kerubi afunikaye
JF-Expert Member
- May 20, 2013
- 1,183
- 1,057
Hizi noti sijui zimetengenezwa wapi!nimekaa nchi hii miaka mingi sijawahi kuona noti mbovu zinazowahi kuharibika kama hizi!zinaleta usumbufu sana kwenye transactions hasa huku kwetu tunaolipa nauli za daladala,chips yai,unga kilo moja,supu ya pweza,sadaka n.k kila siku kukunjana mashati tu!Niwataarifu tu enyi mliokalia viti vya kuzunguuka huko wizara ya fedha na BOT kuwa hizi noti zenu za sh 500 zimegeuka kero kubwa.Kwa kweli hii ni kashfa kwa vyombo vikubwa kama Benki kuu kutokuwa makini na kutengeneza vitu vya ajabu ajabu namna hii.hebu tafuteni mbadala wa noti hizi jamani,kulikoni?mbona enzi za Nyerere na Mwinyi tulikuwa na noti nzuri,walizitengenezea wapi zile noti zilizokuwa na signature za akina Msuya?Maji,umeme,barabara mtunyime,hata noti nazo?ina shida gani serikali hii jamani,jamani,jamaaanii..ah,ee Mungu,this country..!!