Jenerali Ambamba
JF-Expert Member
- Sep 8, 2014
- 3,344
- 2,526
Wakuu naomba kuendelea kusisitiza kuwa tena kwa Kiswahili na maneno mepesi kabisa ili kila mtu aelewe, naona serikali na watu baadhi hapa wanapotosha sana.
Pesa za ESCROW zilihifadhiwa Benki Kuu na TANESCO ili kupisha na kusubiri uamuzi wa mahakama ya usuluhishi ya Uingereza juu ya tozo/gharama kubwa ambazo TANESCO ilikuwa inailipa IPTL, hivyo TANESCO ikalalamika.
Kabla ya uamuzi kutolewa na mahakama ya usuluhishi {ambapo tayari sasa umetoka} pesa hizo zikatolewa kinyemela.
PESA NI ZA UMMA AU SI ZA UMMA?
Sehemu ya pesa hizo zingekuwa za UMMA (TANESCO), IPTL, na TRA. Mahakama ya usuluhishi ingekubaliana na hoja kuwa ni kweli IPTL TANESCO gharama kubwa hivyo wakokotoe tena, basi TAIFA lingepata mgao wake hapo halali na IPTL ikapata mgao wake halali, TRA nayo ikapata mgao wake
Sasa tatizo nini?
wezi hawa hawakutaka kusubiri maamuzi ya mahakama ya usuluhishi hivyo baada ya kuwarubuni viongozi wa serikali nao wakarubunika kirahisi.
Pesa za ESCROW zilihifadhiwa Benki Kuu na TANESCO ili kupisha na kusubiri uamuzi wa mahakama ya usuluhishi ya Uingereza juu ya tozo/gharama kubwa ambazo TANESCO ilikuwa inailipa IPTL, hivyo TANESCO ikalalamika.
Kabla ya uamuzi kutolewa na mahakama ya usuluhishi {ambapo tayari sasa umetoka} pesa hizo zikatolewa kinyemela.
PESA NI ZA UMMA AU SI ZA UMMA?
Sehemu ya pesa hizo zingekuwa za UMMA (TANESCO), IPTL, na TRA. Mahakama ya usuluhishi ingekubaliana na hoja kuwa ni kweli IPTL TANESCO gharama kubwa hivyo wakokotoe tena, basi TAIFA lingepata mgao wake hapo halali na IPTL ikapata mgao wake halali, TRA nayo ikapata mgao wake
Sasa tatizo nini?
wezi hawa hawakutaka kusubiri maamuzi ya mahakama ya usuluhishi hivyo baada ya kuwarubuni viongozi wa serikali nao wakarubunika kirahisi.