Serikali, tumieni mbinu hizi ili kukabiliana na vuguvugu la Katiba nchini

NAMBA MOJA AJAYE NCHINI

JF-Expert Member
Oct 29, 2019
8,462
17,291
Maji yakimwagika hayazoleki!

Katiba iliyopo mliiona ni mbovu wenyewe mkaanzisha mchakato wa katiba mpya wenyewe!Wala sio Mbowe wala Lisu wala Upinzani nchini!

Kuendelea kutumia jeshi la polisi kuzuia hiki mlichokianzisha wenyewe ni kujiua wenyewe kisiasa na kupoteza uhalali wa serikali yenu wenyewe!kwani upinzani haukuanzisha huu mchakato bali ninyi! Upinzani unaisaidia serikali kutimiza azma ya wananchi kupata katiba mpya itakayosaidia mchakato wa kupata serikali zijazo nchini.

Ili kujifichia aibu fanyeni yafuatayo:-
1. Anzisheni makongamano endelevu ya mapungufu ya katiba iliyopo ili ku spin makongamano ya katiba mpya ya upinzani yanayoendelea ili kuonyesha mna nia ya dhati ya mabadiliko na mkisema katiba iliyopo wananchi hawaijui tena fanyeni hivyo kwa miaka mitano hadi 2025!

2. Anzisheni somo la Katiba kuanzia shule za msingi hadi sekondari na vyuo mkitaka katiba ieleweke kwa wote!!hii ni ku buy time hadi wakati wa uchaguzi ujao.

3. Muanzishe Baraza la mpito la uchaguzi la maridhiano kwa ajili ya uchaguzi ujao huku mkisisitiza muda wa kupitisha katiba mpya hautoshi!!Baraza lihusishe wenyeviti wa siasa woote nchini. Huku mkisisitiza demokrasia itatamalaki na kurejesha asilimia 40 ya wabunge wa upinzani katika uchaguzi ujao 2025.

3. Mwisho kabisa !!Uchaguzi ujao Katiba mpya iwe ndio ajenda na ilani ya chama tawala ili mpate dola tena!mkisha shika dola mtaanza mchakato wa katiba mpya kuipitisha na mapendekezo yake.

Mkifanya hayo mtapona kwa kipindi hiki cha presha hizi za upinzani! Kuliko kutumia Jeshi la Polisi na kuchafua taswira ya nchi yetu kimataifa.

Ni mimi mtia nia wa Urais 2040 kunapo majaaliwa ya Baba Mwenyezi!!!
 
Angalau ni mbinu ya kiistaarabu ya kuanza nayo ili kuendana na vugu vugu kuliko silaha za moto!!!Ikumbukwe katiba iliyopo sio wote wameisoma na kuijua !hivyo ni fursa nzuri kwa wananchi kuijua katiba yao!!!

Bila kupinga maelezo yako mengine, hivi huu utapeli wa kusema eti katiba iliyopo sio wote wameielewa huwa mnautoa wapi? Katiba ya mwaka 1977 ilipatikana baada ya kila mtu kuelewa iliyokuwepo? Wakati wa rasimu ya Warioba watu wote walikuwa wameshaelewa katiba iliyopo? Mbona kwenye uchaguzi viongozi hupatikana bila watu wote waliojiandikisha kupiga kura? Huu utetezi dhaifu kwanini bado mnaendelea kuutumia?
 
Bila kupinga maelezo yako mengine, hivi huu utapeli wa kusema eti katiba iliyopo sio wote wameielewa huwa mnautoa wapi? Katiba ya mwaka 1977 ilipatikana baada ya kila mtu kuelewa iliyokuwepo? Wakati wa rasimu ya Warioba watu wote walikuwa wameshaelewa katiba iliyopo? Mbona kwenye uchaguzi viongozi hupatikana bila watu wote waliojiandikisha kupiga kura? Huu utetezi dhaifu kwanini bado mnaendelea kuutumia?
Bora hii ni ya kisiasa zaidi kuliko Barabara kuwekewa vizuizi kisa mwenyekiti kaja kwenye kongamano!!!
 
Bora hii ni ya kisiasa zaidi kuliko Barabara kuwekewa vizuizi kisa mwenyekiti kaja kwenye kongamano!!!

Ccm hawana ushawishi tena wa kisiasa, wala uwezo wa kukabiliana na hoja za kisiasa. Njia pekee ni matumizi ya mabavu. Mama wa kambo alianza vizuri, ila wanaccm wenzake wakamkumbusha ukweli kuwa chama chao kimeshapoteza mvuto, kuruhusu chama chenye mvuto kuteka hisia za wananchi ni kuchimba shimo kwa chama chao.Namna pekee ni kutumia mabavu.
 
Naona Mama samia kachukua ushauri namba tatu hapo juu!!Lakini amefeli kuishawishi CHADEMA!!!Kumbe niliandika ya msingi Sana kipindi hicho!!!Haya maono nilitoa wapi!?nadhani karama ipo ndani MWANGU!!!wenye mamlaka muanze kuni fikiria !!!
 
Naona Mama samia kachukua ushauri namba tatu hapo juu!!Lakini amefeli kuishawishi CHADEMA!!!Kumbe niliandika ya msingi Sana kipindi hicho!!!Haya maono nilitoa wapo!!!?nadhani karma ipo ndani MWANGU!!!wenye mamlaka mianze kuni fikiria !!!
Hahahah kwakweli
 
Back
Top Bottom