Pakawapakawa
Senior Member
- Nov 19, 2012
- 110
- 20
Ndugu wana JF, wana CCM kupongeza nii tabia ya woga au uenda wazimu?. Mara nyingi tumekuwa tukisikia na hasa kutoka Bungeni na kwenye mikutano mbalimbali wa chama yenye wajumbe "makini"! na wengi kutoka Chama Tawala (CCM) wakisifu na kupongeza usikivu wa serikali ya CCM. Hata hivyo hao hao wamekuwa walalamishi wakubwa juu ya utendaji mbovu wa serikali yetu!. Na si hao tu, bali uongozi wa chama kuanzia ngazi ya shina hadi Taifa tunaona wanavyo lalamika. Je kulalamika ni tabia au pongezi zinazotolewa ni kujipanga mafuta kwa mgongo wa chupa?.