Richard
JF-Expert Member
- Oct 23, 2006
- 14,939
- 20,398
Serikali mpya ya dharura ya umoja wa kitaifa inatarajiwa kuapishwa rasmi nchini Israeli mapema kesho.
Serikali hiyo itaundwa na vyama vya Likud, Blue and White, Shas,United Torah Judaism, Labor na chama cha Derech Eretz.
Waziri mkuu Benjamin Netanyahu anatarajiwa kutangaza ajenda ya Marekani ya kuhakikisha theluthi tatu ya ukanda wa Magharibi inakuwa sehemu ya kudumu ya Israeli
Itakumbukwa kuwa mwezi January raisi Donald Trump alitangaza kuwa mpango mpya wa Marekani "Vision of Peace Plan" kati ya Israeli na Palestina ni wa kuhakikisha kwamba theluthi tatu au asilimia 30 ya ukanda wa Magharibi au West Bank unakuwa sehemu na makazi ya kudumu ya Israeli jambo ambalo Palestina imelikataa katakata
Mike Pompeo aliwasili mjini Jerusalem jana jioni kushuhudia pamoja na masuala mengine kitendo cha waziri mkuu wa sasa Benjamin Netanyahu akikabidhi jukumu ya kutangaza kuwa asilimia 30 ya ukanda wa magharibi sasa ni sehemu na makazi ya kudumu ya Israeli.
Mike Pompeo angeweza kuzungumza na Netanyau pamoja na Benny Gantz ambae ataongoza serikali ya mseto kwa pamoja na Netanyahu ni wa kutoka chama cha upinzani kwa njia ya simu ya video au video conferencing au njia ya simu ya kawaida lakini kitendo cha kusafiri na kutua Jeresalem kinaashiria umuhimu wa Pompeo kuwepo hapo.
Benjamin Netanyahu ambae anaongoza taifa la Israeli kwa miaka 11 sasa, anaachia madaraka makubwa ya uwaziri mkuu na hata nafasi ya kuwa naibu waziri mkuu baada ya uamuzi wa mahakama kuu kuwa tuhuma anazokabiliwa nazo za rrushwa na ufisadi zinamfanya asiweze kuendelea kuwa waziri mkuu wa Isralei kwa asilimia 100.
Ndani ya miaka mitatu, serikali mpya ya umoja wa kitaifa itakuwa ikingozwa kwa pamoja na bwana Bennie Gantz ambae zamani alliwahi kuwa mnadhimu mkuu wa jeshi la ulinzi la Israeli IDF na ndie aliekuwa spika wa bunge la Israeli ya Knesset akiwakilisha chama cha Blue and White..
Benjamin Netanyahu ataendelea kuwa waziri mkuu huku Gantz akiwa waziri wa ulinzi na naibu waziri mkuu kwa miezi 18 na baada baada ya hapo Gantz atakuwa waziri mkuu huku Netanyahu akiwa naibu wake.
Katika makubaliano ya kuunda serikali ya mseto Netanyahu na Gantz wamekubaliana kwamba yeye (Netanyahu ataendelea kuwa na sauti juu ya uteuzi wa mwanasheria mkuu wa serikali na pia ataendelea kuishi kwenya makazi yake ya sasa. hii inampa ahueni bwana Netanyahu kwani ikiwa mwanasheria mpya serikali atakuwepo ataweza kupendekeza Netanyahu kuondolewa kwenye nafasi ya uwaziri mkuu.
Pia wamekubaliana kwamba endapo mahakama kuu itamwondoa madarakani bwana Netanyahu kutokana na kukutwa na hatia ya ufisadi basi bwana Gantz atapaswa kuitisha uchaguzi mkuu.
Pia nafasi za waziri wa sheria na ile ya mambo ya nje zimeenda kwa watu wa Blue and White bwana Avi Niseenkorn wakati bwana Gabi Ashkenazi ambae pia ni mnadhimu mkuu wa zamani wa IDF anakuwa wazri wa mambo ya nje. Hivyo Israeli itakuwa na majenerali wa zamani bwana Gantz akiwa waziri wa ulinzi na Ashkenazi akiwa wazri wa mambo ya nje.
Mpangp mpya wa Marekani juu ya ugawaji wa sehemu hiyo ya ukanda wa magharibi unaipa Israeli uwezo mkubwa wa kutawala kijeshi eneo hilo, sehemu kubwa ya ardhi ya eneo hilo na pia sehemu zote za Jerusalem na makazi yote ya kudumu ya waisraeli.
Nchi za Umoja wa ulaya zikiongozwa na Ufaransa, Ireland na Belgium zimeripotiwa kutishia kuiwekea vikwazo vya kiuchumi Israeli endapo itavunja sheria za kimataifa pindi itakapojitangazia kuwa sehemu hiyo ya ukanda wa magharibi ni yake.
Kitendo cha raisi Donald Trump kumtuma bwana Pompeo harakaharaka kwenda Jerusalem na kuhakikisha mpango huo unatekelezwa ni kitendo cha raisi Trump kujitafutia kura zaidi kwa kuzingatia kwamba kampeni zake za uraisi zinategemea masuala kama hayo pamoja na jinsi gani ameongoza vita dhidi ya ugonjwa COVID-19
Ndoto za Palestina kuwa na haki ya kumiliki ardhi ndani ya ukanda wa Magharibi zimepunguzwa nguvu kubwa kutokana na sasa Israeli kufundi kuongozwa na majenerali wa zamani wa jeshi la IDF ambao tayari wameagiza idara ya ujasusi wa ndani ya Shin Belt kuhakikisha kila raia wakiwemo waisraeli wenyewe, anachunguzwa mienendo yake wakiwepo wapalestina khasa kwa kutumia vita dhidi ya ugonjwa wa Covid-19.
Ufuatiliaji huo wa lazima au Surveillance Powers unahusisha kuchungua simu za mikononi khasa wale wanaowasiliana na waathirika wa COVID-19.
Utawala wa Palestina unaongoza sehemu ya ukanda wa Magharibi umeomba kiasi cha dola milioni 120 ili kuzitumia kubapambana na ugonjwa wa COVID -19 ambao mpaka Jumatatu walikuwapo wagonjwa 449 na vifo vinne.
Asilimia 17 ya idadi ya watu hawana ajira na robo tatu ya wakazi hao wanategemea misaada kutoka nje
Richard na vyanzo mbalimbali.
Serikali hiyo itaundwa na vyama vya Likud, Blue and White, Shas,United Torah Judaism, Labor na chama cha Derech Eretz.
Waziri mkuu Benjamin Netanyahu anatarajiwa kutangaza ajenda ya Marekani ya kuhakikisha theluthi tatu ya ukanda wa Magharibi inakuwa sehemu ya kudumu ya Israeli
Itakumbukwa kuwa mwezi January raisi Donald Trump alitangaza kuwa mpango mpya wa Marekani "Vision of Peace Plan" kati ya Israeli na Palestina ni wa kuhakikisha kwamba theluthi tatu au asilimia 30 ya ukanda wa Magharibi au West Bank unakuwa sehemu na makazi ya kudumu ya Israeli jambo ambalo Palestina imelikataa katakata
Mike Pompeo aliwasili mjini Jerusalem jana jioni kushuhudia pamoja na masuala mengine kitendo cha waziri mkuu wa sasa Benjamin Netanyahu akikabidhi jukumu ya kutangaza kuwa asilimia 30 ya ukanda wa magharibi sasa ni sehemu na makazi ya kudumu ya Israeli.
Mike Pompeo angeweza kuzungumza na Netanyau pamoja na Benny Gantz ambae ataongoza serikali ya mseto kwa pamoja na Netanyahu ni wa kutoka chama cha upinzani kwa njia ya simu ya video au video conferencing au njia ya simu ya kawaida lakini kitendo cha kusafiri na kutua Jeresalem kinaashiria umuhimu wa Pompeo kuwepo hapo.
Benjamin Netanyahu ambae anaongoza taifa la Israeli kwa miaka 11 sasa, anaachia madaraka makubwa ya uwaziri mkuu na hata nafasi ya kuwa naibu waziri mkuu baada ya uamuzi wa mahakama kuu kuwa tuhuma anazokabiliwa nazo za rrushwa na ufisadi zinamfanya asiweze kuendelea kuwa waziri mkuu wa Isralei kwa asilimia 100.
Ndani ya miaka mitatu, serikali mpya ya umoja wa kitaifa itakuwa ikingozwa kwa pamoja na bwana Bennie Gantz ambae zamani alliwahi kuwa mnadhimu mkuu wa jeshi la ulinzi la Israeli IDF na ndie aliekuwa spika wa bunge la Israeli ya Knesset akiwakilisha chama cha Blue and White..
Benjamin Netanyahu ataendelea kuwa waziri mkuu huku Gantz akiwa waziri wa ulinzi na naibu waziri mkuu kwa miezi 18 na baada baada ya hapo Gantz atakuwa waziri mkuu huku Netanyahu akiwa naibu wake.
Katika makubaliano ya kuunda serikali ya mseto Netanyahu na Gantz wamekubaliana kwamba yeye (Netanyahu ataendelea kuwa na sauti juu ya uteuzi wa mwanasheria mkuu wa serikali na pia ataendelea kuishi kwenya makazi yake ya sasa. hii inampa ahueni bwana Netanyahu kwani ikiwa mwanasheria mpya serikali atakuwepo ataweza kupendekeza Netanyahu kuondolewa kwenye nafasi ya uwaziri mkuu.
Pia wamekubaliana kwamba endapo mahakama kuu itamwondoa madarakani bwana Netanyahu kutokana na kukutwa na hatia ya ufisadi basi bwana Gantz atapaswa kuitisha uchaguzi mkuu.
Pia nafasi za waziri wa sheria na ile ya mambo ya nje zimeenda kwa watu wa Blue and White bwana Avi Niseenkorn wakati bwana Gabi Ashkenazi ambae pia ni mnadhimu mkuu wa zamani wa IDF anakuwa wazri wa mambo ya nje. Hivyo Israeli itakuwa na majenerali wa zamani bwana Gantz akiwa waziri wa ulinzi na Ashkenazi akiwa wazri wa mambo ya nje.
Mpangp mpya wa Marekani juu ya ugawaji wa sehemu hiyo ya ukanda wa magharibi unaipa Israeli uwezo mkubwa wa kutawala kijeshi eneo hilo, sehemu kubwa ya ardhi ya eneo hilo na pia sehemu zote za Jerusalem na makazi yote ya kudumu ya waisraeli.
Nchi za Umoja wa ulaya zikiongozwa na Ufaransa, Ireland na Belgium zimeripotiwa kutishia kuiwekea vikwazo vya kiuchumi Israeli endapo itavunja sheria za kimataifa pindi itakapojitangazia kuwa sehemu hiyo ya ukanda wa magharibi ni yake.
Kitendo cha raisi Donald Trump kumtuma bwana Pompeo harakaharaka kwenda Jerusalem na kuhakikisha mpango huo unatekelezwa ni kitendo cha raisi Trump kujitafutia kura zaidi kwa kuzingatia kwamba kampeni zake za uraisi zinategemea masuala kama hayo pamoja na jinsi gani ameongoza vita dhidi ya ugonjwa COVID-19
Ndoto za Palestina kuwa na haki ya kumiliki ardhi ndani ya ukanda wa Magharibi zimepunguzwa nguvu kubwa kutokana na sasa Israeli kufundi kuongozwa na majenerali wa zamani wa jeshi la IDF ambao tayari wameagiza idara ya ujasusi wa ndani ya Shin Belt kuhakikisha kila raia wakiwemo waisraeli wenyewe, anachunguzwa mienendo yake wakiwepo wapalestina khasa kwa kutumia vita dhidi ya ugonjwa wa Covid-19.
Ufuatiliaji huo wa lazima au Surveillance Powers unahusisha kuchungua simu za mikononi khasa wale wanaowasiliana na waathirika wa COVID-19.
Utawala wa Palestina unaongoza sehemu ya ukanda wa Magharibi umeomba kiasi cha dola milioni 120 ili kuzitumia kubapambana na ugonjwa wa COVID -19 ambao mpaka Jumatatu walikuwapo wagonjwa 449 na vifo vinne.
Asilimia 17 ya idadi ya watu hawana ajira na robo tatu ya wakazi hao wanategemea misaada kutoka nje
Richard na vyanzo mbalimbali.