Serikali msiwafutie Watoto matokeo, toeni matokeo yao haraka. Hawana hatia. Tatizo ni Mfumo

Mambo ya mkoloni yametoka wapi mbona unahorojoka kama mwendawazimu?

Huyo mkoloni ndiye aliyewafundisha kuziweka mahakama kwenye kapu la mfalme?

Unaona sasa linchi linavyoenda kilevi?

Mwenzio huyu hajui hata kama kuna mahakama! Kaamua kumpigia magoti magufuli ili ampe HISANI!

Huyo mfalme wenu amsaidie basi! Ampe hiyo HISANI.... si nilisikiaga anajiita mtetezi wa wanyonge sijui?
Utopolo tupu!
 
Kufutwa matokeo ipo tangu mkoloni mkuu kawadanganye watoto wenzako!
Unatumia nguvu kubwa Sana kuitetea serikali yako kuliko hata unayoitumia kumtafuta Mungu
Cha kukushauri tumia jina lako halisi ikiwezekana uweke na contact yako
Ukifanya hivyo soon utapata uteuzi
Mwenzako nishaula.
 
Acha utopolo wewe kijana kwani kufutiwa matokeo imeanza wakati wa Magufuli tu? Pia kama unajua inavyoratibiwa kwanini hukuripoti mapema ili washughulikiwi. Acha sheria ichukue mkondo wake kama ambavyo watz wamekubaliana.
Soma tena main thread nlivyoanza.
Afu nimekuheshimu.

Better late than Never.
 
Acha utopolo wewe kijana kwani kufutiwa matokeo imeanza wakati wa Magufuli tu? Pia kama unajua inavyoratibiwa kwanini hukuripoti mapema ili washughulikiwi. Acha sheria ichukue mkondo wake kama ambavyo watz wamekubaliana.
Ubongo mgando, yaani akili yako haiwezi badirika na kuwa bora,, always to embrace the dictatorship regime.

Umekariri solution moja ya zaman,, huwezi badirika ili mradi umemkingia bwanako.

Wanaowaza wamejaribu kuona tatizo liko wapi ,,,na hicho chanzo ndicho kiwajibike na siyo kumuwajibisha mtoto mdogo aliyeitwa na kuambiwa kaandike hiki na mwalimu wake.
 
Naongea wazi kabisa hapa. Kwa miaka mingi Serikali imekuwa ikihukumu maisha ya wahitimu wa darasa la saba kimakosa mno.

Ipo hivi...

Watendaji na wasimamizi wa elimu ya msingi wao ndio viongozi wa kuratibu cheating. Hili liko wazi kabisa na NECTA wanalijua.

Walimu wakuu wa shule za msingi hupigwa mikwara na ma RC, RAS, REO, DED, DEO, DAS, WARATIBU WA ELIMU etc. Wafanye vyovyote iwezekanavyo KUWAFAULISHA watoto. Nasisitiza KUWAFAULISHA. Na mbinu zote za kuwafaulisha huratibiwa na Walimu Wakuu na Waratibu wa Elimu katani. Wanafunzi hupokea tu maelekezo. Hawana hatia.

That being said, nawaambia NECTA na namwabia Rais Magufuli. Achieni matokeo ya vijana hao haraka. Hawahusiki.

Wajibisheni mamlaka husika, nimezitaja hapo juu. Vigezo vyote vilivyoandikwa/semwa na NECTA kuwafutia matokeo vijana hao hakuna hata kimoja kilichosababishwa na mwanafunzi. Kumbukeni hawa ni watoto wadogo sana na hufuata orders toka kwa walimu wao.

Ni muda muafaka sasa umefika, kuacha tabia ya kumfurahisha mkuu wenu. Yote haya yanafanyika kumfurahisha MAGUFULI. HII SI SAWA.

Shule zotee za uma hufake/hucheat ili tu kumpemdezesha mkuu wenu.

OMBI.

Rais Magufuli iamuru NECTA itoe matokeo ya vijana hawa 1059. Then deal with your SYSTEM.
Sifa mbili mpya za kimfumo za Watanzania zilizojitokeza miaka ya karibuni na zaidi Awamu hii ni sote ni wavivu wapiga domo vijiweni na kila mahali, na pili ni tumekuwa wezi wa kila kitu mpaka hatuaminiki tena tunaiba hata mali za Umma na kura ili viongozi wetu washinde kwa kishindo.
 
Naunga mkono hoja. Mtoto wa miaka 12 anawezaje kuiba mtihani shuleni Kama mission haijafanywa na Walimu? Na akiambiwa majibu haya hapa mtoto kama huyo ana utashi wa kukataa?
You Wonder.... I wonder.

Haki tena nakwambia hili halipiti bure..
 
Mtanganyika mwenzio amemwangukia magufuli kwanini unamzuia? muache atoe ya moyoni ati!?

Huko Danganyika Republic mahakama zote zimetiwa kwenye kapu la mfalme. Mambo yote yanaamuliwa na mfalme kwenye geto lake.

Hii ingelikuwa ni nchi halisi (a true republic) ungeona wananchi wanachacharika kwenda mahakamani kuweka ZUIO na kuiomba mahakama IWAAMRISHE maafisa wa NECTA kutoa matokeo.

That is called "checks and balances". Mihimili ya nchi inatizamana na kuwekana sawa.

Sasa huko Tanganyika, mahakama zote ziko kwenye kapu la mfalme. Ukikohoa unapigwa rungu la utosi.
There u r.
 
Ubongo mgando, yaani akili yako haiwezi badirika na kuwa bora,, always to embrace the dictatorship regime.

Umekariri solution moja ya zaman,, huwezi badirika ili mradi umemkingia bwanako.

Wanaowaza wamejaribu kuona tatizo liko wapi ,,,na hicho chanzo ndicho kiwajibike na siyo kumuwajibisha mtoto mdogo aliyeitwa na kuambiwa kaandike hiki na mwalimu wake.
Napingana naye alipoonyesha kuwa NECTA wanafanya hivyo ili kumridhisha Magufuli mkuu! Hilo la mgando wa akili nafikiri wewe ndiyo zimeganda zaidi kuliko kawaida!
 
Mtoa mada hilo swala dr msonde leo ameongelea kupitia tbc baada ya kubanwa sana na mtangazaji majibu yake amesema hiyo imekula kwao maana hata hao wanafunzi wamefanya makosa maana kupitia seminar mbali mbali walionywa kutokufanya udanganyifu au wangetoa taarifa mapema.

Pia amesema adhabu kali itatolewa kwa waalimu pamoja na wasimamizi walio husika baada ya uchunguzi kukamilika.
Kwa taarifa kamili fatilia tbc aridhio leo jioni utasikia mengi kuhusu hilo swala.
 
Naongea wazi kabisa hapa. Kwa miaka mingi Serikali imekuwa ikihukumu maisha ya wahitimu wa darasa la saba kimakosa mno.

Ipo hivi...

Watendaji na wasimamizi wa elimu ya msingi wao ndio viongozi wa kuratibu cheating. Hili liko wazi kabisa na NECTA wanalijua.

Walimu wakuu wa shule za msingi hupigwa mikwara na ma RC, RAS, REO, DED, DEO, DAS, WARATIBU WA ELIMU etc. Wafanye vyovyote iwezekanavyo KUWAFAULISHA watoto. Nasisitiza KUWAFAULISHA. Na mbinu zote za kuwafaulisha huratibiwa na Walimu Wakuu na Waratibu wa Elimu katani. Wanafunzi hupokea tu maelekezo. Hawana hatia.

That being said, nawaambia NECTA na namwabia Rais Magufuli. Achieni matokeo ya vijana hao haraka. Hawahusiki.

Wajibisheni mamlaka husika, nimezitaja hapo juu. Vigezo vyote vilivyoandikwa/semwa na NECTA kuwafutia matokeo vijana hao hakuna hata kimoja kilichosababishwa na mwanafunzi. Kumbukeni hawa ni watoto wadogo sana na hufuata orders toka kwa walimu wao.

Ni muda muafaka sasa umefika, kuacha tabia ya kumfurahisha mkuu wenu. Yote haya yanafanyika kumfurahisha MAGUFULI. HII SI SAWA.

Shule zotee za uma hufake/hucheat ili tu kumpemdezesha mkuu wenu.

OMBI.

Rais Magufuli iamuru NECTA itoe matokeo ya vijana hawa 1059. Then deal with your SYSTEM.
Mkuu hawa makada wa CCM wakiambiwa kuwa inahitajika taasisi imara ili iweze kuiongoza nchi hii kwa ufanisi hawaelewi. Wao kila kitu kwao ni itikadi tu ya chama chao, weledi, utaalamu, ujuzi na miiko ya kazi wanavipuuzia. Wanaona ni sifa kumsifu na kumuabudu mtu mmoja mwenye nguvu za kikatiba ambaye anaongoza nchi kwa hisia na matamanio yake.

Jambo hili linawafanya wafanye jambo lolote lile ambalo wanatambua ya dhati kuwa wanamfurahisha boss wao. Kama walitumika ili kumfanya ashinde kwa kishindo ktk uchaguzi mkuu kwa hila na hadaa, watatumia pia mbinu zile zile za wizi waliozoea na kufundishwa ili kufanikisha malengo yao binafsi ktk nafasi zao za kazi.

Sent from my Nokia 2.1 using JamiiForums mobile app
 
watendaji wawajibishwe, kwanza huu mtihani sioni kama una tija...wangekuwa wa form 4 au 6 hapo sana....
 
Cheating ilikua shule binafsi,sasa ni serikali ya awamu ya tano!

Kama serikali inafanya cheating ya kura,mitihani si ni mboga tu?

Hatuna nchi,tunajidanganya!

Hii awamu ya tano ni majambazi pure,bure kabisa!

Nasikitika vyombo vya habari vipo kimya.
What is this country. !?

Na wazazi ambao watoto wao wamedhulumiwa haki hii ya kufurahia kuhitimu kwa wanao watakaa kimya..

What is this country.!?

Lakini wanasheria nguli kina Kibatala na wengineo wako wapi!?

Damn.

Mtoto huyu wa miaka 12, 13, 14 tumeathiri maisha yake yote kwa kumuita 'cheat' bila hatia yeyote.

This mustn't go unsaid..
 
Naongea wazi kabisa hapa. Kwa miaka mingi Serikali imekuwa ikihukumu maisha ya wahitimu wa darasa la saba kimakosa mno.

Ipo hivi...

Watendaji na wasimamizi wa elimu ya msingi wao ndio viongozi wa kuratibu cheating. Hili liko wazi kabisa na NECTA wanalijua.

Walimu wakuu wa shule za msingi hupigwa mikwara na ma RC, RAS, REO, DED, DEO, DAS, WARATIBU WA ELIMU etc. Wafanye vyovyote iwezekanavyo KUWAFAULISHA watoto. Nasisitiza KUWAFAULISHA. Na mbinu zote za kuwafaulisha huratibiwa na Walimu Wakuu na Waratibu wa Elimu katani. Wanafunzi hupokea tu maelekezo. Hawana hatia.

That being said, nawaambia NECTA na namwabia Rais Magufuli. Achieni matokeo ya vijana hao haraka. Hawahusiki.

Wajibisheni mamlaka husika, nimezitaja hapo juu. Vigezo vyote vilivyoandikwa/semwa na NECTA kuwafutia matokeo vijana hao hakuna hata kimoja kilichosababishwa na mwanafunzi. Kumbukeni hawa ni watoto wadogo sana na hufuata orders toka kwa walimu wao.

Ni muda muafaka sasa umefika, kuacha tabia ya kumfurahisha mkuu wenu. Yote haya yanafanyika kumfurahisha MAGUFULI. HII SI SAWA.

Shule zotee za uma hufake/hucheat ili tu kumpemdezesha mkuu wenu.

OMBI.

Rais Magufuli iamuru NECTA itoe matokeo ya vijana hawa 1059. Then deal with your SYSTEM.
Elimu yetu imekua na simanzi siku zote, waruhusu shule kutafuta waalimu kokote duniani sio lazima kutoka hapa TZ, kwani waalimu ni zao la wanafunzi walioanguka mitihani, Waalimu kazi ni kupiga watoto ili wafaulu, lakini wanachofundisha hakieleweki, wanaofundisha hawaelewi wanachokifundisha, hatuwezi kubadilisha sisi wenyewe lazima tutachanganye maarifa yawengine, Inasikitisha sana, anahukumiwa Watoto wasio na makosa
 
Acha utopolo wewe kijana kwani kufutiwa matokeo imeanza wakati wa Magufuli tu? Pia kama unajua inavyoratibiwa kwanini hukuripoti mapema ili washughulikiwi. Acha sheria ichukue mkondo wake kama ambavyo watz wamekubaliana.
Na MATOKEO ya uchaguzi yatafutwa??
 
Back
Top Bottom