Serikali na CCM acheni kumpa Tundu Lissu umaarufu wa bure!

Inaonekana makada wengi hampendi jinsi Magufuli anavyolishughulikia swala la Lissu...

Hata hivyo nimependa ulivyojenga hoja zako.!
Serikali ni taasisi kubwa sana na haiwezi kuepuka lawama kwa mambo mbali mbali kwa sababu jukumu lake ni kulinda Raia wake.

Kama nilivyosema, serikali kutuhumiwa kutaka kuua au kuua siyo jambo geni kutokana na majukumu yake. Kuanzia serikali ya Mwl. Nyerere mpaka Kikwete zimewahi kutuhumiwa kutaka kuua au kuua.

Ujinga unaojitokeza ni pale baadhi ya viongozi wakuu wa CCM na Serikali wanapoanza kurumbana na Lissu wakati sio wasemaji wa taasisi iliyopewa kisheria jukumu la kiuchunguzi.
 
MsemajiUkweli

Likely uko sawa na sahihi kabisa.

Lakini tukumbuke kuwa it is hard one and half a year tangu hili la jaribio la kisiasa kumuua huyu bwana litokee, yet, hakuna uchunguzi ama upelelezi wowote ulio/unaofanyika mpaka sasa!!

Kibaya zaidi, wenye wajibu wa kutenda haya wanatoa majibu ya ajabu kidogo na yenye kuzua shaka zaidi na kuhalalisha hata kuzipa nguvu hoja na hisia za nani anahusika na kutaka kumuua huyu ndugu na kwa sababu gani....

Technically, serikali ilianza kukosea miezi miezi miwili ya mwanzo tangu kutokea kwa shambulio hilo. Laiti ingefanya jambo hata la kuzugia tu ktk kipindi hicho lakini lenye kuonekana kwa umma kama alivyofanyaga Afande Seleman Kova kwenye tukio la kutekwa na kuteswa kwa Dr Ulimboka, ni wazi, the story could be different today.....

Lakini masikini hawa (Serikali) hawakufanya chochote cha maana na matokeo yake ni haya unayolalamikia sasa, yet unataka wataalamu wa uchunguzi ndiyo waseme badala ya akina Dr Bashiru Ally, Wilson Masilingi, Job Ndugai...!!

Acha waseme maana ni wao wenyewe ndiyo wamechukua nafasi za wataalamu. Laiti wangekuwa smart, wangeweza kuwatumia wataalamu hawa vyema ku - cover udhaifu na ujinga wao. Lakini things are opposite kabisa...!!

Mfano, ilikuwa ni kosa la kiufundi sana sana kisiasa kuchukua maamuzi ya kutomlipia huyu bwana gharama za matibabu yake kwa sababu zinazotajwa na kurudiwa rudiwa hata leo...!!

Kwenye hili kila mtu anashangaa na ataendelea kushangaa hata kujiuliza kulikoni mtu ambaye alikuwa kwenye coma mahututi na kupata fahamu baada ya wiki kadhaa unang'ang'ana tu eti hakufuata taratibu za matibabu na ndiyo maana hatalipiwa gharama ambayo kimsingi ni haki yake kisheria?

Busara tu ya kawaida iko wapi ktk hili??? Hivi ni kweli tunadhani wakati wowote na ktk mazingira yoyote sheria/taratibu zaweza kufanya kazi?

Je, siyo mara nyingi tu hata Rais Magufuli mwenyewe analazimika kuvunja mpaka katiba achilia mbali sheria, kanuni na taratibu ili mradi kuruhusu jambo fulani lifanyike? Je, si zaidi sana kwa ishu kama hii ihusuhuyo uhai wa binadamu???

Kwa kweli maswali ni mengi mno lakini itoshe tu kusema, binafsi nimekuelewa sana kwa mara ya kwanza ktk hili japo huwa tunatofautiana sana tu kwenye nyingi ya posts/mawazo yako mengi mengine.....

Hii inaonesha kuwa hukubaliani na namna serikali inavyoli - handle swala la mbunge Lissu...

Na kwa kuongezea tu, ni kuwa, hakuna kosa baya lililofanyika kama kwa Balozi wa Tanzania huko Marekani Bw. Wilson Masilingi kwenda kujibizana na Tundu Lissu kwenye International media (TV) huku ndani ya moyo na nafsi yake akitambua kabisa kuwa hana majibu ya hoja za TL na Watanzania kwa ujumla....!!

Na hili ndiyo tatizo. Kuwa, ukiwa na kiongozi mjinga juu yako, ni lazima atakuwa anatoa maagizo ya kijinga tu kwa subordinates wake na hivyo wanapoyatekeleza nao wataonekana ni wajinga tu....!!

Na basi tu, ni kwa sababu ya hali ya mambo, lakini hilo lilijidhirisha hata kwa mwendesha kipindi (mtangazaji) na washiriki wengine wa kipindi kile, kuwa Balozi hana hoja, amepwaya na lengo la Tundu Lissu likawa limetimia...!!
Kwa kiwango kikubwa ninakubaliana na angalizo lako!
 
Nimekuwa kimya na mtazamaji kuhusiana na suala hili la Tundu Lissu lakini baada ya kuangalia kwa muda nimegundua madhaifu mengi sana kwa upande wa serikali katika kukabiliana na yanayojiri kwenye suala hili.

Serikali na CCM wamekuwa reactive badala ya kuwa proactive ambapo matokeo yake wanafanya makosa mengi ya msingi hasa mahusiano ya umma.

Serikali na viongozi wa juu wa CCM kukimbizana na Lissu kwenye vyombo vya habari ili kujibu hoja zake ni ujinga wa kiwango cha juu kwa sababu kufanya hivyo ni kujiweka wazi kwenye maswali ambayo hanaya majibu ya kisiasa bali kiuchunguzi. Kimantiki taasisi ya kiuchunguzi wa makosa ya jinai haiwezi kutoa majibu ya uchunguzi kama uchunguzi haujakamilika lakini pia hata yakitolewa huwa yanatolewa kitaalam na kwa uangalifu mkubwa sana bila kujali mwathirika/waathirika wanafikra zipi.

Lissu akiwa anahojiwa na waandishi wa habari bila kuwepo maafisa wa serikali ni faida kwa serikali na CCM kuliko ofisa wa serikali na CCM kuwepo pia katika mahojiano hayo. Mahojiano yake katika kipindi cha HARDtalk bila uwepo wa ofisa wa serikali yaliinufaisha zaidi serikali kuliko muhojiwa. Hata pale alipotoa shutuma, mtangazaji alimwambia aache kutoa shutuma ambazo anaowatuhumu hawapo ili wazijibu.

Ni ujinga kwa serikali kudhani kuwa kinachofanyika hapa Tanzania hakijulikani katika makorido ya watawala wa Ulaya na Marekani na kwa maana hiyo wanakwenda kujibu tuhuma za upotoshaji. In fact, watawala wa Ulaya na Marekani wanajua hata yale yanayosemwa ndani ya Ikulu ya Magogoni nchini achilia mbali anayoyasema Lissu. Kwa maana hii, kama Lissu anayosema ni kweli au uwongo watakuwa wanajua.

Kwa mfano, juzi Gazeti la The New York Times la Marekani ambalo lina mahusiano ya karibu sana na majasusi wa Marekani lilipewa audio yenye maongezi ya mwana mfalme, Mohammed bin Salman akiwaambia watu wake wa karibu kuwa atatumia risasi kama Jamal Khashoggi hatarudi Saudi Arabia na kuachana na ukosoaji wa serikali. Hii inaonyesha kuwa kila anachokisema na kukifanya ndani ya nyumba yake kinajulikana kwa majasusi wa nchi ya Marekani.

Hii ina maana kuwa serikali inapoteza muda kujitetea kwenye suala la Tundu Lissu na demokrasia kwa sababu watawala wa Ulaya na Marekani wanajua kama ni kweli au uwongo.

Serikali lazima waelewe kuwa anachokitaka Tundu Lissu ni reaction ambayo ni reactive kutoka serikalini ili aendeleze marumbano na mijadala kwenye vyombo vya habari ya ndani na nje.

Ninakumbuka kwa mara yangu ya kwanza kusafiri katika nchi za Ulaya nilipewa ushauri kuwa ukimuona mtu anakuchokoza au kukuchochea unachotakiwa ni kutoonyesha hisia au kujibu. Kutoonyesha hisia au kujibu kutamfanya akose sababu ya kuendelea kukuchochea au kukuchokoza lakini kikubwa zaidi ataona anachofanya ni ujinga na kuachana na uchochezi au uchokozi.

Serikali ikikaa kimya hata wale wanaomuhoji Lissu watachoka kwa sababu kutakuwa hakuna reaction kutoka serikalini. Kukosa reaction kutoka serikalini ina maana hata mahojiano yanakuwa hayahitajiki (redundant). Serikali lazima waelewe dhana ya Newton's third law of motion. No force, no reaction lakini kikubwa zaidi uendeshaji wa serikali ni sawa na mbio za masafa marefu(marathon). Kuna wapiga kelele wataibuka na baadaye watapotea.

Watu wenye fikra pana wanaomfahamu Lissu hawashangai na kile anachokisema bali wanachoshangaa ni jinsi ambavyo viongozi wa juu wa CCM na serikali wanavyojibishana naye kwenye vyombo vya habari.

Kwa mtu mwenye fikra pana na anamfahamu vizuri Lissu atajua hupenda sana kujionyesha mbele ya watu/hadhara (limelight) lakini pia hufurahia sana (relish) kama kuna reaction bila kujali kama ni nzuri au mbaya. Waingereza huita Attention seeking behaviour. Lissu anachokitafuta kwa CCM na serikali ni kukimbizana au kujibishana naye kwenye media akiwa ndiye focal point.

Mpaka sasa malengo yake kwa kiwango kikubwa yamefanikiwa kutokana na ujinga wa viongozi wa juu wa serikali na CCM ambao wengi wao hawajui ukubwa na umuhimu wa vyeo vyao. Eti Katibu Mkuu wa chama tawala CCM anajibishana na Mjumbe wa Kamati Kuu wa chama cha upinzani CHADEMA, Tundu Lissu? This is beyond stupidity.

Lissu anatakiwa arumbane na wanachama wa kawaida wa CCM na sio viongozi wa juu wa chama. Majibu ya hoja za Lissu kuhusu shambulio lazima yajibiwe na taasisi rasmi za uchunguzi na sio kila kiongozi wa serikali.

Hawa viongozi wa CCM na serikali hawakujifunza makosa waliyoyafanya kwa Mange Kimambi baada ya kumkuza na kupata followers wengi kutokana na kujibishana naye. Makosa yaleyale wanayarudia kwa Tundu Lissu.

Katika dhana ile ile ya Attention seeking behaviour, Ninajua pia Lissu atapenda sana akirudi nchini akamatwe akiwa uwanja wa ndege ili kutimiza Newton's third law of motion ambapo matokeo yake yatakuwa kumpa umaarufu wa bure lakini kikubwa zaidi hata waliokuwa hawaamini aliyokuwa anayasema nwataamini niya kweli. Ninawaomba sana serikali wasimkamate siku akiingia nchini bali wamuache tu. No force, no rection.

Ninakumbuka mwaka 1995 wakati Augustino Mrema akiwa mpinzani maarufu nchini, kila alipobebwa waliombeba walipigwa mabomu na vitendo hivyo vilizidi kumfanya maarufu mpaka Mwalimu Nyerere alipotumia busara na kuwambia polisi, “Kwa kuwa wanaotaka kumbeba Mrema wapo, waacheni wambebe. Wambebe hata kama watakuwa wanapokezana kama machela (jeneza), waacheni.” Polisi walipotii agizo la Baba wa Taifa, la kuacha kuwapiga mabomu, Mrema naye kama shani hakubebwa tena. Mwl. Nyerere alitumia dhana ya Newton's third law of motion. No force, no reaction.

Tuliona pia huko Kenya, baada ya wapinzani kuamua kumuapisha Raila Odinga kuongoza Kenya baada kutangaza kwamba hamtambui Uhuru Kenyatta kama kiongozi aliyechaguliwa kwa njia halali, polisi waliwaacha wafanye hivyo na matokeo yake kitendo hicho kikaonekana nicha kijinga.

Huko Venezuela tumeona kiongozi wa upinzani akifanya kama alivyofanya Raila Odinga lakini dhumuni lake lilikuwa ni kutaka polisi wawazuie ili mapigano yatokee ambayo yangekuwa ni sababu ya Marekani kuingia kimabavu katika nchi hiyo kwa kisingizio cha kuzuia mauwaji. Serikali ya Rais Madulo ikajua janja yao na ikamuacha Juan Guaidó ajiapishe bila kumuingilia kwa kutumia nguvu ya polisi/jeshi. No force, no reaction. Uamuzi wa polisi/jeshi kumuacha ajiapishe kumeua malengo ya Marekani ya kuingiza majeshi Venezuela.

CCM na Serikali lazima waelewe kuwa hoja sio Lissu anatumiwa na ''mabeberu'' bali hoja ni jinsi gani wataweza kuzuia njama za ''Mabeberu'' kwa sababu ''mabeberu'' kuwatumia watu sio jambo jimpya.

Kuna Mzee mmoja aliwahi kunipa ushauri kwa maneno haya, Ukimya hukuvisha nguo ya utulivu na hukukinga na haja ya kutoa visingizio lakini pia jawabu fasihi kabisa kwa mpumbavu ni kutomjibu.

Nimalizie kwa kusema, Serikali na viongozi wa juu wa CCM lazima watambue kuwa hata kukaa kimya ni jibu kwa sababu hakuna serikali hapa duniani ambayo haijawahi kutuhumiwa kutaka kuua au kuua raia.[/QUOt hapa serikali ikitaka kumzima lissu ni kuitisha uchunguzi huru wa kuchunguza matukio yote ya utekaji na kupoteza watu kama kina bene Santana na Azory na kupona Roma na wengine wote
 
Umenikumbusha Mwalimu Nyerere alivyowaambia wanaccm kwamba wamwache Mrema abebwe kadri awezavyo.

Na akamshauri Mrema agombee ubunge kwani urais hauwezi, Mrema akabisha na kuamua kugombea urais, matokeo yake kila mtu anayafahamu.
Mrema mpaka sasa hujutia ushauri wa Mwl. Nyerere kwa sababu hakuuchukua.
 
Serikali ni taasisi kubwa sana na haiwezi kuepuka lawama kwa mambo mbali mbali kwa sababu jukumu lake ni kulinda Raia wake.

Kama nilivyosema, serikali kutuhumiwa kutaka kuua au kuua siyo jambo geni kutokana na majukumu yake. Kuanzia serikali ya Mwl. Nyerere mpaka Kikwete zimewahi kutuhumiwa kutaka kuua au kuua.

Ujinga unaojitokeza ni pale baadhi ya viongozi wakuu wa CCM na Serikali wanapoanza kurumbana na Lissu wakati sio wasemaji wa taasisi iliyopewa kisheria jukumu la kiuchunguzi.

..sidhani kama kukaa kimya ingesaidia.

..hoja za TL ni hoja ambazo hazihitaji muda mrefu kuzipatia majibu.

..nilitegemea uishauri serekali ishirikishe WACHUNGUZI WA KIMATAIFA na itoe taarifa na maendeleo ya uchunguzi kwa wakati.

..pia nilitegemea uishauri serekali imlipie matibabu TL ambaye ni mnadhimu wa kambi ya upinzani bungeni.

..kwa kweli inatia AIBU na INALICHAFUA TAIFA kwamba kiongozi wa bunge la Tz ameshambuliwa kigaidi halafu Bunge na Serekali yake wamekataa kumtibu.

..Again, TL angekuwa hana hoja kama angetibiwa na Bunge, na serekali ingekubali maombi ya familia kwamba wachunguzi toka nje washirikishwe.
 
Ni ushauri wenye mantiki kwa serikali, kosa kubwa lililofanyika toka mwanzo ni kujiangaisha na mpuuzi kama Tundu Lissu, ni mtu anayetafuta sifa binafsi kwa masllahi yake, anaungwa mkono na wapiuuzi wachache wasioipend serikali. Serikali iachane kujishughulisha naye.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hakuna serikali ipendwayo na watu wote duniani na nikosa kusema wasioipenda serikali flan ni wapuuzi, basi na wewe ni mpuuzi kupenda kila serikali ijayo.
 
Mwakilishi wa Wananchi kapigwa Risasi ndani ya makazi ya wabunge na Mawaziri, akitokea Bungeni kuwakilisha wananchi wake alafu unakuja na hoja nyepesi eti CCM na Serikali waache kumpa TL umaarufu..

CCM hao hao kupitia Spika walikataa kugharamia Pesa za Matibabu ,sababu kubwa ilikuwa ni nini kama siyo wahusika wa tukio.

Ni vyema leo TL yupo hai angalau tunaweza kuwafahamu kwa kauli zao,wakiwa majukwaani wanajinasibu nchi ya Amani,alafu Mwakilishi wa Wananchi anapigwa Risasi kadhaa mchana kweupe mpaka leo hakuna Uchunguzi wowote wa kitaalamu uliokwisha fanyika kuhusiana na tukio lile.
Acha waendelee kujianika ubaya wao kwa kumjibu TL, maana nafsi zinawasuta, alafu usijitie sana eti wewe Bonge la mshauri au na wewe unatafuta umarufu humu JF.
 
Leo naona umelala vizuri na akili zako ziko sawa sawia...

Nakubaliana na hili.

Lakini kumbuka kuwa hata hizo taasisi za kiuchunguzi unazotaka ziwe ndizo zinasema zinakaliwa na makada wa CCM haohao!!
Hoja sio ukada bali ni utaalam. Majibu ya kitaalam ni tofauti na majibu ya mtu asiye mtaalam
 
Hoja sio ukada bali ni utaalam. Majibu ya kitaalam ni tofauti na majibu ya mtu asiye mtaalam


Katika mazingira ya utendaji kazi ktk nchi yetu professionally, ni ngumu sana kutenganisha na maslahi yako kisiasa - ukada wa chama...

Na unielewe tafadhali, nasema hivi si kwa sbb currently CCM ndiyo wanatawala....

Bali hata ikitokea leo CHAUMA, Chama Cha Wakulima nk wakashika dola, mkondo wa kiutendaji kwa mfumo wa kiutawala tulionao usiotenganisha dola na chama, utawafuata!!
 
Nimekuwa kimya na mtazamaji kuhusiana na suala hili la Tundu Lissu lakini baada ya kuangalia kwa muda nimegundua madhaifu mengi sana kwa upande wa serikali katika kukabiliana na yanayojiri kwenye suala hili.

Serikali na CCM wamekuwa reactive badala ya kuwa proactive ambapo matokeo yake wanafanya makosa mengi ya msingi hasa mahusiano ya umma.

Serikali na viongozi wa juu wa CCM kukimbizana na Lissu kwenye vyombo vya habari ili kujibu hoja zake ni ujinga wa kiwango cha juu kwa sababu kufanya hivyo ni kujiweka wazi kwenye maswali ambayo hanaya majibu ya kisiasa bali kiuchunguzi. Kimantiki taasisi ya kiuchunguzi wa makosa ya jinai haiwezi kutoa majibu ya uchunguzi kama uchunguzi haujakamilika lakini pia hata yakitolewa huwa yanatolewa kitaalam na kwa uangalifu mkubwa sana bila kujali mwathirika/waathirika wanafikra zipi.

Lissu akiwa anahojiwa na waandishi wa habari bila kuwepo maafisa wa serikali ni faida kwa serikali na CCM kuliko ofisa wa serikali na CCM kuwepo pia katika mahojiano hayo. Mahojiano yake katika kipindi cha HARDtalk bila uwepo wa ofisa wa serikali yaliinufaisha zaidi serikali kuliko muhojiwa. Hata pale alipotoa shutuma, mtangazaji alimwambia aache kutoa shutuma ambazo anaowatuhumu hawapo ili wazijibu.

Ni ujinga kwa serikali kudhani kuwa kinachofanyika hapa Tanzania hakijulikani katika makorido ya watawala wa Ulaya na Marekani na kwa maana hiyo wanakwenda kujibu tuhuma za upotoshaji. In fact, watawala wa Ulaya na Marekani wanajua hata yale yanayosemwa ndani ya Ikulu ya Magogoni nchini achilia mbali anayoyasema Lissu. Kwa maana hii, kama Lissu anayosema ni kweli au uwongo watakuwa wanajua.

Kwa mfano, juzi Gazeti la The New York Times la Marekani ambalo lina mahusiano ya karibu sana na majasusi wa Marekani lilipewa audio yenye maongezi ya mwana mfalme, Mohammed bin Salman akiwaambia watu wake wa karibu kuwa atatumia risasi kama Jamal Khashoggi hatarudi Saudi Arabia na kuachana na ukosoaji wa serikali. Hii inaonyesha kuwa kila anachokisema na kukifanya ndani ya nyumba yake kinajulikana kwa majasusi wa nchi ya Marekani.

Hii ina maana kuwa serikali inapoteza muda kujitetea kwenye suala la Tundu Lissu na demokrasia kwa sababu watawala wa Ulaya na Marekani wanajua kama ni kweli au uwongo.

Serikali lazima waelewe kuwa anachokitaka Tundu Lissu ni reaction ambayo ni reactive kutoka serikalini ili aendeleze marumbano na mijadala kwenye vyombo vya habari ya ndani na nje.

Ninakumbuka kwa mara yangu ya kwanza kusafiri katika nchi za Ulaya nilipewa ushauri kuwa ukimuona mtu anakuchokoza au kukuchochea unachotakiwa ni kutoonyesha hisia au kujibu. Kutoonyesha hisia au kujibu kutamfanya akose sababu ya kuendelea kukuchochea au kukuchokoza lakini kikubwa zaidi ataona anachofanya ni ujinga na kuachana na uchochezi au uchokozi.

Serikali ikikaa kimya hata wale wanaomuhoji Lissu watachoka kwa sababu kutakuwa hakuna reaction kutoka serikalini. Kukosa reaction kutoka serikalini ina maana hata mahojiano yanakuwa hayahitajiki (redundant). Serikali lazima waelewe dhana ya Newton's third law of motion. No force, no reaction lakini kikubwa zaidi uendeshaji wa serikali ni sawa na mbio za masafa marefu(marathon). Kuna wapiga kelele wataibuka na baadaye watapotea.

Watu wenye fikra pana wanaomfahamu Lissu hawashangai na kile anachokisema bali wanachoshangaa ni jinsi ambavyo viongozi wa juu wa CCM na serikali wanavyojibishana naye kwenye vyombo vya habari.

Kwa mtu mwenye fikra pana na anamfahamu vizuri Lissu atajua hupenda sana kujionyesha mbele ya watu/hadhara (limelight) lakini pia hufurahia sana (relish) kama kuna reaction bila kujali kama ni nzuri au mbaya. Waingereza huita Attention seeking behaviour. Lissu anachokitafuta kwa CCM na serikali ni kukimbizana au kujibishana naye kwenye media akiwa ndiye focal point.

Mpaka sasa malengo yake kwa kiwango kikubwa yamefanikiwa kutokana na ujinga wa viongozi wa juu wa serikali na CCM ambao wengi wao hawajui ukubwa na umuhimu wa vyeo vyao. Eti Katibu Mkuu wa chama tawala CCM anajibishana na Mjumbe wa Kamati Kuu wa chama cha upinzani CHADEMA, Tundu Lissu? This is beyond stupidity.

Lissu anatakiwa arumbane na wanachama wa kawaida wa CCM na sio viongozi wa juu wa chama. Majibu ya hoja za Lissu kuhusu shambulio lazima yajibiwe na taasisi rasmi za uchunguzi na sio kila kiongozi wa serikali.

Hawa viongozi wa CCM na serikali hawakujifunza makosa waliyoyafanya kwa Mange Kimambi baada ya kumkuza na kupata followers wengi kutokana na kujibishana naye. Makosa yaleyale wanayarudia kwa Tundu Lissu.

Katika dhana ile ile ya Attention seeking behaviour, Ninajua pia Lissu atapenda sana akirudi nchini akamatwe akiwa uwanja wa ndege ili kutimiza Newton's third law of motion ambapo matokeo yake yatakuwa kumpa umaarufu wa bure lakini kikubwa zaidi hata waliokuwa hawaamini aliyokuwa anayasema nwataamini niya kweli. Ninawaomba sana serikali wasimkamate siku akiingia nchini bali wamuache tu. No force, no rection.

Ninakumbuka mwaka 1995 wakati Augustino Mrema akiwa mpinzani maarufu nchini, kila alipobebwa waliombeba walipigwa mabomu na vitendo hivyo vilizidi kumfanya maarufu mpaka Mwalimu Nyerere alipotumia busara na kuwambia polisi, “Kwa kuwa wanaotaka kumbeba Mrema wapo, waacheni wambebe. Wambebe hata kama watakuwa wanapokezana kama machela (jeneza), waacheni.” Polisi walipotii agizo la Baba wa Taifa, la kuacha kuwapiga mabomu, Mrema naye kama shani hakubebwa tena. Mwl. Nyerere alitumia dhana ya Newton's third law of motion. No force, no reaction.

Tuliona pia huko Kenya, baada ya wapinzani kuamua kumuapisha Raila Odinga kuongoza Kenya baada kutangaza kwamba hamtambui Uhuru Kenyatta kama kiongozi aliyechaguliwa kwa njia halali, polisi waliwaacha wafanye hivyo na matokeo yake kitendo hicho kikaonekana nicha kijinga.

Huko Venezuela tumeona kiongozi wa upinzani akifanya kama alivyofanya Raila Odinga lakini dhumuni lake lilikuwa ni kutaka polisi wawazuie ili mapigano yatokee ambayo yangekuwa ni sababu ya Marekani kuingia kimabavu katika nchi hiyo kwa kisingizio cha kuzuia mauwaji. Serikali ya Rais Madulo ikajua janja yao na ikamuacha Juan Guaidó ajiapishe bila kumuingilia kwa kutumia nguvu ya polisi/jeshi. No force, no reaction. Uamuzi wa polisi/jeshi kumuacha ajiapishe kumeua malengo ya Marekani ya kuingiza majeshi Venezuela.

CCM na Serikali lazima waelewe kuwa hoja sio Lissu anatumiwa na ''mabeberu'' bali hoja ni jinsi gani wataweza kuzuia njama za ''Mabeberu'' kwa sababu ''mabeberu'' kuwatumia watu sio jambo jimpya.

Kuna Mzee mmoja aliwahi kunipa ushauri kwa maneno haya, Ukimya hukuvisha nguo ya utulivu na hukukinga na haja ya kutoa visingizio lakini pia jawabu fasihi kabisa kwa mpumbavu ni kutomjibu.

Nimalizie kwa kusema, Serikali na viongozi wa juu wa CCM lazima watambue kuwa hata kukaa kimya ni jibu kwa sababu hakuna serikali hapa duniani ambayo haijawahi kutuhumiwa kutaka kuua au kuua raia.
Ujumbe mzuri kama utafuatwa ingawa sijui kama wahusika wataupokea

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umeandika vizuri lakini kuna usemi wa kizungu unaosema "Silence means Yes" (kukaa kimya maana yake unakubali kinachosemwa,tafsiri isiyo rasmi) sasa wewe unasemaje "kuwa hata kukaa kimya ni jibu"unamaanisha jibu la ndiyo?:Lazima Serikali ijibu mapigo sisi back benchers tutaamua.
Umesema vema

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Baada ya wiki mbili tatu hii issue ya TL itakuwa imefyekelewa mbali..imekufa kifo cha mende
 
Serikali aigombani na lissu ata siku moja bali ccm ndo inagombana na lissu we angalia vizur unasema serikali sababu wengi wao ni watumishi wa serikali mama ako akiwa mwalimu na akikupiga nyumbani kisa ujasafisha chumba chako uwezi sema mwalimu kakupiga hapo anakua ni mama ako sasa lissu amepigwa na watu ambao wana sare za jeshi wala kitambulisho cha uajili serikalini uwezi sema serikali mana yanayotokea yote ayafanani na serikali ata mama samia alienda kama yeye na sio serikali kumuona lissu ndugai maamuzi yake ni tofauti na katiba sheria na taratibu zote wanavunja sheria za nchi ingekua kwingine wangeshitakiwa mana wanavunja sheria


Sent from my iPhone using JamiiForums
Samahani, sielewi vizuri hoja yako.

Naomba unifafanulie zaidi,
 
Ukishaanza kukiogopa kimvuli chako mwenyewe hakuna kitu utaacha kukiogopa.

Lakini pia kukaa kimya ni kiashirio kikubwa kuwa kile kinachosemwa ni kweli. Na utakapojibu ndipo itajulikana ukweli zaidi kutokana na majibu utakayojibu.

Mpaka wao wameamua kumjibu sidhani kama walikurupuka tu, ila naamini walishakaa chini wakajadiliana na wakaafikiana wafanye hivyo.

Ila mwisho wa siku, siku zote daima milele panapo ukweli uongo hukaa pembeni.

Ahsante.
Umejibu vzr sana!

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

43 Reactions
Reply
Back
Top Bottom