Serikali: Rushwa ya ngono vyuoni inazalisha wataalam wasio na vigezo

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,806
11,968
Ongezeko la vitendo vya ukatili wa jinsia na rushwa ya ngono kwenye vyuo vikuu inatajwa kuathiri tasnia ya elimu Nchini na matokeo yake ni kupatikana kwa wahitimu wasio na uwezo kutokana na baadhi yao kupata shahada zao pasi na kuzitolea jasho.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Amon Mpanju amesema hayo.

Kutoka na ongezeko la matukio ya aina hiyo katika Vyuo Vikuu limefanya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kuzindua Dawati la Jinsia katika Chuo Kikuu cha Dodoma, ndipo katika uzinduzi huo Mpanju akaeleza athari za vitendo hivyo.

“Matukio kama hayo yanasababisha kuzalisha wataalam ambao hawana vigezo, natoa wito kwa madawati kama haya kufanya kazi kwa usiri,” - Mpanju.

Naye, Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Profesa James Mdoe amesema yakiwemo manyanyaso ya kijinsia au mengine akili haiwezi kufanya kazi, hivyo sio rahisi kwa wanafunzi kufikia ndoto zao.
 
Kuna scandal ya boss na staff wa UN wakilana kwenye gari la UN huko Lebanon 🇱🇧. UN kwanza wajitahidi kuwa wasafi kabla ya kuekekeza vidole huko.

Kuna case mwana dada kapeleka report kwa “wanene wa trapping “ hao wanene wakamtonya mtaka utelezi asiende huko hotelini kuna mtego.
 
Hii rushwa itaisha siku tu kutakapokuwa na mfumo mwingine kabisa wa kuwasahihishia wana chuo, na wenye mfanano na ule wa NECTA.

Ila kwa huu mfumo wa sasa wa kumuachia mwanadamu mmoja anayeitwa lecturer!! maamuzi makubwa juu ya hatma ya mwanadamu mwingine, kamwe haitoisha.
Hapa ndo GPA za vyuo vikuu naonaga takataka kabisa ......mie naamini matokeo ya kidato cha NNE na sita tu
 
Hapa ndo GPA za vyuo vikuu naonaga takataka kabisa ......mie naamini matokeo ya kidato cha NNE na sita tu
Uko sahihi kabisa. Tena elimu ya form six ndiyo inayoongoza kwa utamu. Kwanza unasoma miaka michache! Halafu unasoma masomo machache!

Hivyo kupata Division One ni rahisi mpaka basi. Ila siyo chuo. Wale jamaa wamepeaa mamlaka makubwa sana, kiasi cha kugeuka kuwa waharibifu kwa dada na mama zetu
 
Hii rushwa itaisha siku tu kutakapokuwa na mfumo mwingine kabisa wa kuwasahihishia wana chuo, na wenye mfanano na ule wa NECTA.

Ila kwa huu mfumo wa sasa wa kumuachia mwanadamu mmoja anayeitwa lecturer!! maamuzi makubwa juu ya hatma ya mwanadamu mwingine, kamwe haitoisha.
Upo sahihi. Huyu kitila alishawahi kutufanyia mambo ya kipuuzi sana pale UDSM.
 
Kukosekana kwa maadili katika utumishi wa umma ni hatar katika mpya kiongozi wa serikali yeyote Yule akijiingiza katika mambo kama hayo afutwe kazi wengine huku wanabeba mimba mume hajulikani angalau pawe na ndo eti mkuu wa wilaya haya yote ni miongoni mwa ukosefu wa maaadili
 
Malipo Ni hapa hapa duniani mhadhiri badala ya kuwa Kama mlezi kwa wanafunzi yeye ndio anakuwa fisi mla nyama sijui utajisikiaje mwanao umempeleka chuo anageuzwa na kuliwa na mhadhiri ambaye anatakiwa kuelimisha
 
Ongezeko la vitendo vya ukatili wa jinsia na rushwa ya ngono kwenye vyuo vikuu inatajwa kuathiri tasnia ya elimu Nchini na matokeo yake ni kupatikana kwa wahitimu wasio na uwezo kutokana na baadhi yao kupata shahada zao pasi na kuzitolea jasho.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Amon Mpanju amesema hayo.

Kutoka na ongezeko la matukio ya aina hiyo katika Vyuo Vikuu limefanya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kuzindua Dawati la Jinsia katika Chuo Kikuu cha Dodoma, ndipo katika uzinduzi huo Mpanju akaeleza athari za vitendo hivyo.

“Matukio kama hayo yanasababisha kuzalisha wataalam ambao hawana vigezo, natoa wito kwa madawati kama haya kufanya kazi kwa usiri,” - Mpanju.

Naye, Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Profesa James Mdoe amesema yakiwemo manyanyaso ya kijinsia au mengine akili haiwezi kufanya kazi, hivyo sio rahisi kwa wanafunzi kufikia ndoto zao.
Sasa mmechukua hatua zipi juu ya hilo.
 
Back
Top Bottom