Tungekuwa tunaongelea sana neno la kumzuia na kumlinda mtoto mjamzito kupata mimba akiwa shule ingesaidia sana kuliko kuendelea na mtoto mjamzito kuendelea au kutoendelea na shule.....kujadili hivi ni kukubaliana na tatizo..

Tutapambane zaidi na mbinu za kumlinda mtoto wa kike awe salama na ikiwezekana na wa kiume awe salama pia...

Ikigundulika binti kaingiliwa na mtu mzima hata bila kupewa mimba basi mhusika atiwe mbaroni akatumikie 30yrs....ikigundulika mchezo huu wanafanya wenyewe kwa wenyewe watoto walio shule basi wazazi waitwe watoto wahamishwe shule tofauti tofauti na adhabu kali, ikiwa pamoja na wazazi wote kuilipa faini serikali..Ulinzi huu uendane sambamba na ulinzi wa maadili ya jamii nzima...
Kama Nyerere alianzisha elimu ya watu wazima na ikawezekana, iweje leo uwe mjadala kama msichana akipata mimba arudi aun asirudi shule?

Juu ya kuwalinda wasichana na mahusiano, hilo lipo tayari. Hata kisheria juu ya hukumu kwa atayepatikana kuwachezea hawa watoto. Lakini tatizo bado lipo, ndio maana ni muhimu kujadili juu ya hatma ya huyu mhusika msichana aliyepata mimba licha ya kuwepo sheria ngumu kwa mwanaume aliyehusika na hayo.
 
Apate mimba, azae tu kwani sheria inamlinda, awape jukumu la malezi baba na mama yake, arudi shule, ahitimu apate cheti cha mtoto na elimu.. After 30 yrs amsimange mume wake anaetoka jela kwa mafanikio makubwa...
 
Kumfunga baba aliyempa mwanafunzi mimba ni kumyima mtoto aliyezaliwa haki ya kuwa na baba.
 
Definitely mkuu mtoto ws kike aliyepata mimba aruhusiwe kuendelea na masomo yake,serikali impe grants ya mtoto aliyezaliwa na muda wa mapumziko apewe haki ya kumnyonyesha mtoto wake.
 
Mi siungi mkono hilo suala, ni kuzidisha umalaya kwa watoto wa shule. Na kuhamasisha hata wale waliotaka kuzaa wakiwa wadogo kutimiza ndoto zao hizo kwani kinachozuiaga zaido ni shule.

Lakini pia hata ile nguvu ya kumsaka aliempa hiyo mimba itapungua mno, familia ya kiumeni ikiafikiana na ile ya kike kutunza mtoto na kulipa fidia usitegemee kesi hapo ni mwendo wa kulindana tu ukizingatia mtoto wa kike ataendelea kusoma hivyo hajaaribiwa kiivo zaidi ya kupoteza muda ambao kwa wakati huo huyo bint hauna thaman sana.

Na mbona huwa wanasoma japo si kwa kurudi shule za serikali, wengi hukimbilia private. Ingebaki hivyo hivyo ila hii kwa hapa kwetu tusitegemee matokeo mazuri .
 
Binafsi Kama mwalimu kwa muda wa zaidi ya miaka kumi sasa nimekuwa nikishuhudia watoto wakikatiza masomo yao kila mwaka,kwa uzoefu wangu watoto walio wengi takribani asilimia 99.99 ya wapatao mimba Ni wale ambao darasani hawajiwezi,yaani hata daraja la nne ni kulipata kwa watoto Hawa ni shida,na Mara nyingi utakuta ni wale walio kata tamaa kiasi kwamba hata ukisema warudi shuleni sidhani Kama watakuwa tayari kurudi.

Mimi Kama binafsi naunga hoja ya watoto waliozaa kurudi shuleni huku nikikosoa kwanini tumekumbilia kwenye tiba badala ya kung'ang'ana na kinga kwanza?, Kusema kuwa mtoto aliyejufungua arudi shule bila ya kumpa mikakati ya kujilinda na mimba ni sawa na kuwaruhusu hawa wengine ambao hawajapatwa na tatizo hili nao wapate,hivyo ni vyema serikali iangalie njia sahihi za kuwasaidia watoto wa shule jinsi ya kupambana na mimba za utotoni na sio kuja na suruhu ya kuwarudisha shuleni bila kutatua changamoto zinazo wakabili .

Hivyo Kama Mimi nikipewa nafasi hii ya kutafuta suruhu ya hii changamoto ya mimba kwa wanafunzi ningesema kuwa watoto wapewe elimu ya uzazi na pia wafundishwe njia za uzazi wa mpango hili ndilo litakuwa mwarobaini wa mimba kwa watoto wetu.kila Mara huwa napenda kutolea mfano mkoa wa Lindi ulivyo na mwamko juu ya elimu ya uzazi wa mpango,nimefundisha Lindi kwa miaka 7 lakini case za mimba nilizozishuhudia hazizidi kumi, vituko nilivyovishudia Kanda ya ziwa ni hatari kwa mwaka mmoja huwezi kosa watoto kumi ambao hukatiza masomo yao juu ya mimba.

Hivyo serikali iache kuzunguka mbuyu, elimu ya uzazi wa mpango kwa Kanda ya ziwa ni duni Sana,wao wanaamini kuwa ukitumia sindano,vitanzi na njiti utakuwa mgumba au kupata shida Wakati wa kujifungua ,ukiangalia kwa umakini utaona kuwa jamii hii Haina elimu sahihi juu ya Jambo husika .

Hivyo wakati serikali ikisisitiza watoto waliopata mimba kurudi mashuleni,inapaswa pia kuja na mikakati ya kuzuia mimba hizo,moja ya mikakati ni utoaji elimu ya uzazi sambamba na matumizi ya njia za uzazi wa mpango.

Pia serikali ipate watu sahihi wa kuzunguka nchi nzima ili kutoa elimu mashuleni juu ya afya ya uzazi na njia za uzazi wa mpango sambamba na kuongeza kipengere katika masomo amabacho kitaeleza namna ya kujikinga na magonjwa ya zinaa pamoja na mimba za utotoni.
 
Minadhani tungeangalia namna bora ya kuzuia hili tatizo la mimba za utotoni mfano kupitisha sheria ya kunyonga yeyote atakae pata mimba akiwa chini ya umri wa utu uzima na hajabakwa tukihakikisha hili swala limewafikia familia zote na wakapatikana kama mia ivii wa mfano hili swala litabaki kuwa ni historia katika taifa letu
 
Aendelee na serikali ichukue jukumu la kuwaanzishia shule zao maalumu na watoe incentives kwa wadau binafsi na ngos kuiunga mkono serikali kuanzisha shule za wanafunzi wazazi ili wasiwaambukize wenzao upataji mimba. Hii itasaidia kupunguza utoaji mimba wa kiholela.

Bahati mbaya CCM hawafikiri kwa jinsi hii bali wanapongezana kwa kulipatia ufumbuzi tatizo la maji Daisalamu.
 
Binafsi Kama mwalimu kwa muda wa zaidi ya miaka kumi sasa nimekuwa nikishuhudia watoto wakikatiza masomo yao kila mwaka,kwa uzoefu wangu watoto walio wengi takribani asilimia 99.99 ya wapatao mimba Ni wale ambao darasani hawajiwezi,yaani hata daraja la nne ni kulipata kwa watoto Hawa ni shida,na Mara nyingi utakuta ni wale walio kata tamaa kiasi kwamba hata ukisema warudi shuleni sidhani Kama watakuwa tayari kurudi.

Mimi Kama binafsi naunga hoja ya watoto waliozaa kurudi shuleni huku nikikosoa kwanini tumekumbilia kwenye tiba badala ya kung'ang'ana na kinga kwanza?, Kusema kuwa mtoto aliyejufungua arudi shule bila ya kumpa mikakati ya kujilinda na mimba ni sawa na kuwaruhusu hawa wengine ambao hawajapatwa na tatizo hili nao wapate,hivyo ni vyema serikali iangalie njia sahihi za kuwasaidia watoto wa shule jinsi ya kupambana na mimba za utotoni na sio kuja na suruhu ya kuwarudisha shuleni bila kutatua changamoto zinazo wakabili .

Hivyo Kama Mimi nikipewa nafasi hii ya kutafuta suruhu ya hii changamoto ya mimba kwa wanafunzi ningesema kuwa watoto wapewe elimu ya uzazi na pia wafundishwe njia za uzazi wa mpango hili ndilo litakuwa mwarobaini wa mimba kwa watoto wetu.kila Mara huwa napenda kutolea mfano mkoa wa Lindi ulivyo na mwamko juu ya elimu ya uzazi wa mpango,nimefundisha Lindi kwa miaka 7 lakini case za mimba nilizozishuhudia hazizidi kumi, vituko nilivyovishudia Kanda ya ziwa ni hatari kwa mwaka mmoja huwezi kosa watoto kumi ambao hukatiza masomo yao juu ya mimba.

Hivyo serikali iache kuzunguka mbuyu, elimu ya uzazi wa mpango kwa Kanda ya ziwa ni duni Sana,wao wanaamini kuwa ukitumia sindano,vitanzi na njiti utakuwa mgumba au kupata shida Wakati wa kujifungua ,ukiangalia kwa umakini utaona kuwa jamii hii Haina elimu sahihi juu ya Jambo husika .

Hivyo wakati serikali ikisisitiza watoto waliopata mimba kurudi mashuleni,inapaswa pia kuja na mikakati ya kuzuia mimba hizo,moja ya mikakati ni utoaji elimu ya uzazi sambamba na matumizi ya njia za uzazi wa mpango.

Pia serikali ipate watu sahihi wa kuzunguka nchi nzima ili kutoa elimu mashuleni juu ya afya ya uzazi na njia za uzazi wa mpango sambamba na kuongeza kipengere katika masomo amabacho kitaeleza namna ya kujikinga na magonjwa ya zinaa pamoja na mimba za utotoni.
Well said and written from experience by a proffessional teacher (Applause for you)
 
Hili swala halikubaliki msikitini, halikubaliki kanisani chuo kikukuu mpaka kindagateni. Lakini chakushangaza mleta mada angalia sijamsikia mtu yoyote kutoka katika taasisi hizi za kidini akisema chochote wote kimya nini maana yake? sasa mleta mada hata wewe unaonekena unatuonea sisi waumini kwani tunaamini kuwa misikitini na makanisani yaani mashek, wachungaji na mapadre ndiyo hasa ulitakiwa uwatupie swali hili au hoja hii.

Maisha yanakwenda haraka sana ukisoma katika historia na kuuliza wazee wanasema zamani kabla ya wageni kuja watoto wa kike walipelekwa kutailiwa na walifundishwa mambo mengi na wote walikuwa bikira, kiasili heshima ya mtoto wa kike, heshima ya familia ya mtoto wakike, heshima ya ndoa ililetwa na mtoto wa kike kujitunza mpaka muda utakapofika sasa hii ya Chif Hangaya siielewi.

Nyakati za mwisho zimekaribia.
 
Hili swala halikubaliki msikitini, halikubaliki kanisani chuo kikukuu mpaka kindagateni. Lakini chakushangaza mleta mada angalia sijamsikia mtu yoyote kutoka katika taasisi hizi za kidini akisema chochote wote kimya nini maana yake? sasa mleta mada hata wewe unaonekena unatuonea sisi waumini kwani tunaamini kuwa misikitini na makanisani yaani mashek, wachungaji na mapadre ndiyo hasa ulitakiwa uwatupie swali hili au hoja hii.

Maisha yanakwenda haraka sana ukisoma katika historia na kuuliza wazee wanasema zamani kabla ya wageni kuja watoto wa kike walipelekwa kutailiwa na walifundishwa mambo mengi na wote walikuwa bikira, kiasili heshima ya mtoto wa kike, heshima ya familia ya mtoto wakike, heshima ya ndoa ililetwa na mtoto wa kike kujitunza mpaka muda utakapofika sasa hii ya Chif Hangaya siielewi.

Nyakati za mwisho zimekaribia.

Fanya utafiti kidogo tu mfano hapo Pemba ujue bikira zinavyo lindwa. Yesu akasema Ambaye hana dhambi awe wakwanza kumpopoa yule mwanamke mhanga wa kufumaniwa.
 
Binafsi Kama mwalimu kwa muda wa zaidi ya miaka kumi sasa nimekuwa nikishuhudia watoto wakikatiza masomo yao kila mwaka,kwa uzoefu wangu watoto walio wengi takribani asilimia 99.99 ya wapatao mimba Ni wale ambao darasani hawajiwezi,yaani hata daraja la nne ni kulipata kwa watoto Hawa ni shida,na Mara nyingi utakuta ni wale walio kata tamaa kiasi kwamba hata ukisema warudi shuleni sidhani Kama watakuwa tayari kurudi.

Mimi Kama binafsi naunga hoja ya watoto waliozaa kurudi shuleni huku nikikosoa kwanini tumekumbilia kwenye tiba badala ya kung'ang'ana na kinga kwanza?, Kusema kuwa mtoto aliyejufungua arudi shule bila ya kumpa mikakati ya kujilinda na mimba ni sawa na kuwaruhusu hawa wengine ambao hawajapatwa na tatizo hili nao wapate,hivyo ni vyema serikali iangalie njia sahihi za kuwasaidia watoto wa shule jinsi ya kupambana na mimba za utotoni na sio kuja na suruhu ya kuwarudisha shuleni bila kutatua changamoto zinazo wakabili .

Hivyo Kama Mimi nikipewa nafasi hii ya kutafuta suruhu ya hii changamoto ya mimba kwa wanafunzi ningesema kuwa watoto wapewe elimu ya uzazi na pia wafundishwe njia za uzazi wa mpango hili ndilo litakuwa mwarobaini wa mimba kwa watoto wetu.kila Mara huwa napenda kutolea mfano mkoa wa Lindi ulivyo na mwamko juu ya elimu ya uzazi wa mpango,nimefundisha Lindi kwa miaka 7 lakini case za mimba nilizozishuhudia hazizidi kumi, vituko nilivyovishudia Kanda ya ziwa ni hatari kwa mwaka mmoja huwezi kosa watoto kumi ambao hukatiza masomo yao juu ya mimba.

Hivyo serikali iache kuzunguka mbuyu, elimu ya uzazi wa mpango kwa Kanda ya ziwa ni duni Sana,wao wanaamini kuwa ukitumia sindano,vitanzi na njiti utakuwa mgumba au kupata shida Wakati wa kujifungua ,ukiangalia kwa umakini utaona kuwa jamii hii Haina elimu sahihi juu ya Jambo husika .

Hivyo wakati serikali ikisisitiza watoto waliopata mimba kurudi mashuleni,inapaswa pia kuja na mikakati ya kuzuia mimba hizo,moja ya mikakati ni utoaji elimu ya uzazi sambamba na matumizi ya njia za uzazi wa mpango.

Pia serikali ipate watu sahihi wa kuzunguka nchi nzima ili kutoa elimu mashuleni juu ya afya ya uzazi na njia za uzazi wa mpango sambamba na kuongeza kipengere katika masomo amabacho kitaeleza namna ya kujikinga na magonjwa ya zinaa pamoja na mimba za utotoni.
VETA ipo kwa ajili yao!!!! Mwalim ongeza na ilo husisahu kabisa... VETA IPO KWA AJILI YAO
 
.unataka akijifungua aende wapi?
Kikubwa kutoa elimu ya uzazi kwa Hawa watoto.ikitokea amepata mimba asifanyiwe ukatili wa kufukuzwa shule.
Maana unakatisha ndoto zake.
 
Minadhani tungeangalia namna bora ya kuzuia hili tatizo la mimba za utotoni mfano kupitisha sheria ya kunyonga yeyote atakae pata mimba akiwa chini ya umri wa utu uzima na hajabakwa tukihakikisha hili swala limewafikia familia zote na wakapatikana kama mia ivii wa mfano hili swala litabaki kuwa ni historia katika taifa letu
Huu sio mwarobaini mkuu,je wewe waweza fumba jicho lako lililo zima hata kwa wiki moja lisiweze kuona? Unaelewa maana ya bareghe ,je ni nini hutokea Wakati wa bareghe ? Wazazi na serikali tuache kukwepa majukumu kwa kuamini kuwa watoto wetu hawafanyi ngono ili Hali mambo nitofauti,hata sheria ya miaka 30 sio suruhu kwa hili tatizo maana wanaofungwa ni wale wanaokosa pesa za kuyasawazisha mambo pindi yanapoharibika.

Mkuu amini nakuambia kwa miaka zaidi ya kumi niko katika field ya ualimu, watoto wanapata Sana mimba Cha kushangaza sijawahi kuona hata mtu mmoja amefungwa kwa kumpa mimba mwanafunzi kwa maeneo niliyowahi fanyia kazi,Mara nyingi wazazi humalizana na watesi wa watoto wao kimya kimya tu.

Hata Kama hili Jambo litamkuta mwanangu wa kike ,siwezi kubali mgoni wangu akafungwe huku mzigo wa malezi ukibaki kwangu jumlisha na uadui toka kwa familia ya kijana,kwanini nisitatue Jambo hili kwa hekima huku mjukuu wangu akibaki na baba yake,nimfunge mkwe wangu nutajibu nini kwa mjukuu wangu akishajitambua,?

Tuacheni kukwepa majukumu,elimu Ni mhimu Sana kwa pande zote mbili yaani mbakaji na mbakwaji, makundi haya yakipata elimu tutakuwa tumetatua changamoto ya mimba kwa watoto wetu .

ELIMU! ELIMU! ELIMU!
 
Kumfunga baba aliyempa mwanafunzi mimba ni kumyima mtoto aliyezaliwa haki ya kuwa na baba.
Na mababa wengine waliofungwa magereza kwa makosa mengine, vipi haki za watoto wao kuwa na baba?!
Kama hivyo basi hatafungwa mtu..
 
Back
Top Bottom