Serikali na CCM acheni kumpa Tundu Lissu umaarufu wa bure!

Umeandika mengi lakini umesukumwa zaidi na mapenzi kwa chama tawala, unaweza kupuuza au kutomjibu mtu kama anachosema ni uongo, lakini kama mambo mengi yanayodaiwa ni ya kweli utajitahidi kukanusha kwa kuwa hata kama ni uongo ukisemwa kwa muda mrefu unakuwa ukweli na hili serikali inalijua.
Pili mimi nataka msikae kimya mkanushe kwa kujibu hoja, kwa mfano anasema Magufuli anaminya demokrasia, sasa nyinyi mnatakiwa mtuonyeshe ni kwa kiwango gani Magufuli ametanua demokrasia kwa watu. Anasema anafanya manunuzi bila kufuata sheria ya manunuzi, tuonyesheni ni kwa namna gani mchakato wa manunuzi ulifanyika na bunge kushiriki. Anasema mlikula pesa za tetemeko Bukoba, tuonyeshe ni namna gani waathirika walipata pesa. Mambo yako mengi sana. Wewe unashauri wakae kimya huo ni ushauri wa ovyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kukanusha na kurumbana ni vitu viwili tofauti. CCM na Serikali wanachofanya ni kurumbana.

Kama kukanusha serikali walishakanusha, sasa kuendelea kurumbana tena wakitumia viongozi wa juu wa chama na serikali ni ujinga wa kiwango cha juu.

Hili suala sio kama wimbo eti CCM na serikali wanaimba kila mara. Hata wimbo hufika kipindi ambacho unachuja na kukosa waimbaji.
 
Kama nilivyokuuliza kwenye hoja uliojibu, wanajitetea ili kuua soo kwa nani? Kama ni kwa watawala wa Ulaya na Marekani wanajua kabla hata ya kujitetea.

Wanaua soo hapahapa nyumbani maana bado kuna watu wanajua Nyerere ni rais wa nchi hii. Toka Magufuli ameingia madarakani amebana vyombo vya habari mpaka anadhani kachukua na ufahamu wetu, hivyo anajua tunasubiri yeye na serikali yake ndio watuambie ukweli, na yeye anaamini tunaamini anachotuambia yeye ndio ukweli.
 
Laiti wangempa haki yake ya kumlipia matibabu, mheshimiwa rais angelaani lile tendo la kupigwa risasi, spika angemtembelea hospitalini, kejeli na matusi zisingetolewa na CCM ndani na nje ya Bunge, mshahara wake usingetishiwa kukatwa, spika angeacha nia ya kumfuta ubunge Lissu- kwa haya abayoyasema Lissu hakuna ambaye angemwaamini
Nimekuwa kimya na mtazamaji kuhusiana na suala hili la Tundu Lissu lakini baada ya kuangalia kwa muda nimegundua madhaifu mengi sana kwa upande wa serikali katika kukabiliana na yanayojiri kwenye suala hili.

Serikali na CCM wamekuwa reactive badala ya kuwa proactive ambapo matokeo yake wanafanya makosa mengi ya msingi hasa mahusiano ya umma.

Serikali na viongozi wa juu wa CCM kukimbizana na Lissu kwenye vyombo vya habari ili kujibu hoja zake ni ujinga wa kiwango cha juu kwa sababu kufanya hivyo ni kujiweka wazi kwenye maswali ambayo hanaya majibu ya kisiasa bali kiuchunguzi. Kimantiki taasisi ya kiuchunguzi wa makosa ya jinai haiwezi kutoa majibu ya uchunguzi kama uchunguzi haujakamilika lakini pia hata yakitolewa huwa yanatolewa kitaalam na kwa uangalifu mkubwa sana bila kujali mwathirika/waathirika wanafikra zipi.

Lissu akiwa anahojiwa na waandishi wa habari bila kuwepo maafisa wa serikali ni faida kwa serikali na CCM kuliko ofisa wa serikali na CCM kuwepo pia katika mahojiano hayo. Mahojiano yake katika kipindi cha HARDtalk bila uwepo wa ofisa wa serikali yaliinufaisha zaidi serikali kuliko muhojiwa. Hata pale alipotoa shutuma, mtangazaji alimwambia aache kutoa shutuma ambazo anaowatuhumu hawapo ili wazijibu.

Ni ujinga kwa serikali kudhani kuwa kinachofanyika hapa Tanzania hakijulikani katika makorido ya watawala wa Ulaya na Marekani na kwa maana hiyo wanakwenda kujibu tuhuma za upotoshaji. In fact, watawala wa Ulaya na Marekani wanajua hata yale yanayosemwa ndani ya Ikulu ya Magogoni nchini achilia mbali anayoyasema Lissu. Kwa maana hii, kama Lissu anayosema ni kweli au uwongo watakuwa wanajua.

Kwa mfano, juzi Gazeti la The New York Times la Marekani ambalo lina mahusiano ya karibu sana na majasusi wa Marekani lilipewa audio yenye maongezi ya mwana mfalme, Mohammed bin Salman akiwaambia watu wake wa karibu kuwa atatumia risasi kama Jamal Khashoggi hatarudi Saudi Arabia na kuachana na ukosoaji wa serikali. Hii inaonyesha kuwa kila anachokisema na kukifanya ndani ya nyumba yake kinajulikana kwa majasusi wa nchi ya Marekani.

Hii ina maana kuwa serikali inapoteza muda kujitetea kwenye suala la Tundu Lissu na demokrasia kwa sababu watawala wa Ulaya na Marekani wanajua kama ni kweli au uwongo.

Serikali lazima waelewe kuwa anachokitaka Tundu Lissu ni reaction ambayo ni reactive kutoka serikalini ili aendeleze marumbano na mijadala kwenye vyombo vya habari ya ndani na nje.

Ninakumbuka kwa mara yangu ya kwanza kusafiri katika nchi za Ulaya nilipewa ushauri kuwa ukimuona mtu anakuchokoza au kukuchochea unachotakiwa ni kutoonyesha hisia au kujibu. Kutoonyesha hisia au kujibu kutamfanya akose sababu ya kuendelea kukuchochea au kukuchokoza lakini kikubwa zaidi ataona anachofanya ni ujinga na kuachana na uchochezi au uchokozi.

Serikali ikikaa kimya hata wale wanaomuhoji Lissu watachoka kwa sababu kutakuwa hakuna reaction kutoka serikalini. Kukosa reaction kutoka serikalini ina maana hata mahojiano yanakuwa hayahitajiki (redundant). Serikali lazima waelewe dhana ya Newton's third law of motion. No force, no reaction lakini kikubwa zaidi uendeshaji wa serikali ni sawa na mbio za masafa marefu(marathon). Kuna wapiga kelele wataibuka na baadaye watapotea.

Watu wenye fikra pana wanaomfahamu Lissu hawashangai na kile anachokisema bali wanachoshangaa ni jinsi ambavyo viongozi wa juu wa CCM na serikali wanavyojibishana naye kwenye vyombo vya habari.

Kwa mtu mwenye fikra pana na anamfahamu vizuri Lissu atajua hupenda sana kujionyesha mbele ya watu/hadhara (limelight) lakini pia hufurahia sana (relish) kama kuna reaction bila kujali kama ni nzuri au mbaya. Waingereza huita Attention seeking behaviour. Lissu anachokitafuta kwa CCM na serikali ni kukimbizana au kujibishana naye kwenye media akiwa ndiye focal point.

Mpaka sasa malengo yake kwa kiwango kikubwa yamefanikiwa kutokana na ujinga wa viongozi wa juu wa serikali na CCM ambao wengi wao hawajui ukubwa na umuhimu wa vyeo vyao. Eti Katibu Mkuu wa chama tawala CCM anajibishana na Mjumbe wa Kamati Kuu wa chama cha upinzani CHADEMA, Tundu Lissu? This is beyond stupidity.

Lissu anatakiwa arumbane na wanachama wa kawaida wa CCM na sio viongozi wa juu wa chama. Majibu ya hoja za Lissu kuhusu shambulio lazima yajibiwe na taasisi rasmi za uchunguzi na sio kila kiongozi wa serikali.

Hawa viongozi wa CCM na serikali hawakujifunza makosa waliyoyafanya kwa Mange Kimambi baada ya kumkuza na kupata followers wengi kutokana na kujibishana naye. Makosa yaleyale wanayarudia kwa Tundu Lissu.

Katika dhana ile ile ya Attention seeking behaviour, Ninajua pia Lissu atapenda sana akirudi nchini akamatwe akiwa uwanja wa ndege ili kutimiza Newton's third law of motion ambapo matokeo yake yatakuwa kumpa umaarufu wa bure lakini kikubwa zaidi hata waliokuwa hawaamini aliyokuwa anayasema nwataamini niya kweli. Ninawaomba sana serikali wasimkamate siku akiingia nchini bali wamuache tu. No force, no rection.

Ninakumbuka mwaka 1995 wakati Augustino Mrema akiwa mpinzani maarufu nchini, kila alipobebwa waliombeba walipigwa mabomu na vitendo hivyo vilizidi kumfanya maarufu mpaka Mwalimu Nyerere alipotumia busara na kuwambia polisi, “Kwa kuwa wanaotaka kumbeba Mrema wapo, waacheni wambebe. Wambebe hata kama watakuwa wanapokezana kama machela (jeneza), waacheni.” Polisi walipotii agizo la Baba wa Taifa, la kuacha kuwapiga mabomu, Mrema naye kama shani hakubebwa tena. Mwl. Nyerere alitumia dhana ya Newton's third law of motion. No force, no reaction.

Tuliona pia huko Kenya, baada ya wapinzani kuamua kumuapisha Raila Odinga kuongoza Kenya baada kutangaza kwamba hamtambui Uhuru Kenyatta kama kiongozi aliyechaguliwa kwa njia halali, polisi waliwaacha wafanye hivyo na matokeo yake kitendo hicho kikaonekana nicha kijinga.

Huko Venezuela tumeona kiongozi wa upinzani akifanya kama alivyofanya Raila Odinga lakini dhumuni lake lilikuwa ni kutaka polisi wawazuie ili mapigano yatokee ambayo yangekuwa ni sababu ya Marekani kuingia kimabavu katika nchi hiyo kwa kisingizio cha kuzuia mauwaji. Serikali ya Rais Madulo ikajua janja yao na ikamuacha Juan Guaidó ajiapishe bila kumuingilia kwa kutumia nguvu ya polisi/jeshi. No force, no reaction. Uamuzi wa polisi/jeshi kumuacha ajiapishe kumeua malengo ya Marekani ya kuingiza majeshi Venezuela.

CCM na Serikali lazima waelewe kuwa hoja sio Lissu anatumiwa na ''mabeberu'' bali hoja ni jinsi gani wataweza kuzuia njama za ''Mabeberu'' kwa sababu ''mabeberu'' kuwatumia watu sio jambo jimpya.

Kuna Mzee mmoja aliwahi kunipa ushauri kwa maneno haya, Ukimya hukuvisha nguo ya utulivu na hukukinga na haja ya kutoa visingizio lakini pia jawabu fasihi kabisa kwa mpumbavu ni kutomjibu.

Nimalizie kwa kusema, Serikali na viongozi wa juu wa CCM lazima watambue kuwa hata kukaa kimya ni jibu kwa sababu hakuna serikali hapa duniani ambayo haijawahi kutuhumiwa kutaka kuua au kuua raia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni ushauri wenye mantiki kwa serikali, kosa kubwa lililofanyika toka mwanzo ni kujiangaisha na mpuuzi kama Tundu Lissu, ni mtu anayetafuta sifa binafsi kwa masllahi yake, anaungwa mkono na wapiuuzi wachache wasioipend serikali. Serikali iachane kujishughulisha naye.

Sent using Jamii Forums mobile app
mwaka huu mutavishwa mapampas kawa mjinga sasa kama mjinga simumuache na ujinga wake mabashite ya ccm mulidhani ni kimo kifupi mutaipata wacha jiwe awe kichuguu sasa
 
Nimekuwa kimya na mtazamaji kuhusiana na suala hili la Tundu Lissu lakini baada ya kuangalia kwa muda nimegundua madhaifu mengi sana kwa upande wa serikali katika kukabiliana na yanayojiri kwenye suala hili.

Serikali na CCM wamekuwa reactive badala ya kuwa proactive ambapo matokeo yake wanafanya makosa mengi ya msingi hasa mahusiano ya umma.

Serikali na viongozi wa juu wa CCM kukimbizana na Lissu kwenye vyombo vya habari ili kujibu hoja zake ni ujinga wa kiwango cha juu kwa sababu kufanya hivyo ni kujiweka wazi kwenye maswali ambayo hanaya majibu ya kisiasa bali kiuchunguzi. Kimantiki taasisi ya kiuchunguzi wa makosa ya jinai haiwezi kutoa majibu ya uchunguzi kama uchunguzi haujakamilika lakini pia hata yakitolewa huwa yanatolewa kitaalam na kwa uangalifu mkubwa sana bila kujali mwathirika/waathirika wanafikra zipi.

Lissu akiwa anahojiwa na waandishi wa habari bila kuwepo maafisa wa serikali ni faida kwa serikali na CCM kuliko ofisa wa serikali na CCM kuwepo pia katika mahojiano hayo. Mahojiano yake katika kipindi cha HARDtalk bila uwepo wa ofisa wa serikali yaliinufaisha zaidi serikali kuliko muhojiwa. Hata pale alipotoa shutuma, mtangazaji alimwambia aache kutoa shutuma ambazo anaowatuhumu hawapo ili wazijibu.

Ni ujinga kwa serikali kudhani kuwa kinachofanyika hapa Tanzania hakijulikani katika makorido ya watawala wa Ulaya na Marekani na kwa maana hiyo wanakwenda kujibu tuhuma za upotoshaji. In fact, watawala wa Ulaya na Marekani wanajua hata yale yanayosemwa ndani ya Ikulu ya Magogoni nchini achilia mbali anayoyasema Lissu. Kwa maana hii, kama Lissu anayosema ni kweli au uwongo watakuwa wanajua.

Kwa mfano, juzi Gazeti la The New York Times la Marekani ambalo lina mahusiano ya karibu sana na majasusi wa Marekani lilipewa audio yenye maongezi ya mwana mfalme, Mohammed bin Salman akiwaambia watu wake wa karibu kuwa atatumia risasi kama Jamal Khashoggi hatarudi Saudi Arabia na kuachana na ukosoaji wa serikali. Hii inaonyesha kuwa kila anachokisema na kukifanya ndani ya nyumba yake kinajulikana kwa majasusi wa nchi ya Marekani.

Hii ina maana kuwa serikali inapoteza muda kujitetea kwenye suala la Tundu Lissu na demokrasia kwa sababu watawala wa Ulaya na Marekani wanajua kama ni kweli au uwongo.

Serikali lazima waelewe kuwa anachokitaka Tundu Lissu ni reaction ambayo ni reactive kutoka serikalini ili aendeleze marumbano na mijadala kwenye vyombo vya habari ya ndani na nje.

Ninakumbuka kwa mara yangu ya kwanza kusafiri katika nchi za Ulaya nilipewa ushauri kuwa ukimuona mtu anakuchokoza au kukuchochea unachotakiwa ni kutoonyesha hisia au kujibu. Kutoonyesha hisia au kujibu kutamfanya akose sababu ya kuendelea kukuchochea au kukuchokoza lakini kikubwa zaidi ataona anachofanya ni ujinga na kuachana na uchochezi au uchokozi.

Serikali ikikaa kimya hata wale wanaomuhoji Lissu watachoka kwa sababu kutakuwa hakuna reaction kutoka serikalini. Kukosa reaction kutoka serikalini ina maana hata mahojiano yanakuwa hayahitajiki (redundant). Serikali lazima waelewe dhana ya Newton's third law of motion. No force, no reaction lakini kikubwa zaidi uendeshaji wa serikali ni sawa na mbio za masafa marefu(marathon). Kuna wapiga kelele wataibuka na baadaye watapotea.

Watu wenye fikra pana wanaomfahamu Lissu hawashangai na kile anachokisema bali wanachoshangaa ni jinsi ambavyo viongozi wa juu wa CCM na serikali wanavyojibishana naye kwenye vyombo vya habari.

Kwa mtu mwenye fikra pana na anamfahamu vizuri Lissu atajua hupenda sana kujionyesha mbele ya watu/hadhara (limelight) lakini pia hufurahia sana (relish) kama kuna reaction bila kujali kama ni nzuri au mbaya. Waingereza huita Attention seeking behaviour. Lissu anachokitafuta kwa CCM na serikali ni kukimbizana au kujibishana naye kwenye media akiwa ndiye focal point.

Mpaka sasa malengo yake kwa kiwango kikubwa yamefanikiwa kutokana na ujinga wa viongozi wa juu wa serikali na CCM ambao wengi wao hawajui ukubwa na umuhimu wa vyeo vyao. Eti Katibu Mkuu wa chama tawala CCM anajibishana na Mjumbe wa Kamati Kuu wa chama cha upinzani CHADEMA, Tundu Lissu? This is beyond stupidity.

Lissu anatakiwa arumbane na wanachama wa kawaida wa CCM na sio viongozi wa juu wa chama. Majibu ya hoja za Lissu kuhusu shambulio lazima yajibiwe na taasisi rasmi za uchunguzi na sio kila kiongozi wa serikali.

Hawa viongozi wa CCM na serikali hawakujifunza makosa waliyoyafanya kwa Mange Kimambi baada ya kumkuza na kupata followers wengi kutokana na kujibishana naye. Makosa yaleyale wanayarudia kwa Tundu Lissu.

Katika dhana ile ile ya Attention seeking behaviour, Ninajua pia Lissu atapenda sana akirudi nchini akamatwe akiwa uwanja wa ndege ili kutimiza Newton's third law of motion ambapo matokeo yake yatakuwa kumpa umaarufu wa bure lakini kikubwa zaidi hata waliokuwa hawaamini aliyokuwa anayasema nwataamini niya kweli. Ninawaomba sana serikali wasimkamate siku akiingia nchini bali wamuache tu. No force, no rection.

Ninakumbuka mwaka 1995 wakati Augustino Mrema akiwa mpinzani maarufu nchini, kila alipobebwa waliombeba walipigwa mabomu na vitendo hivyo vilizidi kumfanya maarufu mpaka Mwalimu Nyerere alipotumia busara na kuwambia polisi, “Kwa kuwa wanaotaka kumbeba Mrema wapo, waacheni wambebe. Wambebe hata kama watakuwa wanapokezana kama machela (jeneza), waacheni.” Polisi walipotii agizo la Baba wa Taifa, la kuacha kuwapiga mabomu, Mrema naye kama shani hakubebwa tena. Mwl. Nyerere alitumia dhana ya Newton's third law of motion. No force, no reaction.

Tuliona pia huko Kenya, baada ya wapinzani kuamua kumuapisha Raila Odinga kuongoza Kenya baada kutangaza kwamba hamtambui Uhuru Kenyatta kama kiongozi aliyechaguliwa kwa njia halali, polisi waliwaacha wafanye hivyo na matokeo yake kitendo hicho kikaonekana nicha kijinga.

Huko Venezuela tumeona kiongozi wa upinzani akifanya kama alivyofanya Raila Odinga lakini dhumuni lake lilikuwa ni kutaka polisi wawazuie ili mapigano yatokee ambayo yangekuwa ni sababu ya Marekani kuingia kimabavu katika nchi hiyo kwa kisingizio cha kuzuia mauwaji. Serikali ya Rais Madulo ikajua janja yao na ikamuacha Juan Guaidó ajiapishe bila kumuingilia kwa kutumia nguvu ya polisi/jeshi. No force, no reaction. Uamuzi wa polisi/jeshi kumuacha ajiapishe kumeua malengo ya Marekani ya kuingiza majeshi Venezuela.

CCM na Serikali lazima waelewe kuwa hoja sio Lissu anatumiwa na ''mabeberu'' bali hoja ni jinsi gani wataweza kuzuia njama za ''Mabeberu'' kwa sababu ''mabeberu'' kuwatumia watu sio jambo jimpya.

Kuna Mzee mmoja aliwahi kunipa ushauri kwa maneno haya, Ukimya hukuvisha nguo ya utulivu na hukukinga na haja ya kutoa visingizio lakini pia jawabu fasihi kabisa kwa mpumbavu ni kutomjibu.

Nimalizie kwa kusema, Serikali na viongozi wa juu wa CCM lazima watambue kuwa hata kukaa kimya ni jibu kwa sababu hakuna serikali hapa duniani ambayo haijawahi kutuhumiwa kutaka kuua au kuua raia.
Usicheze na damu ya mtu..hiyo mifano ya akina Mrema, sijui Vdenezuela na Kenya haina nafasi hapa. Damu ya mtu msicheze nayo!
 
Kukanusha na kurumbana ni vitu viwili tofauti. CCM na Serikali wanachofanya ni kurumbana.

Kama kukanusha serikali walishakanusha, sasa kuendelea kurumbana tena wakitumia viongozi wa juu wa chama na serikali ni ujinga wa kiwango cha juu.

Hili suala sio kama wimbo eti CCM na serikali wanaimba kila mara. Hata wimbo hufika kipindi ambacho unachuja na kukosa waimbaji.
Serikali waliishakanusha? Ni lini walieleza sababu za kuondoa ulinzi kwenye nyumba za viongozi wa serikali siku Lisu anamiminiwa risasi? Ni lini serikali iliishaeleza sababu za kuondolewa kwa kamera za CCTV kwenye nyumba anayoishi Dk. Kalemani baada ya Lisu kushambuliwa?
 
Jaribu kufanya jambo, kisha uliyemfanyia awe anakutangaza uone kama utakaa kimya. Unasema hivyo maana hukushirikishwa kwenye ye shambulio lake. Hao wanaomjibu ndio waliomshambulia.
Unajuaje kama hakushirikishwa?
 
mzee usituletee porojo mm tu naweza kulichunguza wala haihitaji mwaka lakini POLISI TZ wapo kulinda CCM tu ibaki madarakani wala sio vyenginevyo WEWE KESI YA MASHEIKH WA UWAMSHO SASA HUU NI MWAKA WA TANO BADO WANACHUNGUZA TU kama ni kweli POLISI wa TAnzania hawafai ni bora likavunywa wakaanza mwanzo kuanzia zero

Nadhani hujaelewa mantiki ya andiko langu
 
Hapa kwetu ukisema polisi walae pembeni wawaache wapinzani ujue Nchi tunababa, tuseme Ukweli CCM ipo kwa nguvu ya polisi tu.

ukiaema uhaguzi uwe wa huru na wa haki bila kuingiliwa na polisi tunashinda asubuhi saa nne. ukisema Mikutano ya siasa ifanyike bila kuingiliwa na policcm basi ujue Magu hana chake. Ukisema Lissu ashuke JNIA kwa uhuru kabisa utaona mwenyewe hayo mapolezi yake hayajawahi kutokea duniani.
Ulichoandika ni dhana tu kulingana na mtazamo wako.

Wasomi wazuri hutumia research katika kufikia mahitisho ya hoja ulizozisema.

Hata hivyo ninashukuru kwa mchango wako kifikra.
 
Ulichoandika ni dhana tu kulingana na mtazamo wako.

Wasomi wazuri hutumia research katika kufikia mahitisho ya hoja ulizozisema.

Hata hivyo ninashukuru kwa mchango wako kifikra.
Uchaguzi wa kinondoki 17 feb 2018 bila polisi ccm ingeshimda vipiUchaguzi wa kule Kakonko kigoma bola polisi wngeshinda vipi ccm hadi USs embassy ikhibitisha kuwa uchaguzi haukuwa huru na uligubigwa na virugu na vitisho. Hili nalo unataka research?? Nyie ndio wasomi wa hovyo.
 
Kwa hiyo wewe unamzidi fikra Jpm na ikulu inayowatuma kumjibu??

Braza hata ingekuwa wewe usingevumilia Lisu ana sababisha Damage kubwa sana, ukizingatia ukeweli unauma.
Nilichofanya nimetoa mtazamo wangu kifikra. Hoja ya kusema namzidi au simzidi fikra JPM ni mtazamo wako.
 
Kwa kiwango flani ulichokiandika kina leta mantiki, lakini changamoto nyingine inakuja kwamba , jambo likisemwa muda mrefu sana bila kukanushwa hugeuka kuwa kweli.

Hivyo mara moja moja kuna umuhimu wa kumjibu.
Serikali imeishakanusha,

Hoja yangu ni viongozi wa juu wa CCM na serikali kuanza kufukuzana na Lissu kwenye media eti wanaenda kumjibu hoja zake.

Huu ni ujinga wa hali ya juu kwa sababu wanachokifanya hakiwajengi bali kinawabomoa zaidi kwa sababu wanaingia kwenye mtego wa Lissu ambao anataka warumbane.
 
Suala la ''silence means Yes'' ni hisia tu kwa sababu usemi ni dhana inayotokana na mazingira.

Ni bora serikali ikakaa kimya kuliko kutoa majibu ya kisiasa wakati wana vyombo vya kiuchunguzi na wataalam wake waliofundishwa jinsi ya kuwasiliana na umma katika mazingira ya kiuchunguzi.

Serikali kutoa majibu ya kisiasa ni kuji-incriminate bila kujua.

Kumbe jibu ulikuwa nalo; tena fupi na la hakika zaidi. Ungeliweka hili mbele na wazi, pasingekuwa na haja ya kupoteza muda na hayo mengine yaliyomo kwenye bandiko.
 
Tatizo ni kwamba ukiwa na madaraka unaamini sana katika kile ambacho madaraka yanaweza kufanya, matokeo yake unakuwa mbali na kile ambacho madaraka hayawezi kufanya. Hapa ndipo penye hekima na akili.

Ukiwa na bunduki unakuwa unaamini sana katika kile ambacho bunduki inaweza kufanya kuliko kila ambacho bunduki haiwezi kufanya.

Zana yoyote yaweza tawala akili ya mwanadamu.

In short, artificial produces artificial.
Hoja yako ni fikirishi.
 
JF bado tuna vichwa vizuri

bandiko zuri sana, tactic nzuri kwa CCM

makosa mbalimbali ya CDM ndio ya CCM pia, hakuna brainy za kuamua nini kifanyike na wakati gani na nani afanye
Nashukuru sana kwa mchango wako.

Tuendelee kuelimishana kwa sababu Jamiiforums ya sasa inaanza kujaa wajinga ambao hawaelewi kama ni wajinga.
 
Kinachonifurahisha ni ujumbe wangu umefikia kwa sababu umesoma mpaka ukajua ni history ndefu naya hovyo hovyo!

Nakushukuru sana!
Hata kwa kuanzisha uzi huu tayari umeendeleza malumbano kuhusu Lissu & co.

Mimi nadhani, serikali yetu kwa maana ya viongozi, wajue kuwa kunyamazisha watu kutasababisha watu waongee zaidi, hata kwa njia kama hizi anazotumia Lissu.
Walianziwa kina Mawazo , Saa 8, Agwanda, Roma nk nk. Watu walichukulia poa, waliokuwa wakiyatenda hawakudhani kuwa litalipuka. Sasa hili la Lissu limekuwa la kinyama zaidi na nafikiri aliyekuwa anamkinga boss asichafuke, amemchafua zaidi kwa kutokutumia hekima.

Pili Maghufuli na serikali yake hawana haja ya kuwa na alleg na democracy. Kwa sababu na yeye democracy ndiyo imemfikisha hapo alipo. Asizuie wengine kujaribu bahati zao ki halali.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimekuelewa sana, ndio maana nikasema wakiusikiliza ushauri huu, watajiepusha na fedheha za ziada.
Kuna utovu wa busara na hekima kama ulivyoeleza hapo awali. Unakumbuka BWM alituhumiwa sana kuhusu mgodi, watu waliongea sana, alibaki kimya bila kujibu chochote iwe ilikua kweli au uongo lakini aliamua kujibu kwa kunyamaza.

Mithali 17:28. Hata mpumbavu akinyamaza, huhesabiwa hekima; Akifumba midomo yake, huhesabiwa ufahamu
Ninakubaliana na angalizo lako.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom