MsemajiUkweli
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 13,172
- 23,974
- Thread starter
- #161
Serikali ni taasisi kubwa sana na haiwezi kuepuka lawama kwa mambo mbali mbali kwa sababu jukumu lake ni kulinda Raia wake.Inaonekana makada wengi hampendi jinsi Magufuli anavyolishughulikia swala la Lissu...
Hata hivyo nimependa ulivyojenga hoja zako.!
Kama nilivyosema, serikali kutuhumiwa kutaka kuua au kuua siyo jambo geni kutokana na majukumu yake. Kuanzia serikali ya Mwl. Nyerere mpaka Kikwete zimewahi kutuhumiwa kutaka kuua au kuua.
Ujinga unaojitokeza ni pale baadhi ya viongozi wakuu wa CCM na Serikali wanapoanza kurumbana na Lissu wakati sio wasemaji wa taasisi iliyopewa kisheria jukumu la kiuchunguzi.