kutia ndani viongozi wa serikali na kuharibu mali za mabilioni ya fedha.

Kila inapotokea ajali, viongozi wanakuja na maneno matamu sana ya ahadi kurekebisha sehemu hii, ambayo ni fupi sana, kama kilomita moja na nusu tu. Miaka nenda miaka rudi hakuna kilichofanyika.

Mnataka nani afe hapo ili mchukue hatua, Waziri Mkuu? Au mnataka Watanzania wangapi wafe kabla ya kuchukua hatua?

Hii barabara si kwa ajili ya watu wa Mbeya tu, na kumbukeni kunapotokea ajali hata wasafiri wanaokwenda airport Songwe wanaathirika. Kama serikali ya CCM iliweza kutoa ahadi za papo kwa hapo kujenga barabara za lami zisizo kwenye mipango ya serikali wakati wa kampeni, mnashindwaje kutenga fungu ili kuweka njia nne katika hii sehemu ya barabara kuu Tanzania?

Kwako wewe Tulia kama Mbunge wa Mbeya. Umuhimu wa kuweka njia nne katika hii barabara ya Mbeya, kuanzia Uyole hadi sehemu ya Airport Songwe, haupaswi kuwa jambo ambalo unatakiwa uambiwe. Msongamano wa magari na ajali zinazotokea maeneo ya Mwanjelwa ni jambo lililowazi hata kwa mtu asiye na PhD, sasa kwa nini kwako liwe gumu kuliona?

Wiki hii imetokea ajali nyingine tena ambapo loli la shaba limegonga magari matano hivi. Vifo ambavyo vingeweza kutokea hapa inatisha kuwazia.

Natoa wito kwa wakazi wa Mbeya kwamba mnapaswa kuja juu kudai haki yenu ya kuendelea kuishi ili sehemu hii ijengwe njia nne. Daini kwamba tozo za miamala za mwezi ujao lazima zipelekwe hapa Mbalizi kujenga njia nne kwa sababu kuna hatari za vifo, papewe kipao mbele kwenye kutumia fedha za tozo.

Na kwa nini watu wa Mbeya mnaridhika na msongamano uliopo Mwanjelwa wakati uwezo wa kudai hii barabara ipanuliwe sehemu hii kuwa njia nne toka Uyole hadi Songwe airport serikali inao ila inawapuuza? Nyie ndio mnalisha karibu asilimia 50% ya Tanzania lakini serikali inakosa kuonyesha shukurani kwenu kwa kitu kidogo kama kurekebisha hii sehemu ya Songwe ili watu wasiendelee kufa. Mnakubali mabilioni yakajenge international airport Chato na kufanyiwa matamasha ya ngoma. Si mliambiwa mkimtosa Sugu mambo yenu yatanyooshwa? Wake up!

1631260818479.png
 
Hii ni zaidi ya hatari
Watu wa Mbeya hodari kwenye uchawi tu, lakini hapa ilikuwa piga ua hakieleweki hadi parekebishwe! Kila siku wanaahidiwa tu, lakini wanafurahia kuna tu viongozi wao wanakata viuno kucheza ngoma. Hakuna sehemu inanikera nikienda Mbeya kama hii sehemu wanaita Mwanjelwa. Msongamano wa watu, magari, machinga, baiskeli, daladala lakini wao wanajionea sawa tu. Sijui kama huyo Mbunge wao Tulia anatumia helikopta akiwa Mbeya haoni hizi kero?

Kama kuna watu wanahitaji kukumbushwa wajibu wao kwa kupopolewa na mawe tena, basi na liwe! Mbeya hampaswi kuchezewa kama watoto wadogo, asee🤣🤣🤣
 
Yaani nilikuwa nasubiri kwa hamu watu wa Mbeya waje na comments hapa. Naona wanaona aibu sijui ukweli unauma?
 
Hakuna kitu kinakera kama ahadi za uwongo wa wanasiasa. Na mbaya zaidi ni pale ambapo wanaahidi uongo kwa vitu ambavyo vinagharimu maisha ya watu. Kwa nini wanasiasa wanapenda kusema uongo?

Tuchukulie huu mteremko wa Mbalizi unapotoka Mbeya mjini kwenda Songwe airport, Mbozi Tunduma na hata Zambia, Zimbabwe, Botswana, Afrika Kusini, Congo nk. Ni barabara muhimu sana hii, na sehemu hii imeua watu wengi kutia ndani viongozi wa serikali na kuharibu mali za mabilioni ya fedha.

Kila inapotokea ajali, viongozi wanakuja na maneno matatu sana ya ahadi kurekebisha sehemu hii, ambayo ni fupi sana, kama kilomita moja na nusu tu. Miaka nenda miaka rudi hakuna kilichofanyika.

Mnataka nani afe hapo ili mchukue hatua, Waziri Mkuu? Au mnataka Watanzania wangapi wafe kabla ya kuchukua hatua?

Hii barabara si kwa ajili ya watu wa Mbeya tu, na kumbukeni kunapotokea ajali hata wasafiri wanaokwenda airport Songwe wanaathirika. Kama serikali ya CCM iliweza kutoa ahadi za papo kwa hapo kujenga barabara za lami zisizo kwenye mipango ya serikali wakati wa kampeni, mnashindwaje kutenga fungu ili kuweka njia nne katika hii sehemu ya barabara kuu Tanzania?

Kwako wewe Tulia kama Mbunge wa Mbeya. Umuhimu wa kuweka njia nne katika hii barabara ya Mbeya, kuanzia Uyole hadi sehemu ya Airport Songwe, haupaswi kuwa jambo ambalo unatakiwa uambiwe. Msongamano wa magari na ajali zinazotokea maeneo ya Mwanjelwa ni jambo lililowazi hata kwa mtu asiye na PhD, sasa kwa nini kwako liwe gumu kuliona?

Wiki hii imetokea ajali nyingine tena ambapo loli la shaba limegonga magari matano hivi. Vifo ambavyo vingeweza kutokea hapa inatisha kuwazia.

Natoa wito kwa wakazi wa Mbeya kwamba mnapaswa kuja juu kudai haki yenu ya kuendelea kuishi ili sehemu hii ijengwe njia nne. Daini kwamba tozo za miamala za mwezi ujao lazima zipelekwe hapa Mbalizi kujenga njia nne kwa sababu kuna hatari za vifo, papewe kipao mbele kwenye kutumia fedha za tozo.

Na kwa nini watu wa Mbeya mnaridhika na msongamano uliopo Mwanjelwa wakati uwezo wa kudai hii barabara ipanuliwe sehemu hii kuwa njia nne toka Uyole hadi Songwe airport serikali inao ila inawapuuza? Nyie ndio mnalisha karibu asilimia 50% ya Tanzania lakini serikali inakosa kuonyesha shukurani kwenu kwa kitu kidogo kama kurekebisha hii sehemu ya Songwe ili watu wasiendelee kufa. Mnakubali mabilioni yakajenge international airport Chato na kufanyiwa matamasha ya ngoma. Si mliambiwa mkimtosa Sugu mambo yenu yatanyooshwa? Wake up!

View attachment 1931739
mpaka dhambi ya kuiba kura za sugu mtakapotubu, endeleeni kuchuma dhambi.
 
Hakuna kitu kinakera kama ahadi za uwongo wa wanasiasa. Na mbaya zaidi ni pale ambapo wanaahidi uongo kwa vitu ambavyo vinagharimu maisha ya watu. Kwa nini wanasiasa wanapenda kusema uongo?

Tuchukulie huu mteremko wa Mbalizi unapotoka Mbeya mjini kwenda Songwe airport, Mbozi Tunduma na hata Zambia, Zimbabwe, Botswana, Afrika Kusini, Congo nk. Ni barabara muhimu sana hii, na sehemu hii imeua watu wengi kutia ndani viongozi wa serikali na kuharibu mali za mabilioni ya fedha.

Kila inapotokea ajali, viongozi wanakuja na maneno matatu sana ya ahadi kurekebisha sehemu hii, ambayo ni fupi sana, kama kilomita moja na nusu tu. Miaka nenda miaka rudi hakuna kilichofanyika.

Mnataka nani afe hapo ili mchukue hatua, Waziri Mkuu? Au mnataka Watanzania wangapi wafe kabla ya kuchukua hatua?

Hii barabara si kwa ajili ya watu wa Mbeya tu, na kumbukeni kunapotokea ajali hata wasafiri wanaokwenda airport Songwe wanaathirika. Kama serikali ya CCM iliweza kutoa ahadi za papo kwa hapo kujenga barabara za lami zisizo kwenye mipango ya serikali wakati wa kampeni, mnashindwaje kutenga fungu ili kuweka njia nne katika hii sehemu ya barabara kuu Tanzania?

Kwako wewe Tulia kama Mbunge wa Mbeya. Umuhimu wa kuweka njia nne katika hii barabara ya Mbeya, kuanzia Uyole hadi sehemu ya Airport Songwe, haupaswi kuwa jambo ambalo unatakiwa uambiwe. Msongamano wa magari na ajali zinazotokea maeneo ya Mwanjelwa ni jambo lililowazi hata kwa mtu asiye na PhD, sasa kwa nini kwako liwe gumu kuliona?

Wiki hii imetokea ajali nyingine tena ambapo loli la shaba limegonga magari matano hivi. Vifo ambavyo vingeweza kutokea hapa inatisha kuwazia.

Natoa wito kwa wakazi wa Mbeya kwamba mnapaswa kuja juu kudai haki yenu ya kuendelea kuishi ili sehemu hii ijengwe njia nne. Daini kwamba tozo za miamala za mwezi ujao lazima zipelekwe hapa Mbalizi kujenga njia nne kwa sababu kuna hatari za vifo, papewe kipao mbele kwenye kutumia fedha za tozo.

Na kwa nini watu wa Mbeya mnaridhika na msongamano uliopo Mwanjelwa wakati uwezo wa kudai hii barabara ipanuliwe sehemu hii kuwa njia nne toka Uyole hadi Songwe airport serikali inao ila inawapuuza? Nyie ndio mnalisha karibu asilimia 50% ya Tanzania lakini serikali inakosa kuonyesha shukurani kwenu kwa kitu kidogo kama kurekebisha hii sehemu ya Songwe ili watu wasiendelee kufa. Mnakubali mabilioni yakajenge international airport Chato na kufanyiwa matamasha ya ngoma. Si mliambiwa mkimtosa Sugu mambo yenu yatanyooshwa? Wake up!

View attachment 1931739
Hiyo sehemu ni hatari sana, Nakumbuka kuna gari moja ya mafuta MT Meru iliwahi kufeli kupanda hapo ikarudi nyuma aloo mbona ilikua balaa, na ule mlima nyoka kama unaitafuta Uyole ni shida.

Sema watu wengi tu wakiwa wanapaona hivi tu kwenye picha wanapachukulia pa kawaida sana ila ukifikapo utaona uhatari wake, pamekaa vibaya mno na ni rahisi sana kuchukua roho za watu endapo ajali ikitokea.
 
inasikitisha sana, wao wanatembea na vx na vingora.
Hilo ndio nakataa. Kwa nini Watanzania tunapenda kusema tu kusikitika bila kufanya kitu? Hizi ajali za hapa Mbalizi Mbeya zinaepukika kabisa.

Kwa mfano, barabara ya Morogoro kwenye mabonde kati ya Chalinze na Bwawani ilikuwa inaua sana. Ajali ziliisha pale wakati serikali ilipoamua kuweka climbing lanes kwenye hicho kipande.

Sasa kwa nini pale Mbeya sehemu ya Mbalizi hawafanyi hivo, kipande cha chini ya kilomita mbili tu?
 
Hakuna kitu kinakera kama ahadi za uwongo wa wanasiasa. Na mbaya zaidi ni pale ambapo wanaahidi uongo kwa vitu ambavyo vinagharimu maisha ya watu. Kwa nini wanasiasa wanapenda kusema uongo?

Tuchukulie huu mteremko wa Mbalizi unapotoka Mbeya mjini kwenda Songwe airport, Mbozi Tunduma na hata Zambia, Zimbabwe, Botswana, Afrika Kusini, Congo nk. Ni barabara muhimu sana hii, na sehemu hii imeua watu wengi kutia ndani viongozi wa serikali na kuharibu mali za mabilioni ya fedha.

Kila inapotokea ajali, viongozi wanakuja na maneno matatu sana ya ahadi kurekebisha sehemu hii, ambayo ni fupi sana, kama kilomita moja na nusu tu. Miaka nenda miaka rudi hakuna kilichofanyika.

Mnataka nani afe hapo ili mchukue hatua, Waziri Mkuu? Au mnataka Watanzania wangapi wafe kabla ya kuchukua hatua?

Hii barabara si kwa ajili ya watu wa Mbeya tu, na kumbukeni kunapotokea ajali hata wasafiri wanaokwenda airport Songwe wanaathirika. Kama serikali ya CCM iliweza kutoa ahadi za papo kwa hapo kujenga barabara za lami zisizo kwenye mipango ya serikali wakati wa kampeni, mnashindwaje kutenga fungu ili kuweka njia nne katika hii sehemu ya barabara kuu Tanzania?

Kwako wewe Tulia kama Mbunge wa Mbeya. Umuhimu wa kuweka njia nne katika hii barabara ya Mbeya, kuanzia Uyole hadi sehemu ya Airport Songwe, haupaswi kuwa jambo ambalo unatakiwa uambiwe. Msongamano wa magari na ajali zinazotokea maeneo ya Mwanjelwa ni jambo lililowazi hata kwa mtu asiye na PhD, sasa kwa nini kwako liwe gumu kuliona?

Wiki hii imetokea ajali nyingine tena ambapo loli la shaba limegonga magari matano hivi. Vifo ambavyo vingeweza kutokea hapa inatisha kuwazia.

Natoa wito kwa wakazi wa Mbeya kwamba mnapaswa kuja juu kudai haki yenu ya kuendelea kuishi ili sehemu hii ijengwe njia nne. Daini kwamba tozo za miamala za mwezi ujao lazima zipelekwe hapa Mbalizi kujenga njia nne kwa sababu kuna hatari za vifo, papewe kipao mbele kwenye kutumia fedha za tozo.

Na kwa nini watu wa Mbeya mnaridhika na msongamano uliopo Mwanjelwa wakati uwezo wa kudai hii barabara ipanuliwe sehemu hii kuwa njia nne toka Uyole hadi Songwe airport serikali inao ila inawapuuza? Nyie ndio mnalisha karibu asilimia 50% ya Tanzania lakini serikali inakosa kuonyesha shukurani kwenu kwa kitu kidogo kama kurekebisha hii sehemu ya Songwe ili watu wasiendelee kufa. Mnakubali mabilioni yakajenge international airport Chato na kufanyiwa matamasha ya ngoma. Si mliambiwa mkimtosa Sugu mambo yenu yatanyooshwa? Wake up!

View attachment 1931739
Huyo aliyepita kabla yake, awamu yake huo mlima haukuwepo.
 
Huyo aliyepita kabla yake, awamu yake huo mlima haukuwepo.
Hatuongei juu ya mtu bali serikali ya CCM ambayo ndio inaidhinisha mipango ya fedha. Aliyepita kabla yake hakuwa na serikali ya Chadema, na kwa kuwa kulikuwa na CCM walifanya makusudi kuwakomoa watu wa Mbeya.

Lakini si walisema muondoeni Sugu tawape maendeleo? So?
 
Poleni wana Mbeya
Nalog off
Tunapoongea damu za wanachi kumwagika sehemu hii, ni literally, ona damu hii iliyopotea kwa uzembe tu wa hii serikali, si afadhali ingemwagiga katika harakati za kuwaondoa watu waovu na wadhulumaji nchini?

1631281504433.png
 
Hatuongei juu ya mtu bali serikali ya CCM ambayo ndio inaidhinisha mipango ya fedha. Aliyepita kabla yake hakuwa na serikali ya Chadema, na kwa kuwa kulikuwa na CCM walifanya makusudi kuwakomoa watu wa Mbeya.

Lakini si walisema muondoeni Sugu tawape maendeleo? So?
Kwani Dr Tulia ni mtu au Chama ?
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom