Serikali na Wizara ya Afya muwe makini na hizi quarantine mlizotenga kwa ajili ya wagonjwa wa Corona

Jaslaws

JF-Expert Member
May 31, 2011
6,016
5,284
Heshima kwenu,

Naomba niende moja kwa moja kwenye mada. Kama mwananchi kuna jambo limekuwa likiniumiza sana. Serikali walitenga baadhi ya hoteli kwa ajili ya watu wanaotoka nje kukaa huku wakichunguzwa ugonjwa wa Corona, moja wapo wa hoteli zilizotengwa ni FQ village iko Ukonga Stakishari.

Sasa kilichonifanya kuandika hapa ni kutokuwa na uaminifu kwa askari wanaolinda hizo hotel, wamekuwa wakiwaruhusu hawa watu kutoka na kuingia mtaani, kwa mfano juzi walikuwa bar jirani na hiyo hotel inaitwa Kiliman bar wanakula pombe tena katikati ya watu bila kujitenga. Jana pia nimepita maeneo hayo wanasema hata supu wanakunywa kila asubuhi.

Nawaza kwa bahati mbaya kuna mtu anao huo ugonjwa na ile sharing ya bar tutakufa kama kuku

Naomba Serikali wafuatilie kisha wachukue hatua kabla ya dhahama.
 
Who care?
Your government doesn't care.
Kiufupi serikali yetu ipo disorganized sana.

Yani wanakuwa organized tu kama issue ikiwa ni chadema.

Hii ni mara ya pili mtu anakuja kulalamika kuhusu issue ya karantini.

Ni kama hakuna mtu ambaye yupo responsible kufuatilia.

JKT wangepewa hili jukumu wasimamie basi kwa sababu sijui task force sijui nani wanasubiri mshahar tu basi
 
We wa pili unalalamikia FQ

Sent using Jamii Forums mobile app
ooh kweli..??atleast basi walichukulie kwa uzito..maana watatuua hawa wajinga mbaya zaid mpaka wazungu wanatoka..mimi aliyenishirkisha hili swala ni mpishi wa FQ nikafanya uchukunguzi bar yajirani wao walikiri kwamba ni kweli wanaenda pale.
 
watumishi wa serikali ya bongo km issue haina posho na vichenchi chechi vya kubania hakuna mtumishi utayemuona anajishughulisha na hilo jambo kabisa..
 
ooh kweli..??atleast basi walichukulie kwa uzito..maana watatuua hawa wajinga mbaya zaid mpaka wazungu wanatoka..mimi aliyenishirkisha hili swala ni mpishi wa FQ nikafanya uchukunguzi bar yajirani wao walikiri kwamba ni kweli wanaenda pale.
Kuna mtu anaenda kupoteza kazi , whistleblowers hawawekwagi hadharani, mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Heshima kwenu,

Naomba niende moja kwa moja kwenye mada. Kama mwananchi kuna jambo limekuwa likiniumiza sana. Serikali walitenga baadhi ya hoteli kwa ajili ya watu wanaotoka nje kukaa huku wakichunguzwa ugonjwa wa Corona, moja wapo wa hoteli zilizotengwa ni FQ village iko Ukonga Stakishari.

Sasa kilichonifanya kuandika hapa ni kutokuwa na uaminifu kwa askari wanaolinda hizo hotel,wamekuwa wakiwaruhusu hawa watu kutoka na kuingia mtaani, kwa mfano juzi walikuwa bar jirani na hiyo hotel inaitwa Kiliman bar wanakula pombe tena katikati ya watu bila kujitenga. Jana pia nimepita maeneo hayo wanasema hata supu wanakunywa kila asubuhi.

Nawaza kwa bahati mbaya kuna mtu anao huo ugonjwa na ile sharing ya bar tutakufa kama kuku

Naomba Serikali wafuatilie kisha wachukue hatua kabla ya dhahama.
Kama ni kweli basi sisi ni watu wa ajabu sana hapa duniani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Woi Tanzania nchi yangu. Rushwa Hadi kwa vitu visivyotakiwa. Corona Ni janga la kidunia lakini Polisi bado wanapokea rushwa kuruhusu walio karantini kutoka nje ya hotel na kutangamana na watu???

Jamani Waziri Ummy ameskia hizi habari, najua jamii forum inavisitiwa na watu wengi mwenye access na viongozi jamani habari hii ifikishwe hata Kama Ni fununu better safe than sorry.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
We wa pili unalalamikia FQ

Sent using Jamii Forums mobile app
Who care?
Your government doesn't care.
Kiufupi serikali yetu ipo disorganized sana.

Yani wanakuwa organized tu kama issue ikiwa ni chadema.

Hii ni mara ya pili mtu anakuja kulalamika kuhusu issue ya karantini.

Ni kama hakuna mtu ambaye yupo responsible kufuatilia.

JKT wangepewa hili jukumu wasimamie basi kwa sababu sijui task force sijui nani wanasubiri mshahar tu basi
mimi watatu nimemsikia mama wa mfanyakazi wa hoteri hiyo akituhadithia namna mwanae anavyosema jinsi hao waliopo karantini wanavyohatarisha maisha ya wengne na hata hao wafanyakazi wanaowahudumia kisa tu wana fuba la kutosha na inasemekama anaewalea hvyo ni mmiliki sa hoteri hiyo kwa kuwa wanampa pesa ya ziada nyingi zaidi hvyo huruhusu wafanye wanavyotaka wao bira bugudha akadai bintye anaogopa kutoa taarifa pengne kuna mkono wa mtumkubwa nikamwambia anwambie bintye asiogope serikali pamoja na mapungufu yake lkn haiwezi kushiriki ujinga ila kuna wachache wachumia tumbo nikampa zile namba za dharura za corona nikamwambia ampe bintiye apige aeleze hizo habari kwa kina na wala hawatajua maboss zake km ni yeye na namba yke haitajulikana
sasa sijajua amepga ama vipi mana hii story jana jioni ndo tulikuwa tunazungumza na huyo mama na hizo namba nimempa jana jioni
hila ni kweli kabisa wanachofanya katika hizo hoteri sio kabisa ni hatari

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huu ni ujinga wa watendaji, wakati mwingine serikali inalaumiwa bure!

Watanzania sijui tuna shida gani, Wewe unaona kabisa hapa Kuna shida bado nawewe unashiriki kufanya uovu halafu baadae unaanza kulaumu serikali.

Kila mtu lazima atimize wajibu wake ndiyo mambo yaenda, ingekuwa Mimi ndiyo mwenye hotel, I swear kila mtu angekaa chumbani kwake na hakuna ambaye angeonana na mwenzake achilia mbali kwenda nje ya hotel.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani nchi yetu sijui aliyeturoga nani na yupo wapi tatizo kama hili watu wanafanya upuuzi, ndiyo maana wenzetu huko bakora zilitembea, ila sie huku kama ni bakora zianze kwa wale wasimamizi wa hizo kesi, chakujiuliza wewe umeambiwa ukae humo unatoka kwenda wapi au mpaka Baba zao na mama zao waumwe ndiyo watatulia? Serikali ianze kuwataja majina wote walio quarantine na wagonjwa ili tukikutana nao mtaani washughulikiwe vizuri.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Daaah nimebaki na mshangao tu, Mungu atusaidie tu, hii nchiii aisee.
 
Back
Top Bottom